< 1 Samweli 6 >
1 Basi sanduku la BWANA lilikaa katika nchi ya Wafilisti kwa miezi saba.
So the Arke of the Lord was in the countrey of the Philistims seuen moneths.
2 Ndipo Wafilisti wakawaita makuhani na waganga; wakawaambia, “Tulifanyie nini sanduku la BWANA? Twambieni jinsi ambavyo tunapaswa kulirudisha sanduku katika nchi yake.”
And the Philistims called the priests and the soothsayers, saying, What shall we doe with the Arke of the Lord? tell vs wherewith we shall send it home againe.
3 Makuhani na waganga wakasema, “Kama mtalirudisha sanduku la Mungu wa Israeli, msilipeleke bila zawadi; kwa namna yoyote ile mpelekeeni sadakaa ya hatia. Hapo ndipo mtapona, na mtajua ni kwanini mkono wake hadi sasa haujaondoka juu yenu.”
And they sayd, If you send away the Arke of the God of Israel, send it not away emptie, but giue vnto it a sinne offering: then shall ye be healed, and it shall be knowen to you, why his hand departeth not from you.
4 Ndipo wakawauliza, “Sadaka ya hatia itakuwa nini kwamba tunampelekea?” Wakawajibu, “Majipu matano ya dhahabu na panya watano wa dhahabu, Idadi hiyo ya watano ni sawa na idadi ya viongozi wa Wafilisti. Kwa sababu tauni ya aina moja iliwashambulia ninyi na viongozi wenu.
Then sayd they, What shalbe the sinne offring, which we shall giue vnto it? And they answered, Fiue golden emerods and fiue golden mise, according to the number of the princes of the Philistims: for one plague was on you all, and on your princes.
5 Kwa hiyo, nilazima mtengeneze mifano ya majipu yenu, na mifano ya panya wenu ambayo huiharibu nchi, na mpeni utukufu Mungu wa Israeli. Labda ataondoa mkono wake kutoka juu yenu, kutoka juu ya miungu yenu, na kutoka juu ya nchi yenu.
Wherefore ye shall make the similitudes of your emerods, and the similitudes of your mise that destroy the land: so ye shall giue glory vnto the God of Israel, that he may take his hand from you, and from your gods, and from your land.
6 Kwanini mfanye mioyo yenu kwa migumu, kama vile Wamisri na Farao walifanya mioyo yao kuwa migumu? Hicho ni kipindi ambacho Mungu wa Israeli aliwashughilikia sana; Je, Wamisri hawakuwaachilia watu, na wakaondoka?
Wherefore then should ye harden your hearts, as the Egyptians and Pharaoh hardened their hearts? when he wrought wonderfully among them, did they not let them goe, and they departed?
7 Basi sasa, andaeni mkokoteni mpya pamoja na ng'ombe wawili wake wanaonyonyesha, ambao hawajawahi kufungwa nira. Wafungeni ng'ombe hao kwenye mkokoteni, lakini warudisheni wale ndama wao nyumbani.
Now therefore make a new cart, and take two milch kine, on whome there hath come no yoke: and tye the kine to the cart, and bring the calues home from them.
8 Kisha lichukueni sanduku la BWANA na kuliweka ndani ya mkokoteni. Wekeni ndani ya kasha yale maumbo ya dhahabu mnayompelekea ambyo ni sadaka ya hatia kando yake. Ndipo mlipeleke lipate kuondoka.
Then take the Arke of the Lord, and set it vpon the cart, and put the iewels of gold which ye giue it for a sinne offering in a coffer by the side thereof, and send it away, that it may go.
9 Kisha muwe makini; kama litapanda kwenda kwa njia hadi nchini mwake hadi Beth Shemeshi, basi mjue kuwa BWANA ndiye aliyetenda pigo hili kubwa. Lakini kama halitakwenda, ndipo tutajua kwamba siyo mkono wake uliotupatia mateso; badala yake tutajua kuwa yaliyotupata ilikuwa ni kwa bahati mbaya tu.
And take heede, if it goe vp by the way of his owne coast to Beth-shemesh, it is he that did vs this great euill: but if not, we shall know then, that it is not his hand that smote vs, but it was a chance that happened vs.
10 Watu hao wakafanya kama walivyoambiwa, walichukuwa ng'ombe wawili wanaonyonyesha, wakawafunga kwenye mkokoteni, na kuwabakiza ndama wao nyumbani.
And the men did so: for they tooke two kine that gaue milke, and tied them to the cart, and shut the calues at home.
11 Wakaliweka sanduku la BWANA juu ya mkokoteni, pamoja na lile kasha lililobeba panya wa dhahabu na yale maumbo ya majipu yao.
So they set the Arke of the Lord vpon the cart, and the coffer with the mise of golde, and with the similitudes of their emerods.
12 Hao ng'ombe waliondoka moja kwa moja kuelekea Beth Shemeshi. Walikwenda kwa kuifuata nija moja kuu, wakiteremka walipokuwa wakienda, na hwakugeuka upande wa kushoto au kulia. Viongozi wa Wafilisti walifuata kwa nyuma hadi mpaka wa Beth Shemeshi.
And the kine went the streight way to Beth-shemesh, and kept one path and lowed as they went, and turned neither to the right hand nor to the left: also the Princes of the Philistims went after them, vnto the borders of Beth-shemesh.
13 Nao watu wa Beth Shemeshi walikuwa wakivuna ngano yao katika bonde. Waliponyanyua macho yao juu na kuliona sanduku, wakafurahi.
Nowe they of Beth-shemesh were reaping their wheate haruest in the valley, and they lift vp their eyes, and spied the Arke, and reioyced when they sawe it.
14 Huo mkokoteni ulifikia ndani ya shamba la Yoshua wa Beth Shemeshi na ukasimama hapo. Kulikuapo jiwe kubwa mahali hapo, wakatayarisha kuni kutokana na mkokoteni huo, na wakawatoa ng'ombe hao kama sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya BWANA.
And the cart came into the fielde of Ioshua a Beth-shemite, and stood still there. There was also a great stone, and they claue the wood of the cart, and offered the kine for a burnt offring vnto the Lord.
15 Walawi walilitelemsha sanduku la BWANA chini pamoja na kasha lake lililoyatunza yale maumbo ya dhahabu, wakaweka vitu hivyo juu ya hilo jiwe kubwa. Watu wa Beth Shemeshi walitoa sadaka za kuteketezwa na kutoa dhabihu kwa BWANA siku iyo hiyo.
And the Leuites tooke downe the Arke of the Lord, and the coffer that was with it, wherein the iewels of golde were, and put them on the great stone, and the men of Beth-shemesh offred burnt offring, and sacrificed sacrifices that same day vnto the Lord.
16 Hao viongozi watano wa Wafilisti walipoona hayo, walirejea Ekroni siku iyo hiyo.
And when the fiue Princes of ye Philistims had seene it, they returned to Ekron the same day.
17 Haya ndiyo majipu ya dhahabu ambayo Wafilisti walirudisha kama sadaka ya hatia kwa BWANA: moja kwa ajili ya Ashdodi, moja kwa Gaza, moja kwa Ashkeloni, moja kwa Gathi, na moja kwa Ekroni.
So these are the golden emerods, which the Philistims gaue for a sinne offering to the Lord: for Ashdod one, for Gaza one, for Askelon one, for Gath one, and for Ekron one,
18 Idadi ya wale panya wa dhahabu ilikuwa sawa na ile ya idadi ya miji yote ya Wafilisti inayomilikiwa na viongozi watano, kwa miji iliyojengewa maboma na vijiji vya mashambani. Lile jiwe kubwa, ambalo kando yake waliweka sanduku la BWANA, lipo kama ushuhuda hadi leo katika shamba la Yoshua Mbeth- Shemeshi.
And golden mise, according to the number of all the cities of the Philistims, belonging to the fiue princes, both of walled townes, and of townes vnwalled, vnto the great stone of Abel, whereon they set the Arke of the Lord: which stone remaineth vnto this day in the fielde of Ioshua the Beth-shemite.
19 BWANA akawashambulia baadhi ya watu wa Bethi Shemeshi kwa sababu walichungulia ndani ya sanduku lake. Aliwaua watu sabini. Watu wakaomboleza, kwa sababu BWANA aliwapa watu pigo kubwa mno.
And hee smote of the men of Beth-shemesh, because they had looked in the Arke of the Lord: he slew euen among the people fiftie thousand men and three score and ten men. and the people lamented, because the Lord had slaine the people with so great a slaughter.
20 Watu wa Bethi Shemeshi wakasema, “Ni nani mwenye uwezo wa kushindana na BWANA, huyu Mungu mtakatifu? Na atampandia nani akitoka kwetu.”” Je, ni nani awezaye kusimama mbele ya BWANA, huyu Mungu mtakatifu? Na ni kwa nani ambako sanduku litaenda likitoka hapa.”
Wherefore the men of Beth-shemesh said, Who is able to stand before this holy Lord God? and to whom shall he go from vs?
21 Wakawatuma wajumbe kwenda kwa wenyeji wa Kiriath Yearimu, wakisema, “Wafilisti wamelirudisha sanduku la BWANA; teremkeni na mkalipeleke kwenu.”
And they sent messengers to the inhabitans of Kiriath-iearim, saying, The Philistims haue brought againe the Arke of the Lord: come ye downe and take it vp to you.