< 1 Samweli 18 >
1 Daudi alipokuwa amemaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ilishikana na roho ya Daudi, na Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe.
Lorsque David eut achevé de parler à Saül, l’âme de Jonathas s’attacha à l’âme de David, et Jonathas l’aima comme son âme.
2 Sauli akamweka kazini Daudi siku hiyo, hakumwacha arudi nyumbani kwa baba yake.
Ce même jour, Saül prit David, et ne le laissa pas retourner dans la maison de son père.
3 Kisha Yonathani na Daudi wakafanya makubaliano ya urafiki kwa sababu Yonathani alimenda kama roho yake mwenyewe.
Et Jonathas fit alliance avec David, parce qu’il l’aimait comme son âme.
4 Yonathani akavua kanzu aliyokuwa amevaa na kumpa Daudi, akampa na vazi lake la kivita, pamoja na upanga, upinde, na mshipi.
Jonathas se dépouilla du manteau qu’il portait et le donna à David, ainsi que son armure, jusqu’à son épée, jusqu’à son arc et jusqu’à sa ceinture.
5 Daudi alikwenda popote ambapo Sauli alimtuma, naye alifanikiwa. Sauli akamteua Daudi awe mkuu wa wapiganaji. Jambo hili lilipendeza machoni pa watu na katika macho ya watumishi wa Sauli.
Quand David sortait, partout où l’envoyait Saül, il réussissait; Saül le mit à la tête des gens de guerre, et il plaisait à tout le peuple, même aux serviteurs du roi.
6 Wakati wanarudi nyumbani kutoka kuwapiga Wafilisti, wanawake walitoka miji yote ya Israeli, wakiimba na kucheza, ili kukutana na mfalme Sauli, wakiwa na matowazi, wenye furaha, na wakiwa na ala za muziki.
Quand ils firent leur entrée, lorsque David revint après avoir tué le Philistin, les femmes sortirent de toutes les villes d’Israël, en chantant et en dansant, au-devant du roi Saül, avec joie, au son des tambourins et des harpes.
7 Hao wanawake waliimba kwa kupokezana huku wakicheza; Wakiimba: “Sauli ameua maelfu yake, Na Daudi ameua makumi elfu yake.”
Les femmes, les danseuses, se répondaient et disaient: Saül a tué ses mille, et David ses dix mille.
8 Sauli alikasirika sana, na wimbo huu haukumpendeza. Naye akasema, “Wamemsifia Daudi juu ya makumi elfu, lakini wamenisifia melfu tu mimi! Atapata kitu gani zaidi isipokuwa ufalme?
Saül fut très irrité, et ces paroles lui déplurent: il dit: « On donne dix mille à David, et à moi on donne les mille! Il ne lui manque plus que la royauté. »
9 Kuanzia siku hiyo na kuendelea, Sauli alimuangalia Daudi kwa mashaka.
Et Saül voyait David de mauvais œil, à partir de ce jour.
10 Kesho yake yule roho ya ubaya kutoka kwa Mungu ikamwingia Sauli kwa nguvu. Naye akawa anafanya kama mwendawazimu nyumbani mwake. Hivyo Daudi akapiga kifaa chake, kama alivyofanya kila siku. Sauli alikuwa na mkuki wake mkononi.
Le lendemain, un mauvais esprit envoyé de Dieu fondit sur Saül, et il eut des transports au milieu de sa maison. David jouait de la harpe, comme les autres jours, et Saül avait sa lance à la main.
11 Sauli akatupa mkuki wake, kwani alifikiri, “Nitampigilia ukutani.” Lakini Daudi mara mbili aliepa uwepo wa Sauli.
Saül brandit sa lance, disant en lui-même: « Je frapperai David et la paroi »; mais David se détourna de devant lui par deux fois.
12 Sauli alimwogopa Daudi, kwa sababu BWANA alikuwa pamoja naye, lakini hakuwa na Sauli tena.
Saül craignait David, car Yahweh était avec David et s’était retiré de Saül, —
13 Hivyo Sauli alimuondoa Daudi mbele yake na akamteua kuwa kamanda wa kikosi cha askari elfu moja. Kwa namna hii David alitoka na kuingia mbele ya watu.
et Saül l’éloigna de sa personne, et il l’établit chef de mille hommes; et David sortait et rentrait devant le peuple.
14 Daudi alikuwa akistawi kwa mambo yake yote, maana BWANA alikuwa pamoja naye.
David se montrait habile dans toutes ses entreprises, et Yahweh était avec lui.
15 Sauli alipoona kwamba Daudi anastawi, alimwogopa.
Saül, voyant qu’il était très habile, avait peur de lui;
16 Lakini Israeli yote na Yuda walimpenda Daudi, maana alitoka na kuingia mbele yao.
mais tout Israël et Juda aimaient David, parce qu’il sortait et rentrait devant eux.
17 Kisha Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa ni binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupatia awe mke wako. Ila tu uwe jasiri kwa ajili yangu na upigane vita vya BWANA.” Maana Sauli alifikiri, “Usije mkono wangu ukawa juu yake, ila acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
Saül dit à David: « Voici que je te donnerai pour femme ma fille aînée Mérob; seulement montre-toi plein de vaillance et soutiens les guerres de Yahweh. » Or Saül se disait: « Que ma main ne soit pas sur lui, mais que sur lui soit la main des Philistins! »
18 Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, na maisha yangu yana nini, au hata maisha ya familia ya baba yangu katika Israeli, kiasi cha kuwa mkwe wa mfalme?” 1 Samweli 18-19-19
David répondit à Saül: « Qui suis-je et qu’est-ce que ma vie, qu’est-ce que la famille de mon père en Israël, pour que je devienne le gendre du roi? »
19 Lakini wakati ambao Merabu, binti Sauli, ilipasa kuwa ameolewa na Daudi, aliozwa kwa Adrieli Mmeholathi.
Mais, au moment de donner Mérob, fille de Saül, à David, on la donna pour femme à Hadriel de Molathi.
20 Lakini Mikali, binti Sauli, alimpenda Daudi. Na watu walimwambia Sauli, na jambo hilo likampendeza.
Michol, fille de Saül, aima David. On en informa Saül, et cela lui plut.
21 Ndipo Sauli akafikiri, “Nitampatia huyu awe mke wake, ili uwe mtego kwake, na hivyo mkono wa Wafilisti pengine uwe juu yake.” Kwa hiyo Sauli akamwambia Daudi mara ya pili, “Wewe utakuwa mkwe wangu.”
Saül se disait: « Je la lui donnerai, afin qu’elle soit pour lui un piège, et que la main des Philistins soit sur lui. » Et Saül dit à David, pour la seconde fois: « Tu vas aujourd’hui devenir mon gendre. »
22 Sauli akawaamuru watumishi wake, “Ongeeni na Daudi kwa njia ya siri, na mseme, 'Tazama, mfalme anakufurahia, na watumishi wake wote wanakupenda. Sasa basi, uwe mkwe wa mfalme.'”
Et Saül donna cet ordre à ses serviteurs: « Parlez confidentiellement à David, et dites-lui: Le roi t’a pris en affection, et tous ses serviteurs t’aiment; sois donc maintenant le gendre du roi. »
23 Hivyo watumishi wa Sauli wakayasema maneno haya kwa Daudi. Na Daudi akasema, “Kwenu ninyi mnaona ni jambo dogo kuwa mkwe wa mfalme, mimi ni maskini, na heshima yangu ni ndogo.”
Les serviteurs de Saül dirent ces paroles aux oreilles de David, et David répondit: « Est-ce peu de chose à vos yeux que de devenir le gendre du roi? Moi, je suis un homme pauvre et d’humble origine. »
24 Watumishi wa Sauli wakarudisha kwake taarifa ya maneno ambayo Daudi aliyasema.
Les serviteurs de Saül lui firent rapport en ces termes: « David a tenu ce langage. »
25 Na Sauli akasema, “Hivi ndivyo mtakavyo mwambia Daudi, 'Mfalme haitaji mahari yoyote, isipokuwa govi mia moja za Wafilisti, ili ajilipize kisasi kwa adui wa mfalme.”' Basi Sauli alifikiri atamwangusha Daudi kwa mkono wa Wafilisti.
Saül dit: « Vous parlerez ainsi à David: Le roi ne demande aucune dot, mais cent prépuces de Philistins, pour être vengé des ennemis du roi. » Saül pensait faire ainsi tomber David dans la main des Philistins.
26 Watumishi wake walipomwambia maneno haya, yakamvutia Daudi awe mkwe wa mfalme.
Les serviteurs de Saül rapportèrent ces paroles à David, et cela plut à David, à savoir devenir le gendre du roi.
27 Kabla siku hizo hazijapita, Daudi aliondoka na watu wake na kuwaua Wafilisti mia mbili. Daudi akazileta govi zao, na kumkadhi mfalme kulingana na idadi yake, ili aweze kufanyika mkwe wa mfalme. Kwa hiyo Sauli akamwoza Mikali, binti yake, awe mkewe.
Les jours n’étaient pas accomplis que David, s’étant levé, partit avec ses gens et tua aux Philistins deux cents hommes; et David apporta leurs prépuces et en remit au roi le nombre complet, afin de devenir son gendre. Alors Saül lui donna pour femme sa fille Michol.
28 Basi Sauli aliona na kufahamu kwamba BWANA alikuwa pamoja na Daudi. Mikali, binti Sauli, akampenda Daudi.
Saül vit et comprit que Yahweh était avec David; et Michol, fille de Saül, aimait David.
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi. Sauli akawa adui wa Daudi daima.
Et Saül craignit David de plus en plus, et Saül fut hostile à David tous les jours.
30 Ndipo wakuu wa Wafilisti wakajitokeza kwa ajili ya vita, na mara zote walipojitokeza Daudi alifanikiwa zaidi kuliko watumishi wote wa Sauli, hivyo jina lake likapata heshima kubwa.
Les princes des Philistins faisaient des excursions et, chaque fois qu’ils sortaient, David par son habileté remportait plus de succès que tous les serviteurs de Saül; et son nom devint très célèbre.