< 1 Samweli 18 >

1 Daudi alipokuwa amemaliza kuongea na Sauli, roho ya Yonathani ilishikana na roho ya Daudi, na Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe.
And it came to pass, when he had made an end of speaking to Saul, that the soul of Jonathan was knit with the soul of David, and Jonathan loved him as his own soul.
2 Sauli akamweka kazini Daudi siku hiyo, hakumwacha arudi nyumbani kwa baba yake.
And Saul took him that day, and would no more let him go home to his father's house.
3 Kisha Yonathani na Daudi wakafanya makubaliano ya urafiki kwa sababu Yonathani alimenda kama roho yake mwenyewe.
Then Jonathan and David made a covenant, because he loved him as his own soul.
4 Yonathani akavua kanzu aliyokuwa amevaa na kumpa Daudi, akampa na vazi lake la kivita, pamoja na upanga, upinde, na mshipi.
And Jonathan stripped himself of the robe that was upon him, and gave it to David, and his apparel, even to his sword, and to his bow, and to his belt.
5 Daudi alikwenda popote ambapo Sauli alimtuma, naye alifanikiwa. Sauli akamteua Daudi awe mkuu wa wapiganaji. Jambo hili lilipendeza machoni pa watu na katika macho ya watumishi wa Sauli.
And David went out wherever Saul sent him, and behaved himself wisely. And Saul set him over the men of war, and it was good in the sight of all the people, and also in the sight of Saul's servants.
6 Wakati wanarudi nyumbani kutoka kuwapiga Wafilisti, wanawake walitoka miji yote ya Israeli, wakiimba na kucheza, ili kukutana na mfalme Sauli, wakiwa na matowazi, wenye furaha, na wakiwa na ala za muziki.
And it came to pass as they came, when David returned from the slaughter of the Philistine, that the women came out of all the cities of Israel, singing and dancing, to meet king Saul, with timbrels, with joy, and with instruments of music.
7 Hao wanawake waliimba kwa kupokezana huku wakicheza; Wakiimba: “Sauli ameua maelfu yake, Na Daudi ameua makumi elfu yake.”
And the women sang one to another as they played, and said, Saul has slain his thousands, and David his ten thousands.
8 Sauli alikasirika sana, na wimbo huu haukumpendeza. Naye akasema, “Wamemsifia Daudi juu ya makumi elfu, lakini wamenisifia melfu tu mimi! Atapata kitu gani zaidi isipokuwa ufalme?
And Saul was very angry, and this saying displeased him, and he said, They have ascribed to David ten thousands, and to me they have ascribed but thousands, and what can he have more but the kingdom?
9 Kuanzia siku hiyo na kuendelea, Sauli alimuangalia Daudi kwa mashaka.
And Saul eyed David from that day and forward.
10 Kesho yake yule roho ya ubaya kutoka kwa Mungu ikamwingia Sauli kwa nguvu. Naye akawa anafanya kama mwendawazimu nyumbani mwake. Hivyo Daudi akapiga kifaa chake, kama alivyofanya kila siku. Sauli alikuwa na mkuki wake mkononi.
And it came to pass on the morrow, that an evil spirit from God came mightily upon Saul, and he prophesied in the midst of the house. And David played with his hand, as he did day by day, and Saul had his spear in his hand.
11 Sauli akatupa mkuki wake, kwani alifikiri, “Nitampigilia ukutani.” Lakini Daudi mara mbili aliepa uwepo wa Sauli.
And Saul cast the spear, for he said, I will smite David even to the wall. And David turned away from his presence twice.
12 Sauli alimwogopa Daudi, kwa sababu BWANA alikuwa pamoja naye, lakini hakuwa na Sauli tena.
And Saul was afraid of David because Jehovah was with him, and was departed from Saul.
13 Hivyo Sauli alimuondoa Daudi mbele yake na akamteua kuwa kamanda wa kikosi cha askari elfu moja. Kwa namna hii David alitoka na kuingia mbele ya watu.
Therefore Saul removed him from him, and made him his captain over a thousand, and he went out and came in before the people.
14 Daudi alikuwa akistawi kwa mambo yake yote, maana BWANA alikuwa pamoja naye.
And David behaved himself wisely in all his ways, and Jehovah was with him.
15 Sauli alipoona kwamba Daudi anastawi, alimwogopa.
And when Saul saw that he behaved himself very wisely, he was afraid of him.
16 Lakini Israeli yote na Yuda walimpenda Daudi, maana alitoka na kuingia mbele yao.
But all Israel and Judah loved David, for he went out and came in before them.
17 Kisha Sauli akamwambia Daudi, “Huyu hapa ni binti yangu mkubwa Merabu. Nitakupatia awe mke wako. Ila tu uwe jasiri kwa ajili yangu na upigane vita vya BWANA.” Maana Sauli alifikiri, “Usije mkono wangu ukawa juu yake, ila acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake.”
And Saul said to David, Behold, my elder daughter Merab, I will give her to thee for a wife. Only be thou valiant for me, and fight Jehovah's battles. For Saul said, Let not my hand be upon him, but let the hand of the Philistines be upon him.
18 Daudi akamwambia Sauli, “Mimi ni nani, na maisha yangu yana nini, au hata maisha ya familia ya baba yangu katika Israeli, kiasi cha kuwa mkwe wa mfalme?” 1 Samweli 18-19-19
And David said to Saul, Who am I, and what is my life, or my father's family in Israel, that I should be son-in-law to the king?
19 Lakini wakati ambao Merabu, binti Sauli, ilipasa kuwa ameolewa na Daudi, aliozwa kwa Adrieli Mmeholathi.
But it came to pass at the time when Merab, Saul's daughter, should have been given to David, that she was given to Adriel the Meholathite to wife.
20 Lakini Mikali, binti Sauli, alimpenda Daudi. Na watu walimwambia Sauli, na jambo hilo likampendeza.
And Michal, Saul's daughter, loved David, and they told Saul, and the thing pleased him.
21 Ndipo Sauli akafikiri, “Nitampatia huyu awe mke wake, ili uwe mtego kwake, na hivyo mkono wa Wafilisti pengine uwe juu yake.” Kwa hiyo Sauli akamwambia Daudi mara ya pili, “Wewe utakuwa mkwe wangu.”
And Saul said, I will give him her, that she may be a snare to him, and that the hand of the Philistines may be against him. Therefore Saul said to David, Thou shall this day be my son-in-law a second time.
22 Sauli akawaamuru watumishi wake, “Ongeeni na Daudi kwa njia ya siri, na mseme, 'Tazama, mfalme anakufurahia, na watumishi wake wote wanakupenda. Sasa basi, uwe mkwe wa mfalme.'”
And Saul commanded his servants, saying, Converse with David secretly, and say, Behold, the king has delight in thee, and all his servants love thee. Now therefore be the king's son-in-law.
23 Hivyo watumishi wa Sauli wakayasema maneno haya kwa Daudi. Na Daudi akasema, “Kwenu ninyi mnaona ni jambo dogo kuwa mkwe wa mfalme, mimi ni maskini, na heshima yangu ni ndogo.”
And Saul's servants spoke those words in the ears of David. And David said, Does it seem to you a light thing to be the king's son-in-law, seeing that I am a poor man, and lightly esteemed?
24 Watumishi wa Sauli wakarudisha kwake taarifa ya maneno ambayo Daudi aliyasema.
And the servants of Saul told him, saying, On this manner David spoke.
25 Na Sauli akasema, “Hivi ndivyo mtakavyo mwambia Daudi, 'Mfalme haitaji mahari yoyote, isipokuwa govi mia moja za Wafilisti, ili ajilipize kisasi kwa adui wa mfalme.”' Basi Sauli alifikiri atamwangusha Daudi kwa mkono wa Wafilisti.
And Saul said, Thus shall ye say to David, The king does not desire any dowry, but a hundred foreskins of the Philistines, to be avenged of the king's enemies. Now Saul thought to make David fall by the hand of the Philistines.
26 Watumishi wake walipomwambia maneno haya, yakamvutia Daudi awe mkwe wa mfalme.
And when his servants told David these words, it pleased David well to be the king's son-in-law. And the days were not expired.
27 Kabla siku hizo hazijapita, Daudi aliondoka na watu wake na kuwaua Wafilisti mia mbili. Daudi akazileta govi zao, na kumkadhi mfalme kulingana na idadi yake, ili aweze kufanyika mkwe wa mfalme. Kwa hiyo Sauli akamwoza Mikali, binti yake, awe mkewe.
And David arose and went, he and his men, and killed of the Philistines two hundred men. And David brought their foreskins, and they gave them in full number to the king, that he might be the king's son-in-law. And Saul gave him Michal his daughter to wife.
28 Basi Sauli aliona na kufahamu kwamba BWANA alikuwa pamoja na Daudi. Mikali, binti Sauli, akampenda Daudi.
And Saul saw and knew that Jehovah was with David, and Michal, Saul's daughter, loved him.
29 Sauli akazidi kumwogopa Daudi. Sauli akawa adui wa Daudi daima.
And Saul was yet the more afraid of David, and Saul was David's enemy continually.
30 Ndipo wakuu wa Wafilisti wakajitokeza kwa ajili ya vita, na mara zote walipojitokeza Daudi alifanikiwa zaidi kuliko watumishi wote wa Sauli, hivyo jina lake likapata heshima kubwa.
Then the rulers of the Philistines went forth, and it came to pass, as often as they went forth, that David behaved himself more wisely than all the servants of Saul, so that his name was very precious.

< 1 Samweli 18 >