< 1 Samweli 14 >
1 Siku moja, Yonathani mwana wa Sauli alimwambia mbeba silaha wake aliye mdogo, “Njoo, hebu twende hadi upande mwingine kwenye ngome ya Wafilisti.” Lakini hakumjulisha baba yake.
Et il arriva un certain jour que Jonathas, fils de Saül, dit au jeune homme, son écuyer: Viens et passons jusqu’à la garnison des Philistins, qui est au-delà de ce lieu. Mais il ne déclara point cela à son père.
2 Sauli alikuwa akikaa nje ya mji wa Gibea chini ya mti wa mkomamanga ulio katika Migroni. Takribani watu mia sita walikwa pamoja naye,
Or, Saül demeurait à l’extrémité de Gabaa, sous le grenadier qui était à Magron; et le peuple était avec lui, au nombre d’environ six cents hommes.
3 akiwemo Ahiya mwana wa Ahitubu (nduguye Ikabodi) mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa BWANA huko Shilo, aliyevaa naivera. Watu hao hawakujua kwamba Yonathani ameondoka.
Et Achias, fils d’Achitob frère d’Ichabod, fils de Phinéès qui était né d’Héli, prêtre du Seigneur à Silo, portait un ephod. Mais le peuple aussi ignorait où était allé Jonathas.
4 Katikati ya vichochoro, ambavyo Yonathani alinuia kuvipita hadi ngome ya Wafilisti, kulikuwa na mwamba wenye mteremko mkali upande mmoja, na mteremko mkali upande mwingine. Jabali moja liliitwa Bosesi, na jingine liliitwa Sene.
Or, il y avait entre les montées par lesquelles Jonathas s’efforçait de passer jusqu’à la garnison des Philistins, des pierres très hautes des deux côtés, et des rochers de part et d’autre coupés à pic en forme de dents: le nom de l’un était Bosès, et le nom de l’autre. Séné.
5 Lile jabali lenye mteremko mkali zaidi liliinuka upande wa kaskazini mbele ya Mikmashi, na jingine upande wa kusini mbele ya Geba.
Un des rochers avançait vers l’aquilon, vis-à-vis de Machmas et l’autre vers le midi, contre Gabaa.
6 Yonathani akamwambia kijana mbeba silaha, “Njoo, na tuvuke hadi ngome ya hawa wasiotahiriwa. Pengine BWANA atatenda kwa niaba yetu, kwa maana hakuna kitu kiwezacho kumzuia BWANA asiokoe kwa wengi au kwa watu wachache.”
Or, Jonathas dit au jeune homme, son écuyer: Viens, passons jusqu’à la garnison de ces incirconcis; peut-être que le Seigneur agira pour nous, parce qu’il n’est pas difficile au Seigneur de sauver avec un grand ou avec un petit nombre.
7 Mbeba silaha wake akajibu, “Fanya kila kitu kilicho ndani ya moyo wako. Songa mbele, tazama, niko pamoja nawe, nitatii maagizo yako yote.”
Et son écuyer lui répondit: Faites tout ce qui vous plaira; allez où vous désirez, et je serai avec vous partout où vous voudrez.
8 Ndipo Yonathani akasema, “Tutavuka twende kwa watu hao, na tutajionesha wenyewe kwao.
Et Jonathas reprit: Voici que nous allons vers ces hommes-là. Lors donc que nous leur apparaîtrons,
9 Kama watatuambia, 'Subirini hapo hadi tutakapokuja kwenu' - basi tutabaki katika sehemu yetu na hatutavuka kwenda kwao.
S’ils nous parlent de cette sorte: Demeurez-là, jusqu’à ce que nous allions à vous, demeurons à notre place et ne montons pas vers eux.
10 Lakini kama watajibu, 'Njoni kwetu,' ndipo tutavuka; kwa sababu BWANA amewaweka mkononi mwetu. Hii ndiyo itakuwa ishara yetu.”
Mais s’ils disent: Montez vers nous, montons, parce que le Seigneur les a livrés en nos mains: ce sera pour nous le signe.
11 Kwa hiyo wote wawili wakajifunua mbele ya ngome ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Angalia, Webrania wanakuja kutokea kwenye mashimo walimojificha.”
Ils apparurent donc soudain l’un et l’autre à la garnison des Philistins; et les Philistins dirent: Voici les Hébreux qui sortent des cavernes dans lesquelles ils étaient cachés.
12 Ndipo watu wa ile ngome wakamwita Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njoni huku kwetu, tutawaonesha jambo fulani.” Na Yonathani akamwambia mbeba silaha wake; “Nifuate nyuma yangu, kwa sababu BWANA amewaweka katika mkono wa Israeli.”
Et les hommes de la garnison parlèrent à Jonathas et à son écuyer, et dirent: Montez vers nous, et nous vous montrerons quelque chose. Alors Jonathas dit à son écuyer: Montons, suis-moi; car le Seigneur les a livrés aux mains d’Israël.
13 Yonathani alipanda juu kwa mikono na miguu yake, na mbeba silaha akimfuata nyuma yake. Wafilisti waliuwawa mbele ya Yonathani, na mbeba silaha wake akiwaua baadhi nyuma yake.
Jonathas monta donc, grimpant avec les mains et les pieds, et son écuyer derrière lui. C’est pourquoi les uns tombaient devant Jonathas; les autres, son écuyer qui le suivait, les tuait.
14 Hilo shambulio la kwanza walilofanya Yonathani na mbeba silaha wake, waliua watu wapatao ishirini katika urefu wa nusu handaki kwenye eka moja ya ardhi.
Ce fut là la première défaite des Philistins, dans laquelle Jonathas et son écuyer tuèrent environ vingt hommes, dans la moitié d’un arpent, laquelle une paire de bœufs a coutume de labourer en un jour.
15 Kukawa na hofu kubwa katika kambi, uwandani, na katika watu. Hata ngome ya jeshi na watekaji nyara nao wakawa na hofu kubwa
Et il fut fait un miracle dans le camp et dans la campagne; et aussi tous les gens de leur garnison, qui étaient venus pour piller, furent frappés de stupeur, et le pays fut troublé: ainsi il arriva comme un miracle de Dieu.
16 Ndipo walinzi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona kundi la askari wa Wafilisti likitawanyika, wakienda kule na huku.
Et les sentinelles de Saül, qui étaient à Gabaa-Benjamin, regardèrent, et voilà une multitude étendue par terre, et une autre fuyant çà et là.
17 Kisha Sauli akawaambia watu aliokuwa nao, “Mjihesabu ili muone nani hayupo hapa.”Walipokuwa wamehesabu, wakagundua kuwa Yonathani na mbebaji wa silaha zake hawapo.
Alors Saül dit au peuple qui était avec lui: Cherchez, et voyez qui est sorti de notre camp. Or, lorsqu’on eut cherché, on trouva que Jonathas et son écuyer n’y étaient pas.
18 Sauli akamwambia Ahiya, “Lete hapa naivera ya Mungu”- kwa maana siku hiyo Ahiya alivaa naivera akiwa pamoja na askari wa Israeli.
Saül dit donc à Achias: Approchez l’arche de Dieu (car l’arche de Dieu était en ce jour-là avec les enfants d’Israël).
19 Wakati Sauli akiongea na kuhani, kelele na ghasia kubwa iliendelea na kuongezeka katika kambi ya Wafilisti. dipo sauli akamwambia kuhani, “Acha kazi unayofanya.”
Et pendant que Saül parlait au prêtre, un grand tumulte s’éleva dans le camp des Philistins; et il se fortifiait peu à peu, puis il retentissait plus distinctement. Alors Saül dit au prêtre: Retirez votre main.
20 Sauli na watu wote aliokuwa nao wakajipanga na kwenda kwenye mapigano. Upanga wa kila Mfilisti ulikwa juu ya Mfilisti mwenzake, na kulikuwa na ghasia kubwa.
Saül jeta un grand cri, ainsi que tout le peuple qui était avec lui; et ils vinrent jusqu’au lieu du combat: et voilà que le glaive de l’un avait été tourné contre l’autre, °t qu’il y avait eu un très grand carnage.
21 Basi Waebrania ambao mwanzoni walijiunga na Wafilisti, na kwenda kwenye kambi yao, wao pia waliungana na Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
Mais les Hébreux aussi qui avaient été avec les Philistins hier et avant-hier, montèrent avec eux dans le camp, retournèrent pour être avec les Israélites qui étaient avec Saül et Jonathas.
22 Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika milima karibu na Efraimu waliposikia kwamba Wafilisti wamekimbia, nao pia wakawafuata Wafilisti nakuwafukuza kwenye hiyo vita.
De même tous les Israélites qui s’étaient cachés dans la montagne d’Ephraïm, apprenant que les Philistins avaient fui, s’unirent aux leurs pour le combat. Or, il y avait avec Saül environ dix mille hommes.
23 Hivyo siku hiyo BWANA aliwaokoa Israeli, na mapigano yalivuka kupitiliza Beth aveni.
Et le Seigneur sauva en ce jour-là Israël; et le combat, parvint jusqu’à Béthaven.
24 Siku hiyo watu wa Israeli walifadhaika kwa sababu Sauli aliwaweka watu chini ya kiapo akasema, “Na alaaniwe mtu atakaye kula chakula kabla ya jioni na kabla sijalipiza kisasi kwa maadui zangu.” Hivyo hakuna hata mmoja kati ya watu wote aliyeonja chakula.
Et les hommes d’Israël se réunirent en ce jour-là; mais Saül adjura le peuple, disant: Maudit l’homme qui mangera du pain avant le soir, jusqu’à ce que je me sois vengé de mes ennemis! Et tout le peuple ne mangea pas de pain.
25 Ndipo watu wote wakaingia msituni na kuona asali ikiwa juu ya ardhi.
Et tout le bas peuple du pays vint dans le bois dans lequel il y avait du miel sur la face des champs.
26 Watu walipoingia humo msituni, asali ilitiririka, lakini hakuna aliyeweka mkono wake kinywani kwa maana watu waliogopa kiapo.
Le peuple entra donc dans ce bois, et il parut du miel qui coulait, et nul ne porta la main à sa bouche; car le peuple craignait le serment.
27 Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kwamba baba yake amewaagiza watu kwa kiapo. Akanyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya kwenye sega la asali. Kisha akanyoosha mkono wake hadi kinywani mwake, na macho yake yakaangaziwa.
Mais Jonathas n’avait pas entendu, lorsque son père adjurait le peuple; il étendit donc l’extrémité de la baguette qu’il tenait à la main, et il la trempa dans un rayon du miel, puis il porta sa main à sa bouche, et ses yeux devinrent brillants.
28 Ndipo mmoja wa watu hao, akamwambia, “Baba yako aliwaagiza watu kwa mkazo na kwa kiapo, kwa kusema, 'Alaaniwe mtu atakaye kula chakula kwa siku ya leo,' ingawa watu wamedhoofika kwa ajili ya njaa.”
Mais quelqu’un du peuple prenant la parole, dit: Votre père a hé par serment le peuple, disant: Maudit l’homme qui mangera du pain aujourd’hui! (or le peuple était défaillant.)
29 Baadaye Yonathani alisema, “Baba yangu amefanya matatizo katika nchi. Angalia jinsi macho yangu alivyotiwa nuru kwa sababu nilionja asali hii kidogo.
Et Jonathas répondit: Mon père a troublé le pays: Vous avez vu, vous-mêmes, que mes yeux sont devenus brillants, parce que j’ai goûté un peu de ce miel;
30 Je, siyo vivuri sana kama leo watu wangekula bila kizuizi nyara walizopata kutoka kwa maadui zao? Kwa sababu sasa mauaji hayakuwa makubwa katikati ya Wafilisti.”
Qu’eut-ce été, si le peuple eût mangé du butin de ses ennemis, qu’il a trouvé? La défaite des Philistins n’eût-elle pas été plus grande?
31 Siku hiyo waliwashambulia Wafilisti kutoka Mikmashi hadi Aiyaloni. Na watu walikuwa wamechoka sana.
Les Hébreux battirent donc en ce jour-là les Philistins depuis Machmas jusqu’à Aïalon. Mais le peuple fut très fatigué,
32 Hivyo watu wakazivamia nyara na kuchukua kondoo, ng'ombe na ndama na kuwachinja hapo chini. Watu walikula nyama zao pamoja na damu.
Et s’étant tourné du côté du butin, il prit des brebis, des bœufs et des veaux; ils les tuèrent sur la terre, et le peuple les mangea avec le sang.
33 KIsha wakamwambia Sauli, “Tazama, watu wanamtenda BWANA dhambi kwa kula pamoja na damu.” Sauli akasema, “Mmetenda isivyo haki. Sasa, viringisheni jiwe kubwa kwangu.” Sauli akasema,
Mais on l’annonça à Saul, en disant que le peuple avait péché contre le Seigneur, en mangeant de la chair avec le sang. Et Saül dit: Vous avez prévariqué, roulez près de moi une grande pierre.
34 “Nendeni kati watu, na muwaambie, 'Kila mtu alete ng'ombe na kondoo wake, wawachinje hapa, na kuwala. Msimtende BWANA dhambi kwa kula na damu.”' Kwa hiyo watu wote wakaleta kila mtu na ng'ombe wake usiku huo na kuwachinja mahali hapo.
Et Saul ajouta: Répandez-vous çà et là dans le peuple, et dites-leur, que chacun m’amène son bœuf et son bélier; tuez-les sur cette pierre, et mangez-en, et vous ne pécherez pas contre le Seigneur, en mangeant la chair avec le sang. C’est pourquoi tout le peuple amena son bœuf par la main jusqu’à la nuit; et ils les tuèrent là.
35 Sauli akamjengea BWANA madhabahu, ambayo ilikuwa ya kwanza kwake kumjengea BWANA.
Or, Saul bâtit un autel au Seigneur; et ce fut alors pour la première fois qu’il commença à bâtir un autel au Seigneur.
36 Ndipo Sauli akasema, “Haya tuwafukuze Wafilisti usiku na kuwateka nyara hadi asubuhi; tusimwache hata mtu mmoja akiwa hai.” Nao wakamjibu, “Fanya unaloona linakupendeza.” Lakini kuhani akasema, “Hebu na tumkaribie Mungu mahali hapa.”
Saül dit ensuite: Fondons sur les Philistins pendant la nuit, et ravageons-les jusqu’à ce que brille la lumière du matin, et n’en laissons pas un seul homme. Et le peuple répondit: Tout ce qui paraît bon à vos yeux, faites-le. Alors le prêtre dit: Approchons-nous ici de Dieu.
37 Sauli alitaka kumuuliza Mungu maswali zaidi, “Je, inanipasa kuwafukuza Wafilisti? Je, utawaweka katika mkono wa Israeli?” Lakini siku hiyo BWANA hakumjibu kitu.
Et Saül consulta le Seigneur: Est-ce que je poursuivrai les Philistins? et les livrerez-vous aux mains d’Israël? Et il ne lui répondit point en ce jour-là.
38 Ndipo Sauli akasema, “Njoni hapa, viongozi wote wa watu; mjue na kuona jinsi dhambi hii ilivyotokea leo.
Et Saül dit: Faites venir ici tous les chefs du peuple; sachez et voyez par qui a eu lieu le péché en ce jour.
39 Kwa maana, kama BWANA aishivyo, aliyewaokoa Israeli, hata kama angekuwa mwanangu Yonathani, atapaswa kufa.” Lakini hakuna hata mtu mmoja miongoni mwa watu aliye mjibu neno.
Le Seigneur, sauveur d’Israël, vit! Si c’est par Jonathas, mon fils, qu’il a été commis, il mourra sans rémission. Sur quoi nul d’entre tous ne le contredit.
40 Basi akawaambia Waisraeli wote, “Simameni upande mmoja, na mimi na Yonathani tutasimama upande mwingine.” Kisha watu wakamwambia Sauli, “Fanya lile unaloona jema kwako.”
Et il dit à tout Israël: Séparez-vous, vous d’une part, et moi, avec Jonathas, mon fils, je serai de l’autre part. Et le peuple répondit à Saül: Ce qui paraît bon à vos yeux, faites-le.
41 Kwa hiyo, Sauli akamwambia BWANA, Mungu wa Israeli, “Tuoneshe Thumimu.” Yonathani na Sauli wakatwaliwa, lakini watu walinusurika kuchaguliwa.
Et Saül dit au Seigneur Dieu d’Israël: Faites connaître pourquoi est-ce que vous n’avez pas répondu à votre serviteur aujourd’hui? Si c’est en moi ou en Jonathas mon fils qu’est cette iniquité, montrez-le; ou si cette iniquité est dans votre peuple, montrez votre sainteté. Et Jonathas et Saül tombèrent au sort, et le peuple sortit innocent.
42 Basi Sauli akasema, “Tupa mawe ya bahati nasibu tuone kati yangu na mwanangu Yonathani.” Ndipo Yonathani akatwaliwa.
Alors Saül dit: Jetez le sort entre moi et entre Jonathas, mon fils. Et Jonathas tomba au sort.
43 Kisha Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie umefanya nini.” Yonathani akamwambia baba yake, “Nilionja asali kidogo kwa kutumia ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwangu. Niko hapa; Nitakufa.”
Or, Saül dit à Jonathas: Indique-moi ce que tu as fait. Et Jonathas le lui indiqua, et dit: Je n’ai fait que goûter avec l’extrémité de la baguette, qui était en ma main, un peu de miel, et voici que je meurs.
44 Sauli akasema, “Mungu afanye hivyo na kuzidi hata kwangu, kama Yonathani hautakufa.”
Et Saül répondit: Que Dieu me fasse ceci, et qu’il ajoute cela, si tu ne meurs de mort, Jonathas.
45 Basi watu wakamuuliza Sauli, “Je, inampasa Sauli afe, ni nani aliyetekeleza ushindi huu mkubwa kwa ajili ya Israeli? Mbali na hayo! Kama BWANA aishivyo, hata unywele mmoja wa kichwa chake hautaanguka chini, kwa maana leo amefanya kazi pamoja na Mungu.” Hivyo hao watu walimuokoa Yonathani ili asife.
Mais le peuple dit à Saül: Quoi donc! Jonathas mourra, lui qui a procuré le salut à Israël par cette grande victoire? Cela ne se peut: le Seigneur vit! il ne tombera pas un cheveu de sa tête sur la terre, parce qu’il a agi avec Dieu aujourd’hui. Le peuple délivra donc Jonathas, pour qu’il ne mourût pas.
46 Basi Sauli akasita kuwafuatia Wafilisti, nao wakarudi katika makao yao.
Après cela Saül se retira, et il ne poursuivit pas les Philistins: or, les Philistins s’en allèrent chez eux.
47 Sauli alipoanza kutawala juu ya Israeli, alipigana na adui zake wote kila upande. Alipigana dhidi ya Moabu, dhidi ya watu wa Amoni, Edomu, wafalme wa Zoba, na Wafilisti. Popote alipogeukia aliwapiga kwa adhabu adui zake.
Et Saül, son règne sur Israël affermi, combattait aux alentours contre tous ses ennemis, contre Moab, contre les enfants d’Ammon, contre Edom, contre les rois de Soba et contre les Philistins; et partout où il se portait, il était vainqueur.
48 Alitenda kwa ushujaa mkubwa na kuwashinda Waamaleki. Aliwaokoa Israeli kutoka mikono ya watu ambao waliwateka nyara.
Ensuite, son armée assemblée, il battit Amalec, et délivra Israël de la main de ses dévastateurs.
49 Basi wana wa Sauli walikuwa ni hawa Yonathani, Ishvi, na Malkishua. Na majina ya binti zake wawili yalikuwa ni haya, Merabu mzaliwa wa kwanza, na mdogo aliitwa Mikali.
Or, les fils de Saül furent Jonathas, Jessui et Melchisua; et les noms de ses deux filles étaient, le nom de l’aînée, Mérob, et le nom de la plus jeune, Michol;
50 Jina la mke wa Sauli aliitwa Ahinoamu; naye alikuwa binti Ahimaasi. Na jina la Jemedari wa jeshi lake aliitwa Abneri mwana wa Neri, baba mdogo wa Sauli.
Et le nom de la femme de Saül, Achinoam, fille d’Achimaas; et le nom du prince de sa milice, Abner, fils de Ner, oncle paternel de Saül.
51 Kishi alikuwa baba yake Sauli; na Neri alikuwa baba yake na Abneri, wote walikuwa wana wa Abieli.
Mais Cis fut père de Saül, et Ner père d’Abner, fils d’Abiel.
52 Kulikuwa na mapigano makali dhidi ya Wafilisti katika siku zote za Sauli. Naye alipomwona mtu yeyote mwenye nguvu, au mtu yeyote jasiri, alimuunganisha kwake.
Mais il y eut une puissante guerre contre les Philistins, durant tous les jours de Saül; car tout homme qu’il avait vu vaillant et propre au combat, il l’associait à lui.