< 1 Petro 1 >
1 Petro, mtume wa Yesu Kristo, kwa wageni wa utawanyiko, kwa wateule, katika Ponto yote, Galatia, Kapadokia, Asia, na Bithinia,
panta-gAlAtiyA-kappadakiyA-AziyA-bithuniyAdezeSu pravAsino ye vikIrNalokAH
2 kutokana na ufahamu wa Mungu, Baba, kwa kutakaswa na Roho Mtakatifu, kwa utiifu wa Yesu Kristo, na kwa kunyunyuziwa damu yake. Neema iwe kwenu, na amani yenu iongezeke.
piturIzvarasya pUrvvanirNayAd AtmanaH pAvanena yIzukhrISTasyAjJAgrahaNAya zoNitaprokSaNAya cAbhirucitAstAn prati yIzukhrISTasya preritaH pitaraH patraM likhati| yuSmAn prati bAhulyena zAntiranugrahazca bhUyAstAM|
3 Mungu Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na abarikiwe. Katika ukuu wa rehema yake, alitupa kuzaliwa upya kwa ujasiri wa urithi kupitia ufufuo wa Yesu Kristo kutoka katika wafu,
asmAkaM prabho ryIzukhrISTasya tAta Izvaro dhanyaH, yataH sa svakIyabahukRpAto mRtagaNamadhyAd yIzukhrISTasyotthAnena jIvanapratyAzArtham arthato
4 kwa urithi usioangamia, hautakua na uchafu wala kupungua. Umehihifadhiwa mbinguni kwa ajili yenu.
'kSayaniSkalaGkAmlAnasampattiprAptyartham asmAn puna rjanayAmAsa| sA sampattiH svarge 'smAkaM kRte saJcitA tiSThati,
5 Kwa uwezo wa Mungu mnalindwa kupitia imani kwa wokovu ambao upo tayari kufunuliwa katika nyakati za mwisho.
yUyaJcezvarasya zaktitaH zeSakAle prakAzyaparitrANArthaM vizvAsena rakSyadhve|
6 Furahini katika hili, ingawaje sasa ni lazima kwenu kujisikia huzuni katika majaribu ya aina mbalimbali.
tasmAd yUyaM yadyapyAnandena praphullA bhavatha tathApi sAmprataM prayojanahetoH kiyatkAlaparyyantaM nAnAvidhaparIkSAbhiH klizyadhve|
7 Hii, ni kwa sababu imani yenu iweze kujaribiwa, imani ambayo ni ya thamani kuliko dhahabu, ambayo inapotea katika moto ambao hujaribu imani yenu. Hii hutokea ili imani yenu ipate kuzaa sifa, utukufu, na heshima katika ufunuo wa Yesu Kristo.
yato vahninA yasya parIkSA bhavati tasmAt nazvarasuvarNAdapi bahumUlyaM yuSmAkaM vizvAsarUpaM yat parIkSitaM svarNaM tena yIzukhrISTasyAgamanasamaye prazaMsAyAH samAdarasya gauravasya ca yogyatA prAptavyA|
8 Hamjamuona yeye, lakini mnampenda. Hamumuoni sasa, lakini mnaamini katika yeye na mna furaha isiyoweza kuelezeka kwa furaha ambayo imejawa na utukufu.
yUyaM taM khrISTam adRSTvApi tasmin prIyadhve sAmprataM taM na pazyanto'pi tasmin vizvasanto 'nirvvacanIyena prabhAvayuktena cAnandena praphullA bhavatha,
9 Sasa mnapokea wenyewe matokeo ya imani yenu, wokovu wa nafsi zenu.
svavizvAsasya pariNAmarUpam AtmanAM paritrANaM labhadhve ca|
10 Manabii walitafuta na kuuliza kwa umakini kuhusu wokovu huu, kuhusu neema ambayo ingekuwa yenu.
yuSmAsu yo 'nugraho varttate tadviSaye ya IzvarIyavAkyaM kathitavantaste bhaviSyadvAdinastasya paritrANasyAnveSaNam anusandhAnaJca kRtavantaH|
11 Walitafuta kujua ni aina gani ya wokovu ambao ungekuja. Walitafuta pia kujua ni muda gani Roho wa Kristo aliye ndani yao alikuwa anazungumza nini nao. Hii ilikua inatokea wakati alipokuwa anawaambia mapema kuhusu mateso ya Kristo na utukufu ambao ungemfuata.
vizeSatasteSAmantarvvAsI yaH khrISTasyAtmA khrISTe varttiSyamANAni duHkhAni tadanugAmiprabhAvaJca pUrvvaM prAkAzayat tena kaH kIdRzo vA samayo niradizyataitasyAnusandhAnaM kRtavantaH|
12 Ilifunuliwa kwa manabii kwamba walikua wanayatumikia mambo haya, na si kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yenu - masimulizi ya mambo haya kupitia wale wanaoleta injili kwenu kwa njia ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, mambo ambayo hata malaika wanatamani kufunuliwa kwake.
tatastai rviSayaiste yanna svAn kintvasmAn upakurvvantyetat teSAM nikaTe prAkAzyata| yAMzca tAn viSayAn divyadUtA apyavanataziraso nirIkSitum abhilaSanti te viSayAH sAmprataM svargAt preSitasya pavitrasyAtmanaH sahAyyAd yuSmatsamIpe susaMvAdapracArayitRbhiH prAkAzyanta|
13 Kwa hiyo fungeni viuno vya akili zenu. Muwe watulivu katika fikra zenu. Muwe na ujasiri mkamilifu katika neema ambayo italetwa kwenu wakati wa kufunuliwa kwa Yesu Kristo.
ataeva yUyaM manaHkaTibandhanaM kRtvA prabuddhAH santo yIzukhrISTasya prakAzasamaye yuSmAsu varttiSyamAnasyAnugrahasya sampUrNAM pratyAzAM kuruta|
14 Kama watoto watiifu, msifungwe wenyewe na tamaa ambazo mlizifuata wakati mlipokua hamna ufahamu.
aparaM pUrvvIyAjJAnatAvasthAyAH kutsitAbhilASANAM yogyam AcAraM na kurvvanto yuSmadAhvAnakArI yathA pavitro 'sti
15 Lakini kama vile aliyewaita alivyo mtakatifu, nanyi, pia, muwe watakatifu katika tabia yenu yote maishani.
yUyamapyAjJAgrAhisantAnA iva sarvvasmin AcAre tAdRk pavitrA bhavata|
16 Kwa kuwa imeandkwa, “Iweni watakatifu, kwa sababu Mimi ni mtakatifu.”
yato likhitam Aste, yUyaM pavitrAstiSThata yasmAdahaM pavitraH|
17 Na kama mkiita “Baba” yule ahukumuye kwa haki kulingana na kazi ya kila mtu, tumia muda wa safari yako katika unyenyekevu.
aparaJca yo vinApakSapAtam ekaikamAnuSasya karmmAnusArAd vicAraM karoti sa yadi yuSmAbhistAta AkhyAyate tarhi svapravAsasya kAlo yuSmAbhi rbhItyA yApyatAM|
18 Mnafahamu kwamba haikuwa kwa fedha au dhahabu - vitu vinavyoharibika- ambavyo mmekombolewa kutoka kwenye tabia zenu za ujinga ambazo mlijifunza kutoka kwa baba zenu.
yUyaM nirarthakAt paitRkAcArAt kSayaNIyai rUpyasuvarNAdibhi rmuktiM na prApya
19 Lakini mmekombolewa kwa damu ya heshima ya Kristo, kama ya kondoo asiye na hila wala doa.
niSkalaGkanirmmalameSazAvakasyeva khrISTasya bahumUlyena rudhireNa muktiM prAptavanta iti jAnItha|
20 Kristo alichaguliwa kabla ya misingi ya dunia, lakini sasa siku hizi za mwisho, amefunuliwa kwenu.
sa jagato bhittimUlasthApanAt pUrvvaM niyuktaH kintu caramadineSu yuSmadarthaM prakAzito 'bhavat|
21 Mnamwamini Mungu kupitia yeye, ambaye Mungu alimfufua toka kwa wafu na ambaye alimpa utukufu ili kwamba imani yenu na ujasiri uwe katika Mungu.
yatastenaiva mRtagaNAt tasyotthApayitari tasmai gauravadAtari cezvare vizvasitha tasmAd Izvare yuSmAkaM vizvAsaH pratyAzA cAste|
22 Mmefanya nafsi zenu kuwa safi kwa utii wa ile kweli, kwa dhumuni la pendo la kidugu lililo na unyofu, hivyo pendaneni kwa bidii toka moyoni.
yUyam AtmanA satyamatasyAjJAgrahaNadvArA niSkapaTAya bhrAtRpremne pAvitamanaso bhUtvA nirmmalAntaHkaraNaiH parasparaM gADhaM prema kuruta|
23 Mmekwisha zaliwa mara ya pili, si kwa mbegu iharibikayo, lakini kutoka katika mbegu isiyoharibika, kupitia uzima na neno la Mungu lililosalia. (aiōn )
yasmAd yUyaM kSayaNIyavIryyAt nahi kintvakSayaNIyavIryyAd Izvarasya jIvanadAyakena nityasthAyinA vAkyena punarjanma gRhItavantaH| (aiōn )
24 Kwa maana “miili yote ni kama majani, na utukufu wake wote ni kama ua la jani. Jani hunyauka, na ua hudondoka,
sarvvaprANI tRNaistulyastattejastRNapuSpavat| tRNAni parizuSyati puSpANi nipatanti ca|
25 lakini neno la Bwana hubakia milele.” Huu ni ujumbe ambao ulitangazwa kama injili kwenu. (aiōn )
kintu vAkyaM parezasyAnantakAlaM vitiSThate| tadeva ca vAkyaM susaMvAdena yuSmAkam antike prakAzitaM| (aiōn )