< 1 Petro 5 >

1 Ninawasihi wazee waliomo miongoni mwenu, mimi, niliye mzee mwenzao na shahidi wa mateso ya Kristo, na ambaye vile vile ni mshirika katika utukufu utakaodhihirika.
Ich richte nun meine Ermahnung an die Ältesten, die unter euch arbeiten — ich bin ein Ältester wie sie; ich habe die Leiden Christi als Augenzeuge gesehen und soll auch teil empfangen an der Herrlichkeit, die sich offenbaren wird —:
2 Kwa hiyo, ninawatia moyo ninyi wazee, lichungeni kundi la Mungu lililo miongoni mwenu. Liangalieni, sio kwa sababu mnapaswa, lakini kwa sababu mnatamani hivyo, kulingana na Mungu. Liaangalieni, sio kwa kupenda pesa za aibu, lakini kwa kupenda.
Weidet die euch anbefohlene Herde Gottes — nicht aus Zwang, sondern aus innerem Herzensdrang, wie es Gott gefällt; nicht aus schnöder Gewinnsucht, sondern mit Lust und Liebe!
3 Msijifanye mabwana juu ya watu waliyochini ya uangalizi wenu, lakini iweni mfano katika kundi.
Tretet nicht als Herren auf in euern Gemeinden, sondern werdet Vorbilder der Herde!
4 Pale Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu isiyopoteza uthamani wake.
Dann werdet ihr bei der Erscheinung des Oberhirten als Ehrenkranz aus unverwelklichen Blumen die Herrlichkeit empfangen.
5 Vilevile, nanyi vijana wadogo, nyenyekeni kwa wakubwa wenu. Ninyi nyote, uvaeni unyenyekevu na kuhudumiana ninyi kwa ninyi, kwani Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa neema wanyenyekevu.
Ebenso ihr jüngeren Leute: gehorcht euern Ältesten! Ihr alle insgesamt, tragt im Verkehr miteinander den Sklavenschurz der Demut. Denn: Gott widersteht den Stolzen, den Demütigen aber gibt er Gnade.
6 Kwa hiyo nyenyekeni chini ya mkono wa Mungu uliyo hodari ili kwamba awainue kwa wakati wake.
So demütigt euch denn unter Gottes gewaltige Hand, damit er euch erhöhe, wenn die rechte Stunde gekommen ist!
7 Mwekeeni fadhaa zenu juu yake, kwa sababu anawajali.
Werft alle eure Sorge auf ihn, denn er nimmt sich euer an!
8 Iweni na busara, iweni waangalifu. Yule adui yenu, ibilisi, kama simba aungurumaye ananyatia, akisaka mtu wa kumrarua.
Seid nüchtern und wachsam! Euer Widersacher, der Teufel, geht umher wie ein brüllender Löwe und sucht, wen er verschlinge.
9 Simameni kinyume chake. Kuweni na nguvu katika imani yenu. Mkijua kwamba ndugu zenu walioko ulimwenguni wanapitia mateso kama hayo.
Dem widersteht in Glaubensfestigkeit und denkt daran, daß eure Brüder in der ganzen Welt dieselben Leiden zu erdulden haben!
10 Baada ya kuteseka kwa muda kitambo, Mungu wa neema yote, aliyewaita katika utukufu wa milele ndani ya Kristo, atawakamilisha, atawaimarisha na kuwatia nguvu. (aiōnios g166)
Gott aber, der Spender aller Gnade, der euch in Christi Jesu Gemeinschaft dazu berufen hat, nach einer kurzen Leidenszeit in seine ewige Herrlichkeit einzugehen, der wir euch vollbereiten, stärken, kräftigen und festgründen. (aiōnios g166)
11 Enzi iwe kwake milele na milele. Amina. (aiōn g165)
Sein ist die Herrlichkeit und Macht in alle Ewigkeit! Amen. (aiōn g165)
12 Namthamini Silwano kama ndugu mwaminifu, na nimewaandikia ninyi kwa ufupi kupitia kwake. Ninawatia moyo na ninashuhudia kwamba nilichokiandika ni neema ya kweli ya Mungu. Simameni ndani yake.
Durch Silvanus, den treuen Bruder, schreibe ich euch diesen Brief; mir scheint, er ist nur kurz. Ich erinnere und bezeuge euch darin: die rechte Gnade Gottes ist euch zuteil geworden. Darin steht fest!
13 Waamini waliloko Babeli, waliochaguliwa pamoja nanyi, wanawasalimu, na Marko mwanangu, anawasalimu.
Die Miterwählte in Babylon und mein Sohn Markus lassen euch grüßen.
14 Salimianeni kila mmoja kwa busu la upendo. Na amani iwe kwenu mliondani ya Kristo.
Grüßt einander mit dem Kuß der Liebe! Friede sei mit euch allen, die ihr in Christi Gemeinschaft steht!

< 1 Petro 5 >