< 1 Petro 5 >
1 Ninawasihi wazee waliomo miongoni mwenu, mimi, niliye mzee mwenzao na shahidi wa mateso ya Kristo, na ambaye vile vile ni mshirika katika utukufu utakaodhihirika.
J'adresse cette exhortation aux anciens qui sont parmi vous, moi qui suis ancien avec eux et témoin des souffrances du Christ, et qui ai part aussi à la gloire qui doit être manifestée:
2 Kwa hiyo, ninawatia moyo ninyi wazee, lichungeni kundi la Mungu lililo miongoni mwenu. Liangalieni, sio kwa sababu mnapaswa, lakini kwa sababu mnatamani hivyo, kulingana na Mungu. Liaangalieni, sio kwa kupenda pesa za aibu, lakini kwa kupenda.
Paissez le troupeau de Dieu qui vous est confié: faites-le, non par contrainte, mais de bon gré, non pour un gain sordide, mais par dévouement,
3 Msijifanye mabwana juu ya watu waliyochini ya uangalizi wenu, lakini iweni mfano katika kundi.
non en dominant sur ceux qui vous sont échus en partage, mais en vous rendant les modèles du troupeau.
4 Pale Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu isiyopoteza uthamani wake.
Et lorsque le souverain Pasteur paraîtra, vous remporterez la couronne de gloire, qui ne se flétrit jamais.
5 Vilevile, nanyi vijana wadogo, nyenyekeni kwa wakubwa wenu. Ninyi nyote, uvaeni unyenyekevu na kuhudumiana ninyi kwa ninyi, kwani Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa neema wanyenyekevu.
De même, jeunes gens, soyez soumis aux anciens. Et tous, soyez ornés d'humilité les uns à l'égard des autres; car Dieu résiste aux orgueilleux, mais il fait grâce aux humbles.
6 Kwa hiyo nyenyekeni chini ya mkono wa Mungu uliyo hodari ili kwamba awainue kwa wakati wake.
Humiliez-vous donc sous la puissante main de Dieu, afin qu'il vous élève quand il en sera temps;
7 Mwekeeni fadhaa zenu juu yake, kwa sababu anawajali.
et déchargez-vous sur lui de tous vos soucis, parce qu'il a soin de vous.
8 Iweni na busara, iweni waangalifu. Yule adui yenu, ibilisi, kama simba aungurumaye ananyatia, akisaka mtu wa kumrarua.
Soyez sobres, veillez! Votre adversaire, le Diable, rôde autour de vous comme un lion rugissant, cherchant qui il pourra dévorer.
9 Simameni kinyume chake. Kuweni na nguvu katika imani yenu. Mkijua kwamba ndugu zenu walioko ulimwenguni wanapitia mateso kama hayo.
Résistez-lui, en demeurant fermes dans la foi, sachant que vos frères, répandus dans le monde, souffrent les mêmes afflictions que vous.
10 Baada ya kuteseka kwa muda kitambo, Mungu wa neema yote, aliyewaita katika utukufu wa milele ndani ya Kristo, atawakamilisha, atawaimarisha na kuwatia nguvu. (aiōnios )
Le Dieu de toute grâce, qui vous a appelés en Christ à sa gloire éternelle, après que vous aurez souffert un peu de temps, vous perfectionnera lui-même, vous affermira, vous fortifiera. (aiōnios )
11 Enzi iwe kwake milele na milele. Amina. (aiōn )
A lui soit la puissance, aux siècles des siècles! Amen. (aiōn )
12 Namthamini Silwano kama ndugu mwaminifu, na nimewaandikia ninyi kwa ufupi kupitia kwake. Ninawatia moyo na ninashuhudia kwamba nilichokiandika ni neema ya kweli ya Mungu. Simameni ndani yake.
Je vous ai écrit ces quelques mots par Silvain, que j'estime être un frère fidèle, pour vous exhorter, et pour vous attester que c'est à la vraie grâce de Dieu que vous êtes attachés.
13 Waamini waliloko Babeli, waliochaguliwa pamoja nanyi, wanawasalimu, na Marko mwanangu, anawasalimu.
L'Église des élus, qui est à Babylone, vous salue, ainsi que Marc, mon fils.
14 Salimianeni kila mmoja kwa busu la upendo. Na amani iwe kwenu mliondani ya Kristo.
Saluez-vous les uns les autres par un baiser fraternel. Que la paix soit avec vous tous qui êtes en Christ!