< 1 Samweli 17 >

1 Basi Wafilisti walikusanya majeshi yao kwa ajili ya vita. Walikusanyika huko Soko, iliyoko Yuda. Nao wakapiga kambi kati ya Soko na Aseka katika Efesdamimu.
The Philistines gathered their army [to fight the Israeli army]. They gathered together near Socoh, in the area where the descendants of Judah lived. They set up their tents at Ephes-Dammim, which is between Socoh and Azekah.
2 Sauli na watu wa Israeli alijikusanya na kuweka kambi katika bonde la Ela, na wakapanga vita kukutana na Wafilisti.
Saul gathered the Israeli army near Elah Valley, and they set up their tents. Then they all took their places, ready to fight the Philistines.
3 Wafilisti walisimama juu ya mlima upande mmoja, na Iraeli nao walisimama juu ya mlima upande mwingine wakitenganishwa na bonde kati yao.
So the Philistine and Israeli armies faced each other. They were on two hills, with a valley between them.
4 Mtu mmoja mwenye nguvu akatoka katika kambi ya Wafilisti, mtu huyo aliitwa Goliathi wa Gathi, kimo chake mikono sita na shubiri moja.
Then Goliath, from Gath [city], came out from the Philistine camp. He was a champion warrior/soldier. He was (over 9 feet/3 meters) tall.
5 Alikuwa na chepeo ya shaba kichwani mwake, na alivaa dirii ya chuma. Hiyo dirii ilikuwa na uzito wa shekeli elfu hamsini za shaba.
He wore a helmet made of bronze [to protect his head], and he wore a coat made of metal plates [to protect his body]. The coat weighed (125 pounds/56 kg.).
6 Alikuwa na mabampa ya shaba kwenye miguu yake na mkuki wa shaba katikati ya mabega yake.
He wore bronze guards/protectors on his legs. He had a long bronze dagger fastened on his back.
7 Ule mpini wa mkuki wake ulikuwa mkubwa, wenye kamba iliyo na kitanzi kwa ajili ya kuutupia kama kamba ya sindano ya mfumaji. Kichwa cha mkuki wake kilikuwa na uzito wa shekeli mia sita za chuma. Aliyembebea ngao alitembea mbele yake.
He also had a big spear. It had a cord on it to enable him to throw it better (OR, which was as thick as a weaver’s beam). The tip of the spear was made of iron and weighed (15 pounds/almost 7 kg.). A soldier carrying a huge shield walked in front of him.
8 Alisimama akayapigia kelele majeshi ya Israeli, “Kwa nini mmekuja na mmejipanga kwa ajili ya vita? Mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli? Chagueni mtu kutoka kwenu ateremke na kuja kwangu.
Goliath stood there and shouted to the Israeli army, “Why are you all lined up for battle? I am the great Philistine [soldier], and I think [RHQ] you are [merely] Saul’s slaves. Choose one man to fight for all of you, and send him down here to me!
9 Kama anaweza kupigana nami na kuniua, hapo ndipo tutakuwa watumwa wenu. Lakini kama nitamshinda na kumuua, basi mtakuwa watumwa wetu na kututumikia.”
If he fights with me and kills me, then my fellow Philistines will all be your slaves. But if I defeat him and kill him, then you Israelis will all be our slaves.
10 Mfilisti huyo akasema tena, “Leo ninayapa changamoto majeshi ya Israeli. Mnipe mtu ili tuweze kupigana naye.”
I defy/challenge you men of the Israeli army. Send me a man who will fight with me!”
11 Sauli na Israeli wote waliposikia alichosema Mfilisti huyo, walikata tamaa na kuogopa sana.
When Saul and all the Israeli soldiers heard that, they were extremely terrified [DOU].
12 Basi Daudi alikuwa mwana wa Mwefraimu wa Bethtelehemu ya Yuda, aliyeitwa Yese. Naye alikuwa na watoto wanane wa kiume. Yese alikuwa mtu mzee katika siku za Sauli, mwenye umri mkubwa kati ya watu.
David was the son of Jesse. Jesse was from the clan of Ephrath. He lived in Bethlehem, in the area where the descendants of Judah lived. Jesse had eight sons. When Saul [was king], Jesse had already become a very old man [DOU].
13 Watoto watatu wakubwa wa Yese walimfuata Sauli vitani. Majina ya watoto wake watatu waliokwenda vitani yalikwa ni Eliabu mzaliwa wa kwanza, aliyemfuata Abinadabu, na watatu aliitwa Shama.
Jesse’s three oldest sons, Eliab and Abinadab and Shammah, had gone with Saul to fight [the Philistines].
14 Daudi ndiye aliyekuwa mdogo kabisa. Hao wakubwa watatu walimfuata Sauli.
David was Jesse’s youngest son. While his three oldest brothers were with Saul,
15 Basi Daudi alikwenda na kurudi akipita kati ya majeshi ya Sauli akiwa na kondoo za baba yake huko Bethtelehemu, ili kuwachunga.
David went back and forth: Sometimes he went to Saul’s camp, and sometimes he stayed in Bethlehem to take care of his father’s sheep.
16 Kwa muda wa siku arobaini yule Mfilisti mwenye nguvu alikuwa akijitokeza asubuhi na jioni kwa ajili ya vita.
For 40 days Goliath came out from the Philistine camp and stood there [taunting the Israeli army/telling the Israelis to choose one man to fight with him]. He did it twice each day, once in the morning and once in the evening.
17 Kisha Yese akamwambia mwanawe Daudi, “Wapelekee kaka zako efa ya bisi na hii mikate kumi, na uzipeleke upesi kule kambini kwa ajili ya kaka zako.
[One day], Jesse said to David, “Here is a sack of roasted grain and ten loaves of bread. Take these quickly to your [older] brothers.
18 Pia peleka hizi jibini kumi kwa jemedari wa kikosi chao cha elfu. Ukawaangalie wako na hali gani kisha uniletee habari kuhusu wanavyoendelea vizuri.
And here are ten large chunks of cheese. Take them to their commander. And see how things are going with your [older] brothers. Then [if they are okay, ] bring back something to show they are all right.”
19 Kaka zako wako pamoja na Sauli na watu wote wa Israeli katika bonde la Ela, wanapigana na Wafilisti.”
His brothers were with Saul and all the other Israeli soldiers, camped alongside Elah Valley, [preparing to] fight the Philistines.
20 Daudi aliamka asubuhi na mapema na kuliacha kundi chini ya uangalizi wa mchungaji. Akachukua vile vitu na kuondoka, kama Yese alivyomwamuru. Akafika kambini wakati jeshi linaondoka kwenda uwanja wa vita wakipiga kelele za vita.
So David arranged for another shepherd to take care of the sheep. Early the next morning he took the food and went to the Israeli camp, as Jesse told him to do. He arrived there just as the Israeli soldiers were forming their ranks and going out to the battlefield. As they went, they were shouting a war cry.
21 Nao Israeli na Wafilisti walijipanga kivita, jeshi dhidi ya jeshi.
The Philistine army and the Israeli army stood [on the hillsides], facing each other, ready for the battle.
22 Daudi aliviacha vitu vyake kwa mtunza mahitaji, akalikimbilia jeshi, na kuwasalimia kaka zake.
David gave the food to the man who was taking care of the war equipment. [He told him to take care of the food that he brought], and then he went and greeted his older brothers.
23 Alipoongea nao, yule mtu mwenye nguvu, Mfilisti wa Gathi, jina lake Goliathi, akajitokeza kutoka majeshi ya Wafilisti, naye akasema maneno yaleyale kama hapo mwanzo. Naye Daudi akayasikia.
While he was talking with them, he saw Goliath coming out from among the Philistine soldiers, shouting [to the Israelis], challenging them [to send a man to fight him]. David heard what Goliath was saying.
24 Watu wote wa Israeli walipomwona Goliathi, walimkimbia na waliogopa sana.
When all the Israeli soldiers saw Goliath, they were terrified and started to ran away.
25 Watu wa Israeli walisema, “Umemuona mtu huyu aliyejitokeza? Amekuja kuipa changamoto Israeli. Basi mfalme atampa mali nyingi mtu atakayemua, atamuozesha binti yake, na familia ya baba yake haitalipa kodi katika Israeli.”
They were saying to each other, “Look at him coming up toward us! And listen to him as he defies us Israelis! The king says that he will give a big reward to whoever kills this man. He also says that he will give his daughter to that man for him to marry her, and that he will no longer require that man’s family to pay taxes.”
26 Daudi akawauliza watu waliosimama karibu naye, “Atafanyiwa nini mtu ambaye atamuua Mfilisti huyu na kuiondolea Israeli fedheha? Ni nani Mfilisti huyu asiyetahiriwa ayatukanaye majeshi ya Mungu aliye hai?”
David talked to some of the men who were standing near him. He said, “What will be given to whoever kills this Philistine and frees us Israelis from this shame/disgrace? And who [does] this heathen Philistine [think he] is, defying/ridiculing the army that serves the all-powerful God?”
27 Ndipo watu wakarudia kile walichokuwa wamesema na kumwambia, “Ndivyo iitakavyofanyika kwa mtu atakayemuua.”
They told him the same thing that the other men had said, about what the king would do for anyone who killed Goliath.
28 Kaka yake mkubwa Eliabu, alisikia wakati akisema na watu. Hasira ya Eliabu ikawaka moto dhidi ya Daudi, naye akamuuliza, “Kwa nini umekuja hapa? Wale kondoo wachache umewaacha na nani huko nyikani? Nakijua kiburi chako, na utundu wa moyo wako; maana umekuja hapa ili uweze kuona mapigano.”
But when David’s oldest brother Eliab heard David talking to the men, he was angry. He said to David, “Why have you come down here? Is someone taking care of those few sheep that you left in the desert? I know you are just a (smart-aleck/brat)! You just want to watch the battle!”
29 Naye Daudi akamjibu, “Nimefanya nini sasa? Mimi si nuliuliza swali tu?
David replied, “Have I done something wrong? I was merely asking a question!”
30 Akamgeukia mtu mwingine na kumwacha huyo, na kusema vivyo hivyo. Nao watu wakajibu vilevile kama mwanzo.
Then he walked over to another man and asked him the same question, but the man gave him the same answer. Each time he asked someone, he received the same answer.
31 Maneno aliyosema Daudi yaliposikika, askari waliyasema tena kwa Sauli, naye akawatuma kwa Daudi.
Finally, someone told king Saul what David had asked, and Saul sent someone to bring David to him.
32 Kisha Daudi akamwambia Sauli, “Pasiwepo moyo wa mtu atakayezimia kwa sababu ya Mfilisti huyo; Mtumishi wako atakwenda kupigana na Mfilisti huyu.”
David told king Saul, “No one should (worry/become a coward) because of that Philistine man. I will go and fight with him!”
33 Sauli akamwambia Daudi, “Huwezi kumpinga Mfilisti ama kupigana naye; wewe ni kijana tu, na yeye amekuwa mtu wa vita tangu ujana wake.”
Saul said to David, “You are only a young man, and he has been a very capable soldier all his life. So you are not able to go and fight with him!”
34 Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake. Mara simba au dubu alikuja akamchukua mwana kondoo kutoka kundini,
David replied, “I have been taking care of my father’s sheep [for many years]. Whenever a lion or a bear came and carried away a lamb,
35 Nilimfukuza na kumshambulia na kumpokonya kutoka kinywani mwake. Na aliponirukia, nilimshika ndevu zake, nilimpiga, na kumuua.
I went after the lion or the bear and attacked it and rescued the lamb from the wild animal’s mouth. Then I grabbed the animal by its jaw/throat and struck it and killed it.
36 Mtumishi wako amekwisha kmuua simba na dubu. N huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa wanyama hao, kwa kuwa ameyadharau majeshi ya Mungu aliye hai.”
I have killed both lions and bears. And [I will do] the same to this heathen Philistine, because he has defied/ridiculed the army of the all-powerful God!
37 Daudi akasema, “BWANA aliyeniokoa kutoka makucha ya simba na makucha ya dubu. Ataniokoa kutoka mkono wa Mfilisti huyu.” Kisha Sauli akamwambia Daudi, “Nenda, BWANA awe pamoja nawe.”
Yahweh has rescued me from paws of lions and bears, and he will rescue me from this Philistine!” Then Saul said to David, “All right, go [and fight him], and [I hope/desire] that Yahweh will help you!”
38 Sauli akamvika Daudi vazi lake la vita. Akamvika chepeo ya shaba kichwani pake, na akamvika koti la chuma.
Then Saul gave to David his own clothes that he always wore in battles, and he gave him a bronze helmet and a coat made of metal plates.
39 Daudi akaufunga upanga wake juu ya vazi la Sauli. Lakini hakuweza kutembea, kwa sababu hakupata mafunzo kwa mavazi hayo. Ndipo Daudi akamwambia Sauli, “Siwezi kwenda kupigana nikiwa na haya, maana sikupata mafunzo kwa haya.” Kwa hiyo Daudi akayavua.
David [put these things on. Then he] fastened his sword over them, and tried to walk. But he could not walk, because he was not accustomed to wearing those things. So David said to Saul, “I cannot fight wearing all these things, because I am not accustomed to [wearing] them!” So he took them off.
40 Akachukua fimbo mkononi mwake na akachagua mawe matano laini kutoka katika kijito; akayaweka kwenye mfuko wake wa kichungaji. Kombeo lake lilikuwa mkononi akawa anamsogelea yule Mfilisti.
Then he took his walking/shepherd’s stick, and he picked up five smooth stones from the brook/stream. He put them in the pouch of his shoulder-bag. Then he put his sling in his hand and started walking toward Goliath.
41 Yule Mfilisti akaja na kumsogelea Daudi, mbeba ngao yake akiwa mbele yake.
Goliath walked toward David, with the soldier who was carrying his shield walking in front of him. When he got near David,
42 Mfilisti alipotazama kila upande na kumuona Daudi, akamdharau, maana alikuwa kijana tu, mwekundu, na umbo la kupendeza.
he looked at David closely. He saw that David had a handsome face and healthy body, but that he was only a young man. So he sneered at David.
43 Ndipo Mfilisti akamuuliza Daudi, “Je, mimi ni mbwa, hata ukanijia na fimbo? Naye Mfilisti kwa miungu yake akamlaani Daudi.
He said to David, “Are you coming to me with a stick because [you think that] I am a dog?” Then he called out to his gods to harm David.
44 Huyo Mfilisti akamwambia Daudi, “Njoo kwangu, na nyama yako nitawatupia ndege wa angani na wanyama wa mwituni.”
He said to David, “Come here to me, and I will [kill you and] give your dead body to the birds and wild animals to eat!”
45 Daudi akamjibu Mfilisti, “Unaniijia kwa upanga, kwa mkuki na mkuki mdogo. Bali mimi nakuijia kwa jina la BWANA wa majeshi, Mungu wa Majeshi ya Israeli, uliyemdharau.
David replied, “You are coming to me with a sword and a dagger and a spear. But I am coming to you (in the name/with the authority) of almighty Yahweh. He is the God whom the army of Israel [worships], and he is the God whom you have defied/ridiculed.
46 Leo BWANA atanipa ushindi dhidi yako, na nitakuua na kukiondoa kichwa chako kwenye kiwiliwili. Leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni walioko duniani mizoga ya jeshi la Wafilisti, ili dunia yote ijue kwamba yupo Mungu katika Israeli,
Today Yahweh will enable me to defeat you. I will strike you down and cut off your head. And [we Israelis will kill] many Philistine [soldiers and] give their bodies to the birds and wild animals to eat. And everyone in the world will [hear about it and] know that we Israeli people worship an [all-powerful] God.
47 na kusanyiko hili lote lijue kwamba BWANA hatoi ushindi kwa upanga wala kwa mkuki. Kwa kuwa vita ni ya BWANA, na atawaweka katika mkono wetu.”
And everyone here will know that Yahweh can rescue people without a sword or a spear. Yahweh always wins his battles, and he will enable us to defeat all of you [Philistines].”
48 Mfilisti aliponyanyuka na kukaribia akutane na Daudi, ndipo Daudi akakimbia kwa haraka kuelekea jeshi la adui ili akutane naye.
As Goliath came closer to attack David, David ran quickly toward him.
49 Daudi aliweka mkono wake mfukoni, akachukua jiwe kutoka humo, akalitupa kwa kombeo, na likampiga Mfilisti kwenye paji la uso, akaanguka chini kifudifudi.
He put his hand into his shoulder-bag and took out one stone. He [put it in his sling and] hurled it toward Goliath. The stone hit Goliath on the forehead and penetrated his skull, and he fell face down onto the ground.
50 Daudi alimshinda Mfilisti kwa kombeo na kwa jiwe moja. Alimpiga huyo Mfilisti na kumuua. Mkononi mwa Daudi hakukuwa na upanga.
Then David ran and stood over Goliath. He pulled Goliath’s sword from its sheath and killed him with it, and then cut off his head. In that way David defeated the Philistine without having his own sword. He used [only] a sling and a stone! When the other Philistines saw that their great warrior was dead, they ran away.
51 Ndipo Daudi akakimbia akasimama juu ya Mfilisti na kutwaa upanga wake, akauchomoa kutoka alani, akamuua, na kukata kichwa chake kwa upanga huo.
52 Ndipo watu wa Israeli na wale wa Yuda wakaamka kwa kelele, na kuwafukuza Wafilisti kuvuka bonde na malango ya Ekroni. Na maiti za Wafilisti walilala katika njia iendayo Shaaraimu, na njia yote kuelekea Gathi na Ekroni.
The Israeli men shouted and ran after them. They pursued them all the way to Gath and to the gates of Ekron [city]. They struck them as they went, with the result that dead/wounded Philistines were lying on the road all the way from Shaaraim to Gath and Ekron [towns].
53 Watu wa Israeli wakarejea kutoka kuwafukuza Wafilisti, na wakateka nyara kambi yao.
When the Israelis returned from chasing the Philistines, they (plundered/took everything from) the Philistine camp.
54 Daudi akachukua kichwa cha Mfilisti na kukipeleka Yerusalemu, lakini akaliweka vazi la vita katika hema lake.
David later took the head of Goliath to Jerusalem, but he kept Goliath’s weapons in his own tent.
55 Sauli alipomuona Daudi akienda kukabiliana na yule Mfilisti, akamwambia Abneri, jemedari wa jeshi, “Abneri, kijana huyu ni mtoto wa nani? Abneri akasema, “Kama uishivyo, mfalme, mimi sijui.”
As Saul watched David going toward Goliath, he said to Abner, the commanded of his army, “Abner, whose son is that young man?” Abner replied, “(As sure as you are alive/Truly) [IDM], I do not know.”
56 Naye mfalme akasema, “Waulize wanaoweza kufahamu, mvulana huyu ni kijana wa nani.”
Then the king said, “Find out whose son he is!”
57 Daudi aliporudi kutoka kumuua yule Mfilisti, Abneri alimchukuwa, na kumleta mbele ya Sauli akiwa na kichwa cha Mfilisti mkononi mwake.
[Later, ] as David returned from killing Goliath, Abner took him to Saul. David was carrying Goliath’s head.
58 Sauli akamuuliza, “Kijana, wewe ni mtoto wa nani? Na Daudi akamjibu, “Mimi ni mtoto wa mtumishi wako Yese Mbethlehemu.”
Saul asked him, “Young man, whose son are you?” David replied, “[Sir, perhaps you have forgotten that] I am the son of your servant Jesse, who has served you faithfully, who lives in Bethlehem.”

< 1 Samweli 17 >