< 1 Petro 4 >
1 Kwa hiyo, kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili, jivikeni silaha za nia ile ile. Yeye aliyeteseka katika mwili ameondokana na dhambi.
Therefore Christ having suffered in the flesh, you also arm yourselves with the same mind: because the one having suffered in carnality has ceased from sin;
2 Mtu huyu haendelei tena kuishi katika tamaa za mwili, bali kwa mapenzi ya Mungu, kwa maisha yake yaliyosalia.
that he may no longer live the remaining time in carnality according to the lusts of men, but in the will of God.
3 Kwa kuwa muda uliopita umetosha kutenda mambo ambayo wamataifa wanataka kufanya- ufisadi, nia mbaya, ulevi, ulafi, sherehe za kipagani na ibada za sanamu zenye machukizo.
For the past time is sufficient to have wrought the will of the heathens, walking in impurities, in lusts, in wine-drinkings, in revelries, in intemperance, and in unlawful idolatries:
4 Wanafikiri ni ajabu mnapojiepusha kutenda mambo hayo pamoja nao, hivyo wananena maovu juu yenu.
in which they are astonished you not running to the same excess of wrath, blaspheming;
5 Watatoa hesabu kwake aliye tayari kuhukumu walio hai na wafu.
who shall give an account to him who is ready to judge the living and the dead.
6 Kwa kusudi hili injili ilihubiriwa kwao waliokwisha kufa, kwamba ijapokuwa walikwisha hukumiwa katika miili yao kama wanadamu, ili waweze kuishi kulingana na Mungu katika roho.
For, unto this the gospel was also preached to the dead, in order that they may indeed be judged according to men in the flesh, but live according to God in the spirit.
7 Mwisho wa mambo yote unakuja. Kwa hiyo, mwe na ufahamu ulio sahihi, na iweni na nia njema kwa ajili ya maombi yenu.
But the end of all things is at hand. Therefore be prudent, and sober unto prayers:
8 Kabla ya mambo yote, eweni na bidii katika upendo kwa kila mmoja, kwa kuwa upendo hautafuti kufunua dhambi za wengine.
before all things having divine love stedfast toward one another; because divine love covers a multitude of sins:
9 Onyesheni ukarimu kwa kila mmoja bila kunung'unika.
being hospitable to one another without grudging;
10 Kama ambavyo kila mmoja wenu alivyopokea karama, itumieni katika kuhudumiana, kama wasimamizi wema wa karama nyingi zilizotolewa bure na Mungu.
as each one received the gift of grace, ministering the same to one another, as the good stewards of the manifold grace of God:
11 Kama mtu akiongea, na iwe kama mausia ya Mungu, na kama mtu akihudumu, na iwe kama uwezo aliopewa na Mungu, ili kwamba kwa kila jambo Mungu apate kutukuzwa kupitia Yesu Kristo. Utukufu na uweza vina Yeye milele na milele. Amina. (aiōn )
if any one speaks, let him speak as the oracles of God; if any one ministers, as from the strength which God supplies; in order that God may be glorified in all things through Jesus Christ; to whom there is glory and power unto the ages of the ages. Amen. (aiōn )
12 Wapendwa, msihesabu jaribu ambalo huja kuwajaribu kama kitu kigeni, ingawa kuna kitu kigeni kilichokuwa kinatukia kwenu.
Beloved, think it not strange concerning the fiery trial among you, coming upon you unto your testing: as some strange thing happening to you:
13 Lakini kwa kadri mnavyozidi kupata uzoefu wa mateso ya Kristo, furahini, ili kwamba mfurahi pia na kushangilia katika ufunuo wa utukufu wake.
but as you participate in the sufferings of Christ, rejoice; in order that you may also rejoice in the revelation of his glory, being glad.
14 Iwapo mmetukanwa kwa ajili ya jina la Kristo, mmebarikiwa, kwa sababu ya Roho wa utukufu na Roho wa Mungu anakaa juu yenu.
If you suffer reproach in the name of Christ, happy are you, because the spirit of the glory and the spirit of God rest on you.
15 Lakini asiwepo yeyote mwenye kuteswa kama muuaji, mwizi, mtenda maovu, au ajishughulishaye na mambo ya wengine.
But let no one of you suffer as a murderer, or a thief, or an evil-doer, or as a meddler in other people's business:
16 Lakini ikiwa mtu anateswa kama Mkristo, asione aibu, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.
but if as a Christian, be not ashamed, but glorify God in this name.
17 Kwa kuwa wakati umefika kwa hukumu kuanzia katika nyumba ya Mungu. Na kama inaanzia kwetu, itakuwaje kwa wale wasioitii injili ya Mungu?
Because it is time that judgment should begin from the house of God: and if it is first from us, what shall be the end of those who obey not the gospel of God?
18 Na kama “mwenye haki anaokolewa kupitia magumu, itakuwaje kwa mtu asiyehaki na mwenye dhambi?”
And if the righteous is scarcely saved, where shall the ungodly and the sinner appear?
19 Kwa hiyo wote wanaoteseka kutokana na mapenzi ya Mungu wakabidhi nafsi zao kwa Muumba mwaminifu ili hali wakitenda mema.
So let those indeed suffering according to the will of God submit their souls to the faithful Creator, in good work.