< 1 Petro 4 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili, jivikeni silaha za nia ile ile. Yeye aliyeteseka katika mwili ameondokana na dhambi.
Christ then having suffered in the flesh, do ye also arm yourselves with the same mind; for he that hath suffered in the flesh hath ceased from sin;
2 Mtu huyu haendelei tena kuishi katika tamaa za mwili, bali kwa mapenzi ya Mungu, kwa maisha yake yaliyosalia.
that ye may no longer live the remaining time in the flesh after the lusts of men, but after the will of God.
3 Kwa kuwa muda uliopita umetosha kutenda mambo ambayo wamataifa wanataka kufanya- ufisadi, nia mbaya, ulevi, ulafi, sherehe za kipagani na ibada za sanamu zenye machukizo.
For sufficient is the time past to have wrought the will of the gentiles, when ye walked in lasciviousness, lusts, excess of wine, revelings, carousings, and abominable idolatries;
4 Wanafikiri ni ajabu mnapojiepusha kutenda mambo hayo pamoja nao, hivyo wananena maovu juu yenu.
at which they are astonished that ye run not with them to the same excess of riot, speaking evil of you;
5 Watatoa hesabu kwake aliye tayari kuhukumu walio hai na wafu.
who shall give account to him that is ready to judge the living and the dead.
6 Kwa kusudi hili injili ilihubiriwa kwao waliokwisha kufa, kwamba ijapokuwa walikwisha hukumiwa katika miili yao kama wanadamu, ili waweze kuishi kulingana na Mungu katika roho.
For to this end was the gospel preached also to the dead, that they might indeed be judged according to men in the flesh, but might live according to God in the spirit.
7 Mwisho wa mambo yote unakuja. Kwa hiyo, mwe na ufahamu ulio sahihi, na iweni na nia njema kwa ajili ya maombi yenu.
But the end of all things is at hand; be ye therefore sober, and watch unto prayer.
8 Kabla ya mambo yote, eweni na bidii katika upendo kwa kila mmoja, kwa kuwa upendo hautafuti kufunua dhambi za wengine.
And above all things have fervent love among yourselves; for love covereth a multitude of sins.
9 Onyesheni ukarimu kwa kila mmoja bila kunung'unika.
Be hospitable to one another without grudging.
10 Kama ambavyo kila mmoja wenu alivyopokea karama, itumieni katika kuhudumiana, kama wasimamizi wema wa karama nyingi zilizotolewa bure na Mungu.
According as each one hath received a gift, minister the same to one another, as good stewards of the manifold grace of God.
11 Kama mtu akiongea, na iwe kama mausia ya Mungu, na kama mtu akihudumu, na iwe kama uwezo aliopewa na Mungu, ili kwamba kwa kila jambo Mungu apate kutukuzwa kupitia Yesu Kristo. Utukufu na uweza vina Yeye milele na milele. Amina. (aiōn g165)
If any one speak, let him speak as uttering the oracles of God; if any minister, let him do it as from the ability which God giveth; that in all things God may be glorified through Jesus Christ, to whom be the glory and the dominion for ever and ever. Amen. (aiōn g165)
12 Wapendwa, msihesabu jaribu ambalo huja kuwajaribu kama kitu kigeni, ingawa kuna kitu kigeni kilichokuwa kinatukia kwenu.
Beloved, be not surprised at the fiery trial which is taking place among you to prove you, as though a strange thing were befalling you;
13 Lakini kwa kadri mnavyozidi kupata uzoefu wa mateso ya Kristo, furahini, ili kwamba mfurahi pia na kushangilia katika ufunuo wa utukufu wake.
but, in so far as ye share in Christ's sufferings, rejoice; that also at the manifestation of his glory ye may rejoice with exceeding joy.
14 Iwapo mmetukanwa kwa ajili ya jina la Kristo, mmebarikiwa, kwa sababu ya Roho wa utukufu na Roho wa Mungu anakaa juu yenu.
If ye are reproached for the name of Christ, happy are ye for the Spirit of glory and of God resteth upon you.
15 Lakini asiwepo yeyote mwenye kuteswa kama muuaji, mwizi, mtenda maovu, au ajishughulishaye na mambo ya wengine.
For let none of you suffer as a murderer, or a thief, or an evil-doer, or as a busybody in other men's matters;
16 Lakini ikiwa mtu anateswa kama Mkristo, asione aibu, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.
but if as a Christian, let him not be ashamed, but let him glorify God in this name.
17 Kwa kuwa wakati umefika kwa hukumu kuanzia katika nyumba ya Mungu. Na kama inaanzia kwetu, itakuwaje kwa wale wasioitii injili ya Mungu?
For the time is come for judgment to begin at the house of God; but if it first begin with us, what will be the end of those who obey not the gospel of God?
18 Na kama “mwenye haki anaokolewa kupitia magumu, itakuwaje kwa mtu asiyehaki na mwenye dhambi?”
and “if the righteous scarcely is saved, where shall the ungodly and the sinner appear?”
19 Kwa hiyo wote wanaoteseka kutokana na mapenzi ya Mungu wakabidhi nafsi zao kwa Muumba mwaminifu ili hali wakitenda mema.
Wherefore let those who suffer according to the will of God commit the keeping of their souls to him in well-doing, as to a faithful Creator.

< 1 Petro 4 >