< 1 Samweli 24 >

1 Sauli aliporudi kuwafukuza Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika jangwa la Engedi.”
And it was just when he returned Saul from after [the] Philistines and people told to him saying there! David [is] in [the] wilderness of En Gedi.
2 Ndipo Sauli akachukua watu elfu tatu waliochaguliwa kutoka Iraeli yote, wakaenda kumtafuta Daudi na watu wake katika miamba ya Mbuzi Mwitu.
And he took Saul three thousand man chosen from all Israel and he went to seek David and men his on [the] face of [the] rocks of the mountain goats.
3 Akafika penye mazizi ya kondoo kando ya njia, mahali palipokuwa na pango. Sauli akaingia ndani yake kujisaidia. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa wamekaa mbali zaidi ndani ya pango lilelile.
And he came to [the] folds of the sheep on the way and [was] there a cave and he went Saul to cover feet his and David and men his in [the] innermost parts of the cave [were] sitting.
4 Watu wake Daudi wakamwambia, “Hii ndiyo siku ambayo BWANA aliisema akikuambia, 'Nitamweka adui wako mkononi mwako, ili umtendee kama unavyotaka.”' Kisha Daudi akainuka na kumnyemelea kwa mbele kimya kimya na kulikata pindo la kanzu ya Sauli.
And they said [the] men of David to him here! the day which he said Yahweh to you here! I [am] about to give (enemy your *Q(K)*) in hand your and you will do to him just as it will be good in view your and he arose David and he cut off [the] skirt of the robe which [belonged] to Saul in secrecy.
5 Baadaye moyo wa Daudi ukamchoma kwa sababu alilikata pindo la kanzu ya Sauli.
And it was after thus and it struck [the] heart of David him on that he had cut off [the] skirt which [belonged] to Saul.
6 Akawaambia watu wake, “BWANA anisamehe, sikupaswa kumtendea jambo hili bwana wangu, Mtiwa mafuta wa BWANA, kwa kunyoosha mkono wangu juu yake, maana yeye ni masihi wa BWANA.”
And he said to men his far be it to me from Yahweh if I will do the thing this to lord my to [the] [one] anointed of Yahweh by stretching out hand my on him for [is] [the] [one] anointed of Yahweh he.
7 Hivyo Daudi akawakemea watu wake kwa maneno haya, na kuwazuia wasimpige Sauli. Sauli akasimama, akatoka pangoni, na kwenda zake.
And he reprimanded David men his by the words and not he permitted them to rise up against Saul and Saul he arose from the cave and he went on the way.
8 Baadaye tena, Daudi akasimama juu, akatoka pangoni, na kumwita Sauli: “Bwana wangu mfalme.” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akasujudu hadi chini na kuonyesha heshima.
And he arose David after thus and he went out (from from the cave *Q(K)*) and he called out after Saul saying O lord my the king and he looked Saul behind him and he bowed low David face [the] ground towards and he bowed down.
9 Daudi akamwambia Sauli, “Kwa nini unawasikiliza watu ambao wanasema, “Angalia, Daudi anatafuta kukudhuru?'
And he said David to Saul why? do you listen to [the] words of someone saying there! David [is] seeking harm your.
10 Leo macho yako yameona jinsi BWANA alivyokuweka mkononi mwangu tulipokuwa ndani ya pango. Wengine waliniambia nikuuwe, lakini nilikuacha hai. Nikasema, 'Sitanyoosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa kuwa ni masihi wa BWANA.'
Here! the day this they have seen eyes your this: he gave you Yahweh - this day - in hand my in the cave and someone said to kill you and it looked with compassion on you and I said not I will stretch out hand my on lord my for [is] [the] [one] anointed of Yahweh he.
11 Tazama, baba yangu, angalia pindo la kanzu yako mkononi mwangu. Kwa maana kama nilikata pindo la kanzu yako na sikukuua, basi ujuwe na uone kwamba sina uovu au kosa katika mkono wangu, na sijafanya dhambi juu yako, ingawa unawinda kuutoa uhai wangu.
And O father my see also see [the] skirt of robe your in hand my for when cut off I [the] skirt of robe your and not I killed you know and see that there not in hand my [is] evil and transgression and not I have sinned to you and you [are] lying in wait for life my to take it.
12 BWANA aamue kati yangu na wewe, na BWANA anilipizie kisasi juu yako, lakini mkono wangu kamwe hautakuwa juu yako.
May he judge Yahweh between me and between you and he will avenge me Yahweh from you and hand my not it will be on you.
13 Kama mithali ya wazee isemavyo, 'Katika waovu hutoka uovu.' Lakini mkono wangu hautakuwa juu yako.
Just as it says [the] proverb of the ancient[s] from wicked [people] it comes forth wickedness and hand my not it will be on you.
14 Mfalme wa Israeli ametoka kumuandama nani? Unamsaka nani? Unasaka mzoga wa mbwa! Unasaka kiroboto!
After whom? has he come out [the] king of Israel after whom? [are] you pursuing after a dog dead after a flea one.
15 BWANA na awe mwamuzi na atoe hukumu kati yangu na wewe, na akaione, na akatetee sababu yangu na aniruhusu kuepuka mkono wako.”
And he will become Yahweh a judge and he will judge between me and between you and may he see and may he conduct case my and may he vindicate me from hand your.
16 Daudi alipomaliza kuongea maneno haya kwa Sauli, Sauli akasema, “Hii ni sauti yako, mwanangu Daudi?” Sauli alinyanyua sauti yake akalia.
And it was - when finished David to speak the words these to Saul and he said Saul ¿ voice your [is] this O son my David and he lifted up Saul voice his and he wept.
17 Akamwambia Daudi, “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi. Kwa sababu umenilipa mazuri, wakati mimi nimekulipa maovu.
And he said to David [are] righteous you more than I for you you have dealt out to me good and I I have dealt out to you evil.
18 Leo umetangaza jinsi ulivyonitendea mazuri, kwa sababu hukuniua wakati BWANA aliponiweka katika rehema yako.
(And you *Q(K)*) you have told this day this: you have done with me good [and] this: he delivered up me Yahweh in hand your and not you killed me.
19 Kwa kuwa mtu akimpata adui yake, atamwacha aende zake salama? Na BWANA akuzawadie mema kwa kile ulichonifanyia leo.
And if he will find anyone enemy his and will he send away? him on a journey good and Yahweh may he reward you good in place of the day this [that] which you have done to me.
20 Basi, najua kwa hakika kwamba utakuwa mfalme na kwamba ufalme wa Israeli utaimarika katika mkono wako.
And therefore here! I know that certainly you will reign and it will be established in hand your [the] kingdom of Israel.
21 Niapie kwa BWANA kwamba baada yangu hautawakatilia mbali uzao wangu, na kwamba hautaliharibu jina langu katika nyumba ya baba yangu.”
And therefore swear an oath! to me by Yahweh if you will cut off offspring my after me and if you will destroy name my from [the] house of father my.
22 Hivyo Daudi akamwapia Sauli kiapo. Kisha Sauli akaenda nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.
And he swore an oath David to Saul and he went Saul to house his and David and men his they went up to the stronghold.

< 1 Samweli 24 >