< 1 Samweli 23 >

1 Wakamwambia Daudi, “Tazama, Wafilisti wanaupiga Keila na wanapora nafaka inayopurwa.”
They told David, “Look, the Philistines are fighting against Keilah and are robbing the threshing floors.”
2 Hivyo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, na akamuuliza,” Je, niondoke niwapige hawa Wafilisti? BWANA akamwambia Daudi, “Nenda ukawapige Wafilisti na kuokoa Keila.”
So David prayed to Yahweh for help and asked him, “Should I go and attack these Philistines?” Yahweh said to David, “Go and attack the Philistines and save Keilah.”
3 Daudi akaambiwa na watu wake, “Angalia, hapa Yuda tunaogopa. Je, si zaidi sana kama tutaenda Keila kupambana na majeshi ya Wafilisti?”
David's men said to him, “See, we are afraid here in Judah. How much more then if we go to Keilah against the armies of the Philistines?”
4 Ndipo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, bado tena, BWANA akamjibu, “Amka, uteremke hadi Keila. Maana nitakupatia ushindi dhidi ya Wafilisti.”
Then David prayed to Yahweh for help yet again. Yahweh answered him, “Arise, go down to Keilah. For I will give you victory over the Philistines.”
5 Daudi na watu wake wakaenda Keila na kupigana na Wafilisti. Wakahamisha ng'ombe wao na kuwapiga kwa mauaji makubwa mno. Hivyo Daudi akawaokoa wenyeji wa Keila.
David and his men went to Keilah and fought with the Philistines. He led away their cattle and struck them with a great slaughter. So David saved the inhabitants of Keilah.
6 Abiathari mwana wa Ahimeleki alipokuwa amekimbilia kwa Daudi huko Keila, alibeba naivera mkononi mwake.
When Abiathar son of Ahimelech had fled to David at Keilah, he came down with an ephod in his hand.
7 Sauli aliambiwa kwamba Daudi amekwenda Keila. Sauli akasema, “Mungu amemweka mkononi mwangu. Bila shaka amefungiwa ndani kwa sababu ameingia katika mji ulio na malango na makomeo.”
Saul was told that David had gone to Keilah. Saul said, “God has given him into my hand. For he is shut in because he has entered a city that has gates and bars.”
8 Sauli akayaita majeshi yake yote kwa ajili ya vita, waende hadi Keila, wamteke Daudi na watu wake.
Saul summoned all his forces for battle, to go down to Keilah, to besiege David and his men.
9 Daudi alijua kwamba Sauli alikuwa anapanga njama za kumdhuru yeye. Ndipo akamwambia kuhani Abiathari kuhani, “Ulete hapa naivera.”
David knew that Saul was plotting harm against him. He said to Abiathar the priest, “Bring the ephod here.”
10 Kisha Daudi akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, mtumishi wako hakika amesikia kwamba Sauli anatafuta namna ya kuja Keila, ili auteketeze mji kwa ajili yangu.
Then David said, “Yahweh, the God of Israel, your servant has indeed heard that Saul seeks to come to Keilah, to destroy the city for my sake.
11 Je, watu wa Keila watanisalimisha mkononi mwake? Je, Sauli atashuka hadi huko, kama mtumishi wako alivyosikia? BWANA, Mungu wa Israeli, nakusihi, tafadhali mwambie mtumishi wako. “BWANA akasema, “Atakuja huko.”
Will the men of Keilah surrender me into his hand? Will Saul come down, as your servant has heard? Yahweh, the God of Israel, I beg you, please tell your servant.” Yahweh said, “He will come down.”
12 Kisha Daudi akauliza, “Je, watu wa Keila watanisalimisha mimi na watu wangu katika mkono wa Sauli?” BWANA akasema, “Watu hao watawasalimisha kwao.”
Then David said, “Will the men of Keilah surrender me and my men into the hand of Saul?” Yahweh said, “They will surrender you.”
13 Kisha Daudi na watu wake, waliokuwa kama mia sita, walitoka na kwenda mbali na Keila, na wakazunguka kila sehemu. Kisha Sauli akaambiwa kwamba Daudi ametoroka kutoka Keila, hivyo akasitisha kumfuatia.
Then David and his men, who were about six hundred, got up and went away from Keilah, and they went from place to place. It was told Saul that David had escaped from Keilah, and he stopped the pursuit.
14 Daudi alikaa ngomeni katika jangwa, kwenye nchi ya milima katika jangwa la Zifu. Kila siku Sauli alimtafuta, lakini Mungu hakumweka mkononi mwake.
David stayed in the strongholds in the wilderness, in the hill country in the wilderness of Ziph. Saul looked for him every day, but God did not give him into his hand.
15 Daudi aliona kwamba Sauli amejitokeza kuangamiza maisha yake; basi Daudi alikuwa katika jjangwa la Zifu huko Horeshi.
David saw that Saul had come out to seek his life; now David was in the wilderness of Ziph at Horesh.
16 Kisha Yonathani, mwana wa Sauli, akaamuka akaenda kwa Daudi huko Horshi, naye akamtia moyo amtumainie Mungu.
Then Jonathan, Saul's son, got up and went to David at Horesh, and strengthened his hand in God.
17 Akamwambia, “Usiogope. Kwa maana mkono wa baba yangu Sauli hautakupata. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, na mimi nitakuwa msaidizi wako. Baba yangu Sauli pia anajua hivyo.”
He said to him, “Do not be afraid. For the hand of Saul my father will not find you. You will be king over Israel, and I will be next to you. Saul my father also knows this.”
18 Basi wote wawili wakafanya agano mbele za BWANA. Kisha Daudi alibaki Horeshi, na Yonathani akaenda nyumbani.
They made a covenant before Yahweh. David remained at Horesh, and Jonathan went home.
19 Nndipo Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea wakisema, “Je, Daudi hakujificha kati yetu kwenye ngome huko Horeshi, juu ya mlima wa Hakila, ulioko kusini mwa Yeshimoni?
Then Ziphites came to Saul at Gibeah and said, “Is not David hiding among us in the strongholds at Horesh, on the hill of Hakilah, which is south of Jeshimon?
20 Basi uje, mfalme! Kulingana na matakwa yako, uje! Kazi yetu itakuwa kumtia katika mkono wa mfalme.”
Now come down, king! According to your desire, come down! Our part will be to surrender him into the king's hand.”
21 Sauli akasema, “Mbarikiwe na BWANA. Kwa sababu mmenihurumia.
Saul said, “May you be blessed by Yahweh. For you have had compassion on me.
22 Nendeni, mhakikishe sawasawa. Tafuteni na kujua maficho yake yako wapi na ni nani amemwona huko. Nimeambiwa kwamba yeye ni mjanja sana.
Go, make even more sure. Learn and find out where his hiding place is and who has seen him there. It is told to me that he is very crafty.
23 Kwa hiyo chunguzeni, mjue sehemu zote anakojificha. Baadaye rudini kwangu mkiwa na taarifa kamili, na kisha nitaongozana nanyi. Ikiwa yupo katika nchi, nitamtafuta kutoka miongoni mwa elfu zote za Yuda.”
So look, and learn all of the places where he hides himself. Come back to me with sure information, and then I will return with you. If he is in the land, I will search him out among all the thousands of Judah.”
24 Ndipo wakaamka na kwenda hadi Zifu mbele ya Sauli. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa katika jangwa la Maoni, huko Araba upande wa kusini mwa Yeshimoni.
Then they rose up and went to Ziph ahead of Saul. Now David and his men were in the wilderness of Maon, in the Arabah to the south of Jeshimon.
25 Sauli na watu wake wakaenda kumtafuta Daudi. Na Daudi akaambiwa habari hiyo, hivyo akateremka hadi kwenye mlima wa miamba na akakaa katika jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hivyo, akamfukuza Daudi katika Jangwa la Maoni.
Saul and his men went to seek him. But David was told of it, so he went down to a rocky hill and lived in the wilderness of Maon. When Saul heard it, he chased David in the wilderness of Maon.
26 Sauli akaenda akawa upande mmoja wa mlima, na Daudi na watu wake walikuwa wakienda upande mwingine wa mlima. Daudi kwa haraka akatoweka akae mbali na Sauli. Kwa sababu Sauli na watu wake walikuwa wakimzunguka Daudi na watu wake wawakamate,
Saul went on one side of the mountain, and David and his men were going on the other side of the mountain. David hurried to get away from Saul. As Saul and his men were surrounding David and his men to take them,
27 mjumbe mmoja akaja kwa Sauli na kusema, “Njoo, harakisha maana Wafilisti wamepanga uvamizi juu ya nchi.”
a messenger came to Saul and said, “Hurry and come, for the Philistines have made a raid against the land.”
28 Kwa hiyo Sauli akarudi asimfuatie Daudi na akaenda kupambana na Wafilisti. Kwa hiyo sehemu ile iliitwa Mwamba wa Maficho.
So Saul returned from pursuing David and went against the Philistines. Therefore that place was called the Rock of Escape.
29 Daudi akapanda kutoka huko na kukaa katika ngome ya Engedi.
David went up from there and lived in the strongholds of Engedi.

< 1 Samweli 23 >