< 1 Samweli 10 >
1 Ndipo Samweli akachukua chupa ya mafuta, akayamimina juu ya kichwa cha Sauli, na akambusu. Akasema, “Je, Mungu hajakutia mafuta uwe mtawala juu ya urithi wake?
Then Samuel took the vial of oil, and poured it upon his head, and kissed him, and said, Is it not because Jehovah has anointed thee prince over his inheritance?
2 Utakapoondoka kwangu leo, utawaona wanaume wawili na kaburi la Raheli, katika nchi ya Benyamini hapo Selsa. Watu hao watakuambia, 'Wale punda mliokuwa mkiwatafuta wamepatikana. Sasa, Baba yako ameacha kuwatunza punda, na ana hofu juu yenu, anasema, “Nitafanya nini kuhusu mwanangu?”
When thou goest from me to-day, thou shalt meet two men by Rachel's sepulchre in the border of Benjamin at Zelzah; and they will say to thee, The asses are found which thou wentest to seek, and behold, thy father has dismissed the matter of the asses, and is anxious about you, saying, What shall I do for my son?
3 Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na utafika katika mwaloni wa Tabori. Utakutana na watu watatu hapo wakienda kwa Mungu huko Betheli, mmoja akibeba wana-mbuzi watatu, mwingine akibeba mikate mitatu, na mwingine akibeba kiriba cha divai.
And thou shalt go on forward from thence, and shalt come to the oak of Tabor, and there shall meet thee three men going up to God, to Bethel, one carrying three kids, and another carrying three cakes of bread, and another carrying a flask of wine.
4 Watawasalimu na watawapatia mikate miwili, kutoka mikononi mwao.
And they will ask after thy welfare, and give thee two loaves, which thou shalt receive of their hands.
5 Baada ya hayo, utafika katika mlima wa Mungu, mahali ilipo ngome ya Wafilisti. Utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakiteremka chini kutoka mahali pa juu wakiwa na kinanda, tari, kinubi na filimbi mbele yao; na watakuwa wakitabiri.
After that thou shalt come to the hill of God, where are the outposts of the Philistines; and it shall come to pass, when thou comest thither, into the city, that thou shalt meet a company of prophets coming down from the high place with lute and tambour and pipe and harp before them; and they themselves prophesying.
6 Roho ya BWANA itakujaza, nawe utatabiri pamoja nao, na utabadilishwa na kuwa mtu tofauti.
And the Spirit of Jehovah will come upon thee, and thou shalt prophesy with them, and shalt be turned into another man.
7 Basi, ishara hizi zikikufikia, fanya lolote ambalo mikono yako itaona ifanye, kwa sababu Mungu yu pamoja nawe.
And it shall be, when these signs shall come to thee, thou shalt do as thy hand shall find; for God is with thee.
8 Nenda ushuke mbele yangu hadi Gilgali. Kisha nitakufuata huko nitoe dhabihu za kuteketezwa na kutoa dhabihu za amani. Nisubiri kwa muda wa siku saba hadi nije kwako na nikuoneshe unachopaswa kufanya.”
And thou shalt go down before me to Gilgal; and behold, I will come down to thee, to offer up burnt-offerings, [and] to sacrifice sacrifices of peace-offerings: seven days shalt thou wait, until I come to thee and inform thee what thou shalt do.
9 Sauli alipotega mgongo amuache Samweli, Mungu akampa moyo mwingine. Ndipo ishara zote hizi zikatimia siku hiyo.
And it was [so] that when he turned his back to go away from Samuel, God gave him another heart; and all those signs came to pass that day.
10 Walipofika mlimani, kundi la manabii lilikutana naye, na Roho ya Mungu ikamjilia kwa nguvu ili atabiri pamoja nao.
And when they came thither to the hill, behold, a company of prophets met him; and the Spirit of God came upon him, and he prophesied among them.
11 Kila mtu aliyemfahamu kabla hajamwona akitabiri pamoja na manabii, watu waliambizana wao kwa wao:”Kitu gani kimempata mtoto wa Kishi? Hivi Sauli ni mmoja wa manabii siku hizi?”
And it came to pass, when all that knew him before saw that, behold, he prophesied among the prophets, then the people said one to another, What is this that has happened to the son of Kish? Is Saul also among the prophets?
12 Mtu mmoja kutoka eneo hilo akajibu, “Na ni nani baba yao?” Kwa sababu ya jambo hili, ukawapo msemo, “Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?”
And a man of that place answered and said, But who is their father? Therefore it became a proverb, Is Saul also among the prophets?
13 Alipomaliza kutabiri, akafika mahali pa juu.
And when he had ended prophesying, he came to the high place.
14 Ndipo baba yake mdogo na akamuuliza Sauli na mtumishi wake, “Mlienda wapi?” Naye akamjibu, “Kuwatafuta punnda; tulipoona kwamba hatuwezi kuwapata, tukaenda kwa Samweli.”
And Saul's uncle said to him and to his servant, Whither went ye? And he said, To seek the asses; and when we saw that they were nowhere, we went to Samuel.
15 Baba yake mdogo akasema, “Tafadhali niambie kile alichosema kwako Samweli,”
And Saul's uncle said, Tell me, I pray thee, what Samuel said to you.
16 Sauli akamjibu baba yake mdogo, “Alituambia waziwazi kwamba punda wamepatikana.” Lakini kuhusu swala la ufalme alilosema Samweli hakumwambia.
And Saul said to his uncle, He told us for certain that the asses were found. But of the matter of the kingdom, of which Samuel had spoken, he told him not.
17 Basi Samweli aliwaita watu pamoja huko Mispa.
And Samuel called the people together to Jehovah to Mizpah.
18 Akwaambia watu wa Israeli, “Hivi ndivyo BWANA, Mungu wa Israeli asemavyo: 'Niliwatoa Israeli kutoka Misri, na niliwaokoa kutoka nchi ya Wamisri, na kutoka mkono wa falme zote zilizowaonea.'
And he said to the children of Israel, Thus saith Jehovah, the God of Israel, I brought up Israel out of Egypt, and delivered you out of the hand of the Egyptians, and out of the hand of all the kingdoms that oppressed you;
19 Lakini leo mmemkataa Mungu wenu, awaokoaye kutoka kwenye majanga na mahangaiko; na mmemwambia, ' Tuwekee mfalme juu yetu; Sasa jihudhurisheni wenyewe mbele za BWANA kwa kabila na jamaa zenu.”
but ye have this day rejected your God, who himself saved you out of all your adversities and your troubles, and have said unto him, [Nay, ] but a king shalt thou set over us. Now therefore present yourselves before Jehovah by your tribes, and by your thousands.
20 Kisha Samweli akawaleta kabila zote za Isareli karibu, na kulichagua kabila la Benyamini.
And Samuel caused all the tribes of Israel to come near, and the tribe of Benjamin was taken.
21 Akawasogeza karibu kabila la Benyamini kwa kufuata jamaa zao; na jamaa ya Wamatri ikachaguliwa; na Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa. Lakini walipokwenda kumtafuta, hakuweza kuonekana.
And he caused the tribe of Benjamin to come near by their families, and the family of Matri was taken; and Saul the son of Kish was taken. And they sought him, but he was not to be found.
22 Kisha watu walitaka kumuuliza Mungu maswali zaidi, “Bado yupo mtu mwingine ajaye?” BWANA akajibu, “Yeye mwenyewe kajificha kwenye mizigo.”
Therefore they inquired of Jehovah further, Will the man yet come hither? And Jehovah answered, Behold, he hath hid himself among the baggage.
23 Wakaenda mbio na kumleta Sauli kutoka humo. Aliposimama kati yao, alikuwa mrefu kuliko watu wote kuanzia mabega yake kwenda juu.
And they ran and fetched him thence; and when he stood among the people, he was higher than any of the people from his shoulders and upward.
24 Kisha Samweli akawaambia watu, “Je, mnamuona mtu ambaye BWANA amemchagua? Hakuna mtu kama yeye kati ya watu wote.” Watu wote wakapiga Kelele, “Mfalme na aishi”
And Samuel said to all the people, See ye him whom Jehovah has chosen, that there is none like him among all the people? And all the people shouted and said, May the king live.
25 Ndipo Samweli akawaambia watu desturi na sheria za ufalme, akaziandika katika kitabu, na kuziweke mbele za BWANA. Baadaye Samweli akawaruhusu watu waondoke kila mtu aende nyumbani kwake.
And Samuel told the people the right of the kingdom, and wrote it in the book, and laid it before Jehovah. And Samuel sent all the people away, every man to his house.
26 Sauli pia alienda nyumbani kwake huko Gibea, akiwa na baadhi ya watu wenye nguvu, wenye mioyo iliyoguswa na Mungu.
And Saul also went home to Gibeah; and with him went the band, whose hearts God had touched.
27 Lakini baadhi ya watu wasiofaa walisema, “Huyu mtu atatuokoaje?” Watu hawa walimdharau Sauli na hawakumletea zawadi zozote. Lakini Sauli alinyamaza kimya.
But the children of Belial said, How should this man save us? And they despised him, and brought him no gifts. But he was as one deaf.