< 1 Samweli 3 >

1 Yule mtoto Samweli alimtumikia BWANA chini ya uangalizi wa Eli. Neno la BWANA halikupatikana kwa wingi siku hizo; hapakuwa na maono ya mara kwa mara ya kinabii.
Cependant, le jeune Samuel était employé au service du Seigneur devant Héli le prêtre; en ces jours-là, la parole du Seigneur était rare; il n'y avait plus de visions faisant connaître ses volontés.
2 Wakati huo, nguvu ya macho ya Eli ilikuwa imefifia kiasi cha kutoweza kuona vizuri, na alikuwa amelala kitandani mwake.
Et en ce temps-là, il advint qu'Héli dormait au lieu accoutumé; ses yeux commençaient à s'affaiblir; il n'y voyait plus.
3 Ile taa ya BWANA bado ilikuwa bado inawaka, na Samweli alikuwa amelala katika nyumba ya BWANA, palipokuwa na sanduku la Mungu.
C'était avant le moment où l'on visitait la lampe de Dieu, et Samuel dormait dans le sanctuaire auprès de l'arche de Dieu.
4 BWANA akamwita Samweli, naye akaitika, “Niko hapa”
Et le Seigneur appela Samuel, Samuel; et l'enfant dit: Me voici.
5 Samweli alimwedea Eli na kusema, “Niko hapa, sababu uliniita.” Eli akasema, “Sikukuita; kalale tena.” Hivyo Samweli akarudi na kulala.
Et il courut auprès d'Héli, et il lui dit: Me voici, puisque tu m'as appelé. Mais Héli répondit: Je ne t'ai point appelé, retourne-l'en et te rendors. Il s'en retourna donc, et il se rendormit.
6 BWANA akamwita tena, “Samweli.” Saamweli aliamka tena na kwenda kwa Eli na kusema, Niko hapa, sababu umeniita.” Eli akajibu, “Sijakuita, mwanangu; kalale tu tena.” 8
Le Seigneur recommença, il appela: Samuel, Samuel; l'enfant alla une seconde fois auprès d'Héli, et il dit: Me voici, puisque tu m'as appelé. Mais le prêtre lui répondit: Je ne t'ai point appelé, retourne-t'en et te rendors.
7 Basi Samweli bado hakuwa na uzoefu kuhusu Bwana, wala hakuwahi kupata ujumbe wowote kutoka kwa BWANA ukifunuliwa kwake.
Or, c'était avant que Samuel connût Dieu, et que la parole du Seigneur lui eût été révélée.
8 BWANA akamwita tena Samweli kwa mara ya tatu. Samweli alinyanyuka tena na kwenda kwa Eli na kusema, “Niko hapa, sababu uliniita,” Ndipo Eli alitambua kwamba BWANA alimwita kijana.
Le Seigneur, continuant, appela Samuel une troisième fois; l'enfant se leva, il alla auprès d'Héli, et il dit: Me voici, puisque tu m'as appelé. Le prêtre comprit alors que le Seigneur avait appelé l'enfant.
9 Kisha Eli aka, mwambia Samweli, “Nenda ukalale tena; ikiwa atakuita tena, sharti useme, 'Sema, BWANA, maana mtumwa wako anasikiliza.”' Hivyo Samweli akaenda na kulala mahali pake tena.
Il dit donc: Retourne-t'en, et rendors-toi, mon fils, et, si l'on t'appelle encore, tu diras: Parlez, votre serviteur vous écoute. Et Samuel s'en retourna, et il se recoucha au lieu accoutumé.
10 BWANA alikuja na kusimama; akaita vilevile kama vile mwanzoni, “Samweli, Samweli.” Ndipo Samweli akasema, “Nena, kwa sababu mtumwa wako anasikiliza.”
Le Seigneur vint, s'arrêta, et l'appela comme les autres fois, et Samuel dit: Parlez, votre serviteur vous écoute.
11 BWANA akasema na Samweli, “Tazama, Niko tayari kufanya jambo katika Israeli ambalo masikio ya kila mmoja akisikia atashtuka. -14
Et le Seigneur dit: Voilà que j'exécute ce que j'ai dit en Israël; quiconque l'ouïra, ses deux oreilles en tinteront.
12 Siku hiyo nitatimiza kila kitu nilichokisema dhidi ya Eli kuhusu nyumba yake, kutoka mwanzo hadi mwisho.
En ce jour-là, je susciterai contre Héli toutes les choses dont j'ai menacé sa famille; je commencerai et j'achèverai.
13 Nimemwambia kwamba niko tayari kuhukumu nyumba yake mara moja kwa ile dhambi aliyoifahamu, kwa sababu watoto wake walijiletea laana juu yao wenyewe na hakuwazuia.
Je lui ai annoncé que je punirais à perpétuité sa famille, à cause des iniquités de ses fils; car ses fils ont outragé Dieu, et il ne les a point réprimandés.
14 Hii ndiyo sababu nimeapa kwa nyumba ya Eli, kwamba dhambi za nyumba yake hazitasahehewa kwa dhabihu au kwa sadaka kamwe.” 16
Non, les choses ne peuvent aller ainsi: j'ai juré à la famille d'Héli que son iniquité ne pouvait être expiée ni par l'encens ni par les sacrifices à perpétuité.
15 Samweli akalala hadi asubuhi; baadaye alifungua milango ya nyumba ya BWANA. Lakini Samweli aliogopa kumwambia Eli kuhusu maono hayo.
Et Samuel resta couché jusqu'au matin; il se leva dès l'aurore, et il ouvrit les portes de la maison du Seigneur. Or, Samuel craignit de raconter sa vision.
16 Kisha Eli akamwita Samweli na kusema, “Samweli, mwanangu.” Samweli akasema, “Niko hapa.” 18
Et Héli dit à Samuel: Samuel, mon enfant. Et il répondit: Me voici.
17 Akamuuliza, “Ni neno gani alilokusemesha? Tafadhali usinifiche jambo hilo. Mungu akutendee hivyo na kukuzidishia, endapo utanificha kitu chochote kati ya yote ambayo amesema nawe.”
Puis, le prêtre reprit: Quelle est la parole qui t'a été dite? ne me cache rien; que le Seigneur te punisse, et qu'il te punisse encore, si tu me caches rien de ce qu'ont ouï tes oreilles.
18 Samweli akamweleza kila kitu; hakumficha jambo lolote. Eli akasema, “Ni BWANA. Na afanye linaloonekana jema kwake.”
Samuel lui répéta donc toutes les paroles du Seigneur, il ne lui cacha rien. Et le prêtre dit: C'est le Seigneur; il fera ce que bon lui semble.
19 Samweli akakua, na BWANA alikuwa pamoja naye na hakuacha kutimiza maneno yake ya unabii.
Et Samuel grandit et prospéra, car le Seigneur était avec lui; et pas une de ses paroles ne fut vaine.
20 Israeli yote tokea Dani hadi Beersheba walijua kwamba Samweli aliteuliwa kuwa nabii wa BWANA.
Et depuis Dan jusqu'à Bersabée, tout Israël sut que Samuel était un fidèle prophète du Seigneur.
21 Naye BWANA alionekana tena huko Shilo, maana alijifunua mwenyewe kwa Samweli huko Shilo kwa neno lake.
Le Seigneur continua de se montrer en Silo, parce que le Seigneur s'était révélé à Samuel. D'une extrémité à l'autre de la terre promise, tout Israël crut que Samuel était un prophète du Seigneur. Or, Héli était très avancé en âge; et ses fils marchaient dans leur voie, et leur voie était mauvaise devant le Seigneur.

< 1 Samweli 3 >