< 1 Samweli 10 >
1 Ndipo Samweli akachukua chupa ya mafuta, akayamimina juu ya kichwa cha Sauli, na akambusu. Akasema, “Je, Mungu hajakutia mafuta uwe mtawala juu ya urithi wake?
Then Samuel took a small jar of olive oil and poured [some of] it on Saul’s head. Then he kissed Saul [on the cheek], and told him, “I am doing this because Yahweh has chosen you to be the leader of his Israeli people.
2 Utakapoondoka kwangu leo, utawaona wanaume wawili na kaburi la Raheli, katika nchi ya Benyamini hapo Selsa. Watu hao watakuambia, 'Wale punda mliokuwa mkiwatafuta wamepatikana. Sasa, Baba yako ameacha kuwatunza punda, na ana hofu juu yenu, anasema, “Nitafanya nini kuhusu mwanangu?”
[And this will prove it to you]: When you leave me today, when you arrive near Rachel’s tomb at Zelzah, in the area where the descendants of Benjamin live, you will meet two men. They will say to you, ‘The donkeys have been found, but now your father is worrying about you, and he is asking people, “Have you seen my son?’”
3 Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na utafika katika mwaloni wa Tabori. Utakutana na watu watatu hapo wakienda kwa Mungu huko Betheli, mmoja akibeba wana-mbuzi watatu, mwingine akibeba mikate mitatu, na mwingine akibeba kiriba cha divai.
When you arrive at the [large] oak tree at Tabor [town], you will see three men coming toward you. They will be on their way to [worship] God at Bethel [town]. One of them will be leading three young goats, one will be carrying three loaves of bread, and one will be carrying a container of wine.
4 Watawasalimu na watawapatia mikate miwili, kutoka mikononi mwao.
They will greet you, and they will offer you two of the loaves of bread. Accept them.
5 Baada ya hayo, utafika katika mlima wa Mungu, mahali ilipo ngome ya Wafilisti. Utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakiteremka chini kutoka mahali pa juu wakiwa na kinanda, tari, kinubi na filimbi mbele yao; na watakuwa wakitabiri.
When you arrive at the hill [where people worship] God near Gibeah [town], where there is the camp where the Philistine soldiers stay, you will meet a group of prophets who will be coming down from the altar on top of the hill. There will be people in front of them who will be playing [various musical instruments]: a harp, a tambourine, a flute, and a lyre. And all of them will be speaking messages that come directly from God.
6 Roho ya BWANA itakujaza, nawe utatabiri pamoja nao, na utabadilishwa na kuwa mtu tofauti.
At that time the Spirit of Yahweh will come upon you, and you also will speak messages that come directly from God. (You will be changed/The Spirit of Yahweh will change you), so that you will become like a different person.
7 Basi, ishara hizi zikikufikia, fanya lolote ambalo mikono yako itaona ifanye, kwa sababu Mungu yu pamoja nawe.
After those things occur, do whatever you think is right to do, and God will (be with/help) you.
8 Nenda ushuke mbele yangu hadi Gilgali. Kisha nitakufuata huko nitoe dhabihu za kuteketezwa na kutoa dhabihu za amani. Nisubiri kwa muda wa siku saba hadi nije kwako na nikuoneshe unachopaswa kufanya.”
Then go ahead of me, down to Gilgal [city], and wait for me there, for seven days. Then I will join you there, to burn sacrifices and offer other sacrifices to enable you to maintain fellowship with God. When I arrive there, I will tell you what [other] things you should do.”
9 Sauli alipotega mgongo amuache Samweli, Mungu akampa moyo mwingine. Ndipo ishara zote hizi zikatimia siku hiyo.
As Saul started to leave there, God changed Saul’s inner being. And all the things that Samuel had predicted happened on that day.
10 Walipofika mlimani, kundi la manabii lilikutana naye, na Roho ya Mungu ikamjilia kwa nguvu ili atabiri pamoja nao.
When Saul and his servant arrived at Gibeah, they saw some prophets who were [speaking messages that came directly from God. As the prophets were] approaching Saul and his servant, God’s Spirit came upon Saul powerfully, and he also began to speak messages from God.
11 Kila mtu aliyemfahamu kabla hajamwona akitabiri pamoja na manabii, watu waliambizana wao kwa wao:”Kitu gani kimempata mtoto wa Kishi? Hivi Sauli ni mmoja wa manabii siku hizi?”
When people who had known Saul previously heard him speaking messages from God as the prophets were doing, they said to each other, “What has happened to this son of Kish? Is he now really one of the (prophets/men who speak messages from God)?”
12 Mtu mmoja kutoka eneo hilo akajibu, “Na ni nani baba yao?” Kwa sababu ya jambo hili, ukawapo msemo, “Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?”
One of the men who lived there replied, “[Saul cannot be a prophet, because] all prophets receive their power to speak messages from God, not from their parents.” And that is why, [when people hear about a report of someone prophesying, they think about what happened to Saul and] say, “[We are surprised about that person becoming a prophet, like] we were surprised to hear that Saul had really become one of the prophets.”
13 Alipomaliza kutabiri, akafika mahali pa juu.
When Saul finished speaking the messages that God gave him, he went to the place where the people offered sacrifices.
14 Ndipo baba yake mdogo na akamuuliza Sauli na mtumishi wake, “Mlienda wapi?” Naye akamjibu, “Kuwatafuta punnda; tulipoona kwamba hatuwezi kuwapata, tukaenda kwa Samweli.”
Later, Saul’s uncle [saw him there, and] asked him, “Where did you go?” Saul replied, “We went to look for the donkeys. When we could not find them, we came here to ask Samuel [if he could tell us where they were].”
15 Baba yake mdogo akasema, “Tafadhali niambie kile alichosema kwako Samweli,”
Saul’s uncle replied, “What did Samuel tell you?”
16 Sauli akamjibu baba yake mdogo, “Alituambia waziwazi kwamba punda wamepatikana.” Lakini kuhusu swala la ufalme alilosema Samweli hakumwambia.
Saul replied, “He assured us that the donkeys had been found.” But he did not tell his uncle what Samuel had said about him becoming the king [of Israel].
17 Basi Samweli aliwaita watu pamoja huko Mispa.
[Later] Samuel summoned the people of Israel to gather at Mizpah to [hear a message from] Yahweh.
18 Akwaambia watu wa Israeli, “Hivi ndivyo BWANA, Mungu wa Israeli asemavyo: 'Niliwatoa Israeli kutoka Misri, na niliwaokoa kutoka nchi ya Wamisri, na kutoka mkono wa falme zote zilizowaonea.'
After they arrived, he said to them, “This is what Yahweh, the God we Israeli people [worship], says: I brought you Israeli people out of Egypt. I rescued your [ancestors] from the power of the rulers of Egypt and from all the other kings who oppressed them.
19 Lakini leo mmemkataa Mungu wenu, awaokoaye kutoka kwenye majanga na mahangaiko; na mmemwambia, ' Tuwekee mfalme juu yetu; Sasa jihudhurisheni wenyewe mbele za BWANA kwa kabila na jamaa zenu.”
I am the one who saves you from all your troubles and difficulties. But today you have rejected me, your God, and you have said, ‘We don’t care! Give us a king!’ So [I will do what you want]. Now have [representatives of] your tribes and [of] your clans stand here in the presence of Yahweh.’”
20 Kisha Samweli akawaleta kabila zote za Isareli karibu, na kulichagua kabila la Benyamini.
When those representatives came near to Samuel, [God indicated that] he had chosen someone from the tribe descended from Benjamin.
21 Akawasogeza karibu kabila la Benyamini kwa kufuata jamaa zao; na jamaa ya Wamatri ikachaguliwa; na Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa. Lakini walipokwenda kumtafuta, hakuweza kuonekana.
Then Samuel told representatives of the tribe of Benjamin to come forward, and God indicated that [from that tribe] he had chosen someone from the family of Matri, and then God indicated that [from the family of Matri] he had chosen Saul, the son of Kish. But when they looked for Saul, they could not find him.
22 Kisha watu walitaka kumuuliza Mungu maswali zaidi, “Bado yupo mtu mwingine ajaye?” BWANA akajibu, “Yeye mwenyewe kajificha kwenye mizigo.”
So they asked Yahweh, “Where is Saul?” Yahweh replied, “He is hiding among the army equipment.”
23 Wakaenda mbio na kumleta Sauli kutoka humo. Aliposimama kati yao, alikuwa mrefu kuliko watu wote kuanzia mabega yake kwenda juu.
So they quickly went there [and found him, ] and brought him [in front of all the people]. They could see that [truly] he was a head taller than anyone else.
24 Kisha Samweli akawaambia watu, “Je, mnamuona mtu ambaye BWANA amemchagua? Hakuna mtu kama yeye kati ya watu wote.” Watu wote wakapiga Kelele, “Mfalme na aishi”
Then Samuel said to all the people there, “This is the man whom Yahweh has chosen to be your king. Among all us Israeli people, there is no one like him!” Then all the people shouted, “We hope that this king will live a long time!”
25 Ndipo Samweli akawaambia watu desturi na sheria za ufalme, akaziandika katika kitabu, na kuziweke mbele za BWANA. Baadaye Samweli akawaruhusu watu waondoke kila mtu aende nyumbani kwake.
Then Samuel told the people what things the king would force them to do, and all the things the king was required to do. He wrote all those things on a scroll, and then he put it in a sacred place in the temple. Then Samuel sent all the people home.
26 Sauli pia alienda nyumbani kwake huko Gibea, akiwa na baadhi ya watu wenye nguvu, wenye mioyo iliyoguswa na Mungu.
When Saul returned to his home in Gibeah [town], a group of men decided to continually accompany Saul. They did that because God (motivated them/put it in their minds) to do that.
27 Lakini baadhi ya watu wasiofaa walisema, “Huyu mtu atatuokoaje?” Watu hawa walimdharau Sauli na hawakumletea zawadi zozote. Lakini Sauli alinyamaza kimya.
But some worthless men said, “(How can this man save us [from our enemies]?/This man will not be able to save us [from our enemies].)” [RHQ] They despised him, and refused to give him any gifts [to show that they would be loyal to him]. But Saul did not say anything [to rebuke them].