< 1 Wafalme 1 >

1 Mfalme Daudi alipokuwa mzee sana, walimfunika kwa nguo, lakini hakupata joto.
And the king David he was old he had come in days and they covered him with clothes and not it was warm to him.
2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Na tutafute msichana bikra kwa ajili ya mfalme bwana wetu. Ili amtumikie na kumtunza. Naye atalala kwenye mikono yake ili bwana mfalme wetu apate joto.
And they said to him servants his let people seek for lord my the king a young woman a virgin and she will stand before the king and let her be of him a nurse and she will lie in bosom your and it will be warm to lord my the king.
3 Kwa hiyo wakatafuta msichana mrembo katika mipaka yote ya Israeli. Wakampata Abishagi Mshunami wakamlte kwa mfalme.
And they sought a young woman beautiful in all [the] territory of Israel and they found Abishag the Shunammite and they brought her to the king.
4 Yule msichana alikuwa mrembo sana. Naye akamtumikia mfalme na kumtunza, Lakini mfalme hakumjua.
And the young woman [was] beautiful up to muchness and she became of the king a nurse and she served him and the king not he knew her.
5 Wakati huo, Adoniya mwana wa Hagithi alijiinua akisema, “Nitakuwa mfalme.” Kwa hiyo akajiandalia magari na wapanda farasi hamsini ili wapige mbio mbele yake.
And Adonijah [the] son of Haggith [was] exalting himself saying I I will become king and he acquired for himself a chariot and horsemen and fifty man [were] running before him.
6 Baba yake alikuwa hajawahi kumsumbua, kwa kusema, “kwa nini umefanya hili na lile?” Adoniya allikuwa mwanamume mzuri sana aliyezaliwa baada ya Absalomu.
And not he had rebuked him father his from days his saying why? thus have you done and also he [was] good of appearance very and him someone bore after Absalom.
7 Akashauriana na Yoabu mwana wa Seruya na Abiathari kuhani. Wakamfuata Adoniya wakamsaidia.
And they were words his with Joab [the] son of Zeruiah and with Abiathar the priest and they helped after Adonijah.
8 Lakini Sadoki kuhani, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Nathani, Shimei, Rei, na watu mashujaa wa Daudi hawakumfuata Adoniya.
And Zadok the priest and Benaiah [the] son of Jehoiada and Nathan the prophet and Shimei and Rei and the mighty [men] who [belonged] to David not they were with Adonijah.
9 Adoniya akataoa dhabihu za Kondoo, na ndama walionona kwenye jiwe la Sohelethi, ambalo liko karibu na Eni Rogeli. Akawakaribisha ndugu zake wote, watoto wa mfalme, wanaume wote wa Yuda, na watumishi wa mfalme.
And he sacrificed Adonijah sheep and cattle and fatling near [the] stone of Zoheleth which [was] beside En Rogel and he invited all brothers his [the] sons of the king and all [the] men of Judah [the] servants of the king.
10 Lakini hakumkaribisha nabii Nathan, Benaya, wanaume mashujaa, au ndugu yake Sulemani.
And Nathan the prophet and Benaiah and the mighty [men] and Solomon brother his not he invited.
11 Kisha Nathani akamwambia Bethisheba mama wa Sulemani, akaisema, “Je, haujasikia kuwa Adoniya mwana wa Hagathi amekuwa mfalme, na Daudi bwana wetu halijui hilo?
And he said Nathan to Bath-sheba [the] mother of Solomon saying ¿ not have you heard that he has become king Adonijah [the] son of Haggith and lord our David not he knows.
12 Kwa hiyo sasa nakupa ushauri, ili kwamba uweze kuokoa maisha yako na maisha ya mwanao Suleimani.
And therefore come let me counsel you please counsel and save life your and [the] life of son your Solomon.
13 Nenda kwa mfalme Daudi; ukamwambie, 'Bwana wangu mfalme, Je, haukumwapia mtumishi wako, ukisema, “Hakika Sulemani mwanao atatawala baada yangu, na ataketi kwenye kiti changu cha enzi?” Kwa nini basi Adoniya anatawala?'
Come and go - to the king David and you will say to him ¿ not you O lord my the king did you swear an oath to maidservant your saying that Solomon son your he will reign after me and he he will sit on throne my and why? has he become king Adonijah.
14 Wakati ukiwa pale ukiongea na mfalme, Nitaingia baada yako na kuthibitisha hayo.
There! still you [are] speaking there with the king and I I will come after you and I will confirm words your.
15 Kwa hiyo Bathisheba akaingia chumbani kwa mfalme. Wakati huo mfalme alikuwa mzee sana, na Abishagi Mshunami alikuwa akimtunza mfalme.
And she went Bath-sheba to the king the room towards and the king he was old very and Abishag the Shunammite [was] serving the king.
16 Bathisheba akaiinama kifudifudi mbele ya mfalme. Na kisha mfalme akasema, “Una haja gani?”
And she bowed low Bath-sheba and she bowed down to the king and he said the king what? [is] to you.
17 Naye akamwambia, “Bwana wangu, ulimwapia mtumishi wako kwa jina la BWANA, Mungu wako, ukisema, 'Hakika Sulemani mwanao atatawala, baada yangu, naye ataketi kwenye kiti changu cha enzi.'
And she said to him O lord my you you swore an oath by Yahweh God your to maidservant your that Solomon son your he will reign after me and he he will sit on throne my.
18 Sasa, tazama, Adoniya ni mfalme, na bwana wangu mfalme hajui jambo hili.
And now here! Adonijah he has become king and now O lord my the king not you know.
19 Ametoa dhabihu ya makisai, ndama walionona, na kondoo wengi, na amewakaribisha wana wote wa mfalme, Abiathari kuhani, na Yoabu jemedari wa jeshi, lakini hajamkaribisha Sulemani mtumishi wako.
And he has sacrificed ox[en] and fatling and sheep to abundance and he has invited all [the] sons of the king and Abiathar the priest and Joab [the] commander of the army and Solomon servant your not he has invited.
20 Mfalme bwana wangu, macho yote ya Israeli yako kwako, yakisubiri usemi wako juu ya nani atakayeti kwenye kiti cha enzi baada yako, bwana wangu.
And you O lord my the king [the] eyes of all Israel [are] on you to tell to them who? will he sit on [the] throne of lord my the king after him.
21 Vinginevyo itatokea, wakati bwana wangu atakapolala na baba zake, kwamba Mimi na mwanangu Sulemani kuhesabiwa wahaini.”
And it will be when lies down lord my the king with ancestors his and I will be I and son my Solomon sinners.
22 Wakati alipokuwa akiendelea na mfalme, nabii Nathani aliingia.
And there! still she [was] speaking with the king and Nathan the prophet he came.
23 Watumshi wakamwambia mfalme, “Nabii Nathani yuko hapa,” Naye alipoingia mbele ya mfalme, akalala kifudifudi mbele ya mfalme na uso wake ukielekea chini.
And people told to the king saying here! Nathan the prophet and he came before the king and he bowed down to the king on face his [the] ground towards.
24 Nathani akamwambia, “Mfalme bwana wangu, Je, umesema, Adoniya atatawala baada yangu, na ataketi kwenye kiti changu cha enzi?
And he said Nathan O lord my the king you have you said? Adonijah he will reign after me and he he will sit on throne my.
25 kwani leo ameshuka na ametoa dhabihu ya makisai, ndama walionona, na kondoo wengi, na amewakaribisha wana wote wa mfalme, jemedari wa jeshi, na Abiatahari kuhani. Nao wanakuka na kunywa mbele zake, na kusema, 'Mfalme Adoniya na aishi milele!'
For - he has gone down this day and he has sacrificed ox[en] and fatling and sheep to abundance and he has invited all [the] sons of the king and [the] commanders of the army and Abiathar the priest and there they [are] eating and drinking before him and they have said may he live the king Adonijah.
26 Lakini mimi, mtumishi wako, Sadoki kuhani, Benaya mwana wa Yehoyada, na mtumishi wako Suleimani, hajatukaribisha.
And me I servant your and Zadok the priest and Benaiah [the] son of Jehoiada and Solomon servant your not he has invited.
27 Je, bwana wangu mfalme amefanya haya pasipo kutuambia sisi, watumishi wako, ni nani atakayeketi kwenye kiti cha enzi baada yake?”
From with lord my the king has it occurred the matter this and not you made known (servant your *Q(K)*) who? will he sit on [the] throne of lord my the king after him.
28 Ndipo mfalme Daudi lipojibu na kusema, “Mwiteni Bathisheba arudi.” Naye akaja akasimama mbele ya mfalme.
And he answered the king David and he said summon for me Bath-sheba and she came before the king and she stood before the king.
29 Mfalme akafanya kiapo akasema, “Kama BWANA aishivyo, ambaye ameniokoa toka tabu zote,
And he swore an oath the king and he said [by] [the] life of Yahweh who he has ransomed life my from every trouble.
30 kama nilivyokuapia kwa BWANA, Mungu wa Israeli, nikisema, 'Sulemani mwanao atatawala baada yangu, naye ndiye atakayeketi kwenye kiti changu cha enzi, mahali pangu,' Nitafanya hivi leo.”
For just as I swore to you by Yahweh [the] God of Israel saying that Solomon son your he will reign after me and he he will sit on throne my in place of me for so I will do the day this.
31 Kisha Bathisheba akalala kifudifudi na sura yake ikielekea chini mbele ya mfalme akasema, “Bwana wangu mfalme Daudi n a aishi milele!”
And she bowed low Bath-sheba face ground and she bowed down to the king and she said may he live lord my the king David for ever.
32 Mflme Daudi akasema, “Niitieni Sadoki kuhani, nabii Nathani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Nao wakaja mbele ya mfalme.
And he said - the king David summon for me Zadok the priest and Nathan the prophet and Benaiah [the] son of Jehoiada and they came before the king.
33 Mfalme akawaambia, “Uwachukue watumishi wangu, bwana wako, na umfanye Sulemani mwanangu apande juu ya nyumba yangu mimi na mkamtelemshe mpaka chini Gihoni.
And he said the king to them take with you [the] servants of lord your and you will cause to ride Solomon son my on the mule which [belongs] to me and you will take down him to Gihon.
34 Na Sadoki kuhani na nabii Nathani wamtawaze awe mfalme wa Israeli na tarumbeta zipigwe, 'Mfalme Suleimani na uishi milele!'
And he will anoint him there Zadok the priest and Nathan the prophet to king over Israel and you will give a blast on the ram's horn and you will say may he live the king Solomon.
35 Kisha njoni mkiwa nyuma yake, naye atakuja na kukaa kwenye kiti changu cha enzi; kwani yeye ndiye atakayekuwa mfalme mahali pangu. Nimemchagua yeye kuwa mtawala wa Israeli na Yuda.”
And you will come up after him and he will come and he will sit on throne my and he he will reign in place of me and him I have appointed to be ruler over Israel and over Judah.
36 Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme, akasema, “Na iwe hivyo! Na BWANA, Mungu wa mfalme bwana wangu, alithibitishe hilo.
And he answered Benaiah [the] son of Jehoiada the king and he said - amen thus may he say Yahweh [the] God of lord my the king.
37 Kama vile BWANA alivyokuwa na mfalme bwana wangu na awe na Sulemani hivyo hivyo, na kuifanya enzi yake kuwa kubwa kuliko zaidi ya enzi ya bwana wangu Daudi.”
Just as he has been Yahweh with lord my the king so (he will be *Q(K)*) with Solomon and may he make great throne his more than [the] throne of lord my the king David.
38 Kwa hiyo Sadoki kuhani, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakerethi na Wapelethi wakamfanya Sulemani akapanda juu ya nyumba ya mfalme Daudi; wakamleta Gihoni.
And he went down Zadok the priest and Nathan the prophet and Benaiah [the] son of Jehoiada and the Kerethite[s] and the Pelethite[s] and they caused to ride Solomon on [the] mule of the king David and they brought him to Gihon.
39 Naye Sadoki kuhani akachukua pembe lenye mafuta hemani akamtia mafuta Sulemani kisha wakapiga tarumbeta, na watu wote wakasema, 'Mfalme Sulemani na aishi milele!'
And he took Zadok the priest [the] horn of oil from the tent and he anointed Solomon and they gave a blast on the ram's horn and they said all the people may he live the king Solomon.
40 Kisha watu wote wakamfuata, na watu wakapiga zomari wakafurahi furaha kubwa mno, kiasi kwamba dunia ikatetemeka kwa sauti zao.
And they went up all the people after him and the people [were] playing [the] flute with flutes and joyful joy great and it was split open the earth by noise their.
41 Kisha Adoniya na wageni wake waliokuwa pamoja naye wakasikia hayo walipomaliza kula. Yoabu alipozisikia sauti za panda, akasema, “Kwa nini jiji lilko katika hali ya taharuki?”
And he heard Adonijah and all those [who] were invited who [were] with him and they they had finished to eat and he heard Joab [the] sound of the ram's horn and he said why? [is] [the] sound of the town in an uproar.
42 Wakati alipokuwa akiongea, Yonatahani mwana wa Abiathari kuhani alifika. Adoniya akamwambia, “Karibu, 'kwa kuwa wewe wastahili kutuletea habari.”
Still he [was] speaking and there! Jonathan [the] son of Abiathar the priest he came and he said Adonijah come for [are] a man of worth you and good you bear news.
43 Naye Yonathani akamjibu Adoniya, “Mfalme bwana wetu Daudi amemfanya Sulemani kuwa mfalme.
And he answered Jonathan and he said to Adonijah indeed lord our the king David he has made king Solomon.
44 Na mfalme amemtuma pamoja naye Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakerethi pamoja na Wapelethi. Wamempandisha Sulemani juu ya nyumba ya mfalme.
And he has sent with him the king Zadok the priest and Nathan the prophet and Benaiah [the] son of Jehoiada and the Kerethite[s] and the Pelethite[s] and they have caused to ride him on [the] mule of the king.
45 Sadoki kuhani na nabii Nathani wamemtawaza kuwa mfalme kule Gihoni, na wametokea huko wakifurahi, ndiyo maana jiji liko katika taharuki. Na hizi ndizo sauti ulizosikia.
And they have anointed him Zadok the priest and Nathan the prophet to king at Gihon and they have gone up from there joyful and it was excited the town that [is] the noise which you have heard.
46 Pia, Sulemani ameketi kwenye kiti cha enzi cha ufalme.
And also he has sat Solomon on [the] throne of royalty.
47 Zaidi ya yote, watumishi wa mfalme walikuja kumbariki mfalme bwana wetu Daudi, wakisema, 'Mungu wako na alifanye jina la Sulemani kuwa zuri kuliko jina lako, na kuifanya enzi yako kuwa kubwa kuliko yako.' na mfalme akasujudu mwenyewe kitandani.
And also they have come [the] servants of the king to bless lord our the king David saying may he make good (God *Q(K)*) [the] name of Solomon more than name your and may he make great throne his more than throne your and he bowed down the king on the bed.
48 Mfalme pia alisema, 'Abarikiwe BWANA, Mungu wa Israeli, ambaye amempa mtu kuketi kwenye enzi yangu siku hii ya leo, na kwamba macho yangu yamejionea hilo.'”
And also thus he has said the king [be] blessed Yahweh [the] God of Israel who he has given this day [one who] sits on throne my and own eyes my [are] seeing.
49 Ndipo wageni wote wa Adoniya walipoogopa sana. Wakasimama na kila mtu akaenda njia yake.
And they trembled and they rose up all those [who] were invited who [belonged] to Adonijah and they went each to way his.
50 Pia Adoniya alimwaogopa Sulemani na akasimama, na akaondoka, akachukua pembe la madhabahuni.
And Adonijah he was afraid of Solomon and he arose and he went and he took hold on [the] horns of the altar.
51 Kisha Sulemani akaambiwa hilo, wakasema, “Tazama, Adoniya amemwogopa mfalme Sulemani, kwa kuwa ameshikilia pembe la madhabahuni, akisema, 'Mfalme Sulemani na aniapie kwanza kuwa hatamwua mtumishi wake kwa upanga.'”
And it was told to Solomon saying there! Adonijah he fears the king Solomon and there! he has taken hold on [the] horns of the altar saying let him swear to me as the day the king Solomon if he will put to death servant his by the sword.
52 Sulemani akasema, “Kama atajionyesha kuwa ni mtu wa kweli, hakuna hata unywele mmoja utakaoanguka duniani, bali kama uovu utaonekana kwake, atakufa.”
And he said Solomon if he will become a son of worth not it will fall one of hair[s] his [the] ground towards and if evil it will be found in him and he will die.
53 Kwa hiyo mfalme Sulemani akatuma watu, waliomleta Adoniya kutoka madhabahuni. Naye akaja akapiga magoti kwa Sulemani, na Sulemani akamwambia, “Nenda nyumbani kwako.”
And he sent the king Solomon and they brought down him from at the altar and he came and he bowed down to the king Solomon and he said to him Solomon go to house your.

< 1 Wafalme 1 >