< 1 Samweli 25 >

1 Basi Samweli akafariki. Waisraeli wote wakakusanyika pamoja na kumwomboleza, na wakamzika nyumbani kwake huko Rama. Kisha Daudi akainuka na akashuka hadi jangwa la Parani.
Samuel mourut. Tout Israël se rassembla, prit le deuil et l'enterra dans sa maison à Rama. David se leva et descendit dans le désert de Paran.
2 Kulikuwa na mtu mmoja huko Maoni, na mali zake zilikuwa huko Karmali. Mtu huyo alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja. Naye alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake huko Karmeli.
Il y avait à Maon un homme dont les biens étaient au Carmel, et cet homme était très grand. Il avait trois mille brebis et mille chèvres, et il tondait ses brebis au Carmel.
3 Na mtu huyo aliitwa Nabali, na jina la mke wake aliitwa Abigaili. Mwanamke huyo alikuwa mwenye busara na mzuri kwa sura. Lakini mwanaume alikwa mkaidi na mwovu katika mambo yake. Alikuwa wa uzao wa nyumba ya Kalebu.
Or le nom de cet homme était Nabal, et le nom de sa femme Abigaïl. Cette femme était intelligente et avait un beau visage; mais l'homme était hargneux et méchant dans ses actions. Il était de la maison de Caleb.
4 Daudi akasikia akiwa jangwani kwamba Nabali alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake.
David apprit dans le désert que Nabal tondait ses brebis.
5 Hivyo Daudi aliwatuma kwake vijana kumi. Akawaambia wale vijana, “Pandeni kwanda Karmeli, mwendeeni Nabali, na mkamsalimie kwa jina langu.
David envoya dix jeunes gens. Il leur dit: « Montez au Carmel, allez vers Nabal, et saluez-le en mon nom.
6 Mtamwambia, 'Uishi katika baraka, Uwe na amani na nyumba yako iwe na amani, na wote ulionao wawe na amani.
Dites-lui: « Longue vie à toi! Que la paix soit avec toi! Que la paix soit avec ta maison! Que la paix soit avec tout ce qui t'appartient!
7 Nasikia kwamba unao wakata manyoya. Wachungaji wako walikuwa pamoja nasi, na hatukuwafanyia ubaya, na muda wote wakiwa Karmeli hawakupotelewa kitu chochote.
J'ai appris que tu as des tondeurs. Vos bergers ont maintenant été avec nous, et nous ne leur avons fait aucun mal. Rien n'a manqué d'eux pendant tout le temps qu'ils ont été au Carmel.
8 Waulize vijana wako, nao watakuambia. Basi vijana wangu wapate kibali machoni pako, maana tumefika siku ya sherehe. Tafadhali utoe cho chote ulicho nacho mkononi kwa watumishi wako na kwa Daudi mwanao.'”
Interrogez vos jeunes gens, et ils vous le diront. Que les jeunes gens trouvent grâce à tes yeux, car nous venons en un jour favorable. Donne, je te prie, tout ce qui te tombe sous la main à tes serviteurs et à ton fils David.'"
9 Vijana wa Daudi walipofika, walimwambia Nabali yote haya kwa niaba ya Daudi na kisha wakasubiri.
Lorsque les jeunes gens de David arrivèrent, ils dirent à Nabal toutes ces paroles au nom de David, et ils attendirent.
10 Nabali akawajibu watumishi wa Daudi, “Daudi ni nani? Na ni nani mwana wa Yese? Siku hizi wapo watumishi wengi wanaotoroka bwana zao.
Nabal répondit aux serviteurs de David et dit: « Qui est David? Qui est le fils de Jessé? Il y a beaucoup de serviteurs qui se séparent de leurs maîtres ces jours-ci.
11 Je, nichukue mkate wangu na maji yangu na nyama yangu ambayo nimewachinjia wakata manyoya wangu, na niwape watu wanaotoka nisikokujua?”
Dois-je donc prendre mon pain, mon eau et la viande que j'ai tuée pour mes tondeurs, et les donner à des hommes dont j'ignore l'origine? ».
12 Hivyo vijana wa Daudi waligeuka na kurudi, nakumwambia kila kitu kilichosemwa.
Et les jeunes gens de David s'en retournèrent sur leur chemin, et vinrent lui rapporter toutes ces paroles.
13 Daudi akawaambia watu wake, “Kila mtu ajifunge upanga wake.” Kila mtu akajifunga upanga wake. Daudi naye pia akajifunga upanga wake. Yapata kama watu mia nne wakafuatana na Daudi, na wengine mia mbili walibaki kulinda mizigo yao.
David dit à ses hommes: « Que chacun mette son épée! » Chaque homme a mis son épée. David mit aussi son épée. Environ quatre cents hommes suivirent David, et deux cents restèrent près des bagages.
14 Lakini kijana mmojawapo alimwambia Abigaili, mke wa Nabali akasema, “Daudi aliwatuma wajumbe kutoka jangwani waje wamsalimu bwana wetu, na yeye akawatukana.
Mais l'un des jeunes gens dit à Abigaïl, la femme de Nabal: « Voici, David a envoyé des messagers du désert pour saluer notre maître, et il les a insultés.
15 Bado watu hawa walitutendea mema. Hatukudhurika na hatukupoteza chochote wakati wote tulipotembea nao tulipokuwa mbugani.
Mais ces hommes ont été très bons avec nous, et nous n'avons pas été blessés, et nous n'avons rien manqué tant que nous avons été avec eux, quand nous étions dans les champs.
16 Walikuwa ukuta wetu usiku na mchana, wakati wote tulikuwa pamoja nao tukichunga kondoo.
Ils étaient pour nous une muraille, de nuit comme de jour, pendant tout le temps que nous étions avec eux à garder les brebis.
17 Kwa hiyo tambua hili na zingatia utafanya nini, maana ubaya unamvizia bwana wetu, na utakuwa juu ya nyumba yake yote. Yeye ni mtu asiyefaa na hakuna awezaye kushauriana naye.”
Maintenant donc, sachez et réfléchissez à ce que vous ferez, car le mal est décidé contre notre maître et contre toute sa maison, car il est si inutile qu'on ne peut pas lui parler. »
18 Ndipo Abigaili akaharakisha na akachukuwa mikate mia mbili, chupa mbili za divai, kondoo watano waliokwisha andaliwa, vipimo vitano vya bisi, vishada mia moja vya zabibu, na mikate mia mbili ya tini na akavipakia juu ya punda.
Alors Abigaïl se hâta de prendre deux cents pains, deux récipients de vin, cinq moutons apprêtés, cinq seahs de grains secs, cent grappes de raisins secs et deux cents gâteaux de figues, et les fit monter sur des ânes.
19 Akamwambia kijana wake, “Tangulia mbele yangu, nami nitakuja nyuma yako.” Lakini hakumwambia mmewe Nabali.
Elle dit à ses jeunes gens: « Passez devant moi. Voici que je viens après vous. » Mais elle ne le dit pas à son mari, Nabal.
20 Alipokuwa akienda juu ya punda wake na kutelemka penye kificho cha mlima, Daudi na watu wake walishuka chini wakimwelekea Abigaili, naye akakutana nao.
Comme elle montait sur son âne et descendait cachée par la montagne, voici que David et ses hommes descendaient vers elle, et elle les rencontra.
21 Basi Daudi alikuwa amesema, “Hakika nimelinda bure vyote alivyonavyo mtu huyu huko nyikani, na vyote alivyonavyo hakuna kilichopotea, pamoja na hayo amenilipa mabaya badala ya mema.
Or David avait dit: « C'est en vain que j'ai gardé tout ce que cet homme a dans le désert, de sorte que rien n'a manqué de tout ce qui lui appartenait. Il m'a rendu le mal pour le bien.
22 Mungu na anitendee hivyo mimi, Daudi, pia iwe zaidi, iwapo nitamwacha hata mtu mmoja wa kwake akiwa hai ifikapo kesho asubuhi.
Que Dieu fasse ainsi aux ennemis de David, et plus encore, si je laisse de tout ce qui lui appartient à la lumière du matin autant que quelqu'un qui urine sur un mur. »
23 Abigaili alipomwona Daudi, aliharakisha na kushuka chini ya punda wake, akalala kifudifudi na kujiinamisha hadi chini.
Lorsqu'Abigaïl vit David, elle se précipita, descendit de son âne, tomba devant David sur sa face et se prosterna à terre.
24 Akamwangukia miguuni pake na kusema, “Juu yangu tu, bwana wangu, na uwe uovu. Tafadhali acha mjakazi wako aseme nawe, tena uyasikilize maneno ya mjakazi wako.
Elle tomba à ses pieds et dit: « C'est à moi, mon seigneur, que revient la faute! Laisse ton serviteur parler à tes oreilles. Écoute les paroles de ta servante.
25 Nakusihi bwana wangu usimjali mtu huyu asiyefaa, Nabali, kwa maana kama jina lake lilivyo, ndivyo alivyo. Jina lake ni Nabali, na upumbavu uko pamoja naye. Lakini mimi mjakazi wako sikuwaona vijana wa bwana wangu, uliowatuma.
Ne permets pas à mon seigneur d'être attentif à ce bon à rien de Nabal, car il est comme son nom. Nabal est son nom, et la folie est avec lui; mais moi, ton serviteur, je n'ai pas vu les jeunes gens de mon seigneur que tu as envoyés.
26 Sasa basi, bwana wangu, kama BWANA aishivyo, na kama unavyoishi, kwa kuwa BWANA amekuondoa kutoka kumwaga damu, na kuacha kulipiza kisasi kwa mkono mwenyewe, basi adui zako, na wale ambao wanatafuta kumfanyia uovu bwana wangu, wawe kama Nabali
Maintenant, mon seigneur, comme l'Éternel est vivant et comme ton âme est vivante, puisque l'Éternel t'a empêché de te rendre coupable par le sang et de te venger de ta propre main, maintenant, que tes ennemis et ceux qui cherchent à nuire à mon seigneur soient comme Nabal.
27 Na sasa zawadi hii ambayo mjakazi wako ameileta kwa bwana wangu, na wapewe vijana ambao wanamfuata bwana wangu.
Maintenant, ce présent que ton serviteur a apporté à mon seigneur, qu'il soit donné aux jeunes gens qui suivent mon seigneur.
28 Tafadhali ulisamehe kosa la mjakazi wako, maana BWANA hakika atamfanyia bwana wangu nyumba imara, kwa sababu bwana wangu anapigana vita vya BWANA; na uovu hautaonekana ndani yako maadamu unaishi.
Je te prie de pardonner la faute de ton serviteur. Car l'Éternel fera de mon seigneur une maison sûre, parce que mon seigneur mène les combats de l'Éternel. Le mal ne se trouvera pas chez toi tous tes jours.
29 Na ingawa watu wangeinuka na kukuandama ili wakuue, bado uhai wa bwana wangu utafungwa katika furushi la walio hai na BWANA Mungu wako; na atayatupa maisha ya adui zako mbali, kama vile kutoka katika mfuko wa kombeo.
Si des hommes se lèvent pour te poursuivre et chercher ton âme, l'âme de mon seigneur sera liée dans le faisceau de vie de Yahvé ton Dieu. Il fera sortir les âmes de tes ennemis comme de la poche d'une fronde.
30 Na itakuwa, BWANA atakapokuwa amemtimizia bwana wangu mambo yote mazuri ambayo amekuahidi, na alivyokufanya kiongozi juu ya Israeli,
Lorsque l'Éternel aura fait à mon seigneur tout le bien qu'il a dit de toi et qu'il t'aura établi chef d'Israël,
31 jambo hili halitakuwa huzuni kwako, wala chukizo moyoni kwa bwana wangu, kwa sababu hukumwaga damu bila sababu, na hujajilipizia kisasi. Na BWANA akikuletea mafanikio, umkumbuke mjakazi wako.”
tu ne seras pas affligé, et mon seigneur ne sera pas offensé, soit que tu aies versé du sang sans raison, soit que mon seigneur se soit vengé. Quand Yahvé aura fait du bien à mon seigneur, souviens-toi de ton serviteur. »
32 Ndipo Daudi akamwambia Abigaili, “BWANA, Mungu wa Israeli, abarikiwe, aliyekutuma uonane na mimi leo.
David dit à Abigaïl: « Béni soit Yahvé, le Dieu d'Israël, qui t'a envoyée aujourd'hui à ma rencontre!
33 Na hekima yako ibarikiwe, nawe umebarikiwa, kwa sababu leo umenizuia nisiwe na hatia ya kumwaga damu, na kutojilipizia kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.
Béni soit ta discrétion, et bénie sois-tu, qui m'a empêché aujourd'hui de me rendre coupable de sang, et de me venger de ma propre main.
34 Kwa kweli, kama BWANA, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye amenizuia nisikuumize, kama usinge harakisha kuja ukutane nami, kwa hakika kesho asubuhi asinge salia hata mtoto mmoja wa kiume kwa Nabali.”
En effet, comme vit Yahvé, le Dieu d'Israël, qui m'a empêché de te faire du mal, si tu ne t'étais pas empressé de venir à ma rencontre, il ne serait pas resté à Nabal, à la lumière du matin, plus qu'un homme qui urine sur un mur. »
35 Kwa hiyo Daudi akavipokea kutoka mkononi mwake vile alivyokuwa amemletea; akamwambia, “Nenda kwa amani hadi nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako na nimekubali.”
Et David reçut de sa main ce qu'elle lui avait apporté. Puis il lui dit: « Monte en paix dans ta maison. Voici que j'ai écouté ta voix et que j'ai exaucé ta demande. »
36 Abigaili akarudi kwa Nabali; tazama, alikuwa akifanya sherehe katika mji wake, kama sherehe ya mfalme; na moyo wa Nabali ulifurahi ndani yake, kwa sababu alikwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia chochote kabisa hadi kulipopambazuka
Abigaïl se rendit auprès de Nabal; et voici qu'il donnait dans sa maison un festin comme celui d'un roi. Le cœur de Nabal était joyeux au-dedans de lui, car il était très ivre. Aussi ne lui dit-elle rien jusqu'à la lumière du matin.
37 Ikawa asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, basi mkewe akamwambia mambo hayo; moyo wake ukafa ndani yake, na akawa kama jiwe.
Le matin, quand le vin eut disparu de Nabal, sa femme lui raconta ces choses; son cœur mourut au dedans de lui, et il devint comme une pierre.
38 Ikawa baada ya siku kumi BWANA alimpiga Nabali naye akafa.
Environ dix jours plus tard, l'Éternel frappa Nabal, de sorte qu'il mourut.
39 Naye Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, akasema, “BWANA abarikiwe, aliyenichukulia hatua ya shutuma yangu kutoka mkono wa Nabali, na kumzuia mtumishi wake asifanye maovu. Na amemrudishia Nabali tendo la uovu juu ya kichwa chake mwenyewe.” Ndipo Daudi akawatuma watu wakaongee na Abigaili, ili amchukue awe mke wake.
Lorsque David apprit que Nabal était mort, il dit: « Béni soit Yahvé, qui a défendu ma cause de la main de Nabal et qui a préservé son serviteur du mal. Yahvé a fait retomber la méchanceté de Nabal sur sa propre tête. » David envoya et parla au sujet d'Abigaïl, pour la prendre pour femme.
40 Watumishi wake Daudi walipofika kwa Abigaili huko Karmeli, wakaongea naye na kusema, “Daudi ametutuma kwako tukuchukue hadi kwake uwe mke wake.”
Lorsque les serviteurs de David furent arrivés auprès d'Abigaïl au Carmel, ils lui parlèrent ainsi: « David nous a envoyés vers toi, pour te prendre pour femme. »
41 Abigaili aliinuka, akainamisha uso chini, na akasema, “Tazama, mjakazi wako ni mtumwa aoshaye miguu ya watumishi wa bwana wangu.”
Elle se leva, se prosterna, le visage contre terre, et dit: « Voici que ta servante est une servante pour laver les pieds des serviteurs de mon seigneur. »
42 Akaharakisha na kuamka, akapanda punda akiwa na vijakazi wake watano waliofuatana naye; akawafuata wajumbe wa Daudi, na akawa mke wake.
Abigaïl se leva précipitamment et monta sur un âne avec ses cinq servantes qui la suivaient; elle suivit les messagers de David et devint sa femme.
43 Daudi pia alimchukua Ahinoamu wa Yezreeli akamwoa; wote wawili wakawa wake zake.
David prit aussi Ahinoam, de Jizreel, et toutes deux devinrent ses femmes.
44 Wakati huo Sauli alikuwa amempa Palti, mwana wa Laishi mtu wa Galimu, Mikali, binti yake, aliyekuwa mke wa Daudi.
Or Saül avait donné Mical, sa fille, la femme de David, à Palti, fils de Laïsh, qui était de Gallim.

< 1 Samweli 25 >