< 1 Samweli 24 >

1 Sauli aliporudi kuwafukuza Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika jangwa la Engedi.”
It happened, when Saul was returned from following the Philistines, that it was told him, saying, "Look, David is in the wilderness of En Gedi."
2 Ndipo Sauli akachukua watu elfu tatu waliochaguliwa kutoka Iraeli yote, wakaenda kumtafuta Daudi na watu wake katika miamba ya Mbuzi Mwitu.
Then Saul took three thousand chosen men out of all Israel, and went to seek David and his men on the rocks of the wild goats.
3 Akafika penye mazizi ya kondoo kando ya njia, mahali palipokuwa na pango. Sauli akaingia ndani yake kujisaidia. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa wamekaa mbali zaidi ndani ya pango lilelile.
He came to the sheep pens by the way, where there was a cave; and Saul went in to relieve himself. Now David and his men were abiding in the innermost parts of the cave.
4 Watu wake Daudi wakamwambia, “Hii ndiyo siku ambayo BWANA aliisema akikuambia, 'Nitamweka adui wako mkononi mwako, ili umtendee kama unavyotaka.”' Kisha Daudi akainuka na kumnyemelea kwa mbele kimya kimya na kulikata pindo la kanzu ya Sauli.
The men of David said to him, "Look, the day of which the LORD said to you, 'Look, I will deliver your enemy into your hand, and you shall do to him as it shall seem good to you.'" Then David arose, and cut off an edge of Saul's robe secretly.
5 Baadaye moyo wa Daudi ukamchoma kwa sababu alilikata pindo la kanzu ya Sauli.
It happened afterward, that David's heart struck him, because he had cut off an edge of Saul's robe.
6 Akawaambia watu wake, “BWANA anisamehe, sikupaswa kumtendea jambo hili bwana wangu, Mtiwa mafuta wa BWANA, kwa kunyoosha mkono wangu juu yake, maana yeye ni masihi wa BWANA.”
He said to his men, "The LORD forbid that I should do this thing to my lord, the LORD's anointed, to put forth my hand against him, since he is the LORD's anointed."
7 Hivyo Daudi akawakemea watu wake kwa maneno haya, na kuwazuia wasimpige Sauli. Sauli akasimama, akatoka pangoni, na kwenda zake.
So David persuaded his men with these words and did not allow them to rise up against Saul. Then Saul got up, and went down the road.
8 Baadaye tena, Daudi akasimama juu, akatoka pangoni, na kumwita Sauli: “Bwana wangu mfalme.” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akasujudu hadi chini na kuonyesha heshima.
Afterward David also got up and left the cave, and called out after Saul, saying, "My lord the king." When Saul looked behind him, David bowed with his face to the ground and did homage.
9 Daudi akamwambia Sauli, “Kwa nini unawasikiliza watu ambao wanasema, “Angalia, Daudi anatafuta kukudhuru?'
David said to Saul, "Why do you listen to men's words, saying, 'Look, David seeks your harm?'
10 Leo macho yako yameona jinsi BWANA alivyokuweka mkononi mwangu tulipokuwa ndani ya pango. Wengine waliniambia nikuuwe, lakini nilikuacha hai. Nikasema, 'Sitanyoosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa kuwa ni masihi wa BWANA.'
Look, this day your eyes have seen how that the LORD had delivered you today into my hand in the cave, but I refused to kill you, and my eye spared you; and I said, 'I will not put forth my hand against my lord; for he is the LORD's anointed.'
11 Tazama, baba yangu, angalia pindo la kanzu yako mkononi mwangu. Kwa maana kama nilikata pindo la kanzu yako na sikukuua, basi ujuwe na uone kwamba sina uovu au kosa katika mkono wangu, na sijafanya dhambi juu yako, ingawa unawinda kuutoa uhai wangu.
Now look, the skirt of your robe in my hand. When I cut off the skirt, and did not kill you, know and see that there is neither evil nor disobedience in my hand, and I have not sinned against you, though you hunt for my life to take it.
12 BWANA aamue kati yangu na wewe, na BWANA anilipizie kisasi juu yako, lakini mkono wangu kamwe hautakuwa juu yako.
May the LORD judge between me and you, and may the LORD avenge me of you; but my hand shall not be on you.
13 Kama mithali ya wazee isemavyo, 'Katika waovu hutoka uovu.' Lakini mkono wangu hautakuwa juu yako.
As the proverb of the ancients says, 'Out of the wicked comes forth wickedness;' but my hand shall not be on you.
14 Mfalme wa Israeli ametoka kumuandama nani? Unamsaka nani? Unasaka mzoga wa mbwa! Unasaka kiroboto!
Against whom has the king of Israel come out? Whom do you pursue? After a dead dog, or one flea?
15 BWANA na awe mwamuzi na atoe hukumu kati yangu na wewe, na akaione, na akatetee sababu yangu na aniruhusu kuepuka mkono wako.”
May the LORD therefore be judge and give sentence between me and you. May he see and plead my cause, and deliver me out of your hand."
16 Daudi alipomaliza kuongea maneno haya kwa Sauli, Sauli akasema, “Hii ni sauti yako, mwanangu Daudi?” Sauli alinyanyua sauti yake akalia.
It came to pass, when David had made an end of speaking these words to Saul, that Saul said, "Is this your voice, my son David?" Saul lifted up his voice, and wept.
17 Akamwambia Daudi, “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi. Kwa sababu umenilipa mazuri, wakati mimi nimekulipa maovu.
He said to David, "You are more righteous than I; for you have done good to me, whereas I have done evil to you.
18 Leo umetangaza jinsi ulivyonitendea mazuri, kwa sababu hukuniua wakati BWANA aliponiweka katika rehema yako.
And you have declared this day how you have dealt well with me, in that the LORD had delivered me up into your hand and you did not kill me.
19 Kwa kuwa mtu akimpata adui yake, atamwacha aende zake salama? Na BWANA akuzawadie mema kwa kile ulichonifanyia leo.
For if a man finds his enemy, will he let him go away unharmed? Therefore may the LORD reward you good for that which you have done this day.
20 Basi, najua kwa hakika kwamba utakuwa mfalme na kwamba ufalme wa Israeli utaimarika katika mkono wako.
Now, look, I know that you shall surely be king, and that the kingdom of Israel shall be established in your hand.
21 Niapie kwa BWANA kwamba baada yangu hautawakatilia mbali uzao wangu, na kwamba hautaliharibu jina langu katika nyumba ya baba yangu.”
Swear now therefore to me by the LORD, that you will not cut off my descendants after me, and that you will not destroy my name out of my father's house."
22 Hivyo Daudi akamwapia Sauli kiapo. Kisha Sauli akaenda nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.
David swore to Saul. Saul went home; but David and his men went up to the stronghold.

< 1 Samweli 24 >