< 1 Petro 5 >
1 Ninawasihi wazee waliomo miongoni mwenu, mimi, niliye mzee mwenzao na shahidi wa mateso ya Kristo, na ambaye vile vile ni mshirika katika utukufu utakaodhihirika.
I want to encourage the elders among you. I'm also an elder, a witness to Christ's sufferings, and I will share in the glory that is to come.
2 Kwa hiyo, ninawatia moyo ninyi wazee, lichungeni kundi la Mungu lililo miongoni mwenu. Liangalieni, sio kwa sababu mnapaswa, lakini kwa sababu mnatamani hivyo, kulingana na Mungu. Liaangalieni, sio kwa kupenda pesa za aibu, lakini kwa kupenda.
Look after God's flock you have been given to care for, watching over it not because you're forced to, but gladly, as God wants you to. Do this willingly, not looking to make a profit from it.
3 Msijifanye mabwana juu ya watu waliyochini ya uangalizi wenu, lakini iweni mfano katika kundi.
Don't be arrogant, lording it over those who have been put in your care, but be an example to the flock.
4 Pale Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu isiyopoteza uthamani wake.
When the chief Shepherd appears, you will receive a glorious crown that will never fade.
5 Vilevile, nanyi vijana wadogo, nyenyekeni kwa wakubwa wenu. Ninyi nyote, uvaeni unyenyekevu na kuhudumiana ninyi kwa ninyi, kwani Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa neema wanyenyekevu.
Young people, do what the elders tell you. Indeed all of you should serve one another in humility, because “God is against the proud, but favors the humble.”
6 Kwa hiyo nyenyekeni chini ya mkono wa Mungu uliyo hodari ili kwamba awainue kwa wakati wake.
Humble yourself before God's powerful hand so that he will lift you up at the appropriate time.
7 Mwekeeni fadhaa zenu juu yake, kwa sababu anawajali.
Surrender all your worries to him, because he cares for you.
8 Iweni na busara, iweni waangalifu. Yule adui yenu, ibilisi, kama simba aungurumaye ananyatia, akisaka mtu wa kumrarua.
Be responsible, and stay alert. The devil, your enemy, is prowling around like a roaring lion looking for someone to devour.
9 Simameni kinyume chake. Kuweni na nguvu katika imani yenu. Mkijua kwamba ndugu zenu walioko ulimwenguni wanapitia mateso kama hayo.
Stand firm against him, trusting in God. Remember that your fellow-believers around the world are going through similar troubles.
10 Baada ya kuteseka kwa muda kitambo, Mungu wa neema yote, aliyewaita katika utukufu wa milele ndani ya Kristo, atawakamilisha, atawaimarisha na kuwatia nguvu. (aiōnios )
After you have suffered for a little while, the God of all grace who called you into his eternal glory in Christ, will himself restore you, support you, strengthen you, and give you a solid foundation. (aiōnios )
11 Enzi iwe kwake milele na milele. Amina. (aiōn )
To him be power forever and ever! Amen. (aiōn )
12 Namthamini Silwano kama ndugu mwaminifu, na nimewaandikia ninyi kwa ufupi kupitia kwake. Ninawatia moyo na ninashuhudia kwamba nilichokiandika ni neema ya kweli ya Mungu. Simameni ndani yake.
With the help of Silvanus, whom I consider a trustworthy brother, I send this letter to you. In these few words I've written I want to encourage you and testify that this is the true grace of God. Stand firm in God's grace!
13 Waamini waliloko Babeli, waliochaguliwa pamoja nanyi, wanawasalimu, na Marko mwanangu, anawasalimu.
The believers here in “Babylon,” chosen together with you, send their greetings to you, as does Mark, my son.
14 Salimianeni kila mmoja kwa busu la upendo. Na amani iwe kwenu mliondani ya Kristo.
Greet each other with a kiss of love. Peace to all of you who are in Christ.