< 1 Samweli 26 >

1 Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi akujificha katika vilima vya Hakila, ambavyo viko mbele ya jangwa?”
The Ziphites came to Saul at Gibeah and said, “Is not David hiding in the hill of Hakilah, which is before Jeshimon?”
2 Kisha Sauli akaamka na kwenda chini ya jangwa la Zifu, akiwa na watu elfu tatu waliochaguliwa katika Israeli, wamtafute Daudi katika jangwa la Zifu.
Then Saul arose and went down to the wilderness of Ziph, having three thousand chosen men of Israel with him, to seek David in the wilderness of Ziph.
3 Sauli akaweka kambi kwenye kilima cha Hakila, kilicho mbele ya jangwa, kando ya barabara. Lakini Daudi alikuwa akikaa nyikani, na akaona kwamba Sauli alikuwa anamfuatia huko jangwani.
Saul camped on the hill of Hakilah, which is before Jeshimon, by the road. But David was staying in the wilderness, and he saw that Saul was coming after him into the wilderness.
4 Hivyo Daudi akawatuma wapelelezi na akafahamu kwamba hakika Sauli alikuwa amekuja.
So David sent out spies and learned that Saul had indeed come.
5 Daudi akaamka na kwenda hadi mahali ambapo Sauli alipiga kambi; akaona mahali alipolala Sauli, na Abneri mwana wa Neri, mkuu wa jeshi lake; Sauli alilala katikati ya kambi, na watu walipiga kambi kumzunguka, na wote wamesinzia.
David arose and went to the place where Saul had camped; he saw the place where Saul lay, and Abner son of Ner, the general of his army; Saul lay in the camp, and the people were camped around him, all asleep.
6 Ndipo Daudi akamwambia Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, ndugu yake Yoabu, “Ni nani atakwenda nami kambini kwa Sauli? Abishai akasema, “Mimi nitashuka pamoja nawe.”
Then David said to Ahimelech the Hittite, and to Abishai son of Zeruiah, the brother of Joab, “Who will go down with me to Saul in the camp?” Abishai said, “I! I will go down with you.”
7 Hivyo Daudi na Abishai wakaliendea jeshi usiku. Na Sauli alikuwapo akisinzia ndani ya kambi, mkuki wake umechomekwa chini pembeni mwa kichwa chake. Abneri na Askari wake wamelala kwa kumzunguka.
So David and Abishai went to the army by night. Saul was there sleeping inside the camp with his spear stuck in the ground beside his head. Abner and his soldiers lay around him.
8 Kisha Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemweka adui yako mkononi mwako. Basi tafadhali acha nimchome mkuki nimtoboe hadi chini kwa pigo moja. Sitampiga mara mbili.”
Then Abishai said to David, “Today God has put your enemy into your hand. Now please let me pin him to the ground with the spear with just one blow. I will not strike him a second time.”
9 Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize; kwa maana nani awezaye kunyoosha mkono wake dhidi ya mtiwa mafuta wa BWANA na asiwe na hatia?”
David said to Abishai, “Do not destroy him; for who can extend his hand against Yahweh's anointed one and be guiltless?”
10 Daudi akasema, “Kama BWANA aishivyo, BWANA atamuua, au siku ya kufa kwake itakuja, au atakwenda katika vita na ataangamia.
David said, “As Yahweh lives, Yahweh will kill him, or his day will come to die, or he will go into battle and perish.
11 BWANA apishe mbali nisinyooshe mkono wangu dhidi ya mtiwa mafuta wake; lakini sasa, nakusihi chukua mkuki uliokichwani pake na jagi la maji, tuondoke.”
May Yahweh forbid that I should extend my hand against his anointed one; but now, I beg you, take the spear that is at his head and the jar of water, and let us go.”
12 Hivyo Daudi akachukua mkuki na jagi la maji kutoka kichwani pa Daudi, wakatoweka. Hakuna mtu aliyewaona au kufahamu habari hii, wala hakuna aliyetoka usingizini, maana wote walisinzia, kwa sababu usingizi mzito kutoka kwa BWANA uliwaangukia.
So David took the spear and the jar of water from Saul's head, and they got away. No one saw them or knew about it, nor did anyone wake up, for they were all asleep, because a deep sleep from Yahweh had fallen on them.
13 Kisha Daudi akaenda upande mwingine na akasimama juu ya mlima mbali sana; ukiwepo umbali mkubwa katikati yao.
Then David went over to the other side and stood on the top of the mountain far off; a great distance was between them.
14 Daudi akawapigia kelele watu hao na Abneri mwana Neri; akisema, “Hujibu neno, Abneri?” Ndipo Abneri akajibu na kusema, “Wewe ni nani unayempigia mfalme kelele?”
David shouted out to the people and to Abner son of Ner; he said, “Do you not answer, Abner?” Then Abner answered and said, “Who are you who is shouting to the king?”
15 Daudi akamwambia Abneri, “Wewe siye mtu jasiri? Ni nani yuko kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukukaa macho kumlinda bwana wako mfalme? Kwa maana mtu fulani aliingia kumuua mfalme, bwana wako.
David said to Abner, “Are not you a courageous man? Who is like you in Israel? Why then have you not kept watch over your master the king? For someone came in to kill the king your master.
16 Jambo hili ulilolifanya siyo zuri. Kama BWANA aishivyo, unapaswa kufa kwa sababu hukumlinda bwana wako, mtiwa mafuta wa BWANA. Na sasa tazama ulipo mkuki wa mfalme, na jagi la maji lililokuwa kichwani pake.”
This thing you have done is not good. As Yahweh lives, you deserve to die because you have not kept watch over your master, Yahweh's anointed one. Now see where the king's spear is and the jar of water that was near his head!”
17 Sauli aliitambua sauti ya Daudi akasema, “Hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Daudi akasema, “Ni sauti yangu, mfalme, bwana wangu.”
Saul recognized David's voice and said, “Is that your voice, my son David?” David said, “It is my voice, my master, king.”
18 Daudi akasema, “Kwa nini bwana wangu anamwandama mtumishi wake? Nimefanya nini? Mkononi mwangu kuna uovu gani?
He said, “Why does my master pursue his servant? What have I done? What evil is in my hand?
19 Kwa hiyo sasa, nakusihi, bwana wangu mfalme asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama ni BWANA ndiye amekuchochea dhidi yangu, na aikubali sadaka; lakini kama ni wanadamu, na walaaniwe mbele za BWANA, maana leo wamenifukuza, nisishikamane na urithi wa BWANA; wameniambia, 'Nenda ukaabudu miungu mingine.'
Now therefore, I beg you, let my master the king listen to the words of his servant. If it is Yahweh who has stirred you up against me, let him accept an offering; but if it is human beings, may they be cursed in the sight of Yahweh, for they have today driven me out, that I should not cling to the inheritance of Yahweh; they have said to me, 'Go worship other gods.'
20 Kwa hiyo, sasa, usiiachilie damu yangu ianguke ardhini mbali na uwepo wa BWANA; kwa kuwa mfalme wa Israeli ametoka nje kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware milimani.”
Now therefore, do not let my blood fall to the earth away from Yahweh's presence; for the king of Israel has come out to look for the one flea as when one hunts a partridge in the mountains.”
21 Kisha Sauli akasema, “Nimefanya dhambi. Rudi, Mwanangu, Daudi; maana sitakudhuru tena, kwa sababu leo maisha yangu yalikuwa yenye thamani machoni pako. Tazama, nimetenda upumbavu na nimekosa sana.”
Then Saul said, “I have sinned. Return, David, my son; for I will harm you no more, because my life was precious in your eyes today. See, I have played the fool and have made a very bad mistake.”
22 Daudi akajibu na akasema, “Tazama, mkuki wako uko hapa, mfalme! Mruhusu kijana mmojawapo aje auchukue na aulete kwako.
David answered and said, “See, your spear is here, king! Let one of the young men come over and get it and bring it to you.
23 Na BWANA amlipe kila mtu kwa ajili ya uadilifu wake na kwa uaminifu wake; kwa sababu leo BWANA alikuweka mkononi mwangu, lakini nisinge mpiga mtiwa mafuta wake.
May Yahweh pay each man for his righteousness and his faithfulness; because Yahweh put you into my hand today, but I would not strike his anointed.
24 Na tazama, kama maisha yako leo yalivyokuwa ya thamani machoni pangu, vivyo hivyo maisha yangu yathaminiwe sana machoni pa BWANA, na aweze kuniokoa katika shida zote.”
See, as your life was precious in my eyes today, so may my life be much valued in the eyes of Yahweh, and may he rescue me out of all trouble.”
25 Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Na ubarikiwe, mwanangu Daudi, ili uweze kutenda mambo makuu, na hakika uweze kufanikiwa.” Ndipo Daudi akaenda zake, na Sauli akarudi kwake.
Then Saul said to David, “May you be blessed, David my son! You will certainly do great things and you will succeed in them.” So David went his way, and Saul returned to his place.

< 1 Samweli 26 >