< 1 Samweli 18 >

1 Daudi alipokuwa amemaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ilishikana na roho ya Daudi, na Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe.
Kiedy przestał rozmawiać z Saulem, dusza Jonatana związała się z duszą Dawida i Jonatan umiłował go jak własną duszę.
2 Sauli akamweka kazini Daudi siku hiyo, hakumwacha arudi nyumbani kwa baba yake.
I Saul wziął go tego dnia, i nie pozwolił mu wrócić do domu swego ojca.
3 Kisha Yonathani na Daudi wakafanya makubaliano ya urafiki kwa sababu Yonathani alimenda kama roho yake mwenyewe.
A Jonatan zawarł z Dawidem przymierze, bo miłował go jak własną duszę.
4 Yonathani akavua kanzu aliyokuwa amevaa na kumpa Daudi, akampa na vazi lake la kivita, pamoja na upanga, upinde, na mshipi.
Jonatan zdjął płaszcz, który miał na sobie, dał go Dawidowi, podobnie jak swoje szaty – aż do miecza, łuku i pasa.
5 Daudi alikwenda popote ambapo Sauli alimtuma, naye alifanikiwa. Sauli akamteua Daudi awe mkuu wa wapiganaji. Jambo hili lilipendeza machoni pa watu na katika macho ya watumishi wa Sauli.
I Dawid wyruszał, dokądkolwiek Saul go posyłał, i postępował roztropnie. Saul ustanowił go więc nad wojownikami, a on zyskał przychylność w oczach całego ludu, a także w oczach sług Saula.
6 Wakati wanarudi nyumbani kutoka kuwapiga Wafilisti, wanawake walitoka miji yote ya Israeli, wakiimba na kucheza, ili kukutana na mfalme Sauli, wakiwa na matowazi, wenye furaha, na wakiwa na ala za muziki.
A gdy wracali, a Dawid [też] wracał po zabiciu Filistyna, kobiety ze wszystkich miast Izraela wyszły na spotkanie królowi Saulowi ze śpiewem, pląsami i radością – z bębnami i gęślami.
7 Hao wanawake waliimba kwa kupokezana huku wakicheza; Wakiimba: “Sauli ameua maelfu yake, Na Daudi ameua makumi elfu yake.”
Kobiety śpiewały na przemian, grały i mówiły: Saul pobił swoje tysiące, ale Dawid swoich dziesiątki tysięcy.
8 Sauli alikasirika sana, na wimbo huu haukumpendeza. Naye akasema, “Wamemsifia Daudi juu ya makumi elfu, lakini wamenisifia melfu tu mimi! Atapata kitu gani zaidi isipokuwa ufalme?
I Saul bardzo się rozgniewał, gdyż nie podobały mu się te słowa. Powiedział: Przyznali Dawidowi dziesiątki tysięcy, a mnie przyznali [tylko] tysiące. Czego mu brak? Tylko królestwa.
9 Kuanzia siku hiyo na kuendelea, Sauli alimuangalia Daudi kwa mashaka.
Od tego dnia Saul nieprzychylnie patrzył na Dawida.
10 Kesho yake yule roho ya ubaya kutoka kwa Mungu ikamwingia Sauli kwa nguvu. Naye akawa anafanya kama mwendawazimu nyumbani mwake. Hivyo Daudi akapiga kifaa chake, kama alivyofanya kila siku. Sauli alikuwa na mkuki wake mkononi.
Następnego dnia zły duch od Boga zstąpił na Saula i on prorokował pośrodku domu, a Dawid grał swą ręką [melodię] – jak przedtem. Saul zaś trzymał w ręku włócznię.
11 Sauli akatupa mkuki wake, kwani alifikiri, “Nitampigilia ukutani.” Lakini Daudi mara mbili aliepa uwepo wa Sauli.
I Saul rzucił włócznię, bo myślał: Przybiję Dawida do ściany. Lecz Dawid dwukrotnie się przed nim uchylił.
12 Sauli alimwogopa Daudi, kwa sababu BWANA alikuwa pamoja naye, lakini hakuwa na Sauli tena.
I Saul [zaczął] bać się Dawida, ponieważ PAN był z nim, a od Saula odstąpił.
13 Hivyo Sauli alimuondoa Daudi mbele yake na akamteua kuwa kamanda wa kikosi cha askari elfu moja. Kwa namna hii David alitoka na kuingia mbele ya watu.
Saul oddalił go więc od siebie i uczynił go dowódcą nad tysiącem, a on wyruszał i powracał przed ludem.
14 Daudi alikuwa akistawi kwa mambo yake yote, maana BWANA alikuwa pamoja naye.
We wszystkich swoich drogach Dawid postępował roztropnie, gdyż PAN [był] z nim.
15 Sauli alipoona kwamba Daudi anastawi, alimwogopa.
Gdy Saul widział, że tak bardzo roztropnie postępuje, bał się go.
16 Lakini Israeli yote na Yuda walimpenda Daudi, maana alitoka na kuingia mbele yao.
Lecz cały Izrael i Juda kochali Dawida, bo on wyruszał i powracał przed nimi.
17 Kisha Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa ni binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupatia awe mke wako. Ila tu uwe jasiri kwa ajili yangu na upigane vita vya BWANA.” Maana Sauli alifikiri, “Usije mkono wangu ukawa juu yake, ila acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
I Saul powiedział do Dawida: Oto moja najstarsza córka Merab. Dam ci ją za żonę, tylko bądź dla mnie dzielnym mężem i prowadź wojny PANA. Saul bowiem mówił sobie [tak]: Niech moja ręka go nie dosięgnie, ale niech go dosięgnie ręka Filistynów.
18 Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, na maisha yangu yana nini, au hata maisha ya familia ya baba yangu katika Israeli, kiasi cha kuwa mkwe wa mfalme?” 1 Samweli 18-19-19
Wtedy Dawid powiedział do Saula: Kim jestem i czym jest moje życie [lub] rodzina mojego ojca w Izraelu, żebym miał zostać zięciem króla?
19 Lakini wakati ambao Merabu, binti Sauli, ilipasa kuwa ameolewa na Daudi, aliozwa kwa Adrieli Mmeholathi.
Gdy jednak przyszedł czas oddania Dawidowi córki Saula, Merab, oddano ją za żonę Adrielowi z Mecholi.
20 Lakini Mikali, binti Sauli, alimpenda Daudi. Na watu walimwambia Sauli, na jambo hilo likampendeza.
Ale Mikal, córka Saula, pokochała Dawida. Gdy więc doniesiono o tym Saulowi, spodobało mu się [to].
21 Ndipo Sauli akafikiri, “Nitampatia huyu awe mke wake, ili uwe mtego kwake, na hivyo mkono wa Wafilisti pengine uwe juu yake.” Kwa hiyo Sauli akamwambia Daudi mara ya pili, “Wewe utakuwa mkwe wangu.”
I Saul powiedział: Dam mu ją, aby była dla niego sidłem i aby ręka Filistynów była na nim. Powiedział więc Saul do Dawida: Zostaniesz dzisiaj moim zięciem z moją drugą [córką].
22 Sauli akawaamuru watumishi wake, “Ongeeni na Daudi kwa njia ya siri, na mseme, 'Tazama, mfalme anakufurahia, na watumishi wake wote wanakupenda. Sasa basi, uwe mkwe wa mfalme.'”
Wtedy Saul nakazał swoim sługom: Powiedzcie do Dawida w tajemnicy: Oto król ma w tobie upodobanie i wszyscy jego słudzy kochają cię. Zostań więc teraz zięciem króla.
23 Hivyo watumishi wa Sauli wakayasema maneno haya kwa Daudi. Na Daudi akasema, “Kwenu ninyi mnaona ni jambo dogo kuwa mkwe wa mfalme, mimi ni maskini, na heshima yangu ni ndogo.”
Słudzy Saula powtórzyli te słowa do uszu Dawida, a Dawid odpowiedział: Czy wam się wydaje, że to błaha rzecz być zięciem króla? Jestem przecież człowiekiem ubogim i mało znaczącym.
24 Watumishi wa Sauli wakarudisha kwake taarifa ya maneno ambayo Daudi aliyasema.
Wtedy słudzy Saula oznajmili mu: Tak powiedział Dawid.
25 Na Sauli akasema, “Hivi ndivyo mtakavyo mwambia Daudi, 'Mfalme haitaji mahari yoyote, isipokuwa govi mia moja za Wafilisti, ili ajilipize kisasi kwa adui wa mfalme.”' Basi Sauli alifikiri atamwangusha Daudi kwa mkono wa Wafilisti.
Saul odpowiedział: Tak powiedzcie Dawidowi: Król nie chce innego wiana jak tylko sto napletków filistyńskich, aby się pomścić na swoich wrogach. Saul planował bowiem, że Dawid wpadnie w ręce Filistynów.
26 Watumishi wake walipomwambia maneno haya, yakamvutia Daudi awe mkwe wa mfalme.
Gdy jego słudzy powtórzyli te słowa Dawidowi, spodobało się to Dawidowi, że ma zostać zięciem króla. A te dni jeszcze się nie wypełniły.
27 Kabla siku hizo hazijapita, Daudi aliondoka na watu wake na kuwaua Wafilisti mia mbili. Daudi akazileta govi zao, na kumkadhi mfalme kulingana na idadi yake, ili aweze kufanyika mkwe wa mfalme. Kwa hiyo Sauli akamwoza Mikali, binti yake, awe mkewe.
Wstał więc Dawid i poszedł, on i jego ludzie, i zabił spośród Filistynów dwustu mężczyzn. Potem Dawid przyniósł ich napletki i oddał je w pełnej liczbie królowi, aby zostać zięciem króla. I Saul dał mu swą córkę Mikal za żonę.
28 Basi Sauli aliona na kufahamu kwamba BWANA alikuwa pamoja na Daudi. Mikali, binti Sauli, akampenda Daudi.
A gdy Saul zobaczył i przekonał się, że PAN jest z Dawidem i że jego córka Mikal go kocha;
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi. Sauli akawa adui wa Daudi daima.
Tym bardziej Saul obawiał się Dawida. I Saul stał się wrogiem Dawida na zawsze.
30 Ndipo wakuu wa Wafilisti wakajitokeza kwa ajili ya vita, na mara zote walipojitokeza Daudi alifanikiwa zaidi kuliko watumishi wote wa Sauli, hivyo jina lake likapata heshima kubwa.
A książęta Filistynów robili wypady. A przy każdym ich wypadzie Dawid postępował roztropniej niż wszyscy słudzy Saula, tak że jego imię stało się bardzo sławne.

< 1 Samweli 18 >