< 1 Samweli 27 >

1 Daudi alisema moyoni mwake, “Basi, siku moja nitaangamia kwa mkono wa Sauli; hakuna jambo zuri kwangu kuliko kutoroka hadi nchi ya Wafilisti; Sauli atakata tamaa asinitafute tena ndani ya mipaka yote ya Israeli; kwa njia hii nitaponyoka kutoka mkono wake.”
Men David sagde til sig selv: »Jeg falder dog en skønne Dag for Sauls Haand. Jeg har ingen anden udvej end at søge Tilflugt i Filisternes Land; saa opgiver Saul at søge efter mig nogetsteds i Israels Land, og jeg er uden for hans Rækkevidde!«
2 Daudi akaondoka na kuvuka, akiwa pamoja na watu mia sita hadi kwa Akishi mwana wa Maoki, mfalme wa Gathi.
David brød da op og drog med sine 600 Mænd over til Maoks Søn, Kong Akisj af Gat;
3 Daudi akaishi na Akishi huko Gathi pamoja na watu wake, na kila mtu na familia yake, na Daudi akiwa na wake zake wawili, Ahinoamu Myezreeli, na Abigaili Mkarmeli aliyekuwa mke wa Nabali.
og David boede hos Akisj i Gat tillige med sine Mænd, som havde deres Familier med, ligesom David havde sine to Hustruer med, Ahinoam fra Jizre'el og Abigajil, Karmeliten Nabals Hustru.
4 Sauli akaambiwa kuwa Daudi amekimbilia Gathi, hivyo hakumtafuta tena.
Da Saul fik at vide, at David var flygtet til Gat, holdt han op at søge efter ham.
5 Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, wanipatie mahali katika mojawapo ya miji ya nchi, ili nikae huko: kwa nini mtumishi wako akae pamoja na wewe katika mji wa kifalme?”
Men David sagde til Akisj: »Hvis jeg har fundet Naade for dine Øjne, lad mig saa faa et Sted at bo i en af Byerne ude i Landet, thi hvorfor skal din Træl bo hos dig i Hovedstaden?«
6 Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi Ziklagi; ndiyo sababu mji wa Ziklagi ni mali ya wafalme wa Yuda hadi leo.
Akisj lod ham da med det samme faa Ziklag; og derfor tilhører Ziklag endnu den Dag i Dag Judas Konger.
7 Idadi ya siku ambazo Daudi aliishi katika nchi ya Wafilisti ulikuwa mwaka mmoja na miezi minne.
Den Tid, David boede i Filisternes Land, udgjorde et Aar og fire Maaneder.
8 Daudi na watu wake walizipiga sehemu mbalimbali, wakiteka nyara Wageshuri, Wagirizi, na Waamaleki; kwa maana mataifa hayo ndio walikuwa wakaaji wa nchi, kwa uelekeo wa kwenda Shuri hadi kufika nchi ya Misri. Walikuwa wamekaa katika nchi hiyo toka nyakati za zamani.
Og David og hans Mænd drog op og plyndrede hos Gesjuriterne, Gizriterne og Amalekiterne; thi de boede i Landet fra Telam hen imod Sjur og hen til Ægypten;
9 Daudi aliipiga nchi na hakumwacha mwanaume wala mwanamke akiwa hai; akatwaa kondoo, ng'ombe, punda, ngamia, na nguo; kisha alirudi na kufika tena kwa Akishi.
og naar David plyndrede Landet, lod han hverken Mænd eller Kvinder blive i Live, men Smaakvæg, Hornkvæg, Æsler, Kameler og Klæder tog han med; naar han saa vendte tilbage og kom til Akisj,
10 Ndipo Akishi humuuliza, “Je, leo umefanya mashambulizi dhidi ya nani?” Daudi humjibu, “Nimefanya dhidi ya kusini mwa Yuda,” au dhidi ya kusini mwa Wayerameeli,” au “dhidi ya kusini mwa Wakeni.”
og han spurgte: »Hvor hærgede I denne Gang?« svarede David: »Idet judæiske Sydland!« eller: »I det jerame'elitiske Sydland!« eller: »I det kenitiske Sydland!«
11 Daudi asingemwacha mwanaume wala mwanamke akiwa hai awalete hadi Gathi, akisema, “ili wasije kututeta, 'Daudi amefanya hivi na vile.”' Hivi ndivyo alivyofanya kwa kipindi chote alichokaa katika nchi ya Wafilisti.
David lod ingen Mand eller Kvinde blive i Live for ikke at maatte tage dem med til Gat; thi han tænkte: »De kunde røbe os og sige: Det og det har David gjort!« Saaledes bar han sig ad, al den Tid han opholdt sig i Filisternes Land.
12 Akishi alimwamini Daudi, akisema, “Amesababisha watu wake Israeli wamchukie kabisa; kwa hiyo atakuwa mtumishi wangu milele.”
Derfor fik Akisj Tillid til David, idet han tænkte: »Han har gjort sig grundig forhadt hos sit Folk Israel; han vil tjene mig for stedse!«

< 1 Samweli 27 >