< 1 Samweli 25 >

1 Basi Samweli akafariki. Waisraeli wote wakakusanyika pamoja na kumwomboleza, na wakamzika nyumbani kwake huko Rama. Kisha Daudi akainuka na akashuka hadi jangwa la Parani.
Hathnukkhu, Samuel a due navah, Isarelnaw pueng teh a khuika awh. Ahni teh Ramah kho a onae im koe a pakawp awh. Devit teh Paran kahrawngum lah a cei.
2 Kulikuwa na mtu mmoja huko Maoni, na mali zake zilikuwa huko Karmali. Mtu huyo alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja. Naye alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake huko Karmeli.
Maon vah tami buet touh ao. Hote tami teh, Karmel kho dawk ka tawnta poung e lah ao teh tu 3000 touh hoi hmae 1000 touh a tawn. Karmel vah tumuen ouk a ngaw.
3 Na mtu huyo aliitwa Nabali, na jina la mke wake aliitwa Abigaili. Mwanamke huyo alikuwa mwenye busara na mzuri kwa sura. Lakini mwanaume alikwa mkaidi na mwovu katika mambo yake. Alikuwa wa uzao wa nyumba ya Kalebu.
Hote tami min teh Nabal doeh. A yu e min teh Abigail. Hote e napui teh, a lungkaang e hoi a meikahawi e lah ao. Hatei a vâ teh, a lung ka patak e hoi a nuen kamathout e lah ao. Ahni teh Kaleb catounnaw doeh.
4 Daudi akasikia akiwa jangwani kwamba Nabali alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake.
Devit ni kahrawngum hoi Nabal ni tumuen a ngaw e hah a panue.
5 Hivyo Daudi aliwatuma kwake vijana kumi. Akawaambia wale vijana, “Pandeni kwanda Karmeli, mwendeeni Nabali, na mkamsalimie kwa jina langu.
Hatdawkvah, Devit ni thoundounnaw 10 touh a patoun teh, hatnavah thoundounaw hah Devit ni Karmel lah takhang awh nateh, Nabal koe na cei awh vaiteh, ka min lahoi kut man awh.
6 Mtamwambia, 'Uishi katika baraka, Uwe na amani na nyumba yako iwe na amani, na wote ulionao wawe na amani.
Hahoi, ka tawnta poung e tami koe hettelah na dei pouh han, nang dawk thoseh, na imthung dawk thoseh, na tawnta e pueng lathueng thoseh roumnae awm seh.
7 Nasikia kwamba unao wakata manyoya. Wachungaji wako walikuwa pamoja nasi, na hatukuwafanyia ubaya, na muda wote wakiwa Karmeli hawakupotelewa kitu chochote.
Na tumuen ka ngaw e tami ao tie ka thai, na tu kakhoumnaw kai koe ouk ao awh teh, runae banghai na poe awh hoeh. Karmel mon dawk ao nathung vah, bang buet touh hai kahmat boihoeh.
8 Waulize vijana wako, nao watakuambia. Basi vijana wangu wapate kibali machoni pako, maana tumefika siku ya sherehe. Tafadhali utoe cho chote ulicho nacho mkononi kwa watumishi wako na kwa Daudi mwanao.'”
Na thoundounnaw pacei haw, a dei awh han doeh. Ka thoundounnaw ni nang koe minhmai kahawi hmawt awh naseh. Kaimanaw teh pawi hnin dawk ka pha awh. Pahren lahoi nang koe kaawm e pueng hah na sannaw hoi na capa Devit poe loe telah tet pouh awh titeh lawk a thui.
9 Vijana wa Daudi walipofika, walimwambia Nabali yote haya kwa niaba ya Daudi na kisha wakasubiri.
Devit e thoundounnaw a pha toteh, Devit ni lawk a thui e patetlah Nabal koe a dei pouh awh teh, duem ao awh.
10 Nabali akawajibu watumishi wa Daudi, “Daudi ni nani? Na ni nani mwana wa Yese? Siku hizi wapo watumishi wengi wanaotoroka bwana zao.
Hatei, Nabal ni Devit e a sannaw koe, Devit teh apimaw. Jesi capa teh apimaw. Atuvah a bawipa ka taran e sannaw nahoehmaw.
11 Je, nichukue mkate wangu na maji yangu na nyama yangu ambayo nimewachinjia wakata manyoya wangu, na niwape watu wanaotoka nisikokujua?”
Ka vaiyei, ka tui, hoi ka tumuen kangawnaw hanelah ka thei pouh e heh nâ lahoi maw a tho awh tie ka panue hoeh e taminaw hah ka poe han namaw.
12 Hivyo vijana wa Daudi waligeuka na kurudi, nakumwambia kila kitu kilichosemwa.
Hatdawkvah, Devit e thoundounnaw karanglah a ban awh teh, Devit koe Nabal ni a dei e naw hah a dei pouh awh.
13 Daudi akawaambia watu wake, “Kila mtu ajifunge upanga wake.” Kila mtu akajifunga upanga wake. Daudi naye pia akajifunga upanga wake. Yapata kama watu mia nne wakafuatana na Daudi, na wengine mia mbili walibaki kulinda mizigo yao.
Devit ni a taminaw koevah, na tahloi koung kava awh telah atipouh teh, tahloi koung a kava awh. Devit ma hai tahloi a kava van. Tami 400 touh ni Devit hnuk a kâbang awh. Tami 200 touh ni hnopainaw a la ring awh.
14 Lakini kijana mmojawapo alimwambia Abigaili, mke wa Nabali akasema, “Daudi aliwatuma wajumbe kutoka jangwani waje wamsalimu bwana wetu, na yeye akawatukana.
Hahoi, thoundoun buet touh ni Nabal e a yu Abigail koevah, khenhaw! Devit ni kahrawngum hoi maimae bawipa kut man hanelah a patounenaw a patoun teh, ahni ni a yue.
15 Bado watu hawa walitutendea mema. Hatukudhurika na hatukupoteza chochote wakati wote tulipotembea nao tulipokuwa mbugani.
Hatei, ahnimanaw teh maimouh koe hroung ahawi awh. Runae banghai na poe boi awh hoeh. Law dawk ao awh nathung bang hno hai pasai awh hoeh.
16 Walikuwa ukuta wetu usiku na mchana, wakati wote tulikuwa pamoja nao tukichunga kondoo.
Tu ka khoum awh navah, ahnimouh koe ka o awh nathung tahroe hoi taran na ring pouh awh.
17 Kwa hiyo tambua hili na zingatia utafanya nini, maana ubaya unamvizia bwana wetu, na utakuwa juu ya nyumba yake yote. Yeye ni mtu asiyefaa na hakuna awezaye kushauriana naye.”
Hatdawkvah, bangmaw na sak han. Kahawicalah pouk haw. Bangkongtetpawiteh, maimae bawipa hoi imthungnaw koe thoenae a sak han toe. Ahni teh tamikahawi hoeh e lah ao dawkvah, apinihai dei thai hoeh telah atipouh.
18 Ndipo Abigaili akaharakisha na akachukuwa mikate mia mbili, chupa mbili za divai, kondoo watano waliokwisha andaliwa, vipimo vitano vya bisi, vishada mia moja vya zabibu, na mikate mia mbili ya tini na akavipakia juu ya punda.
Abigail ni karanglah vaiyei phen 200 touh, misurum kahni touh hoi thawng tangcoung e tu buem panga touh, tavai phen sum panga touh, misurpaw phen 100 touh, thaibunglung ka radip e 200 touh a sin teh, la a phu sak.
19 Akamwambia kijana wake, “Tangulia mbele yangu, nami nitakuja nyuma yako.” Lakini hakumwambia mmewe Nabali.
Hahoi ama koe kaawm e thoundounnaw koevah, ka hmalah pou cet awh. Nangmae hnuklah ka tho han atipouh. Hatei, a vâ Nabal koe dei pouh hoeh.
20 Alipokuwa akienda juu ya punda wake na kutelemka penye kificho cha mlima, Daudi na watu wake walishuka chini wakimwelekea Abigaili, naye akakutana nao.
La dawk a kâcui teh mon rahim a pha navah, Devit hoi a taminaw ahni koe a cathuk e hah a hmu teh, a kâhmo.
21 Basi Daudi alikuwa amesema, “Hakika nimelinda bure vyote alivyonavyo mtu huyu huko nyikani, na vyote alivyonavyo hakuna kilichopotea, pamoja na hayo amenilipa mabaya badala ya mema.
Devit ni ahnie hno buet touh boehai a kahma hoeh nahanelah kahrawngum vah, a tawn e pueng kai ni ayawmyin lah ka ring pouh. Ka hawinae heh thoenae hoi na pathung.
22 Mungu na anitendee hivyo mimi, Daudi, pia iwe zaidi, iwapo nitamwacha hata mtu mmoja wa kwake akiwa hai ifikapo kesho asubuhi.
Tangtho amom khodai totouh a tawn e pueng thung dawk hoi tongpa camo buet touh kangna ka hlung pawiteh Cathut ni Devit heh taran kut dawk a ngai patetlah na tet lawiseh. Hothlak hai hoe na tet yawkaw seh telah lawk yo a kam toe.
23 Abigaili alipomwona Daudi, aliharakisha na kushuka chini ya punda wake, akalala kifudifudi na kujiinamisha hadi chini.
Abigail ni Devit a hmu navah, la van hoi karanglah a kum teh, Devit hmalah a minhmai talai rekkâbet lah a tabo.
24 Akamwangukia miguuni pake na kusema, “Juu yangu tu, bwana wangu, na uwe uovu. Tafadhali acha mjakazi wako aseme nawe, tena uyasikilize maneno ya mjakazi wako.
A khok koe a tabo teh, kai dawk roeroe vah thoe saknae bawt seh. Na sannu ni na hnâthainae koe, lawk ka dei vaiteh, na sannu ni lawk ka dei e hah na thai pouh haw.
25 Nakusihi bwana wangu usimjali mtu huyu asiyefaa, Nabali, kwa maana kama jina lake lilivyo, ndivyo alivyo. Jina lake ni Nabali, na upumbavu uko pamoja naye. Lakini mimi mjakazi wako sikuwaona vijana wa bwana wangu, uliowatuma.
Ka bawipa tamikayon Nabal hah banglahai noutna hanh. A min phung e patetlah doeh ao. Nabal tie patetlah ka pathu e doeh. Kai na sannu ni bawipa nang ni na patoun e thoundounnaw ka hmu hoeh dawk doeh atipouh.
26 Sasa basi, bwana wangu, kama BWANA aishivyo, na kama unavyoishi, kwa kuwa BWANA amekuondoa kutoka kumwaga damu, na kuacha kulipiza kisasi kwa mkono mwenyewe, basi adui zako, na wale ambao wanatafuta kumfanyia uovu bwana wangu, wawe kama Nabali
Hatdawkvah, ka bawipa atuteh, BAWIPA a hring e hoi nang na hring e patetlah khoeroe ka hmawt hoeh. BAWIPA ni thi palawng hoeh hane hoi na kut hoi a moi na pathung hoeh hanelah, na tarannaw hoi bawipa nang dawk a thoenae katawngnaw teh, Nabal patetlah tho awh lawiseh.
27 Na sasa zawadi hii ambayo mjakazi wako ameileta kwa bwana wangu, na wapewe vijana ambao wanamfuata bwana wangu.
Hahoi ka bawipa nang hanelah na sannu ni poehno ka sin e heh, ka bawipa nang koe ka kâbang e thoundounnaw poe lah awm lawiseh.
28 Tafadhali ulisamehe kosa la mjakazi wako, maana BWANA hakika atamfanyia bwana wangu nyumba imara, kwa sababu bwana wangu anapigana vita vya BWANA; na uovu hautaonekana ndani yako maadamu unaishi.
Na sannu ni ka payon e naw hah pankângai ei. Ka bawipa nang teh BAWIPA koe lah taran na tuk dawk thoseh, na hring nathung nang dawk yonpen hane ao hoeh dawk thoseh, BAWIPA ni nang hanelah kacakpounge imthung a kangdue sak han doeh telah atipouh.
29 Na ingawa watu wangeinuka na kukuandama ili wakuue, bado uhai wa bwana wangu utafungwa katika furushi la walio hai na BWANA Mungu wako; na atayatupa maisha ya adui zako mbali, kama vile kutoka katika mfuko wa kombeo.
Nang ka pâlei hane hoi nang ka thet hanelah taminaw ni na ka tawng nakunghai nange BAWIPA Cathut ni ka bawipa e hringnae teh, kahringnaw rahak vah mek a tangoung sin han doeh. Nang e tarannaw e hringnae teh, tâyai hoi pathui e patetlah a thui vaiteh a kahma awh han.
30 Na itakuwa, BWANA atakapokuwa amemtimizia bwana wangu mambo yote mazuri ambayo amekuahidi, na alivyokufanya kiongozi juu ya Israeli,
BAWIPA ni nang dawk hnokahawi na kam pouh e pueng ka bawipa nang dawk a kuep sak teh, Isarel siangpahrang lah na rawi torei teh,
31 jambo hili halitakuwa huzuni kwako, wala chukizo moyoni kwa bwana wangu, kwa sababu hukumwaga damu bila sababu, na hujajilipizia kisasi. Na BWANA akikuletea mafanikio, umkumbuke mjakazi wako.”
A khuekhaw awm laipalah, tami na thet hoeh. Ka bawipa ni moi na pathung hoeh e hah nang hanlah lungmathoenae lah awm roeroe mahoeh. Ka bawipa hanlah lungkuep hoeh nahanlah awm roeroe mahoeh. BAWIPA ni ka bawipa tak dawk hnokahawi a sak toteh, na sannu heh pahnim hanh atipouh.
32 Ndipo Daudi akamwambia Abigaili, “BWANA, Mungu wa Israeli, abarikiwe, aliyekutuma uonane na mimi leo.
Devit ni hai, sahnin nang hoi kâhmo sak hanelah, nang na ka patoun e Isarelnaw e BAWIPA Cathut teh, yawhawi lah awm lawiseh.
33 Na hekima yako ibarikiwe, nawe umebarikiwa, kwa sababu leo umenizuia nisiwe na hatia ya kumwaga damu, na kutojilipizia kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.
Na khopouk thainae teh yawhawinae lah ao vaiteh, sahnin kai teh tami hringnae thei hanelah ka kâcai hoeh nahan, ka kut hoi moipathung laipalah, na kangangkung hai yawhawinae awm lawiseh.
34 Kwa kweli, kama BWANA, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye amenizuia nisikuumize, kama usinge harakisha kuja ukutane nami, kwa hakika kesho asubuhi asinge salia hata mtoto mmoja wa kiume kwa Nabali.”
Bangkongtetpawiteh, nang hah runae na poe hoeh nahanlah hoi, ka ngang e Isarel BAWIPA Cathut teh a hring e patetlah kai hoi kâhmo hanelah karanglah na tho hoehpawiteh, tangtho amom vah Nabal hanelah tongpa buet touh boehai ka pâhlung mahoeh telah Abigail koe a dei pouh.
35 Kwa hiyo Daudi akavipokea kutoka mkononi mwake vile alivyokuwa amemletea; akamwambia, “Nenda kwa amani hadi nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako na nimekubali.”
Ahni ni a sin e poehno a kut dawk e Devit ni a la pouh teh, na onae im koe lah karoumcalah cet haw, nange na lawk ka ngai toe, na minhmai hai ka khet han telah atipouh.
36 Abigaili akarudi kwa Nabali; tazama, alikuwa akifanya sherehe katika mji wake, kama sherehe ya mfalme; na moyo wa Nabali ulifurahi ndani yake, kwa sababu alikwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia chochote kabisa hadi kulipopambazuka
Abigail ni hai Nabal koe bout a cei teh, ahni teh siangpahrang e pawibu patetlah bu a ca, puenghoi a parui dawkvah, a tangtho khodai hoehnahlan totouh banghai dei pouh hoeh.
37 Ikawa asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, basi mkewe akamwambia mambo hayo; moyo wake ukafa ndani yake, na akawa kama jiwe.
Amom lah Nabal teh misur parui e a thangcuem toteh hote hnonaw hah a yu ni a dei pouh. Ama teh a lung a due pouh teh, talung patetlah ao.
38 Ikawa baada ya siku kumi BWANA alimpiga Nabali naye akafa.
Hnin 10 touh hnukkhu BAWIPA ni a hem teh a due.
39 Naye Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, akasema, “BWANA abarikiwe, aliyenichukulia hatua ya shutuma yangu kutoka mkono wa Nabali, na kumzuia mtumishi wake asifanye maovu. Na amemrudishia Nabali tendo la uovu juu ya kichwa chake mwenyewe.” Ndipo Daudi akawatuma watu wakaongee na Abigaili, ili amchukue awe mke wake.
Nabal a due e hah Devit ni a thai toteh, Nabal ni na pacekpahleknae koehoi na rasa teh, na san kai heh thoenae hno dawk hoi na ka hlout sak e BAWIPA teh a min pholennae awm lawiseh. BAWIPA Cathut ni Nabal hawihoehnae hah amae lathueng bout a pha sak toe telah a dei. Devit ni Abigail teh a yu hanelah tami a patoun.
40 Watumishi wake Daudi walipofika kwa Abigaili huko Karmeli, wakaongea naye na kusema, “Daudi ametutuma kwako tukuchukue hadi kwake uwe mke wake.”
Devit e a sannaw teh Abigail onae Karmel mon koe a pha awh toteh, Devit ni a yu hanelah a san kaimouh na patoun awh toe telah atipouh.
41 Abigaili aliinuka, akainamisha uso chini, na akasema, “Tazama, mjakazi wako ni mtumwa aoshaye miguu ya watumishi wa bwana wangu.”
Abigail a thaw teh a hmalah talai dawk a tabo teh, na khenhaw! na sannu he ka bawipa e sannaw e khok pâsu hanelah doeh ka o atipouh.
42 Akaharakisha na kuamka, akapanda punda akiwa na vijakazi wake watano waliofuatana naye; akawafuata wajumbe wa Daudi, na akawa mke wake.
Hathnukkhu Abigail a thaw teh, la dawk a kâcui. A hnukkâbang e a sannu 5 touh hoi Devit ni patounenaw koe a kâbang teh Devit e yu lah ao.
43 Daudi pia alimchukua Ahinoamu wa Yezreeli akamwoa; wote wawili wakawa wake zake.
Hatnavah, Devit ni Jezreel tami Ahinoam hah a yu lah la a tawn toe. Hattoteh kahni touh hoi yu lah reirei a la.
44 Wakati huo Sauli alikuwa amempa Palti, mwana wa Laishi mtu wa Galimu, Mikali, binti yake, aliyekuwa mke wa Daudi.
Hatnavah, Sawl ni a canu Mikhal Devit e a yu teh Gallim tami Laish capa Palti koe yo la a kâhâ toe.

< 1 Samweli 25 >