< 1 Samweli 18 >

1 Daudi alipokuwa amemaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ilishikana na roho ya Daudi, na Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe.
A la suite de son entretien avec Saül, le cœur de Jonathan s’attacha à David, de sorte qu’il l’aima comme lui-même.
2 Sauli akamweka kazini Daudi siku hiyo, hakumwacha arudi nyumbani kwa baba yake.
Saül le retint ce jour même et ne le laissa pas retourner chez son père.
3 Kisha Yonathani na Daudi wakafanya makubaliano ya urafiki kwa sababu Yonathani alimenda kama roho yake mwenyewe.
Pour Jonathan, il fit un pacte avec David, parce qu’il l’aimait comme lui-même;
4 Yonathani akavua kanzu aliyokuwa amevaa na kumpa Daudi, akampa na vazi lake la kivita, pamoja na upanga, upinde, na mshipi.
il se dépouilla du manteau qu’il portait et le donna à David, ainsi que son costume, et jusqu’à son épée, son arc et sa ceinture.
5 Daudi alikwenda popote ambapo Sauli alimtuma, naye alifanikiwa. Sauli akamteua Daudi awe mkuu wa wapiganaji. Jambo hili lilipendeza machoni pa watu na katika macho ya watumishi wa Sauli.
David fit diverses expéditions, réussit partout où l’envoyait Saül, et celui-ci le mit à la tête des guerriers; et il se fit aimer de tout le peuple, comme des serviteurs de Saül.
6 Wakati wanarudi nyumbani kutoka kuwapiga Wafilisti, wanawake walitoka miji yote ya Israeli, wakiimba na kucheza, ili kukutana na mfalme Sauli, wakiwa na matowazi, wenye furaha, na wakiwa na ala za muziki.
Or, quand on rentra, comme David revenait vainqueur du Philistin, les femmes s’avancèrent de toutes les villes d’Israël au-devant du roi Saül, chantant et dansant au son des gais tambourins et des triangles.
7 Hao wanawake waliimba kwa kupokezana huku wakicheza; Wakiimba: “Sauli ameua maelfu yake, Na Daudi ameua makumi elfu yake.”
Et elles chantaient en chœur dans leurs jeux, en disant: "Saül a battu ses mille, Et David ses myriades!"
8 Sauli alikasirika sana, na wimbo huu haukumpendeza. Naye akasema, “Wamemsifia Daudi juu ya makumi elfu, lakini wamenisifia melfu tu mimi! Atapata kitu gani zaidi isipokuwa ufalme?
Saül s’en fâcha fort, trouvant la chose déplaisante; et il dit: "Elles donnent les myriades à David et à moi les mille: il ne lui manque plus que la royauté!"
9 Kuanzia siku hiyo na kuendelea, Sauli alimuangalia Daudi kwa mashaka.
Saül regarda David de mauvais œil, à partir de ce jour.
10 Kesho yake yule roho ya ubaya kutoka kwa Mungu ikamwingia Sauli kwa nguvu. Naye akawa anafanya kama mwendawazimu nyumbani mwake. Hivyo Daudi akapiga kifaa chake, kama alivyofanya kila siku. Sauli alikuwa na mkuki wake mkononi.
Le lendemain, le mauvais esprit envoyé par Dieu s’empara de Saül, et il allait dans la maison, en proie au délire, tandis que David touchait de ses doigts l’instrument, comme il l’avait fait précédemment; et Saül avait sa lance en main.
11 Sauli akatupa mkuki wake, kwani alifikiri, “Nitampigilia ukutani.” Lakini Daudi mara mbili aliepa uwepo wa Sauli.
Saül brandit la lance en disant: "Je clouerai David au mur"; mais David l’évita deux fois.
12 Sauli alimwogopa Daudi, kwa sababu BWANA alikuwa pamoja naye, lakini hakuwa na Sauli tena.
Alors Saül eut peur de David, parce que le Seigneur était avec lui, tandis qu’il avait abandonné Saül
13 Hivyo Sauli alimuondoa Daudi mbele yake na akamteua kuwa kamanda wa kikosi cha askari elfu moja. Kwa namna hii David alitoka na kuingia mbele ya watu.
Saül l’éloigna donc d’auprès de lui et il en fit un chef de mille à son service, de sorte qu’il dut aller et venir à la tête du peuple.
14 Daudi alikuwa akistawi kwa mambo yake yote, maana BWANA alikuwa pamoja naye.
David avait du succès dans toutes ses expéditions, car l’Eternel était avec lui;
15 Sauli alipoona kwamba Daudi anastawi, alimwogopa.
et Saül, voyant combien il réussissait, en fut effrayé.
16 Lakini Israeli yote na Yuda walimpenda Daudi, maana alitoka na kuingia mbele yao.
Mais tout Israël et Juda aimaient David, parce qu’il allait et venait à leur tête.
17 Kisha Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa ni binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupatia awe mke wako. Ila tu uwe jasiri kwa ajili yangu na upigane vita vya BWANA.” Maana Sauli alifikiri, “Usije mkono wangu ukawa juu yake, ila acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
Saül dit à David "Vois, ma fille aînée, Mérab, c’est elle que je veux te donner pour femme, sois-moi seulement un brave guerrier, combattant les combats du Seigneur." (Il ne faut pas que ma main le frappe, pensait Saül, mais plutôt celle des Philistins.)
18 Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, na maisha yangu yana nini, au hata maisha ya familia ya baba yangu katika Israeli, kiasi cha kuwa mkwe wa mfalme?” 1 Samweli 18-19-19
David répondit à Saül: "Qui suis-je, quelle est mon existence, que vaut ma famille en Israël, pour que je devienne gendre du roi?…"
19 Lakini wakati ambao Merabu, binti Sauli, ilipasa kuwa ameolewa na Daudi, aliozwa kwa Adrieli Mmeholathi.
Or, à l’époque où Mérab, fille de Saül, devait être donnée à David, elle fut donnée en mariage à Adriel de Mehola.
20 Lakini Mikali, binti Sauli, alimpenda Daudi. Na watu walimwambia Sauli, na jambo hilo likampendeza.
Mikhal, fille de Saül, conçut de l’amour pour David; Saül en fut informé, et la chose lui plut;
21 Ndipo Sauli akafikiri, “Nitampatia huyu awe mke wake, ili uwe mtego kwake, na hivyo mkono wa Wafilisti pengine uwe juu yake.” Kwa hiyo Sauli akamwambia Daudi mara ya pili, “Wewe utakuwa mkwe wangu.”
car Saül se disait "Je la lui donnerai, afin qu’elle soit un piège pour lui et qu’il tombe sous la main des Philistins." Il dit donc à David: "C’Est par la seconde que tu deviendras mon gendre à présent."
22 Sauli akawaamuru watumishi wake, “Ongeeni na Daudi kwa njia ya siri, na mseme, 'Tazama, mfalme anakufurahia, na watumishi wake wote wanakupenda. Sasa basi, uwe mkwe wa mfalme.'”
Et Saül ordonna à ses serviteurs de dire à David en confidence: "Vois, le roi a de l’affection pour toi, tous ses serviteurs t’aiment; deviens donc gendre du roi."
23 Hivyo watumishi wa Sauli wakayasema maneno haya kwa Daudi. Na Daudi akasema, “Kwenu ninyi mnaona ni jambo dogo kuwa mkwe wa mfalme, mimi ni maskini, na heshima yangu ni ndogo.”
Les serviteurs de Saül parlèrent dans ce sens à l’oreille de David, mais il répondit: "Est-ce peu de chose à vos yeux que de m’allier au roi, moi pauvre et chétif?"
24 Watumishi wa Sauli wakarudisha kwake taarifa ya maneno ambayo Daudi aliyasema.
Les serviteurs de Saül le lui rapportèrent, en disant: "Voilà ce qu’a répondu David."
25 Na Sauli akasema, “Hivi ndivyo mtakavyo mwambia Daudi, 'Mfalme haitaji mahari yoyote, isipokuwa govi mia moja za Wafilisti, ili ajilipize kisasi kwa adui wa mfalme.”' Basi Sauli alifikiri atamwangusha Daudi kwa mkono wa Wafilisti.
Et Saül dit: "Vous direz à David: Le roi n’exige d’autre douaire que cent prépuces de Philistins comme châtiment de ces ennemis du roi." (Saül avait pour but de faire tomber David aux mains des Philistins.)
26 Watumishi wake walipomwambia maneno haya, yakamvutia Daudi awe mkwe wa mfalme.
Ses serviteurs rapportèrent cette parole à David, à qui il plut de devenir le gendre du roi. Et le temps n’était pas encore écoulé,
27 Kabla siku hizo hazijapita, Daudi aliondoka na watu wake na kuwaua Wafilisti mia mbili. Daudi akazileta govi zao, na kumkadhi mfalme kulingana na idadi yake, ili aweze kufanyika mkwe wa mfalme. Kwa hiyo Sauli akamwoza Mikali, binti yake, awe mkewe.
que David se mit en campagne, partit avec ses hommes, défit deux cents Philistins et rapporta leurs prépuces, qu’on livra intégralement au roi, afin qu’il devînt son gendre; et Saül lui donna pour femme sa fille Mikhal.
28 Basi Sauli aliona na kufahamu kwamba BWANA alikuwa pamoja na Daudi. Mikali, binti Sauli, akampenda Daudi.
Saül vit et reconnut que Dieu était avec David, qu’il était aimé de Mikhal, sa fille.
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi. Sauli akawa adui wa Daudi daima.
Et plus que jamais Saül redouta David, et il lui fut hostile sa vie durant.
30 Ndipo wakuu wa Wafilisti wakajitokeza kwa ajili ya vita, na mara zote walipojitokeza Daudi alifanikiwa zaidi kuliko watumishi wote wa Sauli, hivyo jina lake likapata heshima kubwa.
Les chefs des Philistins firent mainte incursion; mais au cours de leurs expéditions, David eut constamment du succès, plus que tous les serviteurs de Saül. Et son nom fut en grand honneur.

< 1 Samweli 18 >