< 1 Petro 3 >
1 Kwa njia hii, ninyi ambao ni wake mnapaswa kujitoa kwa waume zenu wenyewe, ili, hata kama baadhi yao hawajalitii neno, kupitia tabia za wake zao wanaweza kuvutwa pasipo neno,
In the same way you wives must be submissive to your own husbands; so that if some of them will not believe the message, they may apart from the message be won over by the behavior of their wives,
2 kwa sababu wao wenyewe watakuwa wameiona tabia yenu njema pamoja na heshima.
when they see how pure and reverent you are.
3 Hii ifanyike siyo kwa mapambo ya nje—kusuka nywele, vito vya dhahabu, au mavazi ya mtindo.
Your adornment ought not to be the outward adornment of plaited hair and golden jewels and the wearing of beautiful dresses;
4 Lakini badala yake ifanyike kwa utu wa ndani wa moyo, na kuzidi katika uzuri wa unyenyekevu na utulivu wa moyo, ambao ni wa thamani mbele za Mungu.
but rather that hidden personality of the heart, the imperishable ornament of a quiet and gentle spirit, which in the sight of God is indeed precious.
5 Kwa kuwa wanawake watakatifu walijipamba wenyewe kwa njia hii. Walikuwa na imani katika Mungu na waliwatii waume zao wenyewe.
For in this way in the olden time the holy women also, who put their trust in God, used to adorn themselves. They were ever in submission to their own husbands;
6 Kwa njia hii Sara alimtii Ibrahamu na kumwita yeye “bwana” wake. Ninyi sasa ni watoto wake kama mtafanya yaliyo mazuri na kama hamwogopi mabaya.
thus, for example, Sarah obeyed Abraham, calling him lord. And you are daughters of Sarah, if you do what is right, and permit nothing to make you afraid.
7 Kwa njia hiyo hiyo, ninyi wanaume mnapaswa kuishi na wake zenu mkijua kuwa wao ni wenzi wa kike dhaifu, mkiwatambua wao kama wapokeaji wenzenu wa zawadi ya uzima. Fanyeni hivi ili kwamba maombi yenu yasizuiliwe.
In the same way you husbands live with your wives, according to knowledge, honoring your wife as of the weaker sex, yet as an heir with yourself of the grace of life; so that your prayers may not be hindered.
8 Hatimaye, ninyi nyote, muwe na nia moja, wenye huruma, upendo kama ndugu, wanyenyekevu, na wapole.
Finally, you should all be harmonious, sympathetic, loving as brothers, tender-hearted, humble-minded;
9 Msilipe ovu kwa ovu, au tusi kwa tusi. Kinyume chake, mwendelee kubariki, kwa sababu hii mliitwa, ili kwamba muweze kurithi baraka.
not paying back evil for evil or abuse for abuse, but on the contrary giving a blessing. Because for this you have been called - to inherit a blessing.
10 “Yeye atakaye kupenda maisha na kuona siku njema lazima auzuie ulimi wake kwa mabaya na midomo yake kusema hila.
He who would love life and enjoy happy days, Let him keep his tongue from evil, And his lips from speaking guile;
11 Na ageuke na kuacha mabaya na kufanya yaliyo mazuri. Atafute amani na kuifuata.
Let him turn from evil and do good, Let him seek peace, and pursue it.
12 Macho ya Bwana humwona mwenye haki na masikio yake husikia maombi yake. Lakini uso wa Bwana uko kinyume cha wale watendao uovu.”
For the eyes of the Lord are upon the righteous, And his ears are open to their cry; But the face of the Lord is set against evil-doers.
13 Ni nani atakayewadhuru ninyi, ikiwa mwatamani lililo zuri?
Yet who will harm you if you become zealous for the good?
14 Lakini kama mkiteseka kwa haki, mmebarikiwa. Msiogope yale ambayo wao wanayaogopa. Msiwe na wasiwasi.
But even if you should suffer in behalf of righteousness, you are happy. Do not be afraid of their terror, neither be troubled.
15 Badala yake, mmuweke Kristo Bwana katika mioyo yenu kama mtakatifu. Kila mara muwe tayari kumjibu kila mtu anayewauliza ninyi kwa nini mna tumaini katika Mungu. Fanyeni hivi kwa upole na heshima.
But consecrate Christ in your hearts, as Lord. Be always in readiness to make and answer to any one who asks you a reason for the hope that is within you, yet with gentleness and reverence.
16 Muwe na dhamiri njema ili kwamba watu wanaotukana maisha yenu mema katika Kristo waweze kuaibika kwa sababu wanaongea kinyume dhidi yenu kama kwamba mlikuwa watenda maovu.
See that you have a clear conscience, so that, although they speak of you as evil-doers, these libelers of your good Christian lives may be ashamed.
17 Ni vizuri zaidi, ikiwa Mungu anatamani, kwamba mwateseka kwa kufanya mema kuliko kwa kufanya mabaya.
For it is better that you suffer for doing right, if such be God’s will, than for doing wrong;
18 Kristo pia aliteseka mara moja kwa ajili ya dhambi. Yeye ambaye ni mwenye haki aliteseka kwa ajili yetu, ambao hatukuwa wenye haki, ili kwamba atulete sisi kwa Mungu. Alikufa katika mwili, lakini alifanywa mzima katika roho.
because Christ also once for all suffered for sins, the just for the unjust, that he might bring us to God. He was put to death in the flesh, but make alive in spirit.
19 Katika roho, alikwenda na kuzihubiri roho ambazo sasa ziko kifungoni.
(It was in spirit that he went and preached the Word to the spirits who were in prison,
20 Hazikuwa tiifu wakati uvumilivu wa Mungu ulipokuwa unasubiri wakati wa Nuhu, siku za ujenzi wa safina, na Mungu aliokoa watu wachache—nafsi nane—kutoka katika maji.
who in old times had been disobedient, when God’s longsuffering was waiting in the days of Noah, while an ark was building, in which a few persons - eight in number - were saved by water.)
21 Hii ni alama ya ubatizo unaowaokoa ninyi sasa, siyo kama kuosha uchafu kutoka mwilini, lakini kama ombi la dhamiri njema kwa Mungu, kupitia ufufuo wa Yesu Kristo.
Baptism, the counterpart of that, now saves you (not the washing off of the filth of the flesh, but the prayer for a good conscience toward God), through the resurrection of Jesus Christ.
22 Yeye yuko mkono wa kuume wa Mungu. Alikwenda mbinguni. Malaika, mamlaka, na nguvu lazima vimtii yeye.
He is gone into heaven, and is on the right hand of God; to Him angels and authorities and powers have been made subject.