< 1 Samweli 28 >

1 Ikawa katika siku hizo Wafilisti walikusanya majeshi yao pamoja kwa ajili ya vita, wapigane na Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Ujue kwa hakika kwamba utakwenda nami ndani ya jeshi, wewe na watu wako.”
It came about in those days that the Philistines gathered their armies together for battle to fight with Israel. Achish said to David, “Know for certain that you will go out with me in the host, you and your men.”
2 Naye Daudi akamwambia Akishi, “Sasa utajua kile ambacho mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamwambia Daudi, “Basi sasa, nitakufanya uwe mlinzi wangu binafsi daima.”
David said to Achish, “So you will know what your servant can do.” Achish said to David, “So I will make you my bodyguard all your days.”
3 Samweli alikuwa amefariki; Waisraeli wote walimwomboleza na kumzika huko Rama, katika mji wake mwenyewe. Wakati huo Sauli alikuwa amewafukuza kutoka nchini wote walioongea na wafu au pepo.
Now Samuel had died, and all Israel had lamented him and buried him in Ramah, in his own city. Also, Saul had banned from the land those who talked with the dead or with spirits.
4 Wafilisti walijikusanya wao wenyewe wakaja na kuweka kambi huko Shunemu; na Sauli akawakusanya Israeli wote pamoja, na wakaweka kambi yao huko Gilboa.
Then the Philistines gathered themselves together and came and camped at Shunem; and Saul gathered all Israel together, and they camped at Gilboa.
5 Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, aliogopa na moyo wake ukatetemeka sana.
When Saul saw the army of the Philistines, he was afraid, and his heart trembled very much.
6 Sauli alipomuomba BWANA kwa ajili ya msaada, BWANA hakumjibu - si kwa ndoto wala kwa Urimu, wala kwa manabii.
Saul prayed to Yahweh for help, but Yahweh did not answer him—neither by dreams, nor by Urim, nor by prophets.
7 Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, “Mnitafutie mwanamke ambaye anaweza kuongea na wafu, ili ni mwendee na kutafuta msaada wake.” Watumishi wake wakamwambia, “Tazama, yupo mwanamke huko Endori awezaye kuongea na wafu.”
Then Saul said to his servants, “Find me a woman who talks with the dead, so that I may go to her and seek her advice.” His servants said to him, “See, there is a woman in Endor who claims to talk with the dead.”
8 Basi Sauli akajigeuza, akavaa nguo nyingine tofauti, akaondoka yeye pamoja na watu wawili; wakamwendea yule mwanamke wakati wa usiku. Akasema, “Nitabirie, nakuomba, kwa kuongea na wafu, na uniinulie yule nitakayekutajia.”
Saul disguised himself, put on other clothing, and went, he and two men with him; they went to the woman by night. He said, “Divine for me, I beg you, with a spirit, and bring me up whomever I name to you.”
9 Yule mwanamke akamwambia, “Tazama, unajua alichofanya Sauli, jinsi alivyowafukuza kutoka katika nchi wanaoongea na wafu au mizimu. Basi kwa nini mnatega mtego kwa ajili ya uhai wangu, ili kuniua?”
The woman said to him, “See, you know what Saul has done, how he has banned from the land those who talk with the dead or with spirits. So why are you setting a trap for my life, to make me die?”
10 Sauli akamwapia kwa BWANA na kusema, “Kama BWANA aishivyo, hakuna adhabu utakayopata kutokana na jambo hili.”
Saul swore to her by Yahweh and said, “As Yahweh lives, no punishment will happen to you for this thing.”
11 Kisha yule mwanamke akasema, “Je, nikuinulie nani?” Sauli akasema, “Niinulie Samweli.”
Then the woman said, “Whom should I bring up to you?” Saul said, “Bring up Samuel for me.”
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, akalia kwa sauti kuu na kusema na Sauli, akisema, “Kwa nini umenidanganya? Maana wewe ni Sauli.”
When the woman saw Samuel, she cried with a loud voice and spoke to Saul, saying, “Why have you deceived me? For you are Saul.”
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona kitu gani?” Yule mwanamke akamwambia Sauli, “Naona mungu akitoka katika nchi.” Akamuuliza mwanamke,
The king said to her, “Do not be afraid. What do you see?” The woman said to Saul, “I see a god coming up out of the earth.”
14 “Je, anafanana na nani?” Mwanamke akajibu, “Mtu mzee anazuka; naye amevaa kanzu.” Sauli akafahamu kuwa huyo ni Samweli, naye Sauli akainamisha uso wake hadi chini akionesha heshima.
He said to her, “What does he look like?” She said, “An old man is coming up; he is clothed with a robe.” Saul perceived that it was Samuel, and he bowed with his face to the ground and showed respect.
15 Samweli akamwambia Sauli, “Kwa nini umenisumbua na kuniinua juu?” Sauli akajibu, “Nimetaabika sana, maana Wafilisti wamepanga vita dhidi yangu, na Mungu ameniacha na hanipi majibu tena, si kwa manabii, wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita, ili unijulishe kile nitakachofanya.”
Samuel said to Saul, “Why have you disturbed me and brought me up?” Saul answered, “I am very distressed, for the Philistines are waging war against me, and God has left me and does not answer me any more, neither by prophets, nor by dreams. Therefore I have called you, that you may make known to me what I will do.”
16 Samweli akasema, “Kwa kuwa BWANA amekuacha, basi unaniuliza nini, naye amekuwa adui yako?
Samuel said, “What then do you ask me, since Yahweh has left you, and he has become your enemy?
17 BWANA amekutendea kile alichosema kuwa angekifanya. BWANA amerarua ufalme kutoka mkononi mwako na amempa ufalme mtu mwingine - amempa Daudi.
Yahweh has done to you what he said he would. Yahweh has torn the kingdom out of your hand and he has given it to someone else—to David.
18 Kwa sababu hukuitii sauti ya BWANA na hukutekeleza hasira yake kali juu ya Amaleki, kwa hiyo leo naye amefanya hili kwako.
Because you did not obey the voice of Yahweh and did not carry out his fierce wrath on Amalek, he has therefore done this today to you.
19 Zaidi ya hayo, BWANA atamweka Israeli pamoja na wewe katika mkono wa Wafilisti. Kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. BWANA pia ataliweka jeshi la Israeli katika mkono wa Wafilisti.”
Yahweh will give Israel along with you into the hand of the Philistines, and tomorrow you and your sons will be with me. Yahweh will also give the army of Israel into the hand of the Philistines.”
20 Ndipo ghafla Sauli alianguka chini kifudifudi na aliogopa kwa sababu ya yale maneno ya Samweli. Aliishiwa nguvu mwilini mwake, kwa kuwa siku hiyo alikuwa hajala chakula, hata kwa usiku huo wote.
Then Saul immediately fell his full length on the ground and was very afraid because of the words of Samuel. There was no strength in him, for he had eaten no food all that day, neither that whole night.
21 Ndipo yule mwanamke akaja kwa Sauli na akaona kwamba Sauli amepata shida, naye akamwambia, “Tazama, mjakazi wako ameisikiliza sauti yako; Nimeyaweka maisha yangu mkononi mwangu na nimeyasikiliza maneno uliyoniambia.
The woman came to Saul and saw that he was very troubled, She said to him, “See, your woman servant has listened to your voice; I have put my life in my hand and have listened to the words that you said to me.
22 Hivyo basi, nakusihi, sikiliza pia sauti ya mjakazi wako, na uniruhusu nilete chakula kidogo mbele yako. Ule ili upate nguvu za kwenda kule uendako.”
Now therefore, I beg you, listen also to the voice of your woman servant, and let me set a little food in front of you. Eat so that you may gain strength for when you go on your way.”
23 Lakini Sauli alikataa na kusema, “Sitakula.” Lakini watumishi wake, pamoja na yule mwanamke, wakamlazimisha hatimaye alisikiliza sauti zao. Hivyo aliinuka kutoka chini na kukaa kitandani.
But Saul refused and said, “I will not eat.” But his servants, together with the woman, compelled him, and he listened to their voice. So he rose from the ground and sat on the bed.
24 Yule mwanamke alikuwa na ndama mnono hapo nyumbani; akafanya haraka na kumchinja; akachua unga, akaukanda, na akatengeneza mikate isiyotiwa chachu kwa unga huo.
The woman had a fatted calf in the house; she hurried and killed it; she took flour, kneaded it, and baked unleavened bread with it.
25 Akaileta mbele ya Sauli na watumishi wake, nao wakala. Baaadaye waliinuka na kuondoka usiku huo.
She brought it before Saul and his servants, and they ate. Then they got up and left that night.

< 1 Samweli 28 >