< 1 Samweli 15 >

1 Samweli akamwambia Sauli, “BWANA alinituma nikutie mafuta uwe mfalme wa watu wake Israeli. Basi sikiliza maneno ya BWANA.
And Samuel says to Saul, “YHWH sent me to anoint you for king over His people, over Israel; and now, listen to the voice of the words of YHWH.
2 Hivi ndivyo BWANA wa majeshi asemavyo, 'Nilichunguza jinsi Amaleki alivyomfanyia Israeli kwa kuwapinga njiani, walipopanda kutoka Misri.
Thus said YHWH of Hosts: I have looked after that which Amalek did to Israel, that which he laid for him in the way in his going up out of Egypt.
3 Sasa nenda umshambulie Amaleki na ukaangamize kabisa vitu vyote walivyo navyo. Usiwaache, ua wote mwanamme na mwanamke, mtoto na mtoto mchanga, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda.”'
Now go, and you have struck Amalek, and devoted all that he has, and you have no pity on him, and have put to death from man to woman, from infant to suckling, from ox to sheep, from camel to donkey.”
4 Sauli akwaita watu na kuwahesabu katika mji wa Talemu: watu mia mbili elfu waendao kwa miguu, na watu elfu kumi kutoka Yuda.
And Saul summons the people, and inspects them in Telaim, two hundred thousand footmen, and ten thousand [are] men of Judah.
5 Kisha Sauli akaja hadi mji wa Amaleki akangoja huko bondeni.
And Saul comes to a city of Amalek, and lays wait in a valley;
6 Ndipo Sauli akawaambia Wakeni, “Nendeni, muondoke, mkajitenge na Waamaleki, nisije kuwaangamiza pamoja nao. Kwa maana ulionesha wema kwa watu wote wa Israeli, walipotoka Misri.” Kwa hiyo Wakeni wakajitenga na Waamaleki.
and Saul says to the Kenite, “Go, turn aside, go down from the midst of Amalek, lest I consume you with it, and you did kindness with all the sons of Israel, in their going up out of Egypt”; and the Kenite turns aside from the midst of Amalek.
7 Kisha sauli akawashambulia Waamaleki, kutoka Havila hadi kufika Shuri, ulio mashariki mwa Misri.
And Saul strikes Amalek from Havilah [to] your going to Shur, which [is] on the front of Egypt,
8 Basi akamchukua Agagi mfalme wa Waamaleki akiwa hai; aliwaangamiza kabisa watu wote kwa ncha ya upanga.
and he catches Agag king of Amalek alive, and he has devoted all the people by the mouth of the sword;
9 Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi akiwa hai, pamoja na kondoo wazuri, ng'ombe, ndama wanono, na wanakondoo. Kila kitu kilichokuwa kizuri, hawakukiangamiza. Bali waliangamiza kabisa chochote kilichodharaulika na kisicho na thamani.
and Saul has pity—also the people—on Agag, and on the best of the flock, and of the herd, and of the seconds, and on the lambs, and on all that [is] good, and have not been willing to devote them; and all the work, despised and wasted—it they devoted.
10 Baadaye neno la BWANA likamjia Samweli, kusema,
And the word of YHWH is to Samuel, saying,
11 “Inanihuzunisha kwamba nimemchagua Samweli awe mfalme, kwa maana aligeuka nyuma asinifuate na hakutekeleza maagizo yangu.” Samweli alikasirika; akamlilia BWANA usiku kucha.
“I have regretted that I caused Saul to reign for king, for he has turned back from after Me, and he has not performed My words”; and it is displeasing to Samuel, and he cries to YHWH all the night.
12 Samweli aliamka mapema akutane na Sauli wakati wa asubuhi. Samweli aliambiwa, “Sauli alifika Karmeli na amejijengea ukumbusho kwa ajili yake, kisha aligeuka na kuendelea chini hadi Gilgali.” Ndipo
And Samuel rises early to meet Saul in the morning, and it is declared to Samuel, saying, “Saul has come to Carmel, and behold, he is setting up a monument to himself, and goes around, and passes over, and goes down to Gilgal.”
13 Samweli akamwendea Sauli, na Sauli akamwambia, “Umebarikiwa na BWANA! Nami nimetekeleza amri ya BWANA.”
And Samuel comes to Saul, and Saul says to him, “Blessed [are] you of YHWH; I have performed the word of YHWH.”
14 Samweli akasema, “Hicho kilio cha kondoo ni cha nini basi masikioni mwangu, na hiyo milio ya ng'ombe ninayosikia?
And Samuel says, “And what [is] the noise of this flock in my ears—and the noise of the herd which I am hearing?”
15 Sauli akamjibu, “Wao wamewaleta kutoka kwa Waamaleki. Kwa sababu watu waliwaacha hai kondoo wazuri na ng'ombe, kwa ajili ya sadaka kwa BWANA Mungu wako. Zilizobaki tuliziangamiza kabisa.”
And Saul says, “They have brought them from Amalek, because the people had pity on the best of the flock, and of the herd, in order to sacrifice to your God YHWH, and we have devoted the remnant.”
16 Ndipo Samweli akamwambia Sauli, “Subiri nitakumbia kile ambacho BWANA amekisema kwangu usiku.” Sauli akamwambia, “Sema!”
And Samuel says to Saul, “Desist, and I declare to you that which YHWH has spoken to me tonight”; and he says to him, “Speak.”
17 Samweli akasema, “Ingawa wewe ni mdogo machoni pako mwenyewe, je, hukufanywa mkuu wa kabila za Israeli? Na BWANA akakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli;
And Samuel says, “Are you not, if you [are] little in your own eyes, head of the tribes of Israel? And YHWH anoints you for king over Israel,
18 BWANA alikutuma katika safari yako akisema, 'nenda na uangamize kabisa wenye dhambi, Waamaleki, na upigane dhidi yao hadi wameangamizwa.'
and YHWH sends you in the way, and says, Go, and you have devoted the sinners, the Amalekite, and fought against them until they are consumed;
19 Kwa nini basi haukuitii sauti ya BWANA, bali badala yake ulishikilia nyara na ukafanya uovu machoni pa BWANA?”
and why have you not listened to the voice of YHWH—and fly to the spoil, and do evil in the eyes of YHWH?”
20 Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Kweli kabisa niliitii sauti ya BWANA, Na nimeifuata njia ambayo BWANA alinituma. Nimemteka Agagi, mfalme wa Waamaleki, na kuwaangamiza kabisa Waamaleki.
And Saul says to Samuel, “Because—I have listened to the voice of YHWH, and I go in the way which YHWH has sent me, and bring in Agag king of Amalek, and I have devoted Amalek;
21 Lakini watu walichukua baadhi ya nyara-kondoo na ng'ombe, na vitu vizuri vilivyokusudiwa kuangamizwa, ili wavitoe dhabihu kwa BWANA, Mungu wako, huko Gilgali.”
and the people take of the spoil of the flock and herd, the first part of the devoted thing, for sacrifice to your God YHWH in Gilgal.”
22 Samweli akajibu, “Je, BWANA hufurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama ilivyo kuitii sauti yake? Utii ni bora kuliko dhabihu, na kusikia ni bora kuliko mafuta ya beberu.
And Samuel says, “Has YHWH had delight in burnt-offerings and sacrifices as [in] listening to the voice of YHWH? Behold, listening is better than sacrifice; to give attention than fat of rams;
23 Kwa maana uasi ni sawa na dhambi ya uchawi, na ukaidi ni sawa na uovu na udhalimu. Kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, naye pia amekukataa usiwe mfalme.”
for rebellion [is as] a sin of divination, and stubbornness [is as] iniquity and teraphim; because you have rejected the word of YHWH, He also rejects you from [being] king.”
24 Ndipo Sauli akamwambia Samweli, “Nimetenda dhambi; kwa maana nimevunja amri ya BWANA na maneno yako, kwa sababu niliwaogopa watu na kuitii sauti yao.
And Saul says to Samuel, “I have sinned, for I passed over the command of YHWH, and your words; because I have feared the people, I also listen to their voice;
25 Sasa, tafadhali nisamehe dhambi yangu, na urudi nami ili nipate kumcha BWANA.”
and now, please bear with my sin, and return with me, and I bow myself to YHWH.”
26 Samweli akamwambia Sauli, “Sitarudi pamoja na wewe; kwa sababu umekataa neno la BWANA, naye BWANA amekukataa usiwe mfalme juu ya Israeli.”
And Samuel says to Saul, “I do not return with you; for you have rejected the word of YHWH, and YHWH rejects you from being king over Israel.”
27 Samweli alipogeuka kuondoka, Sauli akashika pindo la kanzu yake, na likachanika.
And Samuel turns around to go, and he lays hold on the skirt of his upper robe—and it is torn!
28 Samweli akamwambia, “BWANA ameuchana ufalme wa Israeli kutoka kwako leo na amempa ufalme huo jirani yako, aliye bora kuliko wewe.
And Samuel says to him, “YHWH has torn the kingdom of Israel from you today, and given it to your neighbor who is better than you;
29 Pia, yeye ni Uwezo wa Israeli hatasema uongo wala kubadili nia yake; kwa sababu si mwanadamu, kwamba abadili nia yake.”
and also, the Preeminence of Israel does not lie nor relent, for He [is] not a man that He should relent.”
30 Kisha Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Lakini tafadhali nipe heshima wakati huu mbele ya wakuu wa watu wangu na mbele ya Israeli. Urudi tena pamoja nami, kusudi niweze kumcha BWANA, Mungu wako.”
And he says, “I have sinned; now please honor me before [the] elderly of my people and before Israel, and return with me; and I have bowed myself to your God YHWH.”
31 Hivyo Samweli akamrudia tena Sauli, na Sauli akamcha BWANA.
And Samuel turns back after Saul, and Saul bows himself to YHWH;
32 Kisha Samweli akasema, “Mmlete hapa kwangu Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akafika kwake akiwa amefungwa minyororo na kusema, “Hakika uchungu wa kifo umepita.”
and Samuel says, “Bring Agag king of Amalek to me,” and Agag comes to him daintily, and Agag says, “Surely the bitterness of death has turned aside.”
33 Naye Samweli akamjibu, “Jinsi upanga wako ulivyofanya wanawake wapoteze watoto, vivyo hivyo mama yako naye hatakuwa na mtoto miongoni mwa wanawake.” Kisha Samweli akamkata Agagi vipande vipande mbele za BWANA huko Gilgali.
And Samuel says, “As your sword bereaved women—so is your mother bereaved above women”; and Samuel hews Agag in pieces before YHWH in Gilgal.
34 Samweli akaenda Rama, na Sauli akapanda kwenda nyumbani kwake Gibea ya Sauli.
And Samuel goes to Ramath, and Saul has gone to his house—to Gibeah of Saul.
35 Samweli hakumuona tena Sauli hadi siku ya kifo chake, lakini alimwombolezea Sauli. Na BWANA alijuta kwa kumfanya Sauli awe mfalme juu ya Israeli.
And Samuel has not added to see Saul until the day of his death, for Samuel mourned for Saul, and YHWH regretted that He had caused Saul to reign over Israel.

< 1 Samweli 15 >