< 1 Samweli 5 >

1 Basi Wafilisti wakawa wamelitwaa sanduku la Mungu, wakalileta kutoka Ebenezeri hadi Ashdodi.
А Филистеји узеше ковчег Божји, и однесоше из Евен-Езера у Азот.
2 Wafilisti walilichukua sanduku la Mungu, wakalileta ndani ya nyumba ya Dagoni, na wakalikalisha pembeni mwa Dagoni.
И узевши Филистеји ковчег Божји унесоше га у дом Дагонов, и наместише га до Дагона.
3 Watu wa Ashdodi walipoamka mapema siku ya pili, tazama, Dagoni ilianguka chini kifudifudi mbele ya sanduku la BWANA. Hivyo waliichukua Dagoni na kuisimamisha tena katika sehemu yake.
А сутрадан кад усташе Азоћани рано, а то Дагон лежаше ничице на земљи пред ковчегом Господњим; и они узеше Дагона и метнуше га опет на његово место.
4 Lakini walipoamka mapema kesho yake, tazama, Dagoni alikuwa ameanguka chini kifudifudi mbele ya sanduku la BWANA. Kichwa cha Dagoni na vitanga vyake miwili vilikatika na kulala mlangoni. Kiwiliwili cha Dagoni ndicho kilibaki tu.
А кад сутрадан рано усташе, гле, опет Дагон лежаше ничице на земљи пред ковчегом Господњим, а глава Дагону и обе руке одсечене беху на прагу; само труп од Дагона беше остао.
5 Na hii ndiyo sababu, makuhani wa Dagoni na yeyote aingiae ndani ya nyumba ya Dagoni, hata leo, hawezi kukanyaga mlango wa Dagoni katika Ashdodi.
Зато свештеници Дагонови и који год улазе у дом Дагонов не стају на праг Дагонов у Азоту до данас.
6 Mkono wa BWANA ulikuwa mzito juu ya watu wa Ashdodi. Aliwaangamiza akawatesa kwa majipu, Ashdodi na wilaya zake kwa pamoja.
Тада отежа рука Господња Азоћанима, и мораше их и удараше их шуљевима у Азоту и међама његовим.
7 Watu wa Ashdodi walipotambua kilichokuwa kinatokea, walisema, “Sanduku la Mungu wa Israeli lisikae kwetu, kwa sababu mkono wake ni mzito juu yetu na juu ya mungu wetu Dagoni.”
А кад Азоћани видеше шта је, рекоше да не стоји код нас ковчег Бога Израиљевог; јер је рука Његова тешка над нама и над Дагоном богом нашим.
8 Basi wakawatuma watu wawakusanye pamoja viongozi wote wa Wafilisti; wakawambia, “Tufanye nini na sanduku la Mungu wa Israeli?” Wakawajibu, “Sanduku la Mungu wa Israeli lihamishwe na kupelekwa Gathi.” Basi wakalihamisha hilo sanduku la Mungu wa Israeli hadi huko Gathi.
И послаше, те сабраше к себи све кнезове филистејске, и рекоше им: Шта ћемо чинити с ковчегом Бога Израиљевог? А они рекоше: Да се пренесе у Гат ковчег Бога Израиљевог. И пренесоше ковчег Бога Израиљевог.
9 Lakini baada ya kulipeleka huko, mkono wa BWANA ulikuwa juu ya mji huo, ukasababisha machafuko makubwa. Akawatesa watu wa mji huo, wakubwa kwa wadogo; na majipu yakaota juu ya miili yao.
А кад га пренесоше, би рука Господња на граду с муком врло великом, и стаде бити грађане од малог до великог, и дођоше на њих тајни шуљеви.
10 Basi, wakalipeleka sanduku la Mungu hadi Ekroni. Lakini mara tu sanduku la Mungu lilipoingia Ekroni, watu wa Ekroni walipiga kelele wakisema, “Wametuletea sanduku la Mungu wa Israeli kutuua sisi na watu wetu.”
Зато послаше ковчег Божји у Акарон; а кад дође ковчег Божји у Акарон, повикаше Акароњани говорећи: Донесоше к нама ковчег Бога Израиљевог да помори нас и наш народ.
11 Basi wakawatuma watu wawakusanye pamoja viongozi wote wa Wafilisti; wakawambia, “Lipelekeni mbali sanduku la Mungu wa Israeli, na lirudishwe katika makao yake, ili lisije kutuua sisi na watu wetu.” Kwa maana kulikuwa na hofu ya kutisha mjini mwote; Mkono wa Mungu ulikuwa mzito mno huko.
Зато послаше, те сабраше све кнезове филистејске, и рекоше: Пошљите ковчег Бога Израиљевог нека се врати на своје место, да не помори нас и народ наш. Јер беше смртан страх по целом граду, и врло тешка беше рука Господња онде.
12 Watu ambao hawakufa waliteswa na majipu, na kilio cha mji kilipanda hadi mbinguni.
Јер људи који остајаху живи боловаху од шуљева тако да се вика у граду подизаше до неба.

< 1 Samweli 5 >