< 1 Petro 2 >

1 Kwa hiyo wekeni pembeni uovu wote, udanganyifu, unafiki, wivu na kashifa.
Rid yourselves therefore of all ill-will and all deceitfulness, of insincerity and envy, and of all evil speaking.
2 Kama watoto wachanga, mtamani maziwa safi ya kiroho, ili kwamba mweze kukua ndani ya wokovu,
Thirst, like newly-born infants, for pure milk for the soul, that by it you may grow up to salvation;
3 kama mmeonja kwamba Bwana ni mwema.
if you have had any experience of the goodness of the Lord.
4 Njoni kwake aliye jiwe hai linaloishi ambalo limekataliwa na watu, lakini hilo limechaguliwa na Mungu na ni la thamani kwake.
Come to Him, the ever-living Stone, rejected indeed by men as worthless, but in God's esteem chosen and held in honour.
5 Ninyi pia ni kama mawe yaliyo hai yanayojengwa juu kuwa nyumba ya kiroho, ili kuwa ukuhani mtakatifu ambao hutoa dhabihu za kiroho zinazokubaliwa kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.
And be yourselves also like living stones that are being built up into a spiritual house, to become a holy priesthood to offer spiritual sacrifices acceptable to God through Jesus Christ.
6 Andiko husema hivi, “Tazama, nimeweka katika Sayuni jiwe la pembeni, kuu na lililochaguliwa na la thamani. Yeyote aaminiye katika yeye hataona aibu”.
For it is contained in Scripture, "See, I am placing on Mount Zion a Cornerstone, chosen, and held in honour, and he whose faith rests on Him shall never have reason to feel ashamed."
7 Hivyo heshima ni yenu kwenu ninyi mnaoamini. Lakini, “jiwe lililokataliwa na wajenzi, hili limekuwa jiwe kuu la pembeni”-
To you believers, therefore, that honour belongs; but for unbelievers-- "A Stone which the builders rejected has been made the Cornerstone,"
8 na, “jiwe la kujikwaa na mwamba wa kujikwaa.”Wao hujikwaa, wanaolikataa neno, kwa lile ambalo pia walikuwa wameteuliwa kwalo.
and "a Stone for the foot to strike against, and a Rock to stumble over." Their foot strikes against it because they are disobedient to God's Message, and to this they were appointed.
9 Lakini ninyi ni ukoo uliochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa miliki ya Mungu, ili kwamba mweze kutangaza matendo ya ajabu ya yule aliyewaita kutoka gizani kuja kwenye nuru yake ya ajabu.
But you are a chosen race, a priesthood of kingly lineage, a holy nation, a people belonging specially to God, that you may make known the perfections of Him who called you out of darkness into His marvellous light.
10 Ninyi kwanza hamkuwa watu, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu. Ninyi hamkupokea rehema, lakini sasa mmepokea rehema.
Once you were not a people, but now you are the people of God. Once you had not found mercy, but now you have.
11 Wapendwa, nimewaita kama wageni na wazurujaji kujinyima kutoka kwenye tamaa mbaya za dhambi, ambazo zinapigana vita na roho zenu.
Dear friends, I entreat you as pilgrims and foreigners not to indulge the cravings of your lower natures: for all such cravings wage war upon the soul.
12 Mnapaswa kuwa na tabia njema kati ya mataifa, ili kwamba, kama watawasema kama kwamba mmefanya mambo maovu, wataziangalia kazi zenu njema na kumsifu Mungu katika siku ya kuja kwake.
Live honourable lives among the Gentiles, in order that, although they now speak against you as evil-doers, they may yet witness your good conduct, and may glorify God on the day of reward and retribution.
13 Tii kila mamlaka ya mwanadamu kwa ajili ya Bwana, ikiwa mfalme kama mkuu,
Submit, for the Lord's sake, to every authority set up by man, whether it be to the Emperor as supreme ruler,
14 ikiwa watawala waliotumwa kuwaadhibu watenda mabaya na kuwasifu wale wanaotenda mema.
or to provincial Governors as sent by him for the punishment of evil-doers and the encouragement of those who do what is right.
15 Kwa kuwa ni mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kufanya mema mwanyamazisha mazungumzo ya kipuuzi ya watu wapumbavu.
For it is God's will that by doing what is right you should thus silence the ignorant talk of foolish persons.
16 Kama watu huru, msiutumie uhuru wenu kama kifuniko kwa maovu, bali muwe kama watumishi wa Mungu.
Be free men, and yet do not make your freedom an excuse for base conduct, but be God's bondservants.
17 Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mwogopeni Mungu. Mweshimuni mfalme.
Honour every one. Love the brotherhood, fear God, honour the Emperor.
18 Watumwa, watiini bwana zenu kwa heshima yote, siyo tu bwana walio wazuri na wapole, lakini pia walio waovu.
Household servants, be submissive to your masters, and show them the utmost respect--not only if they are kind and thoughtful, but also if they are unreasonable.
19 Kwa kuwa ni sifa kama yeyote atavumilia maumivu wakati anapoteseka pasipo haki kwa sababu ya dhamiri yake kwa Mungu.
For it is an acceptable thing with God, if, from a sense of duty to Him, a man patiently submits to wrong, when treated unjustly.
20 Ni faida gani iliyopo kama mwadumu kutenda dhambi kisha mwendelee kuadhibiwa? Lakini kama mmefanya mema na ndipo mteseke kwa kuhukumiwa, hii ni sifa njema kwa Mungu.
If you do wrong and receive a blow for it, what credit is there in your bearing it patiently? But if when you do right and suffer for it you bear it patiently, this is an acceptable thing with God.
21 Kwa hili mliitwa, kwa sababu Kristo pia aliteswa kwa ajili yenu, amewaachia mfano kwa ajili yenu kufuata nyayo zake.
And it is to this you were called; because Christ also suffered on your behalf, leaving you an example so that you should follow in His steps.
22 Yeye hakufanya dhambi, wala haukuonekana udanganyifu wowote kinywani mwake.
He never sinned, and no deceitful language was ever heard from His mouth.
23 Wakati yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano, alipoteseka, hakutisha bali alijitoa mwenyewe kwake Yeye ahukumuye kwa haki.
When He was reviled, He did not answer with reviling; when He suffered He uttered no threats, but left His wrongs in the hands of the righteous Judge.
24 Yeye mwenyewe alizibeba dhambi zetu katika mwili wake kwenye mti, ili kwamba tusiwe na sehemu tena katika dhambi, na kwamba tuishi kwa ajili ya haki. Kwa kupigwa kwake ninyi mmepona.
The burden of our sins He Himself carried in His own body to the Cross and bore it there, so that we, having died so far as our sins are concerned, may live righteous lives. By His wounds yours have been healed.
25 Wote mliokuwa mkitangatanga kama kondoo aliyepotea, lakini sasa mmerudi kwa mchungaji na mlinzi wa roho zenu.
For you were straying like lost sheep, but now you have come back to the Shepherd and Protector of your souls.

< 1 Petro 2 >