< 1 Samweli 18 >
1 Daudi alipokuwa amemaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ilishikana na roho ya Daudi, na Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe.
E sucedeu que, acabando ele de falar com Saul, a alma de Jonathan se ligou com a alma de David: e Jonathan o amou, como à sua própria alma.
2 Sauli akamweka kazini Daudi siku hiyo, hakumwacha arudi nyumbani kwa baba yake.
E Saul naquele dia o tomou, e não lhe permitiu que tornasse para casa de seu pai.
3 Kisha Yonathani na Daudi wakafanya makubaliano ya urafiki kwa sababu Yonathani alimenda kama roho yake mwenyewe.
E Jonathan e David fizeram aliança: porque Jonathan o amava como à sua própria alma.
4 Yonathani akavua kanzu aliyokuwa amevaa na kumpa Daudi, akampa na vazi lake la kivita, pamoja na upanga, upinde, na mshipi.
E Jonathan se despojou da capa que trazia sobre si, e a deu a David, como também os seus vestidos, até a sua espada, e o seu arco, e o seu cinto.
5 Daudi alikwenda popote ambapo Sauli alimtuma, naye alifanikiwa. Sauli akamteua Daudi awe mkuu wa wapiganaji. Jambo hili lilipendeza machoni pa watu na katika macho ya watumishi wa Sauli.
E saía David aonde quer que Saul o enviava, e conduzia-se com prudência, e Saul o pôs sobre a gente de guerra: e era aceito aos olhos de todo o povo, e até aos olhos dos servos de Saul.
6 Wakati wanarudi nyumbani kutoka kuwapiga Wafilisti, wanawake walitoka miji yote ya Israeli, wakiimba na kucheza, ili kukutana na mfalme Sauli, wakiwa na matowazi, wenye furaha, na wakiwa na ala za muziki.
Sucedeu porém que, vindo eles, quando David voltava de ferir os philisteus, as mulheres de todas as cidades de Israel sairam ao encontro do rei Saul, cantando, e em danças, com adufes, com alegria, e com instrumentos de música.
7 Hao wanawake waliimba kwa kupokezana huku wakicheza; Wakiimba: “Sauli ameua maelfu yake, Na Daudi ameua makumi elfu yake.”
E as mulheres tangendo, se respondiam umas às outras, e diziam: Saul feriu os seus milhares, porém David os seus dez milhares.
8 Sauli alikasirika sana, na wimbo huu haukumpendeza. Naye akasema, “Wamemsifia Daudi juu ya makumi elfu, lakini wamenisifia melfu tu mimi! Atapata kitu gani zaidi isipokuwa ufalme?
Então Saul se indignou muito, e aquela palavra pareceu mal aos seus olhos, e disse: Dez milhares deram a David, e a mim somente milhares; na verdade, que lhe falta, senão só o reino?
9 Kuanzia siku hiyo na kuendelea, Sauli alimuangalia Daudi kwa mashaka.
E, desde aquele dia em diante, Saul tinha David em suspeita.
10 Kesho yake yule roho ya ubaya kutoka kwa Mungu ikamwingia Sauli kwa nguvu. Naye akawa anafanya kama mwendawazimu nyumbani mwake. Hivyo Daudi akapiga kifaa chake, kama alivyofanya kila siku. Sauli alikuwa na mkuki wake mkononi.
E aconteceu ao outro dia, que o mau espírito da parte de Deus se apoderou de Saul, e profetizava no meio da casa: e David tangia com a sua mão, como de dia em dia: Saul porém tinha na mão uma lança.
11 Sauli akatupa mkuki wake, kwani alifikiri, “Nitampigilia ukutani.” Lakini Daudi mara mbili aliepa uwepo wa Sauli.
E Saul atirou com a lança, dizendo: Encravarei a David na parede. Porém David se desviou dele por duas vezes.
12 Sauli alimwogopa Daudi, kwa sababu BWANA alikuwa pamoja naye, lakini hakuwa na Sauli tena.
E temia Saul a David, porque o Senhor era com ele e se tinha retirado de Saul.
13 Hivyo Sauli alimuondoa Daudi mbele yake na akamteua kuwa kamanda wa kikosi cha askari elfu moja. Kwa namna hii David alitoka na kuingia mbele ya watu.
Pelo que Saul o desviou de si, e o pôs por chefe de mil: e saía e entrava diante do povo.
14 Daudi alikuwa akistawi kwa mambo yake yote, maana BWANA alikuwa pamoja naye.
E David se conduzia com prudência em todos os seus caminhos, e o Senhor era com ele.
15 Sauli alipoona kwamba Daudi anastawi, alimwogopa.
Vendo então Saul que tão prudentemente se conduzia, tinha receio dele.
16 Lakini Israeli yote na Yuda walimpenda Daudi, maana alitoka na kuingia mbele yao.
Porém todo o Israel e Judá amava a David, porquanto saía e entrava diante deles.
17 Kisha Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa ni binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupatia awe mke wako. Ila tu uwe jasiri kwa ajili yangu na upigane vita vya BWANA.” Maana Sauli alifikiri, “Usije mkono wangu ukawa juu yake, ila acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
Pelo que Saul disse a David: Eis que Merab, minha filha mais velha, te darei por mulher; sê-me somente filho valoroso, e guerreia as guerras do Senhor (porque Saul dizia consigo: Não seja contra ele a minha mão, mas sim a dos philisteus).
18 Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, na maisha yangu yana nini, au hata maisha ya familia ya baba yangu katika Israeli, kiasi cha kuwa mkwe wa mfalme?” 1 Samweli 18-19-19
Mas David disse a Saul: Quem sou eu, e qual é a minha vida e a família de meu pai em Israel, para vir a ser genro do rei?
19 Lakini wakati ambao Merabu, binti Sauli, ilipasa kuwa ameolewa na Daudi, aliozwa kwa Adrieli Mmeholathi.
Sucedeu, porém, que ao tempo que Merab, filha de Saul, devia ser dada a David, ela foi dada por mulher a Adriel, meholathita.
20 Lakini Mikali, binti Sauli, alimpenda Daudi. Na watu walimwambia Sauli, na jambo hilo likampendeza.
Mas Michal, a outra filha de Saul amava a David: o que, sendo anunciado a Saul, pareceu isto bom aos seus olhos.
21 Ndipo Sauli akafikiri, “Nitampatia huyu awe mke wake, ili uwe mtego kwake, na hivyo mkono wa Wafilisti pengine uwe juu yake.” Kwa hiyo Sauli akamwambia Daudi mara ya pili, “Wewe utakuwa mkwe wangu.”
E Saul disse: Eu lha darei, para que lhe sirva de laço, e para que a mão dos philisteus venha a ser contra ele. Pelo que Saul disse a David: Com a outra serás hoje meu genro.
22 Sauli akawaamuru watumishi wake, “Ongeeni na Daudi kwa njia ya siri, na mseme, 'Tazama, mfalme anakufurahia, na watumishi wake wote wanakupenda. Sasa basi, uwe mkwe wa mfalme.'”
E Saul deu ordem aos seus servos: falai em segredo a David, dizendo: Eis que o rei te está mui afeiçoado, e todos os seus servos te amam; agora, pois, consente em ser genro do rei.
23 Hivyo watumishi wa Sauli wakayasema maneno haya kwa Daudi. Na Daudi akasema, “Kwenu ninyi mnaona ni jambo dogo kuwa mkwe wa mfalme, mimi ni maskini, na heshima yangu ni ndogo.”
E os servos de Saul falaram todas estas palavras aos ouvidos de David. Então disse David: Parece-vos pouco aos vossos olhos ser genro do rei, sendo eu homem pobre e desprezível?
24 Watumishi wa Sauli wakarudisha kwake taarifa ya maneno ambayo Daudi aliyasema.
E os servos de Saul lhe anunciaram isto, dizendo: Foram tais as palavras que falou David.
25 Na Sauli akasema, “Hivi ndivyo mtakavyo mwambia Daudi, 'Mfalme haitaji mahari yoyote, isipokuwa govi mia moja za Wafilisti, ili ajilipize kisasi kwa adui wa mfalme.”' Basi Sauli alifikiri atamwangusha Daudi kwa mkono wa Wafilisti.
Então disse Saul: Assim direis a David: O rei não tem necessidade de dote, senão de cem prepúcios de philisteus, para se tomar vingança dos inimigos do rei. Porquanto Saul tentava fazer cair a David pela mão dos philisteus.
26 Watumishi wake walipomwambia maneno haya, yakamvutia Daudi awe mkwe wa mfalme.
E anunciaram os seus servos estas palavras a David, e este negócio pareceu bem aos olhos de David, de que fosse genro do rei: porém ainda os dias se não haviam cumprido.
27 Kabla siku hizo hazijapita, Daudi aliondoka na watu wake na kuwaua Wafilisti mia mbili. Daudi akazileta govi zao, na kumkadhi mfalme kulingana na idadi yake, ili aweze kufanyika mkwe wa mfalme. Kwa hiyo Sauli akamwoza Mikali, binti yake, awe mkewe.
Então David se levantou, e partiu ele com os seus homens, e feriram dentre os philisteus duzentos homens, e David trouxe os seus prepúcios, e os entregaram todos ao rei, para que fosse genro do rei: então Saul lhe deu por mulher a sua filha.
28 Basi Sauli aliona na kufahamu kwamba BWANA alikuwa pamoja na Daudi. Mikali, binti Sauli, akampenda Daudi.
E viu Saul, e notou que o Senhor era com David: e Michal, filha de Saul, o amava.
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi. Sauli akawa adui wa Daudi daima.
Então Saul temeu muito mais a David: e Saul foi todos os seus dias inimigo de David.
30 Ndipo wakuu wa Wafilisti wakajitokeza kwa ajili ya vita, na mara zote walipojitokeza Daudi alifanikiwa zaidi kuliko watumishi wote wa Sauli, hivyo jina lake likapata heshima kubwa.
E, saindo os príncipes dos philisteus, sucedeu que, saindo eles, David se conduziu mais prudentemente do que todos os servos de Saul: portanto o seu nome era mui estimado.