< 1 Samweli 20 >

1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akaenda na kumwambia Yonathani, “Nimefanya nini? Uovu wangu ni upi? Dhambi yangu ni ipi kwa baba yako, inayofanya atafute kuutoa uhai wangu.”
Forsothe Dauid fledde fro Naioth, which is in Ramatha, and cam and spak bifor Jonathas, What haue Y do? what is my wickidnesse, and what is my synne ayens thi fadir, for he sekith my lijf?
2 Yonathani akamwambia Daudi, “La hasha; hautakufa. Baba yangu hafanyi jambo kubwa wala dogo bila kunijulisha. Kwa nini inamlazimu baba yangu anifiche jambo hili? La, siyo hivyo?”
And Jonathas seide to hym, Fer be it fro thee, thou schalt not die, for my fadir schal not do ony thing greet ether litil, `no but he schewe firste to me; therfor my fadir kepte preuy fro me this word oneli, forsothe it schal not be.
3 Bado Daudi aliapa tena na akasema, “Baba yako anajua wazi kwamba nimepata kibali machoni pako. Pengine anasema, 'Asije Yonathani akajua jambo hili, labda atahuzunika.' Lakini kweli kama BWANA aishivyo, kama wewe uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
And eft he swoor to Dauid. And Dauid seide, Treuli thi fadir woot, that Y haue founde grace `in thin iyen, and he schal seie, Jonathas wite not this, lest perauenture he be sory; certis the Lord lyueth, `and thi soule lyueth, for, that Y seie so, Y and deeth ben departid oneli bi o degree.
4 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Lolote utakalosema, nitakufanyia.”
And Jonathas seide to Dauid, What euer thing thi soule schal seie to me, Y schal do to thee.
5 Daudi akamwambia Yonathani, “Kesho ni siku ya mwezi mpya, na inanibidi kukaa na kula pamoja na mfalme. Lakini acha niende, ili niweze kujificha katika shamba hadi siku ya tatu jioni.
And Dauid seide to Jonathas, Lo! calendis ben to morewe, and bi custom Y am wont to sitte bi the kyng to ete; therfor suffre thou me, `that Y be hid in the feeld `til to euentid of the thridde dai.
6 Baba yako akinikosa kabisa, ndipo utasema, 'Daudi aliniomba kwa msisitizo ruhusa aondoke kwenda mjini kwake Bethlehemu; kwa sababu huko ni kipindi cha utoaji wa dhabihu ya mwaka kwa familia yao yote.'
If thi fadir biholdith, and axith me, thou schalt answere to hym, Dauid preiede me, that he schulde go swiftli into Bethleem, his citee, for solempne sacrifices ben there to alle the men of his lynage.
7 Kama atasema kuwa ni vyema, 'basi mtumishi wako atakuwa na amani. Lakini kama atakasirika sana, ndipo utajua kwamba ameamua kunitendea uovu.
If he seith, Wel, pees schal be to thi seruaunt; forsothe if he is wrooth, wite thou, that his malice is fillid.
8 Kwa hiyo, umtendee wema mtumishi wako. Kwa maana umemweka mtumishi katika agano la BWANA pamoja na wewe. Lakini kama kuna dhambi ndani yangu, wewe mwenyewe uniuwe; maana kwa nini basi unipeleke kwa baba yako?”
Therfor do thou mercy in to thi seruaunt, for thou madist me thi seruaunt to make with thee the boond of pees of the Lord; sotheli if ony wickidnesse is in me, sle thou me, and brynge thou not in me to thi fadir.
9 Yonathani akasema, “La hasha! Ikiwa ninajua kwamba baba ameamua baya likupate, siwezi kukuambia?”
And Jonathas seide, Fer be this fro me, for it mai not be doon, that Y telle not to thee, if Y knowe certeynli, that the malice of my fadir is fillid ayens thee.
10 Ndipo Daudi akamwambia Yonathani, “Ni nani ataniambia ikiwa imetokea, baba yako akakujibu kwa ukali?”
And Dauid answeride to Jonathas, Who schal telle to me, if in caas thi fadir answerith harde ony thing of me?
11 Yonathani akamwambia Daudi, “Njoo, hebu twende huko shambani.” Ndipo wote wakaondoka kwenda shambani.
And Jonathas seide to Dauid, Come thou, and go we forth in to the feeld. And whanne bothe hadden go in to the feeld,
12 Yonathani akamwambia Daudi, “Na BWANA, Mungu wa Israeli, awe shahidi. Kesho muda kama huu, nitakuwa nimemuuliza baba yangu, au siku ya tatu, tazama, ikiwa kutakuwa na jambo zuri upande wa Daudi; je, nisikutumie taarifa na kulidhihirisha kwako?
Jonathas seide to Dauid, Lord God of Israel, if Y enquere the sentence of my fadir to morewe, ether in the nexte dai aftir, and ony `thing of good is of Dauid, and Y sende not anoon to thee,
13 Na kama ikimpendeza baba yangu akufanyie madhara, Basi BWANA ayafanye hayo kwa Yonathani na kuzidi ikiwa sitakujulisha jambo na kukupeleka mbali, ili kwamba uende kwa amani. Na BWANA awe pamoja nawe, kama alivyokuwa na baba yangu.
and make knowun to thee, God do these thingis to Jonathas, and `adde these thingis. Forsothe if the malice of my fadir contynueth ayens thee, Y schal schewe to thin eere, and Y schal delyuere thee, that thou go in pees; and the Lord be with thee, as he was with my fadir.
14 Kama bado nikiwa hai, hautanionesha uaminifu wa agano la BWANA, kwamba siwezi kufa?
And if Y lyue, do thou the mercies of the Lord to me;
15 Na usivunje kabisa uaminifu wako wa agano kati yako na nyumba yangu, hata wakati BWANA atakapowaodoa kila mmoja wa adui za Daudi kutoka uso wa dunia.”
forsothe if Y am deed, `thou schalt not take awei thi mercy fro myn hows `til in to with outen ende; `and yif Y do it not, whanne the Lord schal drawe out bi the roote the enemyes of Dauid, ech man fro the lond, take he awei Jonathas fro his hows, and seke the Lord of the hond of the enemyes of Dauid.
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi na kusema, “Naye BWANA atawaondoa maadui wa Daudi.”
Therfor Jonathas made boond of pees with the hows of Dauid, and the Lord souyte of the hond of enemyes of Dauid.
17 Yonathani akamtaka Daudi aape tena kwa sababu ya upendo aliokuwa nao juu yake, kwa sababu alimpenda kama alivyopenda roho yake mwenyewe.
And Jonathas addide to swere stedfastli to Dauid, for he louyde Dauid; for he louyde so Dauid, as his owne soule.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni siku ya mwezi mpya. Hautakuwapo, kwa sababu kiti chako kitakuwa wazi.
And Jonathas seide to hym, `Calendis ben to morewe, and thou schalt be souyt;
19 Utakapokuwa umekaa huko siku tatu, uende upesi hadi mahala ulipojificha mara ya kwanza, wakati shughuli ikifanyika, na ukaye karibu jiwe Ezeli.
for thi sittyng schal be souyt til after to morewe. Therfor thou schalt go doun hastili, and thou schalt come in to the place, where thou schalt be hid in the day, whanne it is leueful to worche; and thou schalt sitte bisidis the stoon, `to which the name is Ezel.
20 Nitatupa mishale mitatu pembeni mwa jiwe, kama vile ninalenga kitu fulani.
And Y schal sende thre arowis bisidis that stoon, and Y schal caste as `excercisynge ether pleiynge me at a signe.
21 Kisha nitamtuma kijana wangu na kumwambia, 'Nenda utafute hiyo mishale.' Kama nitamwambia kijana hivi, 'Tazama, mishale iko upande huu wa kwako; kaichukue,” ndipo uje; maana hapo kutakuwa na usalama kwako na siyo madhara, kama BWANA aishivyo.
Y schal sende also and my child, and Y schal seie to hym, Go thou, and brynge to me the arewis.
22 “Lakini kama nikimwambia kijana hivi, 'Tazama, mishale iko mbele yako,' ndipo utakapokwenda zako, maana BWANA ametaka uende zako.
If Y seie to the child, Lo! the arewis ben `with ynne thee, take thou tho; come thou to me, for pees is to thee, and no thing is of yuel, the Lord lyueth. Sotheli if Y speke thus to the child, Lo! the arowis ben biyende thee; go thou in pees, for the Lord deliuerede thee.
23 Kulingana na makubaliano ambayo mimi na wewe tumeongea, angalia, BWANA yupo kati yangu na wewe milele.'”
Forsothe of the word, which thou and Y han spoke, the Lord be bitwixe me and thee til in to with outen ende.
24 Kwa hiyo Daudi akajificha mle shambani. Pindi mwezi ulipoandama, mfalme aliketi chini ale chakula.
Therfor Dauid was hid in the feeld; and the `calendis camen, and the kyng sat to ete breed.
25 Mfalme alikaa juu ya kiti chake, kama kawaida kwenye kiti karibu na ukuta. Yonathani alisimama wima, na Abneri alikaa ubavuni mwa Sauli. Lakini nafasi ya Daudi ilikuwa wazi.
And whanne the kyng hadde seete on his chaier bi custom, `which chaier was bisidis the wal, Jonathas roos, and sat `aftir Abner, and Abner sat at the side of Saul, and the place of Dauid apperide voide.
26 Hata hivyo Sauli hakusema kitu siku hiyo, kwa sababu alifikiri, “Kuna jambo limempata Daudi. Hayuko safi; hakika hayuko safi.”
And Saul spak not ony thing in that dai; for he thouyte, that `in hap it bifelde to hym, that he was not clene `nether purified.
27 Lakini siku ya pili, siku moja baada ya mwandamo wa mwezi, bado nafasi ya Daudi ilikuwa tupu. Ndipo Sauli akamuuliza Yonathani mwanaye, “Kwa nini mwana wa Yese hakuja kwenye chakula, jana na hata leo?”
And whanne the secounde dai aftir the calendis hadde schyned, eft the place of Dauid apperide voide. And Saul seide to Jonathas his sone, Whi cometh not the sone of Isai, nether yisterdai, nether to dai to ete?
28 Yonathani akamjibu Sauli, “Daudi aliomba kwangu ruhusa kwa dhati ili aende Bethlehemu.
And Jonathas answeride to Saul, He preiede me mekeli, that he schulde go in to Bethleem;
29 Alisema, 'Tafadhali niruhusu niende. Maana familia yetu wanayo dhabihu huko mjini, na kaka yangu ameniagiza niwe huko. Basi kama nimepata kibali machoni pako, tafadhali niruhusu niende nikawaone kaka zangu.' Hakuja kwenye meza ya mfalme kwa sababu hii.”
and he seide, Suffre thou me, for solempne sacrifice is in my citee; oon of my britheren clepide me; now therfor if Y foond grace `in thin iyen, Y schal go soone, and `Y schal se my britheren; for this cause he cometh not to the `table of the kyng.
30 Ndipo hasira ya Sauli iliwaka juu ya Yonathani, na akamwambia, “Wee mwana wa mwanamke mkaidi na muasi! Wadhani kwamba sijui kuwa umemchagua Mwana wa Yese kwa ajili ya aibu yako, na kwa aibu ya uchi wa mama yako?
Forsothe Saul was wrooth ayens Jonathas, and seide to hym, Thou sone of a womman `rauyschynge at her owne wille a man, whether Y woot not, that thou louest the sone of Ysay in to thi confusioun, and in to the confusioun of thi schendful modir?
31 Kwa kuwa mwana wa Yese anaishi duniani, siyo wewe wala ufalme wako utakaoimarika. Sasa basi, tuma watu wamlete kwangu, kwa sababu inampasa kufa.”
For in alle the daies in whiche the sone of Isai lyueth on erthe, thou schalt not be stablischid, nether thi rewme; therfor `riyt now sende thou, and brynge hym to me, for he is the sone of deeth.
32 Yonathani akamjibu Sauli baba yake, “Kwa sababu gani inampasa kuuwawa? Amefanya nini?”
Sotheli Jonathas answeride to Saul his fadir, and seide, Whi schal he die? what hath he do?
33 Ndipo Sauli akamtupia mkuki apate kumuua. Kwa hiyo Yonatani akatambua kwamba baba yake alinuia kumuua Daudi.
And Saul took the spere, that he schulde smyte hym, and Jonathas vndirstood, that it was determynd of his fadir, that Dauid schulde be slayn.
34 Yonathani alitoka mezani akiwa na hasira kali bila kula chakula siku ya pili ya mwezi, kwa sababu alimhuzunikia Daudi, na kwa sababu baba yake amemwaibisha.
Therfor Jonathas roos fro the table in `the ire of woodnesse, and he ete not breed in the secounde dai of calendis; for he was sori on Dauid, for his fadir hadde schent him.
35 Ikawa asubuhi, Yonathani akaenda huko shambani kama walivyoahidiana na Daudi, akiwa pamoja na kijana wake.
And whanne the morewtid `hadde schyned, Jonathas cam in to the feeld, and a litil child with hym, bi the couenaunt of Dauid.
36 Akamwambia yule kijana wake, “Kimbia utafute ile mishale niliyoitupa.” Na kijana alikimbia, akatupa mshale mwingine mbele yake.
And Jonathas seide to his child, Go thou, and brynge to me the arowis whiche Y caste. And whanne the child hadde runne, he castide another arowe biyende the child.
37 Kijana alipofika katika eneo ambapo mshale ulitua, ule alioutuma Yonathani, akamwita tena kijana, na kusema, “Huo mshale hauko mbele yako?”
Therfor the child cam to the place of the arowe which Jonathas hadde sent; and Jonathas criede bihynde the `bak of the child, and seide, Lo! the arowe is not there, certis it is biyende thee.
38 Kisha Yonathani akamwita yule kijana, “Upesi, harakisha, usikawie!” Hivyo kijana wa Yonathani akaikusanya mishale na kurudi kwa bwana wake.
And Jonathas criede eft bihynde the bak of the child, `and seide, Haste thou swiftli, stonde thou not. Therfor the child gaderide the arowis of Jonathas, and brouyte to his lord,
39 Lakini huyo kijana hakujua lolote. Ni Yonathani na Daudi tu ndio walijua habari yenyewe.
and outerli he wiste not what was doon; for oonli Jonathas and Dauid knewen the thing.
40 Yonathani akampa kijana wake silaha na kumwambia, “Nenda, uzipeleke mjini.”
Therfor Jonathas yaf hise armeris to the child, and seide to hym, Go thou, bere in to the citee.
41 Punde tu kijana alipoondoka, Daudi akasimama kutokea upande wa kusini, akiwa amelala kifudifudi, akainama mara tatu. Walibusiana wao kwa wao na wote wakalia kwa pamoja, Daudi akilia zaidi.
And whanne the child hadde go, Dauid roos fro the place that `yede to the south; and he felde low `in to the erthe, and worschipide the thridde tyme, and thei kissiden hem silf to gidere, and `wepten to gidere; forsothe Dauid wepte more.
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa sababu wote tumeapa kwa jina la BWANA na tulisema, 'BWANA awe kati yangu na wewe, na awe kati ya uzao wangu na uzao wako, milele.'” Kisha Daudi alisimama na akaondoka, na Yonathani akarudi mjini.
Therfor Jonathas seide to Dauid, Go thou in pees; what euer thingis we bothe han swoore in the `name of the Lord, `and seiden, `The Lord be bitwixe me and thee, and bitwixe my seed and thi seed til in to with outen ende, `be stidfast. And Dauid roos, and yede, but also Jonathas entride in to the citee.

< 1 Samweli 20 >