< 1 Petro 3 >
1 Kwa njia hii, ninyi ambao ni wake mnapaswa kujitoa kwa waume zenu wenyewe, ili, hata kama baadhi yao hawajalitii neno, kupitia tabia za wake zao wanaweza kuvutwa pasipo neno,
Similarly, wives, be submissive to your own husbands, so that even if some are disobedient to the Word, they may be won over, without a word, by the conduct of their wives
2 kwa sababu wao wenyewe watakuwa wameiona tabia yenu njema pamoja na heshima.
(having watched your pure behavior accompanied by respect),
3 Hii ifanyike siyo kwa mapambo ya nje—kusuka nywele, vito vya dhahabu, au mavazi ya mtindo.
whose adorning should not be the outward one of braiding hair and wearing gold, or putting on fine clothing,
4 Lakini badala yake ifanyike kwa utu wa ndani wa moyo, na kuzidi katika uzuri wa unyenyekevu na utulivu wa moyo, ambao ni wa thamani mbele za Mungu.
but rather the hidden person of the heart, with the incorruptible adorning of the gentle and quiet spirit that is of great value before God.
5 Kwa kuwa wanawake watakatifu walijipamba wenyewe kwa njia hii. Walikuwa na imani katika Mungu na waliwatii waume zao wenyewe.
For this is how the holy women who hoped in God in former times also adorned themselves, being submissive to their own husbands,
6 Kwa njia hii Sara alimtii Ibrahamu na kumwita yeye “bwana” wake. Ninyi sasa ni watoto wake kama mtafanya yaliyo mazuri na kama hamwogopi mabaya.
as Sarah obeyed Abraham, calling him ‘lord’, whose (f) daughters you became by doing good and not being afraid of any intimidation.
7 Kwa njia hiyo hiyo, ninyi wanaume mnapaswa kuishi na wake zenu mkijua kuwa wao ni wenzi wa kike dhaifu, mkiwatambua wao kama wapokeaji wenzenu wa zawadi ya uzima. Fanyeni hivi ili kwamba maombi yenu yasizuiliwe.
Similarly, husbands, live together knowledgeably as with a weaker vessel, according honor to the wife especially as being a joint heir of the grace of life, for your prayers not to be hindered.
8 Hatimaye, ninyi nyote, muwe na nia moja, wenye huruma, upendo kama ndugu, wanyenyekevu, na wapole.
Finally, all of you be like-minded, compassionate, loving as brothers, tenderhearted, courteous,
9 Msilipe ovu kwa ovu, au tusi kwa tusi. Kinyume chake, mwendelee kubariki, kwa sababu hii mliitwa, ili kwamba muweze kurithi baraka.
not returning evil for evil or reviling for reviling, but instead blessing, knowing that you were called to this so that you may inherit a blessing.
10 “Yeye atakaye kupenda maisha na kuona siku njema lazima auzuie ulimi wake kwa mabaya na midomo yake kusema hila.
For: “The one who wants to love life and to see good days must refrain his tongue from evil and his lips from speaking deceit;
11 Na ageuke na kuacha mabaya na kufanya yaliyo mazuri. Atafute amani na kuifuata.
he must turn away from evil and do good; he must seek peace, even pursue it.
12 Macho ya Bwana humwona mwenye haki na masikio yake husikia maombi yake. Lakini uso wa Bwana uko kinyume cha wale watendao uovu.”
Because the eyes of the Lord are upon the righteous, and His ears open to their prayer; but the face of the Lord is against those doing evil.”
13 Ni nani atakayewadhuru ninyi, ikiwa mwatamani lililo zuri?
Now who is he who will harm you if you become imitators of the good?
14 Lakini kama mkiteseka kwa haki, mmebarikiwa. Msiogope yale ambayo wao wanayaogopa. Msiwe na wasiwasi.
But even if you should suffer for righteousness' sake, you are blessed. “Do not fear what they fear, neither be troubled.”
15 Badala yake, mmuweke Kristo Bwana katika mioyo yenu kama mtakatifu. Kila mara muwe tayari kumjibu kila mtu anayewauliza ninyi kwa nini mna tumaini katika Mungu. Fanyeni hivi kwa upole na heshima.
Rather, sanctify the Lord God in your hearts, and always be ready with an answer for everyone who asks you a reason concerning the hope that is in you, with meekness and respect;
16 Muwe na dhamiri njema ili kwamba watu wanaotukana maisha yenu mema katika Kristo waweze kuaibika kwa sababu wanaongea kinyume dhidi yenu kama kwamba mlikuwa watenda maovu.
keeping a good conscience, so that wherein they speak against you as evildoers, those who revile your good way of life in Christ may be put to shame.
17 Ni vizuri zaidi, ikiwa Mungu anatamani, kwamba mwateseka kwa kufanya mema kuliko kwa kufanya mabaya.
For it is better to suffer for doing good, should the will of God so determine, than for doing evil.
18 Kristo pia aliteseka mara moja kwa ajili ya dhambi. Yeye ambaye ni mwenye haki aliteseka kwa ajili yetu, ambao hatukuwa wenye haki, ili kwamba atulete sisi kwa Mungu. Alikufa katika mwili, lakini alifanywa mzima katika roho.
Because Christ also suffered on account of sins, once for all, the righteous on behalf of the unrighteous, that He might bring us to God; having been put to death, to be sure, in flesh, but having been made alive in spirit;
19 Katika roho, alikwenda na kuzihubiri roho ambazo sasa ziko kifungoni.
in which He also went and made a proclamation to the spirits in prison
20 Hazikuwa tiifu wakati uvumilivu wa Mungu ulipokuwa unasubiri wakati wa Nuhu, siku za ujenzi wa safina, na Mungu aliokoa watu wachache—nafsi nane—kutoka katika maji.
who formerly were disobedient, when the patience of God kept waiting in the days of Noah, while the Ark was being prepared, in which a few, that is eight, souls were brought safely through water.
21 Hii ni alama ya ubatizo unaowaokoa ninyi sasa, siyo kama kuosha uchafu kutoka mwilini, lakini kama ombi la dhamiri njema kwa Mungu, kupitia ufufuo wa Yesu Kristo.
This is an antitype of baptism, that now saves us also (not the removal of physical filth, but the appeal into God from a good conscience) through the resurrection of Jesus Christ,
22 Yeye yuko mkono wa kuume wa Mungu. Alikwenda mbinguni. Malaika, mamlaka, na nguvu lazima vimtii yeye.
who is at the right hand of God, having gone into heaven, angels and authorities and powers having been made subject to Him.