< 1 Samweli 4 >

1 Neno la Samweli likawafikia Israeli wote. Basi Israeli wakatoka kupigana dhidi ya Wafilisti. Nao wakaweka kambi hapo Ebenezeri, na Wafilisti waliweka kambi yao huko Afeki.
La parole de Samuel s’adressait à tout Israël. Les Israélites marchèrent en guerre contre les Philistins et établirent leur camp près d’Eben-Haézer; celui des Philistins était à Aphek.
2 Nao Wafilisti walijipanga kwa ajili ya vita dhidi ya Waisraeli. Vita ilipopamba moto, Israeli ilishindwa na Wafilisti, wakauawa watu wapatao elfu nne kwenye uwanja wa vita.
Les Philistins s’alignèrent en face d’Israël, la bataille devint générale, les Israélites furent défaits par les Philistins et laissèrent sur le champ de bataille environ quatre mille morts.
3 Watu walipokuja kambini, wazee wa Israeli walisema, “Kwa nini BWANA ametushinda leo mbele ya Wafilisti? Hebu tulilete hapa sanduku la ushuhuda wa BWANA kutoka Shilo, ili kwamba liwe hapa pamoja nasi, ili litufanye tuwe salama kutokana na nguvu za maadui zetu.”
Le peuple étant rentré au camp, les anciens d’Israël se dirent: "D’Où vient que l’Eternel nous a laissé battre aujourd’hui par les Philistins? Faisons venir ici, de Silo, l’arche d’alliance de l’Eternel, afin qu’elle soit au milieu de nous et nous assiste contre nos ennemis."
4 Hivyo waliwatuma watu huko Shilo; kutokea huko walilibeba sanduku la ushuhuda wa BWANA wa majeshi, akaaye juu ya makerubi. Hofni na Finehasi, watoto wawili wa Eli, walikuwapo pamoja na lile sanduku la ushuhuda wa Mungu.
Le peuple envoya donc à Silo, pour en ramener l’arche d’alliance de l’Eternel-Cebaot, qui trône sur les chérubins; là, près de l’arche d’alliance du Seigneur, étaient les deux fils d’Héli, Hophni et Phinéas.
5 Sanduku la ushuhuda wa BWANA lilipofika kambini, watu wote wa Israeli walipiga yowe, na nchi ikavuma.
Lorsque l’arche de l’alliance divine arriva au camp, tout Israël poussa une si grande clameur que le pays en trembla.
6 Wafilisti waliposikia kelele za mayowe, wakasema, “sauti hii ya mayowe katika kambi ya Waebrania inamaanisha nini?” Baadaye walitambua kwamba sanduku la BWANA limefika kambini.
Les Philistins, entendant ces cris de joie, demandèrent: "Que signifie cette bruyante clameur dans le camp des Hébreux?" Et ils apprirent que l’arche de l’Eternel était arrivée dans le camp.
7 Wafilisti waliogopa sana, “Mungu ameingia kambini.” Wakasema, “Ole wetu! Jambo kama hili halijawahi kutokea huko nyuma!
Et les Philistins eurent peur, parce qu’ils disaient: "Dieu est venu dans le camp", et ils ajoutaient: "Malheur à nous! Jamais auparavant pareille chose n’était arrivée.
8 Ole wetu! Ni nani atatulinda dhidi ya nguvu za Mungu mwenye uwezo? Huyu ndiye Mungu aliyewashambulia Wamisri kwa aina tofauti za mapigo mengi jangwani.
Malheur à nous! Qui nous sauvera de la main de ces redoutables dieux? Oui, ce sont ces mêmes dieux qui frappèrent les Egyptiens de tant de plaies dans le désert.
9 Enyi Wafilisti, iweni hodari, na fanyeni kiume, vinginevyo mtakuwa watumwa wa Waebrabia, kama walivyokuwa watumwa wenu. Fanyeni kiume, na piganeni nao.”
Armez-vous de courage, soyez hommes, ô Philistins! Si vous ne voulez subir le joug des Hébreux comme ils ont subi le vôtre; soyez hommes et luttez!"
10 Wafilisti walipigana, na Waisraeli wakashindwa. Kila mtu alikimbilia nyumbani kwake, na mauaji yalikuwa makubwa sana; maana askari wa Israeli elfu thelathini waendao kwa miguu vitani, walianguka.
Et les Philistins attaquèrent, et les Israélites furent battus et s’enfuirent dans leurs tentes: ce fut une défaite considérable, trente mille hommes de pied périrent en Israël.
11 Lile sanduku la Mungu lilichukuliwa, na watoto wa Eli, Hofni na Finehasi waliuawa.
De plus, l’arche du Seigneur fut prise, et les deux fils d’Héli, Hophni et Phinéas, périrent aussi.
12 Mtu mmoja wa Benjamini alikimbia kutoka uwanja wa vita akaja Shilo siku iyo hiyo, aliwasili na mavazi yake yamechanika na matope kichwani pake.
Un Benjamite s’échappa du champ de bataille et arriva à Silo ce même jour, ayant ses vêtements déchirés et la tête couverte de poussière.
13 Alipofika, Eli alikuwa amekaa kitini pake karibu na barabara akitazama kwa sababu moyo wake ulitetemeka kwa ajili ya sanduku la Mungu. Mtu yule alipoingia mjini na kutoa taarifa, mji wote ulilia.
Comme il arrivait, Héli était assis sur son siège, au bord du chemin, dans une attente pleine d’anxiété, à cause de l’arche du Seigneur; l’homme vint répandre la nouvelle dans la ville, qui éclata tout entière en lamentations.
14 Eli aliposikia kelele ya kilio kile, alisema, “Kilio hicho kina maana gani?” Kwa haraka mtu yule alikuja na kumweleza Eli.
En entendant ces cris, Héli demanda: "Qu’est-ce que cette clameur de la foule?" Et l’homme s’empressa d’approcher et de l’apprendre à Héli.
15 Basi Eli alikuwa na umri wa miaka tisini na nane; macho yake yamepofuka, na hakuweza kuona.
Celui-ci avait alors quatre-vingt-dix-huit ans; ses yeux étaient immobiles, il ne pouvait plus voir.
16 Yule mtu akamwambia Eli, “Mimi ndiye nimechomoka kutoka vitani. Nimetoroka kutoka kwenye mapigano leo.” Eli akasema, “Mambo yalienda namna gani, mwanangu?”
"C’Est moi, dit l’homme à Héli, qui viens du champ de bataille, je m’en suis échappé aujourd’hui. Quelle a donc été l’issue, mon fils?" demanda Héli.
17 Yule mtu aliyeleta hizo habari alijibu na kusema, “Israeli wamewakimbia Wafilisti. Pia watu wengi wameuwawa. Watoto wako, Hofni na Finehasi, wamekufa, na sanduku la Mungu limechukuliwa.”.
Le messager répondit: "Israël a pris la fuite devant les Philistins, et le peuple a essuyé de grandes pertes; de plus, tes deux fils Hophni et Phinéas sont morts, et l’arche du Seigneur est prise."
18 Alipotamka sanduku la Mungu, Eli alianguka chali kutoka kwenye kiti chake karibu na mlango. akavunjika shingo lake, na kufariki, kwa sababu alikuwa mzee tena mzito. Naye alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka arobaini.
En l’entendant mentionner l’arche du Seigneur, Héli tomba de son siège à la renverse, du côté de la porte, se brisa la nuque et mourut, car cet homme était vieux et appesanti par l’âge. Il avait gouverné Israël quarante années.
19 Basi mkwewe, mke wa Finihasi, alikuwa mjamzito akikaribia kujifungua. aliposikia habari kwamba sanduku la Mungu limetekwa nyara na kwamba baba mkwe na mme wake wamefariki, alichuchumaa chini akajifungua, lakini utungu wake ulimzidi na ulimtaabisha sana.
Sa bru, la femme de Phinéas, était alors dans un état de grossesse avancée. En apprenant ces nouvelles, que l’arche du Seigneur était prise, que son beau-père et son époux étaient morts, elle s’affaissa et enfanta, brusquement saisie par les douleurs.
20 Alipokaribia kufariki, wanawake waliokuwa wakimhudumia walisema, “Usiogope, maana umejifungua mtoto wa kiume.” Lakini hakuwajibu lolote au kuzingatia alichoambiwa.
La voyant près de mourir, les femmes qui l’assistaient lui dirent: "Ne crains rien, c’est un garçon que tu as mis au monde." Mais, indifférente à leurs paroles, elle ne répondit point.
21 Akamwita mtoto Ikabodi, akisema, “Utukufu umetoweka Israeli!” Kwa sababu sanduku la Mungu limetekwa nyara, na kwa sababu ya kifo cha baba mkwe na mme wake.
Et elle nomma l’enfant I-Cabod, en disant "C’En est fait de la gloire d’Israël!" à cause de la capture de l’arche divine, de la mort de son beau-père et de son époux.
22 Na alisema, “Utukufu umetoweka kutoka Israeli, kwa sababu sanduku la Mungu limetekwa nyala.”
"Oui, dit-elle, plus de gloire pour Israël, maintenant que l’arche divine est prise!"

< 1 Samweli 4 >