< 1 Samweli 2 >
1 Hana aliomba akasema, “moyo wangu wamtukuza BWANA. Pembe yangu imejulikana katika BWANA. Kinywa changu kinatamba dhidi ya maadui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
Mon cœur s'est affermi dans le Seigneur, ma force s'est relevée en mon Dieu, ma bouche s'est dilatée contre mes ennemis; je me suis réjouie, parce que vous m'avez sauvée.
2 Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA, kwa kuwa hakuna mwingine zaidi yako; hakuna mwamba kama Mungu wetu.
Car nul n'est saint comme le Seigneur, nul n'est juste comme mon Dieu, nul n'est saint, hormis vous.
3 Msijivune sana hivyo kwa kiburi; vinywa vyenu visitoke majivuno. Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa; yeye huyapima matendo kwa mizani.
Ne vous glorifiez pas, ne dites point de paroles superbes; que nul mot résonnant ne sorte de votre bouche, parce que le Seigneur est le Dieu des sciences, et que Dieu prépare ses desseins.
4 Pinde za mashujaa zimevunjika, bali wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi.
L'arc des puissants a été énervé, et les faibles se sont revêtus de force.
5 Wale walio na shibe ya kutosha wamejikodisha ili wapate chakula; wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Hata yule aliye kuwa tasa amezaa watoto saba, bali mwanamke mwenye watoto wengi amenyong'onyea.
Ceux qui regorgeaient de biens ont été humiliés, et les pauvres n'ont pas eu de regards pour la terre, parce que la stérile a enfanté sept fois, et que celle qui avait beaucoup d'enfants a perdu sa fécondité.
6 BWANA huua na huuisha. Hushusha kuzimu na huleta tena juu. (Sheol )
Le Seigneur distribue la mort et la vie; il conduit aux enfers et il en ramène. (Sheol )
7 BWANA humfanya maskini, na yeye ndiye humtajirisha mtu. Yeye hudhili, lakini pia hukweza
Le Seigneur appauvrit et il enrichit; il abaisse et il élève;
8 Yeye humwinua juu maskini toka mavumbini: Huwainua wahitaji toka jalalani na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwarithisha kiti cha enzi cha utukufu. Kwa kuwa nguzo za dunia ni za BWANA na ameukalisha ulimwengu juu yake.
Il tire l'indigent de la poussière et le mendiant de la fange, pour les faire asseoir parmi les puissants du peuple, et leur donner en héritage un trône de gloire;
9 Yeye atazilinda nyayo za watu wake waaminifu, bali waovu watanyamazishwa gizani, kwa maana hakuna atayeshinda kwa nguvu zake.
Il accomplit les vœux des suppliants; il bénit les années du juste, tandis que l'homme, par sa propre force, ne peut rien.
10 Wale wampingao BWANA watavunjwa vipande vipande; atawapiga radi kutokea mbinguni. BWANA atahukumu miisho ya dunia; atampa nguvu mfalme wake na kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake.”
Le Seigneur réduit à la faiblesse son adversaire; Le Seigneur est remonté aux cieux; il a fait retentir son tonnerre, il jugera jusqu'aux extrémités de la terre. Il donne à nos rois leur puissance, et il élèvera la force de son Christ.
11 Nndipo Elikana akenda Rama, nyumbani kwake. Na yule mtoto akamtumikia BWANA machoni pa Eli, kuhani.
Après cela, elle laissa l'enfant devant le Seigneur, et elle retourna en Armathaïm. Cependant, l'enfant était employé au service du Seigneur, devant le prêtre Héli.
12 Basi, watoto wa Eli walikuwa wakorofi. Wao hawakumheshimu BWANA.
Et les fils d'Héli le prêtre étaient des enfants de pestilence, ne connaissant pas le Seigneur.
13 Desturi ya makuhani na watu ilikuwa kwamba endapo mtu yeyote ametoa dhabihu, mtumishi wa kuhani angekuja akiwa na uma wa meno matatu mkononi mwake, nyama ilipokuwa inatokoswa.
Or, tel était le droit du prêtre: quand quelqu'un du peuple venait sacrifier, le serviteur du prêtre arrivait aussitôt que les chairs étaient cuites, tenant à la main une fourchette.
14 Naye angeutia uma huo sufuriani, au birikani au chomboni au chunguni; nyama yote ambayo ingeinuliwa na uma huo ingetwaliwa na kuhani mwenyewe. Ndivyo walivyofanya huko Shilo kwa Waisraeli wote waliokwenda huko.
Il la plongeait dans la grande marmite, de terre ou d'airain, et tout ce que saisissait la fourchette était pour le prêtre. Voilà ce qui se faisait à l'égard de tous ceux d'Israël qui venaient en Silo sacrifier au Seigneur.
15 Tena, kabla ya kuteketeza mafuta, mtumishi wa kuhani alikuja, na kumwambia aliyekuwa akitoa dhabihu, “Tenga nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani; kwa sababu hataikubali ile ya kutokosa kutoka kwako, bali tu ile mbichi.”
Et avant que l'on brûlât la graisse, en odeur de suavité pour le Seigneur, le serviteur du prêtre accourait, et disait à l'homme qui offrait le sacrifice Donne-nous de la chair pour que le prêtre la fasse rôtir, et nous ne te prendrons pas de chair bouillie dans la marmite.
16 Ikiwa mtu atamwambia, “Wachome mafuta kwanza, na kisha uchukue kiasi utakacho.” Ndipo angesema, “Hapana, utanipatia sasa hivi; la sivyo; Nitaichukua kwa lazima.”
A quoi l'homme venu pour sacrifier répondait: Laisse-nous d'abord brûler la graisse, comme il convient, et tu prendras pour toi tous les morceaux que ton âme désire. Mais il disait: Non, donne-les-moi tout de suite, ou je les prendrai de force.
17 Dhambi ya vijana hawa ilikuwa mbaya sana mbele za BWANA, kwa sababu waliidharau dhabihu ya BWANA.
Le péché des fils du prêtre était très grand devant le Seigneur, parce qu'ils méprisaient le sacrifice du Seigneur.
18 Lakini Samweli alimtumikia BWANA akiwa mdogo akivaa nguo ya naivera ya kitani.
Cependant, Samuel était employé au service du Seigneur, et l'enfant était revêtu d'un éphod de lin.
19 Kila mwaka mama yake alimtengenezea kanzu dogo na kumletea, wakati wakija na mmewe kutoa dhabihu ya kila mwaka.
Sa mère lui fit en outre un petit manteau double, et elle le lui apporta le jour de la fête, lorsqu'elle monta avec son mari pour faire le sacrifice de la saison.
20 Eli aliwabariki Elikana na mke wake na kusema, “BWANA akupatie watoto zaidi kwa mwanamke huyu kwa sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa BWANA.” Baadaye walirudi nyumbani kwao.
Et Héli bénit Elcana et sa femme, disant: Que le Seigneur, en te donnant des enfants de cette femme, te récompense du serviteur que tu lui as consacré. Et l'homme retourna à sa maison.
21 BWANA alimsaidia tena Hana, akawa amebeba mimba nyingine. Akazaa watoto watatu wa kiume na wa kike wawili. Wakati huo huo mtoto Samweli akakua akiwa mbele za BWANA.
Et le Seigneur visita Anne; elle enfanta encore trois fils et deux filles; et Samuel avait grandi devant le Seigneur.
22 Basi Eli alikuwa mzee sana, akayasikia yote ambayo watoto wake walikuwa wakiwafanyia Waisraeli wote, na jinsi walivyotembea na mwanamke aliyekuwa akitumika katika lango la hema ya kukutania.
Or, Héli était très avancé en âge; il apprit ce que faisaient ses fils aux fils d'Israël.
23 Akawaambia, “Kwa nini mnafanya mambo hayo? Kwa maana nasikia matendo yenu maovu kutoka kwa watu hawa wote.”
Et il leur dit: Pourquoi faites-vous les choses que j'ai ouïes de la bouche de tout le peuple du Seigneur?
24 Sivyo hivyo, watoto wangu, maana hii ninayoisikia siyo taarifa njema. Mnawakosesha watu wa BWANA.
Ne les faites plus, enfants, car la nouvelle que j'ai entendue n'est pas une bonne nouvelle; ne vous conduisez plus ainsi; car ce ne sont pas de bonnes nouvelles quand on me rapporte que vous empêchez le peuple de servir Dieu.
25 “Kama mtu mmoja akimkosea mwenzake, Mungu atamhukumu; Lakini mtu akimkosea BWANA, ni nani atakayemtetea mtu huyo?” Lakini hawakuitii sauti ya baba yao, sababu BWANA alinuia kuwaua.
Si un homme pèche contre un homme, on adressera pour lui des prières au Seigneur; mais s'il a péché contre le Seigneur, qui priera pour lui? Mais ils n'écoutèrent pas la voix de leur père, parce que le Seigneur voulait les détruire.
26 Yule mtoto Samweli aliongezeka umri, na kupata kibali kwa BWANA na kwa watu pia.
Et le jeune Samuel marchait; il était bon avec le Seigneur et avec les hommes.
27 Kisha mtu wa Mungu akamwendea Eli na kumwambia, “BWANA asema, 'Je, sikujifunua mwenyewe kwa nyumba ya baba zako, walipokuwa Misri utumwani nyumbani mwa Farao?
Alors, un homme de Dieu vint auprès d'Héli, et dit: Voici ce que dit le Seigneur: Je me suis révélé à la famille de ton père quand elle était encore en Égypte, esclave dans la maison du Pharaon.
28 Mimi nilimchagua yeye kutoka makabila yote ya Israeli awe kuhani wangu, apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba, na kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu. Niliwapa nyumba ya baba zako dhabihu zote za wana wa Israeli zilizotolewa kwa moto.
J'ai choisi la famille de ton père, parmi les puissants d'Israël, pour me servir, monter à l'autel, brûler de l'encens et porter l'éphod. J'ai donné à la famille de ton père, pour sa nourriture, une part de tout ce que les fils d'Israël offrent en sacrifice.
29 Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu na sadaka ambazo ninazitaka mahali ninapoishi? Kwanini unawaheshimu watoto wako kuliko mimi, kwa kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka ya watu wangu Israeli?'
Pourquoi donc as-tu regardé d'un œil avide mes victimes et mon encens? Pourquoi donc as-tu donné plus de gloire à tes fils qu'à moi, au point qu'ils consomment avant moi les prémices de toutes les victimes d'Israël?
30 Maana, BWANA, Mungu wa Isareli, asema, niliahidi kwamba nyumba yako, na nyumba ya baba yako, yawapasa kwenda mbele zangu milele,' Lakini sasa BWANA asema. 'Mambo haya yapishe mbali. nami nisifanye hivi, maana nitawaheshimu wanaoniheshimu, bali wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.
A cause de cela, voici ce que dit le Seigneur Dieu d'Israël: J'avais dit: Ta famille, la famille de ton père se tiendra près de moi à toujours. Et maintenant, le Seigneur dit: Non, parce que je glorifierai ceux qui me glorifient, et que celui qui me méprise sera méprisé.
31 Tazama, siku zinakuja nitakapoondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako, ili kwamba pasije kuwepo mtu mzee katika nyumba yako.
Voilà que les temps approchent où j'exterminerai ta race, la postérité de ton père.
32 Nawe utalitazama hangaiko katika makao yangu. Ingawa Israeli watapewa jambo jema, hapatakuwapo tena mtu yeyote mzee katika nyumba yako.
Il n'y aura plus jamais en ma maison un seul vieillard de ta race.
33 Yeyote miongoni mwenu nisiye mwondoa kutoka madhabahuni pangu, Nitasababisha macho yenu yaanguke, na ita nitasababisha huzuni maishani mwenu. Wanaume wote waliozaliwa katika familia yako watakufa.
Et celui des tiens que je n'exterminerai pas en l'éloignant de mon autel, ses yeux s'éteindront, sa vie se consumera; et tout le reste périra par le glaive des hommes.
34 Hii ndiyo itakuwa ishara kwako ambayo itawaijia watoto wako wakiume wawili, juu ya Hofni na Finehasi: Wote wawili watakufa siku moja.
Or, voilà pour toi le signe, et il viendra sur tes deux fils, Ophni et Phinéès: ils mourront tous les deux le même jour.
35 Nami nitamwinua juu kuhani wangu mwaminifu atakaye fanya kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu. Nami nitamjengea nyumba madhubuti; naye atakwenda mbele ya mfalme wangu mbarikiwa milele.
Je susciterai alors pour moi un prêtre fidèle, qui pratiquera tout ce qui est en mon cœur et en mon âme; j'édifierai pour lui une maison fidèle, et il passera devant mon Christ, à jamais.
36 Kila mmoja aliyebakia nyumbani mwako atakuja na kusujudu mbele ya mtu huyo, akiomba kipande cha fedha na mkate mmoja, naye atasema, “Tafadhali uniajiri katika moja ya nafasi za kuhani ili niweze kula kipande cha mkate'”'
Celui de ta famille qui survivra, viendra se prosterner devant lui pour une obole, et dira: Admets-moi à l'une de tes distributions sacerdotales, afin que je mange du pain.