< 1 Samweli 20 >
1 Kisha Daudi akakimbia kutoka Nayothi huko Rama akaenda na kumwambia Yonathani, “Nimefanya nini? Uovu wangu ni upi? Dhambi yangu ni ipi kwa baba yako, inayofanya atafute kuutoa uhai wangu.”
And he fled David (from Naioth *Q(k)*) in Ramah and he went and he said - before Jonathan what? have I done what? [is] iniquity my and what? [is] sin my before father your that [is] seeking life my.
2 Yonathani akamwambia Daudi, “La hasha; hautakufa. Baba yangu hafanyi jambo kubwa wala dogo bila kunijulisha. Kwa nini inamlazimu baba yangu anifiche jambo hili? La, siyo hivyo?”
And he said to him far be it not you will die here! (not he does *Q(K)*) father my anything great or anything small and not he uncovers ear my and why? will he hide father my from me the thing this there not [is] this.
3 Bado Daudi aliapa tena na akasema, “Baba yako anajua wazi kwamba nimepata kibali machoni pako. Pengine anasema, 'Asije Yonathani akajua jambo hili, labda atahuzunika.' Lakini kweli kama BWANA aishivyo, kama wewe uishivyo, kuna hatua moja tu kati yangu na mauti.”
And he swore an oath again David and he said certainly he knows father your that I have found favor in view your and he has said may not he know this Jonathan lest he should be grieved and but [by] [the] life of Yahweh and [by] [the] life of self your for about a step between me and between death.
4 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Lolote utakalosema, nitakufanyia.”
And he said Jonathan to David whatever it will say self your so I may do for you.
5 Daudi akamwambia Yonathani, “Kesho ni siku ya mwezi mpya, na inanibidi kukaa na kula pamoja na mfalme. Lakini acha niende, ili niweze kujificha katika shamba hadi siku ya tatu jioni.
And he said David to Jonathan here! a new moon [will be] tomorrow and I certainly I will sit with the king to eat and you will let go me and I will hide myself in the field until the evening third.
6 Baba yako akinikosa kabisa, ndipo utasema, 'Daudi aliniomba kwa msisitizo ruhusa aondoke kwenda mjini kwake Bethlehemu; kwa sababu huko ni kipindi cha utoaji wa dhabihu ya mwaka kwa familia yao yote.'
Certainly [if] he will miss me father your and you will say certainly he asked for himself from me David to run Beth-lehem city his for [the] sacrifice of the days [is] there for all the clan.
7 Kama atasema kuwa ni vyema, 'basi mtumishi wako atakuwa na amani. Lakini kama atakasirika sana, ndipo utajua kwamba ameamua kunitendea uovu.
If thus he will say good safety [belongs] to servant your and if certainly it will burn to him know that it has been determined harm from with him.
8 Kwa hiyo, umtendee wema mtumishi wako. Kwa maana umemweka mtumishi katika agano la BWANA pamoja na wewe. Lakini kama kuna dhambi ndani yangu, wewe mwenyewe uniuwe; maana kwa nini basi unipeleke kwa baba yako?”
And you will do covenant loyalty towards servant your for in [the] covenant of Yahweh you have brought servant your with you and if there in me [is] iniquity put to death me you and to father your why? this will you bring me.
9 Yonathani akasema, “La hasha! Ikiwa ninajua kwamba baba ameamua baya likupate, siwezi kukuambia?”
And he said Jonathan far be it to you that - if ever I will know that it has been determined harm from with father my to come on you and not it will I tell to you.
10 Ndipo Daudi akamwambia Yonathani, “Ni nani ataniambia ikiwa imetokea, baba yako akakujibu kwa ukali?”
And he said David to Jonathan who? will he tell to me or what? will he answer you father your hard.
11 Yonathani akamwambia Daudi, “Njoo, hebu twende huko shambani.” Ndipo wote wakaondoka kwenda shambani.
And he said Jonathan to David come! so we may go out the field and they went out [the] two of them the field.
12 Yonathani akamwambia Daudi, “Na BWANA, Mungu wa Israeli, awe shahidi. Kesho muda kama huu, nitakuwa nimemuuliza baba yangu, au siku ya tatu, tazama, ikiwa kutakuwa na jambo zuri upande wa Daudi; je, nisikutumie taarifa na kulidhihirisha kwako?
And he said Jonathan to David Yahweh [the] God of Israel that I will sound out father my about this time - tomorrow the third and there! good [is] to David and not? then will I send to you and I will uncover ear your.
13 Na kama ikimpendeza baba yangu akufanyie madhara, Basi BWANA ayafanye hayo kwa Yonathani na kuzidi ikiwa sitakujulisha jambo na kukupeleka mbali, ili kwamba uende kwa amani. Na BWANA awe pamoja nawe, kama alivyokuwa na baba yangu.
Thus may he do Yahweh to Jonathan and thus may he add if it will make good to father my harm on you and I will uncover ear your and I will send away you and you will go to peace and may he be Yahweh with you just as he has been with father my.
14 Kama bado nikiwa hai, hautanionesha uaminifu wa agano la BWANA, kwamba siwezi kufa?
And not if still I [am] alive and not you will do with me [the] covenant loyalty of Yahweh and not I will die.
15 Na usivunje kabisa uaminifu wako wa agano kati yako na nyumba yangu, hata wakati BWANA atakapowaodoa kila mmoja wa adui za Daudi kutoka uso wa dunia.”
And not you must cut off covenant loyalty your from with house my until perpetuity and not when cuts off Yahweh [the] enemies of David everyone from on [the] surface of the earth.
16 Basi Yonathani akafanya agano na nyumba ya Daudi na kusema, “Naye BWANA atawaondoa maadui wa Daudi.”
And he made Jonathan with [the] house of David and he will require Yahweh from [the] hand of [the] enemies of David.
17 Yonathani akamtaka Daudi aape tena kwa sababu ya upendo aliokuwa nao juu yake, kwa sababu alimpenda kama alivyopenda roho yake mwenyewe.
And he repeated Jonathan to make swear an oath David in love his him for [the] love of own self his he loved him.
18 Kisha Yonathani akamwambia Daudi, “Kesho ni siku ya mwezi mpya. Hautakuwapo, kwa sababu kiti chako kitakuwa wazi.
And he said to him Jonathan [will be] tomorrow a new moon and you will be missed if it will be empty seat your.
19 Utakapokuwa umekaa huko siku tatu, uende upesi hadi mahala ulipojificha mara ya kwanza, wakati shughuli ikifanyika, na ukaye karibu jiwe Ezeli.
And you will do three times you will come down exceedingly and you will come to the place where you hid yourself there on [the] day of the deed and you will stay beside the stone Ezel.
20 Nitatupa mishale mitatu pembeni mwa jiwe, kama vile ninalenga kitu fulani.
And I [the] three the arrows [its] side I will shoot to send [them] for myself to a target.
21 Kisha nitamtuma kijana wangu na kumwambia, 'Nenda utafute hiyo mishale.' Kama nitamwambia kijana hivi, 'Tazama, mishale iko upande huu wa kwako; kaichukue,” ndipo uje; maana hapo kutakuwa na usalama kwako na siyo madhara, kama BWANA aishivyo.
And there! I will send the lad go find the arrows certainly [if] I will say to the lad there! the arrows - [are] from you and hither fetch it - and come! for safety [belongs] to you and there not [is] anything [by] [the] life of Yahweh.
22 “Lakini kama nikimwambia kijana hivi, 'Tazama, mishale iko mbele yako,' ndipo utakapokwenda zako, maana BWANA ametaka uende zako.
And if thus I will say to the young man there! the arrows [are] from you and beyond go for he has sent away you Yahweh.
23 Kulingana na makubaliano ambayo mimi na wewe tumeongea, angalia, BWANA yupo kati yangu na wewe milele.'”
And the matter which we have spoken I and you here! Yahweh [will be] between me and between you until perpetuity.
24 Kwa hiyo Daudi akajificha mle shambani. Pindi mwezi ulipoandama, mfalme aliketi chini ale chakula.
And he hid himself David in the field and it was the new moon and he sat down the king (to *Q(K)*) the food to eat.
25 Mfalme alikaa juu ya kiti chake, kama kawaida kwenye kiti karibu na ukuta. Yonathani alisimama wima, na Abneri alikaa ubavuni mwa Sauli. Lakini nafasi ya Daudi ilikuwa wazi.
And he sat down the king on seat his as time - on time to [the] seat of the wall and he arose Jonathan and he sat down Abner from [the] side of Saul and it was empty [the] place of David.
26 Hata hivyo Sauli hakusema kitu siku hiyo, kwa sababu alifikiri, “Kuna jambo limempata Daudi. Hayuko safi; hakika hayuko safi.”
And not he spoke Saul anything on the day that for he said [is] an accident it not [is] clean he for not clean.
27 Lakini siku ya pili, siku moja baada ya mwandamo wa mwezi, bado nafasi ya Daudi ilikuwa tupu. Ndipo Sauli akamuuliza Yonathani mwanaye, “Kwa nini mwana wa Yese hakuja kwenye chakula, jana na hata leo?”
And it was from [the] next day of the new moon second and it was empty [the] place of David. And he said Saul to Jonathan son his why? not has he come [the] son of Jesse both yesterday as well as this day to the food.
28 Yonathani akamjibu Sauli, “Daudi aliomba kwangu ruhusa kwa dhati ili aende Bethlehemu.
And he answered Jonathan Saul certainly he asked for himself David from with me to Beth-lehem.
29 Alisema, 'Tafadhali niruhusu niende. Maana familia yetu wanayo dhabihu huko mjini, na kaka yangu ameniagiza niwe huko. Basi kama nimepata kibali machoni pako, tafadhali niruhusu niende nikawaone kaka zangu.' Hakuja kwenye meza ya mfalme kwa sababu hii.”
And he said let go me please for a sacrifice of [the] clan [belongs] to us in the city and he he has commanded to me brother my and therefore if I have found favor in view your let me slip away please so I may see brothers my there-fore not he has come to [the] table of the king.
30 Ndipo hasira ya Sauli iliwaka juu ya Yonathani, na akamwambia, “Wee mwana wa mwanamke mkaidi na muasi! Wadhani kwamba sijui kuwa umemchagua Mwana wa Yese kwa ajili ya aibu yako, na kwa aibu ya uchi wa mama yako?
And it burned [the] anger of Saul on Jonathan and he said to him O son of perverse [woman] of rebelliousness ¿ not do I know that [are] choosing you [the] son of Jesse to own shame your and to [the] shame of [the] nakedness of mother your.
31 Kwa kuwa mwana wa Yese anaishi duniani, siyo wewe wala ufalme wako utakaoimarika. Sasa basi, tuma watu wamlete kwangu, kwa sababu inampasa kufa.”
For all the days which [the] son of Jesse he lives on the earth not you will be established you and kingdom your and therefore send and fetch him to me for [is] a son of death he.
32 Yonathani akamjibu Sauli baba yake, “Kwa sababu gani inampasa kuuwawa? Amefanya nini?”
And he answered Jonathan Saul father his and he said to him why? will he be put to death what? has he done.
33 Ndipo Sauli akamtupia mkuki apate kumuua. Kwa hiyo Yonatani akatambua kwamba baba yake alinuia kumuua Daudi.
And he threw Saul the spear on him to strike him and he knew Jonathan that it had been determined it from with father his to kill David.
34 Yonathani alitoka mezani akiwa na hasira kali bila kula chakula siku ya pili ya mwezi, kwa sababu alimhuzunikia Daudi, na kwa sababu baba yake amemwaibisha.
And he arose Jonathan from with the table in [the] heat of anger and not he ate on [the] day of the new moon second food for he was grieved concerning David for he had put to shame him father his.
35 Ikawa asubuhi, Yonathani akaenda huko shambani kama walivyoahidiana na Daudi, akiwa pamoja na kijana wake.
And it was in the morning and he went out Jonathan the field to [the] appointed time of David and a lad small [was] with him.
36 Akamwambia yule kijana wake, “Kimbia utafute ile mishale niliyoitupa.” Na kijana alikimbia, akatupa mshale mwingine mbele yake.
And he said to lad his run find please the arrows which I [am] about to shoot the lad he ran and he he shot the arrow to make [it] pass beyond him.
37 Kijana alipofika katika eneo ambapo mshale ulitua, ule alioutuma Yonathani, akamwita tena kijana, na kusema, “Huo mshale hauko mbele yako?”
And he came the lad to [the] place of the arrow which he had shot Jonathan and he called out Jonathan after the lad and he said ¿ not [is] the arrow from you and beyond.
38 Kisha Yonathani akamwita yule kijana, “Upesi, harakisha, usikawie!” Hivyo kijana wa Yonathani akaikusanya mishale na kurudi kwa bwana wake.
And he called out Jonathan after the lad quickly make haste! may not you delay and he picked up [the] lad of Jonathan (the arrows *Q(K)*) and he came to master his.
39 Lakini huyo kijana hakujua lolote. Ni Yonathani na Daudi tu ndio walijua habari yenyewe.
And the lad not he knew anything only Jonathan and David they knew the matter.
40 Yonathani akampa kijana wake silaha na kumwambia, “Nenda, uzipeleke mjini.”
And he gave Jonathan weapons his to the lad who [belonged] to him and he said to him go take [them] the city.
41 Punde tu kijana alipoondoka, Daudi akasimama kutokea upande wa kusini, akiwa amelala kifudifudi, akainama mara tatu. Walibusiana wao kwa wao na wote wakalia kwa pamoja, Daudi akilia zaidi.
The lad he went and David he arose from beside the south and he fell to face his [the] ground towards and he bowed down three times and they kissed - each friend his and they wept for each friend his until David he did great things.
42 Yonathani akamwambia Daudi, “Nenda kwa amani, kwa sababu wote tumeapa kwa jina la BWANA na tulisema, 'BWANA awe kati yangu na wewe, na awe kati ya uzao wangu na uzao wako, milele.'” Kisha Daudi alisimama na akaondoka, na Yonathani akarudi mjini.
And he said Jonathan to David go to peace that we have sworn an oath [the] two of us we by [the] name of Yahweh saying Yahweh he will be - between me and between you and between offspring my and between offspring your until perpetuity. And he arose and he went and Jonathan he went the city.