< 1 Samweli 27 >
1 Daudi alisema moyoni mwake, “Basi, siku moja nitaangamia kwa mkono wa Sauli; hakuna jambo zuri kwangu kuliko kutoroka hadi nchi ya Wafilisti; Sauli atakata tamaa asinitafute tena ndani ya mipaka yote ya Israeli; kwa njia hii nitaponyoka kutoka mkono wake.”
And Dauid said in his heart, I shall now perish one day by the hand of Saul: is it not better for me that I saue my selfe in the lande of the Philistims, and that Saul may haue no hope of me to seeke me any more in all the coastes of Israel, and so escape out of his hand?
2 Daudi akaondoka na kuvuka, akiwa pamoja na watu mia sita hadi kwa Akishi mwana wa Maoki, mfalme wa Gathi.
Dauid therefore arose, and he, and the sixe hundreth men that were with him, went vnto Achish the sonne of Maoch King of Gath.
3 Daudi akaishi na Akishi huko Gathi pamoja na watu wake, na kila mtu na familia yake, na Daudi akiwa na wake zake wawili, Ahinoamu Myezreeli, na Abigaili Mkarmeli aliyekuwa mke wa Nabali.
And Dauid dwelt with Achish at Gath, he, and his men, euery man with his housholde, Dauid with his two wiues, Ahinoam the Izreelite, and Abigail Nabals wife the Carmelite.
4 Sauli akaambiwa kuwa Daudi amekimbilia Gathi, hivyo hakumtafuta tena.
And it was tolde Saul that Dauid was fled to Gath: so he sought no more for him.
5 Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, wanipatie mahali katika mojawapo ya miji ya nchi, ili nikae huko: kwa nini mtumishi wako akae pamoja na wewe katika mji wa kifalme?”
And Dauid saide vnto Achish, If I haue nowe founde peace in thine eyes, let them giue me a place in some other citie of the countrey, that I may dwell there: for why should thy seruant dwel in ye head citie of the kingdome with thee?
6 Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi Ziklagi; ndiyo sababu mji wa Ziklagi ni mali ya wafalme wa Yuda hadi leo.
Then Achish gaue him Ziklag that same day: therefore Ziklag pertaineth vnto the kings of Iudah vnto this day.
7 Idadi ya siku ambazo Daudi aliishi katika nchi ya Wafilisti ulikuwa mwaka mmoja na miezi minne.
And the time that Dauid dwelt in the countrey of the Philistims, was foure moneths and certaine dayes.
8 Daudi na watu wake walizipiga sehemu mbalimbali, wakiteka nyara Wageshuri, Wagirizi, na Waamaleki; kwa maana mataifa hayo ndio walikuwa wakaaji wa nchi, kwa uelekeo wa kwenda Shuri hadi kufika nchi ya Misri. Walikuwa wamekaa katika nchi hiyo toka nyakati za zamani.
Then Dauid and his men went vp, and inuaded the Geshurites, and the Girzites, and the Amalekites: for they inhabited the lande from the beginning, from the way, as thou goest to Shur, euen vnto the lande of Egypt.
9 Daudi aliipiga nchi na hakumwacha mwanaume wala mwanamke akiwa hai; akatwaa kondoo, ng'ombe, punda, ngamia, na nguo; kisha alirudi na kufika tena kwa Akishi.
And Dauid smote the lande, and left neither man nor woman aliue, and tooke sheepe, and oxen, and asses, and camels, and apparell, and returned and came to Achish.
10 Ndipo Akishi humuuliza, “Je, leo umefanya mashambulizi dhidi ya nani?” Daudi humjibu, “Nimefanya dhidi ya kusini mwa Yuda,” au dhidi ya kusini mwa Wayerameeli,” au “dhidi ya kusini mwa Wakeni.”
And Achish said, Where haue ye bene a rouing this day? And Dauid answered, Against the South of Iudah, and against the South of the Ierahmeelites, and against the South of ye Kenites.
11 Daudi asingemwacha mwanaume wala mwanamke akiwa hai awalete hadi Gathi, akisema, “ili wasije kututeta, 'Daudi amefanya hivi na vile.”' Hivi ndivyo alivyofanya kwa kipindi chote alichokaa katika nchi ya Wafilisti.
And Dauid saued neither man nor woman aliue, to bring them to Gath, saying, Lest they should tel on vs, and say, So did Dauid, and so will be his maner all the while that he dwelleth in the countrey of the Philistims.
12 Akishi alimwamini Daudi, akisema, “Amesababisha watu wake Israeli wamchukie kabisa; kwa hiyo atakuwa mtumishi wangu milele.”
And Achish beleeued Dauid, saying, He hath made his people of Israel vtterly to abhorre him: therefore he shalbe my seruant for euer.