< 1 Samweli 15 >

1 Samweli akamwambia Sauli, “BWANA alinituma nikutie mafuta uwe mfalme wa watu wake Israeli. Basi sikiliza maneno ya BWANA.
Samuel dit à Saül: « Yahvé m'a envoyé pour t'oindre comme roi sur son peuple, sur Israël. Écoute donc maintenant la voix des paroles de Yahvé.
2 Hivi ndivyo BWANA wa majeshi asemavyo, 'Nilichunguza jinsi Amaleki alivyomfanyia Israeli kwa kuwapinga njiani, walipopanda kutoka Misri.
L'Éternel des armées dit: Je me souviens de ce qu'Amalek a fait à Israël, comment il s'est dressé contre lui sur le chemin de sa montée d'Égypte.
3 Sasa nenda umshambulie Amaleki na ukaangamize kabisa vitu vyote walivyo navyo. Usiwaache, ua wote mwanamme na mwanamke, mtoto na mtoto mchanga, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda.”'
Maintenant, va frapper Amalek, et détruis tout ce qui lui appartient, sans l'épargner; tue l'homme et la femme, l'enfant et le nourrisson, le bœuf et le mouton, le chameau et l'âne ».
4 Sauli akwaita watu na kuwahesabu katika mji wa Talemu: watu mia mbili elfu waendao kwa miguu, na watu elfu kumi kutoka Yuda.
Saül convoqua le peuple et le compta à Télaïm, deux cent mille hommes de pied et dix mille hommes de Juda.
5 Kisha Sauli akaja hadi mji wa Amaleki akangoja huko bondeni.
Saül arriva à la ville d'Amalek, et tendit une embuscade dans la vallée.
6 Ndipo Sauli akawaambia Wakeni, “Nendeni, muondoke, mkajitenge na Waamaleki, nisije kuwaangamiza pamoja nao. Kwa maana ulionesha wema kwa watu wote wa Israeli, walipotoka Misri.” Kwa hiyo Wakeni wakajitenga na Waamaleki.
Saül dit aux Kéniens: « Allez, partez, descendez du milieu des Amalécites, de peur que je ne vous détruise avec eux, car vous avez fait preuve de bonté envers tous les enfants d'Israël lorsqu'ils sont montés d'Égypte. » Les Kéniens s'en allèrent donc du milieu des Amalécites.
7 Kisha sauli akawashambulia Waamaleki, kutoka Havila hadi kufika Shuri, ulio mashariki mwa Misri.
Saül frappa les Amalécites, depuis Havila en allant vers Shur, qui est en face de l'Égypte.
8 Basi akamchukua Agagi mfalme wa Waamaleki akiwa hai; aliwaangamiza kabisa watu wote kwa ncha ya upanga.
Il prit vivant Agag, roi des Amalécites, et il dévora tout le peuple au fil de l'épée.
9 Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi akiwa hai, pamoja na kondoo wazuri, ng'ombe, ndama wanono, na wanakondoo. Kila kitu kilichokuwa kizuri, hawakukiangamiza. Bali waliangamiza kabisa chochote kilichodharaulika na kisicho na thamani.
Mais Saül et le peuple épargnèrent Agag et les meilleurs des brebis, des bœufs, des veaux gras, des agneaux, et tout ce qui était bon, et ne voulurent pas les dévouer par interdit; mais ils dévouèrent par interdit tout ce qui était vil et immonde.
10 Baadaye neno la BWANA likamjia Samweli, kusema,
Et la parole de Yahvé fut adressée à Samuel, en ces termes:
11 “Inanihuzunisha kwamba nimemchagua Samweli awe mfalme, kwa maana aligeuka nyuma asinifuate na hakutekeleza maagizo yangu.” Samweli alikasirika; akamlilia BWANA usiku kucha.
« Je regrette d'avoir établi Saül comme roi, car il s'est détourné de moi et n'a pas exécuté mes commandements. » Samuel se mit en colère, et il cria à Yahvé toute la nuit.
12 Samweli aliamka mapema akutane na Sauli wakati wa asubuhi. Samweli aliambiwa, “Sauli alifika Karmeli na amejijengea ukumbusho kwa ajili yake, kisha aligeuka na kuendelea chini hadi Gilgali.” Ndipo
Samuel se leva de bonne heure pour aller à la rencontre de Saül le matin, et on lui dit: « Saül est arrivé au Carmel, et voici qu'il s'est érigé un monument, il s'est détourné, a passé et est descendu à Gilgal. »
13 Samweli akamwendea Sauli, na Sauli akamwambia, “Umebarikiwa na BWANA! Nami nimetekeleza amri ya BWANA.”
Samuel vint auprès de Saül, et Saül lui dit: « Tu es béni par Yahvé! J'ai exécuté le commandement de l'Éternel. »
14 Samweli akasema, “Hicho kilio cha kondoo ni cha nini basi masikioni mwangu, na hiyo milio ya ng'ombe ninayosikia?
Samuel dit: « Alors, que signifient ce bêlement des brebis à mes oreilles et le mugissement des bêtes que j'entends? »
15 Sauli akamjibu, “Wao wamewaleta kutoka kwa Waamaleki. Kwa sababu watu waliwaacha hai kondoo wazuri na ng'ombe, kwa ajili ya sadaka kwa BWANA Mungu wako. Zilizobaki tuliziangamiza kabisa.”
Saül dit: « Ils les ont amenés de chez les Amalécites, car le peuple a épargné les meilleures brebis et les meilleurs bœufs pour les sacrifier à Yahvé, ton Dieu. Nous avons dévasté le reste. »
16 Ndipo Samweli akamwambia Sauli, “Subiri nitakumbia kile ambacho BWANA amekisema kwangu usiku.” Sauli akamwambia, “Sema!”
Samuel dit alors à Saül: « Reste, et je te dirai ce que Yahvé m'a dit cette nuit. » Il lui dit: « Dis-le. »
17 Samweli akasema, “Ingawa wewe ni mdogo machoni pako mwenyewe, je, hukufanywa mkuu wa kabila za Israeli? Na BWANA akakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli;
Samuel dit: « Bien que tu sois petit à tes propres yeux, n'as-tu pas été établi chef des tribus d'Israël? L'Éternel t'a oint comme roi d'Israël,
18 BWANA alikutuma katika safari yako akisema, 'nenda na uangamize kabisa wenye dhambi, Waamaleki, na upigane dhidi yao hadi wameangamizwa.'
et l'Éternel t'a envoyé en voyage, en disant: Va, détruis les pécheurs, les Amalécites, et combats-les jusqu'à ce qu'ils soient anéantis.
19 Kwa nini basi haukuitii sauti ya BWANA, bali badala yake ulishikilia nyara na ukafanya uovu machoni pa BWANA?”
Pourquoi n'as-tu pas écouté la voix de l'Éternel, mais tu as pris le butin et tu as fait ce qui est mal aux yeux de l'Éternel? ».
20 Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Kweli kabisa niliitii sauti ya BWANA, Na nimeifuata njia ambayo BWANA alinituma. Nimemteka Agagi, mfalme wa Waamaleki, na kuwaangamiza kabisa Waamaleki.
Saül dit à Samuel: « J'ai obéi à la voix de l'Éternel, j'ai suivi le chemin que l'Éternel m'a envoyé, j'ai amené Agag, roi d'Amalek, et j'ai dévasté les Amalécites.
21 Lakini watu walichukua baadhi ya nyara-kondoo na ng'ombe, na vitu vizuri vilivyokusudiwa kuangamizwa, ili wavitoe dhabihu kwa BWANA, Mungu wako, huko Gilgali.”
Mais le peuple a pris sur le butin, des moutons et du bétail, les meilleures choses consacrées, pour les sacrifier à Yahvé ton Dieu à Guilgal. »
22 Samweli akajibu, “Je, BWANA hufurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama ilivyo kuitii sauti yake? Utii ni bora kuliko dhabihu, na kusikia ni bora kuliko mafuta ya beberu.
Samuel dit: « Yahvé prend-il autant de plaisir à offrir des holocaustes et des sacrifices qu'à obéir à la voix de Yahvé? Voici, obéir vaut mieux que le sacrifice, et écouter que la graisse de bélier.
23 Kwa maana uasi ni sawa na dhambi ya uchawi, na ukaidi ni sawa na uovu na udhalimu. Kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, naye pia amekukataa usiwe mfalme.”
Car la rébellion est comme le péché de sorcellerie, et l'entêtement comme l'idolâtrie et les théraphim. Parce que tu as rejeté la parole de Yahvé, il t'a aussi refusé le titre de roi. »
24 Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi; kwa maana nimevunja amri ya BWANA na maneno yako, kwa sababu niliwaogopa watu na kuitii sauti yao.
Saül dit à Samuel: « J'ai péché, car j'ai transgressé le commandement de Yahvé et tes paroles, parce que j'ai craint le peuple et obéi à sa voix.
25 Sasa, tafadhali nisamehe dhambi yangu, na urudi nami ili nipate kumcha BWANA.”
Maintenant, pardonne-moi mon péché et reviens avec moi, afin que je me prosterne devant Yahvé. »
26 Samweli akamwambia Sauli, “Sitarudi pamoja na wewe; kwa sababu umekataa neno la BWANA, naye BWANA amekukataa usiwe mfalme juu ya Israeli.”
Samuel dit à Saül: « Je ne retournerai pas avec toi, car tu as rejeté la parole de l'Éternel et l'Éternel t'a refusé le titre de roi d'Israël. »
27 Samweli alipogeuka kuondoka, Sauli akashika pindo la kanzu yake, na likachanika.
Comme Samuel se retournait pour s'en aller, Saül saisit le pan de sa robe, qui se déchira.
28 Samweli akamwambia, “BWANA ameuchana ufalme wa Israeli kutoka kwako leo na amempa ufalme huo jirani yako, aliye bora kuliko wewe.
Samuel lui dit: « Aujourd'hui, Yahvé t'a arraché le royaume d'Israël et l'a donné à un de tes voisins qui est meilleur que toi.
29 Pia, yeye ni Uwezo wa Israeli hatasema uongo wala kubadili nia yake; kwa sababu si mwanadamu, kwamba abadili nia yake.”
De plus, la force d'Israël ne mentira pas et ne se repentira pas, car il n'est pas homme à se repentir. »
30 Kisha Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali nipe heshima wakati huu mbele ya wakuu wa watu wangu na mbele ya Israeli. Urudi tena pamoja nami, kusudi niweze kumcha BWANA, Mungu wako.”
Il dit alors: « J'ai péché, mais honore-moi maintenant devant les anciens de mon peuple et devant Israël, et reviens avec moi, afin que je me prosterne devant Yahvé ton Dieu. »
31 Hivyo Samweli akamrudia tena Sauli, na Sauli akamcha BWANA.
Samuel retourna donc avec Saül, et Saül se prosterna devant Yahvé.
32 Kisha Samweli akasema, “Mmlete hapa kwangu Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akafika kwake akiwa amefungwa minyororo na kusema, “Hakika uchungu wa kifo umepita.”
Et Samuel dit: « Amène-moi Agag, roi des Amalécites! » Agag est venu le voir avec joie. Agag dit: « L'amertume de la mort est passée. »
33 Naye Samweli akamjibu, “Jinsi upanga wako ulivyofanya wanawake wapoteze watoto, vivyo hivyo mama yako naye hatakuwa na mtoto miongoni mwa wanawake.” Kisha Samweli akamkata Agagi vipande vipande mbele za BWANA huko Gilgali.
Samuel dit: « Comme ton épée a rendu les femmes sans enfants, ta mère sera sans enfants parmi les femmes! » Et Samuel coupa Agag en morceaux devant Yahvé, à Gilgal.
34 Samweli akaenda Rama, na Sauli akapanda kwenda nyumbani kwake Gibea ya Sauli.
Samuel s'en alla à Rama; et Saül monta dans sa maison, à Guibea de Saül.
35 Samweli hakumuona tena Sauli hadi siku ya kifo chake, lakini alimwombolezea Sauli. Na BWANA alijuta kwa kumfanya Sauli awe mfalme juu ya Israeli.
Samuel ne vint plus voir Saül jusqu'au jour de sa mort, mais il prit le deuil de Saül. Yahvé était affligé d'avoir fait de Saül le roi d'Israël.

< 1 Samweli 15 >