< 1 Petro 5 >
1 Ninawasihi wazee waliomo miongoni mwenu, mimi, niliye mzee mwenzao na shahidi wa mateso ya Kristo, na ambaye vile vile ni mshirika katika utukufu utakaodhihirika.
The seniors who are among you, I exhort, who am also a senior, and a witness of the sufferings of Christ, and also a partaker of the glory which is to be revealed.
2 Kwa hiyo, ninawatia moyo ninyi wazee, lichungeni kundi la Mungu lililo miongoni mwenu. Liangalieni, sio kwa sababu mnapaswa, lakini kwa sababu mnatamani hivyo, kulingana na Mungu. Liaangalieni, sio kwa kupenda pesa za aibu, lakini kwa kupenda.
Feed the flock of God, which is with you; exercising the overseer's office, not by constraint, but willingly; neither for the sake of sordid gain, but from good disposition;
3 Msijifanye mabwana juu ya watu waliyochini ya uangalizi wenu, lakini iweni mfano katika kundi.
neither as lording it over the heritage of God, but, being patterns to the flock:
4 Pale Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu isiyopoteza uthamani wake.
and when the Chief Shepherd shall appear, you shall receive the crown of glory which fades not away.
5 Vilevile, nanyi vijana wadogo, nyenyekeni kwa wakubwa wenu. Ninyi nyote, uvaeni unyenyekevu na kuhudumiana ninyi kwa ninyi, kwani Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa neema wanyenyekevu.
For the like reason, you younger persons subject yourselves to the seniors. Yes, all be subject to one another, and be clothed with humility, for God resists the proud but gives favor to the humble.
6 Kwa hiyo nyenyekeni chini ya mkono wa Mungu uliyo hodari ili kwamba awainue kwa wakati wake.
Be humbled, therefore, under the mighty hand of God, that he may exalt you in due time.
7 Mwekeeni fadhaa zenu juu yake, kwa sababu anawajali.
Cast all your anxious care on him, because he cares for you.
8 Iweni na busara, iweni waangalifu. Yule adui yenu, ibilisi, kama simba aungurumaye ananyatia, akisaka mtu wa kumrarua.
Be sober, be vigilant: your adversary, the devil, is walking about as a roaring lion, seeking whom he may devour:
9 Simameni kinyume chake. Kuweni na nguvu katika imani yenu. Mkijua kwamba ndugu zenu walioko ulimwenguni wanapitia mateso kama hayo.
whom resist, steadfast in the faith, knowing that the very same sufferings are accomplished in your brethren, who are in the world.
10 Baada ya kuteseka kwa muda kitambo, Mungu wa neema yote, aliyewaita katika utukufu wa milele ndani ya Kristo, atawakamilisha, atawaimarisha na kuwatia nguvu. (aiōnios )
And may the God of all favor, who has called us to his eternal glory, by Christ Jesus, after you have suffered a little, himself make you complete; support, strengthen, establish you: (aiōnios )
11 Enzi iwe kwake milele na milele. Amina. (aiōn )
to him be the glory and dominion for ever and ever. Amen. (aiōn )
12 Namthamini Silwano kama ndugu mwaminifu, na nimewaandikia ninyi kwa ufupi kupitia kwake. Ninawatia moyo na ninashuhudia kwamba nilichokiandika ni neema ya kweli ya Mungu. Simameni ndani yake.
By Sylvanus, a faithful brother, (as I conclude, ) I have written to you in in few words, exhorting you, and strongly testifying that this is the true favor of God, in which you stand.
13 Waamini waliloko Babeli, waliochaguliwa pamoja nanyi, wanawasalimu, na Marko mwanangu, anawasalimu.
They at Babylon, elected jointly with you, and Mark, my son, salute you.
14 Salimianeni kila mmoja kwa busu la upendo. Na amani iwe kwenu mliondani ya Kristo.
Salute one another with a kiss of love. Peace to you all, who are in Christ Jesus.