< 1 Samweli 16 >
1 BWANA akamwambia Samweli, “Utamlilia Sauli kwa muda gani, ikiwa nimemkataa asiwe mfalme juu ya Israeli? Ijaze pembe yako mafuta na uende. Nitakutuma kwa Yese akaaye Bethlehemu, maana nimejichagulia mfalme katika wanawe.
Hina Gode da Sa: miuelema amane sia: i, “Di da habowali seda Solo ea hou dawa: beba: le da: i dione fofaginanoma: bela: ? E da Isala: ili dunu ilima hina bagade bu mae esaloma: ne, Na da ea logo hedofai dagoi. Be wali di olife susuligi lale, Bedeleheme moilaiga dunu ea dio amo Yesi ea diasuga masa. Bai Na da egefe afae Isala: ili hina bagade hamoma: ne ilegei dagoi.
2 Samweli akasema, “Jinsi gani nitaenda? Kama Sauli akisikia jambo hili, ataniua.” BWANA akasema, “chukua mtamba na useme, 'Nimekuja kutoa dhabihu kwa BWANA.'
Sa: miuele da amane sia: i, “Na da agoane habodane hamoma: bela: ? Solo da amo nabasea, ea da na fane legemu!” Hina Gode da bu adole i, “Di da bulamagau mano gaguli asili, amo Hina Godema gobele salimusa: misi sia: ma.
3 Umwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonesha kile utakachofanya. Utamtia mafuta kwa ajili yangu yule nitakaye kuambia.”
Amo gobele salabe amoga Yesi misa: ne sia: ne, amola Na da dima agoane hamoma: ya adomu. Di da dunu Na dima adomu, amo hina bagade hamoma: ne susuligi sogagala: le ilegema!”
4 Samweli akafanya kama BWANA alivyosema na akaenda Bethlehemu. Wazee wa mji walikuwa wakitetemeka walipokuja kuonana naye na wakasema, “Je, umekuja kwa amani?”
Sa: miuele da Hina Gode Ea adoi defele hamoi. E da Bedeleheme moilaiga asili, moilai ouligisu dunu da beda: ga yagugusa ema misini, amane adole ba: i, “Ba: la: lusu! Di da olofomusa: sofe misibala: ?”
5 Naye akasema, “kwa amani; Nimekuja kutoa dhabihu kwa BWANA. Jitoeni wenyewe kwa BWANA kwa ajili ya dhabihu na muandamane nami,” Na akamweka wakfu Yese na watoto wake kwa BWANA, na baadaye aliwaita wote kwenye dhabihu.
“Ma!” e da adole i. “Na da Hina Godema gobele salimusa: misi. Dilia ledo dodofelalu, nini masunu.” Amola Yesi amola egefe ilia ledo dodofelalu, amo gobele salabe amoga misa: ne sia: i.
6 Walipofika, akamwangalia Eliabu na akajisemea mwenyewe kwamba mtiwa mafuta wa BWANA hakika amesimama mbele yake.
Ilia da doaga: beba: le, Sa: miuele da Yesi egefe Ilaia: be ba: i. Hisu amane sia: i, “Amo dunu da Hina Gode ba: ma: ne lela. Dafawane ewane Hina Gode da ilegei dagoi.”
7 Lakini BWANA akamwambia Samweli, “Usimwangalie sura yake ya nje, au kimo cha umbo lake; kwa sababu nimemkataa. Maana BWANA haangalii kama mtu aangaliavyo; mtu hutazama sura ya nje, bali BWANA huutazama moyo.”
Be Hina Gode da ema amane sia: i, “E goi sedade amola ayeligi noga: i ba: sa amo mae dawa: ma. Na da amo dunu hame ilegei. Bai Na da dunu ilia asigi dawa: suga ilegebe agoane, hame ilegesa. Osobo bagade dunu da dabuagado hou, amo ba: lu ilegesa. Be Na da dunu ea dogo ganodini ba: lu, ilegesa.”
8 Kisha Yese akamwita Abinadabu akamwambia apite mbele ya Samweli. Na Samweli akasema, “Hata huyu BWANA hakumchagua.”
Amalalu, Yesi da egefe eno Abinada: be wele sia: ne, amo Sa: miuelema oule misi. Be Sa: miuele da amane sia: i, “Go hame! Hina Gode da goma hame ilegei.”
9 Kisha Yese akmwambia Shama apite karibu. Na Samweli akasema, “Hata huyu BWANA hakumchagua.”
Amalalu, Yesi da egefe eno amo Siama oule misi. Be Sa: miuele da amane sia: i, “Hame! Hina Gode da goma amolawane hame ilegei.”
10 Yese akawaleta watoto wake saba wakapita mbele ya Samweli. Na Samweli akamwambia Yese, “Hakuna hata mmoja aliyechaguliwa na BWANA kati ya hawa.”
Amanemusu hamonana, Yesi da egefe fesuale amo huluane Sa: miuelema oule misi. Amola Sa: miuele da ema amane sia: i, “Hina Gode da golalima afae hame ilegei.”
11 Kisha Samweli akamuulia Yese, “Je, watoto wako wote wako hapa?” Naye akajibu, “Yupo mdogo kabisa lakini anachunga kondoo.” Samweli akamwambia Yese, “Tuma watu wakamwite; maana hatutakaa chini hadi atakapofika hapa.”
Amalalu, e da Yesima adole ba: i, “Di da mano eno ganabela: ?” Yesi da bu adole i, “Na da mano afae ufidafa gala. Be e da eno sogega sibi ouligilala.” Sa: miuele da amane sia: i, “E goeguda: misa: ne sia: ma. E da goeguda: doaga: sea fawane, ninia da Godema gobele salasu imunu.”
12 Yese akawatuma watu wakamleta. Naye kijana huyu alikuwa mwekundu na mwenye macho mazuri na mwenye muonekano mzuri. BWANA akasema, “Amka, umtie mafuta; maana huyu ndiye.”
Amaiba: le, Yesi da amo mano lala misa: ne sia: si. Amo goi da manebe ba: loba, e da goi ayeligi da: da: loi amola ela: menesi goi ba: i, amola ea si da nenemeginisi ba: i. Hina Gode da Sa: miuelema amane sia: i, “Goefa galu! Ema ilegelesima!”
13 Ndipo Samweli akachukua pembe yenye mafuta na kumtia mafuta katikati ya kaka zake. Roho wa BWANA akamwijia Daudi kwa nguvu tangu siku hiyo na kuendelea. Kisha Samweli akanyanyuka na kwenda Rama.
Sa: miuele da olife susuligi lale, Da: ibidi yolalali ilia midadi amo Da: ibidima unasi. Amo galuwane, Hina Gode Ea A: silibu da Da: ibidi ea da: iga aligila sa: ili, amola ela gilisi amo esoha amola amoinini amoga esalusu. Amalu, Sa: miuele da La: imaga buhagi.
14 Basi Roho wa BWANA akamwacha Sauli, badala yake roho ya ubaya kutoka kwa BWANA ikamsumbua.
Hina Gode Ea A: silibu Hadigidafa da Solo yolesili amola Hina Gode da wadela: i a: silibu Soloma asunasi. Amoga se nababeba: le, Solo da bagadewane gagaba: gilalu.
15 Watumishi wa Sauli wakamwambia, “Tazama, roho ya ubaya kutoka kwa Mungu inakusumbua.
Solo ea hawa: hamosu dunu da ema amane sia: i, “Ninia dawa: , Hina Gode da wadela: i a: silibu dima asunasi, amola amoga di da se nabane gagaba: gilalu.
16 Haya bwana wetu hebu sasa amuru watumishi wako walio mbele yako wamtafute mtu mwenye ujuzi wa kupiga kinubi. Basi ikwa roho wa ubaya kutoka kwa Mungu yuko juu yako, atakipiga kinubi nawe utajisikia vizuri.”
Amaiba: le, hina! Dia da ninima sia: sea, ninia da sani baidama dusu dawa: dunu hogomu. Amasea, wadela: i a: silibu da dima masea, amo dunu da sani baidama dunigala: mu, amasea di da bu noga: mu.”
17 Sauli akawaambia watumishi wake, “Mnitafutie mtu anayeweza kupiga vizuri na mmlete kwangu.”
Solo da amane sia: i, “Defea! Dunu amo da sani baidama noga: le dubi hogole, nama oule misa.”
18 Ndipo kijana mmoja kati yao akajibu, na kusema, “Nimemuona mtoto wa Yese Mbethtelehemu, aliye mjuzi katika kupiga, ni mwenye nguvu, mtu jasiri, mtu wa vita, mwenye busara aongeapo, mtu mzuri kwa uso; na BWANA yuko pamoja naye.”
Solo ea hawa: hamosu dunu afae da amane sia: i “Bedeleheme moilaiga Yesi egefe afae da sani baidama dusu bagade dawa: E da gasa bagade amola ayeligi dunu. E da dadi gagui dunu noga: i amola sia: sia: mu defele esala. Hina Gode da ela esala.”
19 Hivyo Sauli akawatuma wajumbe kwa Yese, na kusema, “Nitumie mtoto wako Daudi, anayewatunza kondoo.” 1 Samweli! 6: 20-21
Amaiba: le, Solo da Yesima sia: agoane sia: na masa: ne dunu asunasi, “Yesi! Dia mano Da: ibidi amo sibi ouligilalebe, go nama misa: ne asunasima.”
20 Yese akamchukua punda aliyebeba mikate, na kiriba cha divai, na mwana-mbuzi, na akamtuma kwa Sauli pamoja na vitu hivyo.
Yesi da Da: ibidima goudi mano afae amola dougi afae (amo da: iya agi gobei lidili legele) amola waini hano bulamagau gadofo dabaga sali afae amo huluane iasisili, Soloma masa: ne, asunasi.
21 Ndipo Daudi akafika kwa Sauli na kuanza kazi yake. Sauli alimpenda sana Daudi, na akawa mbeba silaha wake.
Da: ibidi da Soloma misini doaga: le, ea hawa: hamosu amo hamonanu. Solo da Da: ibidima bagadewane dogolegei. E da Da: ibidi amo ea gegesu liligi gaguli ahoasu dunu hamoma: ne ilegei.
22 Sauli akawatuma wajumbe kwa Yese, akisema, “Mruhusu Daudi awe mbele yangu, maana amepata kibali machoni pangu.”
Amalalu, Solo da Yesima sia: amane sia: si, “Na da Da: ibidima dogolegei. E da na hawa: hamosu ganodini esaloma: ma.”
23 Wakati wowote roho ya usumbufu kutoka kwa Mungu ikiwapo juu ya Sauli, Daudi alichukuwa kinubi na kukipiga. Hivyo Sauli angeburudishwa na kupona, na huyo roho wa usumbufu angemtoka.
Amogainini, Gode Ea da wadela: i a: silibu amo Soloma asunasi, amo mabe ba: loba, Da: ibidi da ea sani baidama lale, dusu. Amalalu, wadela: i a: silibu da Solo yolesili, e da bu noga: le, amola defea hamosu.