< 1 Samweli 24 >
1 Sauli aliporudi kuwafukuza Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika jangwa la Engedi.”
Now when Saul came back from fighting the Philistines, news was given him that David was in the waste land of En-gedi.
2 Ndipo Sauli akachukua watu elfu tatu waliochaguliwa kutoka Iraeli yote, wakaenda kumtafuta Daudi na watu wake katika miamba ya Mbuzi Mwitu.
Then Saul took three thousand of the best men out of all Israel, and went in search of David and his men on the rocks of the mountain goats.
3 Akafika penye mazizi ya kondoo kando ya njia, mahali palipokuwa na pango. Sauli akaingia ndani yake kujisaidia. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa wamekaa mbali zaidi ndani ya pango lilelile.
And on the way he came to a place where sheep were kept, where there was a hollow in the rock; and Saul went in for a private purpose. Now David and his men were in the deepest part of the hollow.
4 Watu wake Daudi wakamwambia, “Hii ndiyo siku ambayo BWANA aliisema akikuambia, 'Nitamweka adui wako mkononi mwako, ili umtendee kama unavyotaka.”' Kisha Daudi akainuka na kumnyemelea kwa mbele kimya kimya na kulikata pindo la kanzu ya Sauli.
And David's men said to him, Now is the time when the Lord says to you, I will give up your hater into your hands to do with him whatever seems good to you. Then David, getting up, took the skirt of Saul's robe in his hand, cutting off the end of it without his knowledge.
5 Baadaye moyo wa Daudi ukamchoma kwa sababu alilikata pindo la kanzu ya Sauli.
And later, David was full of regret for cutting off Saul's skirt.
6 Akawaambia watu wake, “BWANA anisamehe, sikupaswa kumtendea jambo hili bwana wangu, Mtiwa mafuta wa BWANA, kwa kunyoosha mkono wangu juu yake, maana yeye ni masihi wa BWANA.”
And David said to his men, Before the Lord, never let it be said that my hand was lifted up against my lord, the man of the Lord's selection, for the Lord's holy oil has been put on him.
7 Hivyo Daudi akawakemea watu wake kwa maneno haya, na kuwazuia wasimpige Sauli. Sauli akasimama, akatoka pangoni, na kwenda zake.
So with these words David kept his servants back, and did not let them make an attack on Saul. And Saul got up and went on his way.
8 Baadaye tena, Daudi akasimama juu, akatoka pangoni, na kumwita Sauli: “Bwana wangu mfalme.” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akasujudu hadi chini na kuonyesha heshima.
And after that David came out of the hollow rock, and crying after Saul said, My lord the king. And when Saul gave a look back, David went down on his face and gave him honour.
9 Daudi akamwambia Sauli, “Kwa nini unawasikiliza watu ambao wanasema, “Angalia, Daudi anatafuta kukudhuru?'
And David said to Saul, Why do you give any attention to those who say that it is my desire to do you wrong?
10 Leo macho yako yameona jinsi BWANA alivyokuweka mkononi mwangu tulipokuwa ndani ya pango. Wengine waliniambia nikuuwe, lakini nilikuacha hai. Nikasema, 'Sitanyoosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa kuwa ni masihi wa BWANA.'
Look! you have seen today how the Lord gave you up into my hands even now in the hollow of the rocks: and some would have had me put you to death, but I had pity on you: for I said, Never will my hand be lifted up against my lord, who has been marked with the holy oil.
11 Tazama, baba yangu, angalia pindo la kanzu yako mkononi mwangu. Kwa maana kama nilikata pindo la kanzu yako na sikukuua, basi ujuwe na uone kwamba sina uovu au kosa katika mkono wangu, na sijafanya dhambi juu yako, ingawa unawinda kuutoa uhai wangu.
And see, my father, see the skirt of your robe in my hand: for the fact that I took off the skirt of your robe and did not put you to death is witness that I have no evil purpose, and I have done you no wrong, though you are waiting for my life to take it.
12 BWANA aamue kati yangu na wewe, na BWANA anilipizie kisasi juu yako, lakini mkono wangu kamwe hautakuwa juu yako.
May the Lord be judge between me and you, and may the Lord give me my rights against you, but my hand will never be lifted up against you.
13 Kama mithali ya wazee isemavyo, 'Katika waovu hutoka uovu.' Lakini mkono wangu hautakuwa juu yako.
There is an old saying, From the evil-doer comes evil: but my hand will never be lifted up against you.
14 Mfalme wa Israeli ametoka kumuandama nani? Unamsaka nani? Unasaka mzoga wa mbwa! Unasaka kiroboto!
After whom has the king of Israel come out? for whom are you searching? for a dead dog, an insect.
15 BWANA na awe mwamuzi na atoe hukumu kati yangu na wewe, na akaione, na akatetee sababu yangu na aniruhusu kuepuka mkono wako.”
So let the Lord be judge, and give a decision between me and you, and see and give support to my cause, and keep me from falling into your hands.
16 Daudi alipomaliza kuongea maneno haya kwa Sauli, Sauli akasema, “Hii ni sauti yako, mwanangu Daudi?” Sauli alinyanyua sauti yake akalia.
Now when David had said these words to Saul, Saul said, Is this your voice, David, my son? And Saul was overcome with weeping.
17 Akamwambia Daudi, “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi. Kwa sababu umenilipa mazuri, wakati mimi nimekulipa maovu.
And he said to David, You are right and I am wrong: for you have given me back good, but I have given you evil.
18 Leo umetangaza jinsi ulivyonitendea mazuri, kwa sababu hukuniua wakati BWANA aliponiweka katika rehema yako.
And you have made clear to me how good you have been to me today: because, when the Lord gave me up into your hands, you did not put me to death.
19 Kwa kuwa mtu akimpata adui yake, atamwacha aende zake salama? Na BWANA akuzawadie mema kwa kile ulichonifanyia leo.
If a man comes across his hater, will he let him get away safe? so may you be rewarded by the Lord for what you have done for me today.
20 Basi, najua kwa hakika kwamba utakuwa mfalme na kwamba ufalme wa Israeli utaimarika katika mkono wako.
And now I am certain that you will be king, and that the kingdom of Israel will be made strong under your authority.
21 Niapie kwa BWANA kwamba baada yangu hautawakatilia mbali uzao wangu, na kwamba hautaliharibu jina langu katika nyumba ya baba yangu.”
So give me your oath by the Lord, that you will not put an end to my seed after me or let my name be cut off from my father's family.
22 Hivyo Daudi akamwapia Sauli kiapo. Kisha Sauli akaenda nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.
And David gave Saul his oath. And Saul went back to his house; but David and his men went up to their safe place.