< 1 Samweli 18 >
1 Daudi alipokuwa amemaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ilishikana na roho ya Daudi, na Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe.
And it was when finished he to speak to Saul and [the] self of Jonathan it was bound with [the] self of David (and he loved him *Q(k)*) Jonathan like own self his.
2 Sauli akamweka kazini Daudi siku hiyo, hakumwacha arudi nyumbani kwa baba yake.
And he took him Saul on the day that and not he permitted him to return [the] house of father his.
3 Kisha Yonathani na Daudi wakafanya makubaliano ya urafiki kwa sababu Yonathani alimenda kama roho yake mwenyewe.
And he made Jonathan and David a covenant in love his him like own self his.
4 Yonathani akavua kanzu aliyokuwa amevaa na kumpa Daudi, akampa na vazi lake la kivita, pamoja na upanga, upinde, na mshipi.
And he stripped himself Jonathan the robe which [was] on him and he gave it to David and garments his and to sword his and to bow his and to belt his.
5 Daudi alikwenda popote ambapo Sauli alimtuma, naye alifanikiwa. Sauli akamteua Daudi awe mkuu wa wapiganaji. Jambo hili lilipendeza machoni pa watu na katika macho ya watumishi wa Sauli.
And he went out David in every where he sent him Saul he prospered and he appointed him Saul over [the] men of war and it was good in [the] eyes of all the people and also in [the] eyes of [the] servants of Saul.
6 Wakati wanarudi nyumbani kutoka kuwapiga Wafilisti, wanawake walitoka miji yote ya Israeli, wakiimba na kucheza, ili kukutana na mfalme Sauli, wakiwa na matowazi, wenye furaha, na wakiwa na ala za muziki.
And it was when came they when returned David from striking down the Philistine and they came out the women from all [the] cities of Israel (to sing *Q(k)*) and the dancing to meet Saul the king with tambourines with joy and with three-stringed instruments.
7 Hao wanawake waliimba kwa kupokezana huku wakicheza; Wakiimba: “Sauli ameua maelfu yake, Na Daudi ameua makumi elfu yake.”
And they sang the women who were playing and they said he has struck down Saul (thousands his *Q(K)*) and David ten thousands his.
8 Sauli alikasirika sana, na wimbo huu haukumpendeza. Naye akasema, “Wamemsifia Daudi juu ya makumi elfu, lakini wamenisifia melfu tu mimi! Atapata kitu gani zaidi isipokuwa ufalme?
And it burned to Saul exceedingly and it was displeasing in view his the matter this and he said they have ascribed to David ten thousands and to me they have ascribed the thousands and yet for him only the kingship.
9 Kuanzia siku hiyo na kuendelea, Sauli alimuangalia Daudi kwa mashaka.
And he was Saul (looking at *Q(K)*) David from the day that and onwards.
10 Kesho yake yule roho ya ubaya kutoka kwa Mungu ikamwingia Sauli kwa nguvu. Naye akawa anafanya kama mwendawazimu nyumbani mwake. Hivyo Daudi akapiga kifaa chake, kama alivyofanya kila siku. Sauli alikuwa na mkuki wake mkononi.
And it was from [the] next day and it rushed a spirit of God - evil - to Saul and he prophesied in [the] midst of the house and David [was] playing an instrument with hand his as a day - in a day and the spear [was] in [the] hand of Saul.
11 Sauli akatupa mkuki wake, kwani alifikiri, “Nitampigilia ukutani.” Lakini Daudi mara mbili aliepa uwepo wa Sauli.
And he threw Saul the spear and he said I will strike David and the wall and he went around David from before him two times.
12 Sauli alimwogopa Daudi, kwa sababu BWANA alikuwa pamoja naye, lakini hakuwa na Sauli tena.
And he was afraid Saul from to before David for he was Yahweh with him and from with Saul he had turned aside.
13 Hivyo Sauli alimuondoa Daudi mbele yake na akamteua kuwa kamanda wa kikosi cha askari elfu moja. Kwa namna hii David alitoka na kuingia mbele ya watu.
And he removed him Saul from with him and he appointed him for himself a commander of a thousand and he went out and he came before the people.
14 Daudi alikuwa akistawi kwa mambo yake yote, maana BWANA alikuwa pamoja naye.
And he was David to all (ways his *Q(K)*) successful and Yahweh [was] with him.
15 Sauli alipoona kwamba Daudi anastawi, alimwogopa.
And he saw Saul that he [was] successful exceedingly and he was afraid of him.
16 Lakini Israeli yote na Yuda walimpenda Daudi, maana alitoka na kuingia mbele yao.
And all Israel and Judah [were] loving David for he [was] going out and [was] coming before them.
17 Kisha Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa ni binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupatia awe mke wako. Ila tu uwe jasiri kwa ajili yangu na upigane vita vya BWANA.” Maana Sauli alifikiri, “Usije mkono wangu ukawa juu yake, ila acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
And he said Saul to David here! daughter my elder Merab her I will give to you to a wife only become of me a son of strength and fight [the] battles of Yahweh and Saul he said may not it be hand my on him and let it be on him [the] hand of [the] Philistines.
18 Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, na maisha yangu yana nini, au hata maisha ya familia ya baba yangu katika Israeli, kiasi cha kuwa mkwe wa mfalme?” 1 Samweli 18-19-19
And he said David to Saul who? [am] I and who? [are] kinsfolk my [the] clan of father my in Israel that I will be a son-in-law of the king.
19 Lakini wakati ambao Merabu, binti Sauli, ilipasa kuwa ameolewa na Daudi, aliozwa kwa Adrieli Mmeholathi.
And it was at [the] time gave Merab [the] daughter of Saul to David and she she was given to Adriel the Meholathite to a wife.
20 Lakini Mikali, binti Sauli, alimpenda Daudi. Na watu walimwambia Sauli, na jambo hilo likampendeza.
And she loved Michal [the] daughter of Saul David and people told to Saul and it was pleasing the matter in view his.
21 Ndipo Sauli akafikiri, “Nitampatia huyu awe mke wake, ili uwe mtego kwake, na hivyo mkono wa Wafilisti pengine uwe juu yake.” Kwa hiyo Sauli akamwambia Daudi mara ya pili, “Wewe utakuwa mkwe wangu.”
And he said Saul I will give her to him so she may become for him a snare so it may be on him [the] hand of [the] Philistines and he said Saul to David in two [times] you will be a son-in-law to me this day.
22 Sauli akawaamuru watumishi wake, “Ongeeni na Daudi kwa njia ya siri, na mseme, 'Tazama, mfalme anakufurahia, na watumishi wake wote wanakupenda. Sasa basi, uwe mkwe wa mfalme.'”
And he commanded Saul (servants his *Q(K)*) speak to David in secrecy saying here! he delights in you the king and all servants his they love you and therefore be son-in-law to the king.
23 Hivyo watumishi wa Sauli wakayasema maneno haya kwa Daudi. Na Daudi akasema, “Kwenu ninyi mnaona ni jambo dogo kuwa mkwe wa mfalme, mimi ni maskini, na heshima yangu ni ndogo.”
And they spoke [the] servants of Saul in [the] ears of David the words these and he said David ¿ trifling in view your [is] to be son-in-law to the king and I [am] a man poor and lightly esteemed.
24 Watumishi wa Sauli wakarudisha kwake taarifa ya maneno ambayo Daudi aliyasema.
And they told [the] servants of Saul to him saying according to the words these he spoke David.
25 Na Sauli akasema, “Hivi ndivyo mtakavyo mwambia Daudi, 'Mfalme haitaji mahari yoyote, isipokuwa govi mia moja za Wafilisti, ili ajilipize kisasi kwa adui wa mfalme.”' Basi Sauli alifikiri atamwangusha Daudi kwa mkono wa Wafilisti.
And he said Saul thus you will say to David not delight [belongs] to the king in bride-price for for a hundred foreskins of Philistines to avenge himself on [the] enemies of the king and Saul he planned to make fall David by [the] hand of [the] Philistines.
26 Watumishi wake walipomwambia maneno haya, yakamvutia Daudi awe mkwe wa mfalme.
And they told servants his to David the words these and it was pleasing the matter in [the] eyes of David to be son-in-law to the king and not they were completed the days.
27 Kabla siku hizo hazijapita, Daudi aliondoka na watu wake na kuwaua Wafilisti mia mbili. Daudi akazileta govi zao, na kumkadhi mfalme kulingana na idadi yake, ili aweze kufanyika mkwe wa mfalme. Kwa hiyo Sauli akamwoza Mikali, binti yake, awe mkewe.
And he arose David and he went - he and men his and he struck down among the Philistines two hundred man and he brought David foreskins their and people gave in full them to the king to be son-in-law to the king and he gave to him Saul Michal daughter his to a wife.
28 Basi Sauli aliona na kufahamu kwamba BWANA alikuwa pamoja na Daudi. Mikali, binti Sauli, akampenda Daudi.
And he saw Saul and he knew that Yahweh [was] with David and Michal [the] daughter of Saul she loved him.
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi. Sauli akawa adui wa Daudi daima.
And he increased Saul to be afraid of David again and he was Saul an enemy David all the days.
30 Ndipo wakuu wa Wafilisti wakajitokeza kwa ajili ya vita, na mara zote walipojitokeza Daudi alifanikiwa zaidi kuliko watumishi wote wa Sauli, hivyo jina lake likapata heshima kubwa.
And they went out [the] commanders of [the] Philistines and it was - as often as went out they he was successful David more than all [the] servants of Saul and it was esteemed name his exceedingly.