< 1 Samweli 31 >

1 Basi Wafilisti wakapigana dhidi ya Waisraeli. Waisraeli wakakimbia mbele ya Wafilisti na wakaanguka chini wakafa katika mlima wa Gilboa.
Later, the Philistines again fought against the Israelis. The Israelis ran away from them, and (many Israelis were killed/the Philistines killed many Israelis) on Gilboa Mountain.
2 Wafilisti wakamwandama Sauli na wanawe kwa karibu. Wakawaua wanawe Yonathani, Abinadabu, and Malkishua.
The Philistines caught up with Saul and his three sons, and they killed [all three of] his sons, Jonathan and Abinadab and Malchishua.
3 Vita vikamwelemea Sauli, na wapiga upinde wakampata. Akapata maumivu makali kwa sababu yao.
The fighting was very fierce around Saul. When the Philistine (archers/men with bows and arrows) caught up with Saul, they wounded him badly [with their arrows].
4 Kisha Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Chomoa upanga wako unichome nao. Vinginevyo, hawa wasiotahiriwa watakuja na kuninyanyasa.” Lakini mbeba silaha wake hakukubali, kwa kuwa aliogopa sana. Hivyo Sauli alichukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
Saul said to the man who was carrying his weapons, “Take out your sword and kill me with it, in order that these heathen Philistines will not be able to thrust their swords into me and make fun of me [while I am dying].” But the man who was carrying Saul’s weapons was terrified, and refused to do that. So Saul took his own sword and fell on it. [The sword pierced his body and he died].
5 Yule mbeba silaha akaona kwamba Sauli amekufa, yeye naye vivyo hivyo akauangukia upanga wake akafa pamoja naye.
When the man carrying his weapons saw that Saul was dead, he also threw himself on his own sword and died.
6 Kwa hiyo Sauli alikufa, wanawe watatu, na mbeba silaha wake - watu hawa wote walikufa pamoja siku iyo hiyo.
So Saul, three of his sons, and the man who carried Saul’s weapons, all died on that same day.
7 Watu wa Israeli waliokuwa upande mwingine wa bonde, na hao waliokuwa ng'ambo ya Yordani, walipoona kwamba Waisraeli wamekimbia, na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, waliiacha miji yao na kukimbia, nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
When the Israeli people on the north side of the [Jezreel] Valley and on the east side of the Jordan [River] heard that the Israeli army had run away and that Saul and his sons had died, they left their towns and ran away. Then the Philistines came and occupied their towns.
8 IKawa katika siku iliyofuata, Wafilisti wakafika kuchukua nyara za waliokufa, ndipo wakamuona Sauli na wanawe watatu wameanguka juu ya mlima wa Gilboa.
The next day, when the Philistines came to take away the weapons of the dead [Israeli soldiers], they found the bodies of Saul and his three sons on Gilboa Mountain.
9 Nao wakakata kichwa chake na kuondoa silaha zake, na wakawatuma wajumbe kwenda pande zote katika nchi ya Wafilisti kutangaza habari hizo katika mahekalu yao ya sanamu na kwa watu.
They cut off Saul’s head and took his weapons. Then they sent messengers throughout their land, to proclaim the news, in the temple where they kept their idols, and to the other people, [that their army had killed Saul].
10 Wakaziweka silaha zake katika hekalu la Ashtorethi, nao wakakitundika kiwiliwili chake kwenye ukuta wa mji wa Bethi Shani.
They put Saul’s weapons in the temple of [their goddess] Astarte. They also fastened the bodies of Saul [and his sons] to the wall [that surrounded] Beth-Shan [city].
11 Na wenyeji wa Yabeshi Gileadi waliposikia kile Wafilisti walichomfanyia Sauli,
When the people who lived in Jabesh in [the] Gilead [region] heard what the Philistines had done to Saul’s corpse,
12 wapiganaji wote wakainuka na kwenda usiku wote na wakauondoa mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka ukuta wa Bethi Shani. Nao wakaenda Yabeshi na wakaichoma moto hiyo miili huko.
all their bravest soldiers walked all night to Beth-Shan. They took the corpses of Saul and his sons down from the city wall, and they took them back to Jabesh and burned the corpses there.
13 Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, na wakafunga siku saba.
They took the bones and buried them under a [big] tamarisk tree. Then they (fasted/abstained from eating food) for seven days.

< 1 Samweli 31 >