< 1 Samweli 23 >

1 Wakamwambia Daudi, “Tazama, Wafilisti wanaupiga Keila na wanapora nafaka inayopurwa.”
Then they tolde Dauid, saying, Beholde, the Philistims fight against Keilah, and spoyle the barnes.
2 Hivyo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, na akamuuliza,” Je, niondoke niwapige hawa Wafilisti? BWANA akamwambia Daudi, “Nenda ukawapige Wafilisti na kuokoa Keila.”
Therfore Dauid asked counsel of the Lord, saying, Shal I goe and smite these Philistims? And the Lord answered Dauid, Go and smite the Philistims, and saue Keilah.
3 Daudi akaambiwa na watu wake, “Angalia, hapa Yuda tunaogopa. Je, si zaidi sana kama tutaenda Keila kupambana na majeshi ya Wafilisti?”
And Dauids men said vnto him, See, we be afrayde here in Iudah, howe much more if we come to Keilah against the hoste of ye Philistims?
4 Ndipo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, bado tena, BWANA akamjibu, “Amka, uteremke hadi Keila. Maana nitakupatia ushindi dhidi ya Wafilisti.”
Then Dauid asked counsell of the Lord againe. And the Lord answered him, and sayd, Arise, go downe to Keilah: for I wil deliuer the Philistims into thine hand.
5 Daudi na watu wake wakaenda Keila na kupigana na Wafilisti. Wakahamisha ng'ombe wao na kuwapiga kwa mauaji makubwa mno. Hivyo Daudi akawaokoa wenyeji wa Keila.
So Dauid and his men went to Keilah, and fought with the Philistims, and brought away their cattel, and smote them with a great slaughter: thus Dauid saued the inhabitants of Keilah.
6 Abiathari mwana wa Ahimeleki alipokuwa amekimbilia kwa Daudi huko Keila, alibeba naivera mkononi mwake.
(And when Abiathar the sonne of Ahimelech fled to Dauid to Keilah, he brought an Ephod with him)
7 Sauli aliambiwa kwamba Daudi amekwenda Keila. Sauli akasema, “Mungu amemweka mkononi mwangu. Bila shaka amefungiwa ndani kwa sababu ameingia katika mji ulio na malango na makomeo.”
And it was tolde Saul that Dauid was come to Keilah, and Saul sayd, God hath deliuered him into mine hand: for he is shut in, seeing he is come into a citie that hath gates and barres.
8 Sauli akayaita majeshi yake yote kwa ajili ya vita, waende hadi Keila, wamteke Daudi na watu wake.
Then Saul called all the people together to warre, for to go downe to Keilah, and to besiege Dauid and his men.
9 Daudi alijua kwamba Sauli alikuwa anapanga njama za kumdhuru yeye. Ndipo akamwambia kuhani Abiathari kuhani, “Ulete hapa naivera.”
And Dauid hauing knowledge that Saul imagined mischiefe against him, saide to Abiathar the Priest, Bring the Ephod.
10 Kisha Daudi akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, mtumishi wako hakika amesikia kwamba Sauli anatafuta namna ya kuja Keila, ili auteketeze mji kwa ajili yangu.
Then sayde Dauid, O Lord God of Israel, thy seruat hath heard, that Saul is about to come to Keilah to destroy the citie for my sake.
11 Je, watu wa Keila watanisalimisha mkononi mwake? Je, Sauli atashuka hadi huko, kama mtumishi wako alivyosikia? BWANA, Mungu wa Israeli, nakusihi, tafadhali mwambie mtumishi wako. “BWANA akasema, “Atakuja huko.”
Wil the lordes of Keilah deliuer me vp into his hand? and will Saul come downe, as thy seruant hath heard? O Lord God of Israel, I beseech thee, tell thy seruant. And the Lord sayde, He will come downe.
12 Kisha Daudi akauliza, “Je, watu wa Keila watanisalimisha mimi na watu wangu katika mkono wa Sauli?” BWANA akasema, “Watu hao watawasalimisha kwao.”
Then said Dauid, Will the lords of Keilah deliuer me vp, and the men that are with me, into the hand of Saul? And the Lord sayde, They will deliuer thee vp.
13 Kisha Daudi na watu wake, waliokuwa kama mia sita, walitoka na kwenda mbali na Keila, na wakazunguka kila sehemu. Kisha Sauli akaambiwa kwamba Daudi ametoroka kutoka Keila, hivyo akasitisha kumfuatia.
Then Dauid and his men, which were about sixe hundreth, arose, and departed out of Keilah, and went whither they coulde. And it was tolde Saul, that Dauid was fled from Keilah, and he left off his iourney.
14 Daudi alikaa ngomeni katika jangwa, kwenye nchi ya milima katika jangwa la Zifu. Kila siku Sauli alimtafuta, lakini Mungu hakumweka mkononi mwake.
And Dauid abode in the wildernesse in holdes, and remayned in a mountaine in the wildernes of Ziph. And Saul sought him euery day, but God deliuered him not into his hand.
15 Daudi aliona kwamba Sauli amejitokeza kuangamiza maisha yake; basi Daudi alikuwa katika jjangwa la Zifu huko Horeshi.
And Dauid sawe that Saul was come out for to seeke his life: and Dauid was in the wildernes of Ziph in the wood.
16 Kisha Yonathani, mwana wa Sauli, akaamuka akaenda kwa Daudi huko Horshi, naye akamtia moyo amtumainie Mungu.
And Ionathan Sauls sonne arose and went to Dauid into the wood, and comforted him in God,
17 Akamwambia, “Usiogope. Kwa maana mkono wa baba yangu Sauli hautakupata. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, na mimi nitakuwa msaidizi wako. Baba yangu Sauli pia anajua hivyo.”
And said vnto him, Feare not: for the hand of Saul my father shall not finde thee, and thou shalt be King ouer Israel, and I shalbe next vnto thee: and also Saul my father knoweth it.
18 Basi wote wawili wakafanya agano mbele za BWANA. Kisha Daudi alibaki Horeshi, na Yonathani akaenda nyumbani.
So they twaine made a couenant before ye Lord: and Dauid did remaine in the wood: but Ionathan went to his house.
19 Nndipo Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea wakisema, “Je, Daudi hakujificha kati yetu kwenye ngome huko Horeshi, juu ya mlima wa Hakila, ulioko kusini mwa Yeshimoni?
Then came vp the Ziphims to Saul to Gibeah, saying, Doeth not Dauid hide himselfe by vs in holdes, in the wood in the hill of Hachilah, which is on the right side of Ieshimon?
20 Basi uje, mfalme! Kulingana na matakwa yako, uje! Kazi yetu itakuwa kumtia katika mkono wa mfalme.”
Nowe therefore, O King, come downe according to all that thine heart can desire, and our part shall be to deliuer him into the Kinges handes.
21 Sauli akasema, “Mbarikiwe na BWANA. Kwa sababu mmenihurumia.
Then Saul said, Be ye blessed of the Lord: for ye haue had compassion on mee.
22 Nendeni, mhakikishe sawasawa. Tafuteni na kujua maficho yake yako wapi na ni nani amemwona huko. Nimeambiwa kwamba yeye ni mjanja sana.
Goe, I pray you, and prepare ye yet better: know and see his place where he haunteth, and who hath seene him there: for it is sayd to me, He is subtile, and craftie.
23 Kwa hiyo chunguzeni, mjue sehemu zote anakojificha. Baadaye rudini kwangu mkiwa na taarifa kamili, na kisha nitaongozana nanyi. Ikiwa yupo katika nchi, nitamtafuta kutoka miongoni mwa elfu zote za Yuda.”
See therefore and know all the secret places where he hideth himselfe, and come ye againe to me with the certaintie, and I will goe with you: and if he be in the lande, I will searche him out throughout all the thousands of Iudah.
24 Ndipo wakaamka na kwenda hadi Zifu mbele ya Sauli. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa katika jangwa la Maoni, huko Araba upande wa kusini mwa Yeshimoni.
Then they arose and went to Ziph before Saul, but Dauid and his men were in the wildernesse of Maon, in the playne on the right hande of Ieshimon.
25 Sauli na watu wake wakaenda kumtafuta Daudi. Na Daudi akaambiwa habari hiyo, hivyo akateremka hadi kwenye mlima wa miamba na akakaa katika jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hivyo, akamfukuza Daudi katika Jangwa la Maoni.
Saul also and his men went to seeke him, and they told Dauid: wherefore he came downe vnto a rocke, and abode in the wildernesse of Maon. And when Saul heard that, he folowed after Dauid in the wildernes of Maon.
26 Sauli akaenda akawa upande mmoja wa mlima, na Daudi na watu wake walikuwa wakienda upande mwingine wa mlima. Daudi kwa haraka akatoweka akae mbali na Sauli. Kwa sababu Sauli na watu wake walikuwa wakimzunguka Daudi na watu wake wawakamate,
And Saul and his men went on the one side of the mountaine, and Dauid and his men on the other side of the mountaine: and Dauid made haste to get from the presence of Saul: for Saul and his men compassed Dauid and his men round about, to take them.
27 mjumbe mmoja akaja kwa Sauli na kusema, “Njoo, harakisha maana Wafilisti wamepanga uvamizi juu ya nchi.”
But there came a messenger to Saul, saying, Haste thee, and come: for the Philistims haue inuaded the land.
28 Kwa hiyo Sauli akarudi asimfuatie Daudi na akaenda kupambana na Wafilisti. Kwa hiyo sehemu ile iliitwa Mwamba wa Maficho.
Wherefore Saul returned from pursuing Dauid, and went against the Philistims. Therefore they called that place, Sela-hammahlekoth.
29 Daudi akapanda kutoka huko na kukaa katika ngome ya Engedi.
And Dauid went thence, and dwelt in holdes at En-gedi.

< 1 Samweli 23 >