< 1 Wafalme 1 >
1 Mfalme Daudi alipokuwa mzee sana, walimfunika kwa nguo, lakini hakupata joto.
Now king David had become elderly, and he had many days in his lifetime. And though he was covered with clothes, he was not warmed.
2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Na tutafute msichana bikra kwa ajili ya mfalme bwana wetu. Ili amtumikie na kumtunza. Naye atalala kwenye mikono yake ili bwana mfalme wetu apate joto.
Therefore, his servants said to him: “Let us seek, for our lord the king, a young virgin. And let her stand before the king, and warm him, and sleep in his bosom, and provide warmth for our lord the king.”
3 Kwa hiyo wakatafuta msichana mrembo katika mipaka yote ya Israeli. Wakampata Abishagi Mshunami wakamlte kwa mfalme.
And so they sought a beautiful young woman in all the parts of Israel. And they found Abishag, a Shunammite, and they led her to the king.
4 Yule msichana alikuwa mrembo sana. Naye akamtumikia mfalme na kumtunza, Lakini mfalme hakumjua.
Now the girl was exceedingly beautiful. And she slept with the king, and she ministered to him. Yet truly, the king did not know her.
5 Wakati huo, Adoniya mwana wa Hagithi alijiinua akisema, “Nitakuwa mfalme.” Kwa hiyo akajiandalia magari na wapanda farasi hamsini ili wapige mbio mbele yake.
Then Adonijah, the son of Haggith, exalted himself, saying, “I shall reign!” And he appointed for himself chariots and horsemen, with fifty men who would run before him.
6 Baba yake alikuwa hajawahi kumsumbua, kwa kusema, “kwa nini umefanya hili na lile?” Adoniya allikuwa mwanamume mzuri sana aliyezaliwa baada ya Absalomu.
Neither did his father chastise him at any time, saying, “Why have you done this?” Now he, too, was very beautiful, the second in birth, after Absalom.
7 Akashauriana na Yoabu mwana wa Seruya na Abiathari kuhani. Wakamfuata Adoniya wakamsaidia.
And he conferred with Joab, the son of Zeruiah, and with Abiathar, the priest, who gave assistance to the side of Adonijah.
8 Lakini Sadoki kuhani, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Nathani, Shimei, Rei, na watu mashujaa wa Daudi hawakumfuata Adoniya.
Yet truly, Zadok, the priest, and Benaiah, the son of Jehoiada, and Nathan, the prophet, and Shimei and Rei, and the mature men of the army of David were not with Adonijah.
9 Adoniya akataoa dhabihu za Kondoo, na ndama walionona kwenye jiwe la Sohelethi, ambalo liko karibu na Eni Rogeli. Akawakaribisha ndugu zake wote, watoto wa mfalme, wanaume wote wa Yuda, na watumishi wa mfalme.
Then Adonijah, having immolated rams and calves and every kind of fat cattle beside the Stone of the Serpent, which was in the vicinity of the fountain Rogel, summoned all his brothers, the sons of the king, and all the men of Judah, the servants of the king.
10 Lakini hakumkaribisha nabii Nathan, Benaya, wanaume mashujaa, au ndugu yake Sulemani.
But he did not summon Nathan, the prophet, and Benaiah, and all the mature men, and Solomon, his brother.
11 Kisha Nathani akamwambia Bethisheba mama wa Sulemani, akaisema, “Je, haujasikia kuwa Adoniya mwana wa Hagathi amekuwa mfalme, na Daudi bwana wetu halijui hilo?
And so Nathan said to Bathsheba, the mother of Solomon: “Have you not heard that Adonijah, the son of Haggith, has begun to reign, and that our lord David is ignorant of this?
12 Kwa hiyo sasa nakupa ushauri, ili kwamba uweze kuokoa maisha yako na maisha ya mwanao Suleimani.
Now then, come, accept my counsel, and save your life and the life of your son Solomon.
13 Nenda kwa mfalme Daudi; ukamwambie, 'Bwana wangu mfalme, Je, haukumwapia mtumishi wako, ukisema, “Hakika Sulemani mwanao atatawala baada yangu, na ataketi kwenye kiti changu cha enzi?” Kwa nini basi Adoniya anatawala?'
Go and enter to king David, and say to him: ‘Did you not, my lord the king, swear to me, your handmaid, saying: “Your son Solomon shall reign after me, and he himself shall sit on my throne?” Then why does Adonijah reign?’
14 Wakati ukiwa pale ukiongea na mfalme, Nitaingia baada yako na kuthibitisha hayo.
And while you are still speaking with the king there, I will enter after you, and I will complete your words.”
15 Kwa hiyo Bathisheba akaingia chumbani kwa mfalme. Wakati huo mfalme alikuwa mzee sana, na Abishagi Mshunami alikuwa akimtunza mfalme.
And so Bathsheba entered to the king in the bedroom. Now the king was very old, and Abishag, the Shunammite, was ministering to him.
16 Bathisheba akaiinama kifudifudi mbele ya mfalme. Na kisha mfalme akasema, “Una haja gani?”
Bathsheba bowed herself, and she reverenced the king. And the king said to her, “What do you wish?”
17 Naye akamwambia, “Bwana wangu, ulimwapia mtumishi wako kwa jina la BWANA, Mungu wako, ukisema, 'Hakika Sulemani mwanao atatawala, baada yangu, naye ataketi kwenye kiti changu cha enzi.'
And responding, she said: “My lord, you swore to your handmaid, by the Lord your God: ‘your son Solomon will reign after me, and he himself shall sit upon my throne.’
18 Sasa, tazama, Adoniya ni mfalme, na bwana wangu mfalme hajui jambo hili.
And now behold, Adonijah reigns, while you, my lord the king, are ignorant of it.
19 Ametoa dhabihu ya makisai, ndama walionona, na kondoo wengi, na amewakaribisha wana wote wa mfalme, Abiathari kuhani, na Yoabu jemedari wa jeshi, lakini hajamkaribisha Sulemani mtumishi wako.
He has slain oxen, and every kind of fattened cattle, and many rams. And he has summoned all the sons of the king, as well as Abiathar, the priest, and Joab, the leader of the military. But Solomon, your servant, he did not summon.
20 Mfalme bwana wangu, macho yote ya Israeli yako kwako, yakisubiri usemi wako juu ya nani atakayeti kwenye kiti cha enzi baada yako, bwana wangu.
Truly now, my lord the king, the eyes of all of Israel look with favor upon you, that you may indicate to them who ought to sit upon your throne, my lord the king, after you.
21 Vinginevyo itatokea, wakati bwana wangu atakapolala na baba zake, kwamba Mimi na mwanangu Sulemani kuhesabiwa wahaini.”
Otherwise, this will be: when my lord the king sleeps with his fathers, I and my son Solomon will be as sinners.”
22 Wakati alipokuwa akiendelea na mfalme, nabii Nathani aliingia.
And while she was still speaking with the king, Nathan, the prophet, arrived.
23 Watumshi wakamwambia mfalme, “Nabii Nathani yuko hapa,” Naye alipoingia mbele ya mfalme, akalala kifudifudi mbele ya mfalme na uso wake ukielekea chini.
And they announced to the king, saying, “Nathan, the prophet, is here.” And when he had entered in the sight of the king, and he had reverenced prone on the ground,
24 Nathani akamwambia, “Mfalme bwana wangu, Je, umesema, Adoniya atatawala baada yangu, na ataketi kwenye kiti changu cha enzi?
Nathan said: “My lord the king, did you say, ‘Let Adonijah reign after me, and let him sit upon my throne?’
25 kwani leo ameshuka na ametoa dhabihu ya makisai, ndama walionona, na kondoo wengi, na amewakaribisha wana wote wa mfalme, jemedari wa jeshi, na Abiatahari kuhani. Nao wanakuka na kunywa mbele zake, na kusema, 'Mfalme Adoniya na aishi milele!'
For today, he descended, and he immolated oxen, and fattened cattle, and many rams. And he summoned all the sons of the king, and the leaders of the army, along with Abiathar, the priest. And they are eating and drinking before him, and saying, ‘As king Adonijah lives.’
26 Lakini mimi, mtumishi wako, Sadoki kuhani, Benaya mwana wa Yehoyada, na mtumishi wako Suleimani, hajatukaribisha.
But he did not summon me, your servant, and Zadok, the priest, and Benaiah, the son of Jehoiada, and Solomon, your lowly servant.
27 Je, bwana wangu mfalme amefanya haya pasipo kutuambia sisi, watumishi wako, ni nani atakayeketi kwenye kiti cha enzi baada yake?”
Could this word have gone out from my lord the king, and could you not have revealed it to me, your servant, as to who would be seated upon the throne of my lord the king after him?”
28 Ndipo mfalme Daudi lipojibu na kusema, “Mwiteni Bathisheba arudi.” Naye akaja akasimama mbele ya mfalme.
And king David responded, saying, “Summon to me Bathsheba.” And when she had entered before the king, and she had stood before him,
29 Mfalme akafanya kiapo akasema, “Kama BWANA aishivyo, ambaye ameniokoa toka tabu zote,
the king swore and said: “As the Lord lives, who has rescued my soul from all distress,
30 kama nilivyokuapia kwa BWANA, Mungu wa Israeli, nikisema, 'Sulemani mwanao atatawala baada yangu, naye ndiye atakayeketi kwenye kiti changu cha enzi, mahali pangu,' Nitafanya hivi leo.”
just as I swore to you by the Lord God of Israel, saying: ‘Your son Solomon shall reign after me, and he himself shall sit upon my throne in my place,’ so shall I do this day.”
31 Kisha Bathisheba akalala kifudifudi na sura yake ikielekea chini mbele ya mfalme akasema, “Bwana wangu mfalme Daudi n a aishi milele!”
And Bathsheba, having lowered her face to the ground, reverenced the king, saying, “May my lord David live forever.”
32 Mflme Daudi akasema, “Niitieni Sadoki kuhani, nabii Nathani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Nao wakaja mbele ya mfalme.
And king David said, “Summon to me Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, and Benaiah, the son of Jehoiada.” And when they had entered before the king,
33 Mfalme akawaambia, “Uwachukue watumishi wangu, bwana wako, na umfanye Sulemani mwanangu apande juu ya nyumba yangu mimi na mkamtelemshe mpaka chini Gihoni.
he said to them: “Take with you the servants of your lord, and place my son Solomon upon my mule. And lead him to Gihon.
34 Na Sadoki kuhani na nabii Nathani wamtawaze awe mfalme wa Israeli na tarumbeta zipigwe, 'Mfalme Suleimani na uishi milele!'
And let Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, anoint him in that place as the king over Israel. And you shall sound the trumpet, and you shall say, ‘As king Solomon lives.’
35 Kisha njoni mkiwa nyuma yake, naye atakuja na kukaa kwenye kiti changu cha enzi; kwani yeye ndiye atakayekuwa mfalme mahali pangu. Nimemchagua yeye kuwa mtawala wa Israeli na Yuda.”
And you shall ascend after him, and he shall arrive and shall sit upon my throne. And he himself shall reign in my place. And I will command that he be the ruler over Israel and over Judah.”
36 Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme, akasema, “Na iwe hivyo! Na BWANA, Mungu wa mfalme bwana wangu, alithibitishe hilo.
And Benaiah, the son of Jehoiada, responded to the king, saying: “Amen. So says the Lord, the God of my lord the king.
37 Kama vile BWANA alivyokuwa na mfalme bwana wangu na awe na Sulemani hivyo hivyo, na kuifanya enzi yake kuwa kubwa kuliko zaidi ya enzi ya bwana wangu Daudi.”
In the same way that the Lord has been with my lord the king, so may he be with Solomon. And may he make his throne more sublime than the throne of my lord, king David.”
38 Kwa hiyo Sadoki kuhani, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakerethi na Wapelethi wakamfanya Sulemani akapanda juu ya nyumba ya mfalme Daudi; wakamleta Gihoni.
Then Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, descended, with Benaiah, the son of Jehoiada, and the Cherethites and Pelethites. And they placed Solomon on the mule of king David, and they led him to Gihon.
39 Naye Sadoki kuhani akachukua pembe lenye mafuta hemani akamtia mafuta Sulemani kisha wakapiga tarumbeta, na watu wote wakasema, 'Mfalme Sulemani na aishi milele!'
And Zadok, the priest, took the horn of oil from the tabernacle, and he anointed Solomon. And they sounded the trumpet. And all the people said, “As king Solomon lives.”
40 Kisha watu wote wakamfuata, na watu wakapiga zomari wakafurahi furaha kubwa mno, kiasi kwamba dunia ikatetemeka kwa sauti zao.
And the entire multitude ascended after him. And the people were playing on pipes, and rejoicing with great joy. And the earth resounded before the noise of them.
41 Kisha Adoniya na wageni wake waliokuwa pamoja naye wakasikia hayo walipomaliza kula. Yoabu alipozisikia sauti za panda, akasema, “Kwa nini jiji lilko katika hali ya taharuki?”
Then Adonijah, and all who had been summoned by him, heard it. And now the feast had ended. Then, too, Joab, hearing the voice of the trumpet, said, “What is the meaning of this clamor from the tumultuous city?”
42 Wakati alipokuwa akiongea, Yonatahani mwana wa Abiathari kuhani alifika. Adoniya akamwambia, “Karibu, 'kwa kuwa wewe wastahili kutuletea habari.”
While he was still speaking, Jonathan, the son of Abiathar the priest, arrived. And Adonijah said to him, “Enter, for you are a valiant man, and you report good news.”
43 Naye Yonathani akamjibu Adoniya, “Mfalme bwana wetu Daudi amemfanya Sulemani kuwa mfalme.
And Jonathan answered Adonijah: “By no means. For our lord king David has appointed Solomon as king.
44 Na mfalme amemtuma pamoja naye Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakerethi pamoja na Wapelethi. Wamempandisha Sulemani juu ya nyumba ya mfalme.
And he has sent with him Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, and Benaiah, the son of Jehoiada, and the Cherethites and Pelethites. And they have placed him on the mule of the king.
45 Sadoki kuhani na nabii Nathani wamemtawaza kuwa mfalme kule Gihoni, na wametokea huko wakifurahi, ndiyo maana jiji liko katika taharuki. Na hizi ndizo sauti ulizosikia.
And Zadok, the priest, and Nathan, the prophet, have anointed him king, at Gihon. And they are ascending from there, rejoicing, and so the city resounds. This is the noise that you have heard.
46 Pia, Sulemani ameketi kwenye kiti cha enzi cha ufalme.
But also, Solomon sits upon the throne of the kingdom.
47 Zaidi ya yote, watumishi wa mfalme walikuja kumbariki mfalme bwana wetu Daudi, wakisema, 'Mungu wako na alifanye jina la Sulemani kuwa zuri kuliko jina lako, na kuifanya enzi yako kuwa kubwa kuliko yako.' na mfalme akasujudu mwenyewe kitandani.
And the servants of the king, entering, have blessed our lord king David, saying: ‘May God amplify the name of Solomon above your name, and may he magnify his throne above your throne.’ And the king reverenced from his bed.
48 Mfalme pia alisema, 'Abarikiwe BWANA, Mungu wa Israeli, ambaye amempa mtu kuketi kwenye enzi yangu siku hii ya leo, na kwamba macho yangu yamejionea hilo.'”
And he said: ‘Blessed is the Lord, the God of Israel, who today has bestowed someone to sit upon my throne, while my eyes may see it.’”
49 Ndipo wageni wote wa Adoniya walipoogopa sana. Wakasimama na kila mtu akaenda njia yake.
Therefore, all those who had been summoned by Adonijah were terrified. And they all rose up, and each one went his own way.
50 Pia Adoniya alimwaogopa Sulemani na akasimama, na akaondoka, akachukua pembe la madhabahuni.
Then Adonijah, fearing Solomon, rose up and went away. And he took hold of the horn of the altar.
51 Kisha Sulemani akaambiwa hilo, wakasema, “Tazama, Adoniya amemwogopa mfalme Sulemani, kwa kuwa ameshikilia pembe la madhabahuni, akisema, 'Mfalme Sulemani na aniapie kwanza kuwa hatamwua mtumishi wake kwa upanga.'”
And they reported to Solomon, saying: “Behold, Adonijah, fearing king Solomon, has taken hold of the horn of the altar, saying: ‘May king Solomon swear to me this day that he will not put to death his servant with the sword.’”
52 Sulemani akasema, “Kama atajionyesha kuwa ni mtu wa kweli, hakuna hata unywele mmoja utakaoanguka duniani, bali kama uovu utaonekana kwake, atakufa.”
And Solomon said: “If he is a good man, not so much as one hair of his head shall fall to the ground. But if evil is found in him, he shall die.”
53 Kwa hiyo mfalme Sulemani akatuma watu, waliomleta Adoniya kutoka madhabahuni. Naye akaja akapiga magoti kwa Sulemani, na Sulemani akamwambia, “Nenda nyumbani kwako.”
Therefore, king Solomon sent and brought him from the altar. And entering, he reverenced king Solomon. And Solomon said to him, “Go to your own house.”