< 1 Samweli 5 >

1 Basi Wafilisti wakawa wamelitwaa sanduku la Mungu, wakalileta kutoka Ebenezeri hadi Ashdodi.
And the Philistines have taken the Ark of God, and bring it in from Eben-Ezer to Ashdod,
2 Wafilisti walilichukua sanduku la Mungu, wakalileta ndani ya nyumba ya Dagoni, na wakalikalisha pembeni mwa Dagoni.
and the Philistines take the Ark of God and bring it into the house of Dagon, and set it near Dagon.
3 Watu wa Ashdodi walipoamka mapema siku ya pili, tazama, Dagoni ilianguka chini kifudifudi mbele ya sanduku la BWANA. Hivyo waliichukua Dagoni na kuisimamisha tena katika sehemu yake.
And the Ashdodites rise early on the next day, and behold, Dagon is fallen on its face to the earth, before the Ark of YHWH; and they take Dagon, and put it back in its place.
4 Lakini walipoamka mapema kesho yake, tazama, Dagoni alikuwa ameanguka chini kifudifudi mbele ya sanduku la BWANA. Kichwa cha Dagoni na vitanga vyake miwili vilikatika na kulala mlangoni. Kiwiliwili cha Dagoni ndicho kilibaki tu.
And they rise early in the morning on the next day, and behold, Dagon is fallen on its face to the earth, before the Ark of YHWH, and the head of Dagon, and the two palms of its hands are cut off at the threshold, only Dagon’s [body] has been left of him;
5 Na hii ndiyo sababu, makuhani wa Dagoni na yeyote aingiae ndani ya nyumba ya Dagoni, hata leo, hawezi kukanyaga mlango wa Dagoni katika Ashdodi.
therefore the priests of Dagon, and all those coming into the house of Dagon, do not tread on the threshold of Dagon, in Ashdod, until this day.
6 Mkono wa BWANA ulikuwa mzito juu ya watu wa Ashdodi. Aliwaangamiza akawatesa kwa majipu, Ashdodi na wilaya zake kwa pamoja.
And the hand of YHWH is heavy on the Ashdodites, and He makes them desolate, and strikes them with lumps, Ashdod and its borders.
7 Watu wa Ashdodi walipotambua kilichokuwa kinatokea, walisema, “Sanduku la Mungu wa Israeli lisikae kwetu, kwa sababu mkono wake ni mzito juu yetu na juu ya mungu wetu Dagoni.”
And the men of Ashdod see that [it is] so, and have said, “The Ark of the God of Israel does not abide with us, for His hand has been hard on us, and on our god Dagon.”
8 Basi wakawatuma watu wawakusanye pamoja viongozi wote wa Wafilisti; wakawambia, “Tufanye nini na sanduku la Mungu wa Israeli?” Wakawajibu, “Sanduku la Mungu wa Israeli lihamishwe na kupelekwa Gathi.” Basi wakalihamisha hilo sanduku la Mungu wa Israeli hadi huko Gathi.
And they send and gather all the princes of the Philistines to them, and say, “What do we do to the Ark of the God of Israel?” And they say, “Let the Ark of the God of Israel be brought around to Gath”; and they bring around the Ark of the God of Israel;
9 Lakini baada ya kulipeleka huko, mkono wa BWANA ulikuwa juu ya mji huo, ukasababisha machafuko makubwa. Akawatesa watu wa mji huo, wakubwa kwa wadogo; na majipu yakaota juu ya miili yao.
and it comes to pass after they have brought it around, that the hand of YHWH is against the city—a very great destruction; and He strikes the men of the city, from small and to great; and lumps break forth on them.
10 Basi, wakalipeleka sanduku la Mungu hadi Ekroni. Lakini mara tu sanduku la Mungu lilipoingia Ekroni, watu wa Ekroni walipiga kelele wakisema, “Wametuletea sanduku la Mungu wa Israeli kutuua sisi na watu wetu.”
And they send the Ark of God to Ekron, and it comes to pass, at the coming in of the Ark of God to Ekron, that the Ekronites cry out, saying, “They have brought around the Ark of the God of Israel to us, to put us and our people to death.”
11 Basi wakawatuma watu wawakusanye pamoja viongozi wote wa Wafilisti; wakawambia, “Lipelekeni mbali sanduku la Mungu wa Israeli, na lirudishwe katika makao yake, ili lisije kutuua sisi na watu wetu.” Kwa maana kulikuwa na hofu ya kutisha mjini mwote; Mkono wa Mungu ulikuwa mzito mno huko.
And they send and gather all the princes of the Philistines, and say, “Send the Ark of the God of Israel away, and it turns back to its place, and it does not put us and our people to death”; for there has been a deadly destruction throughout all the city, the hand of God has been very heavy there,
12 Watu ambao hawakufa waliteswa na majipu, na kilio cha mji kilipanda hadi mbinguni.
and the men who have not died have been struck with lumps, and the cry of the city goes up into the heavens.

< 1 Samweli 5 >