< 1 Wafalme 9 >

1 Sulemani alipomaliza kulijenga hekalu la BWANA, na ikulu ya mfalme, na baada ya kukamilisha vyote alivyokusudia kufanya,
And it comes to pass, at Solomon’s finishing to build the house of YHWH, and the house of the king, and all the desire of Solomon that he delighted to do,
2 BWANA alionekana kwa Sulemani kwa mara ya pili, kama alivyoonekana kwake kule Gibeoni.
that YHWH appears to Solomon a second time, as He appeared to him in Gibeon,
3 Na BWANA akamwambia, “Nimeyasikia maombi yako na dua zako ambazo umeniomba. Nimeitakasa nyumba hii ambayo umeijenga, kwa ajili yangu, ili niweke jina langu humo milele. Macho yangu na moyo wangu yatakuwa humo kwa nyakati zote.
and YHWH says to him, “I have heard your prayer and your supplication with which you have made supplication before Me; I have hallowed this house that you have built to put My Name there for all time, and My eyes and My heart have been there [for] all the days.
4 Lakini pia na wewe, kama utatembea mbele zangu kama Daudi baba yako alivyotembea kwa haki na unyofu katika moyo wako, ukitii yote niliyokuamuru na kuyashika maagizo na sheria zangu,
And you—if you walk before Me as your father David walked, in simplicity of heart, and in uprightness, to do according to all that I have commanded you, [and] you keep My statutes and My judgments,
5 ndipo nitakapoimarisha kiti cha enzi kwa Israeli milele, kama nilivyomwahidi baba yako Daudi, nikiseama, 'uzao wako hautaondoka katika kiti cha enzi cha Israeli.
then I have established the throne of your kingdom over Israel for all time, as I spoke to your father David, saying, A man of yours is never cut off from [being] on the throne of Israel.
6 Lakini kama utageuka, wewe au watoto wako, na kutozishika amri zangu na maagizo yangu ambayo nimeyaweka mbele zako, na kama utaenda kuabudu miungu mingine na kuisujidia,
If you at all turn back—you and your sons—from after Me, and do not keep My commands [and] My statutes that I have set before you, and have gone and served other gods, and bowed yourselves to them,
7 basi nitaikatilia mbali Israeli kutoka katika ardhi niliyowapa; na nyumba hii niliyoitakasa kwa jina langu, nitaitupilia mbali na macho yangu, na Israeli itakuwa mfano wa kukejeliwa na kitu cha kutusiwa katika mataifa yote.
then I have cut off Israel from the face of the ground that I have given to them, and the house that I have hallowed for My Name I send away from My presence, and Israel has been for an allegory and for a byword among all the peoples;
8 Ijapokuwa hekalu hili limetukuka sasa, kila mtu atakayepita pembeni yake atasituka na kuzoomea. Watajiuliza, 'Kwa nini BWANA amefanya hili katika chi hii na kwa nyumba hii?'
as for this house [that] is high, everyone passing by it is astonished, and has hissed, and they have said, Why has YHWH done this to this land and to this house?
9 Na wengine watajibu, 'Ni kwa sababu walimwacha BWANA, Mungu wao, ambaye aliwaleta mababu zao toka Misri, na sasa wamegeukia miungu mingine ambayo wameiinamia na kuisujudu. Hiyo ndiyo sababu BWANA amewaletea majanga haya yote.”
And they have said, Because that they have forsaken their God YHWH, who brought out their fathers from the land of Egypt, and they lay hold on other gods, and bow themselves to them and serve them; therefore YHWH has brought all this calamity on them.”
10 Ilitokea mwishoni mwa miaka ishirini, Sulemani alikuwa amemaliza kuyajenga majengo yote mawili, hekalu la BWANA na ikulu ya mfalme.
And it comes to pass, at the end of twenty years, that Solomon has built the two houses, the house of YHWH, and the house of the king.
11 Basi Hiramu, mfalme wa Tiro, alikuwa amemletea Sulemani mbao za mierezi na miboreshi, pamoa na dhahabu; vitu vyote ambavyo Sulemani alitamani. Kwa hiyo mfalme Sulemani akampatia Hiramu miji ishirini huko Galilaya.
Hiram king of Tyre has assisted Solomon with cedar-trees, and with fir-trees, and with gold, according to all his desire; then King Solomon gives to Hiram twenty cities in the land of Galilee.
12 Hiramu akaja kutoka Tiro kuiona ile miji ambayo Sulemani alikuwa amempatia, lakini hakupendezwa nayo.
And Hiram comes out from Tyre to see the cities that Solomon has given to him, and they have not been right in his eyes,
13 Kwa hiyo Hiramu akasema, “Ndugu yangu, ni miji gani hii uliynipatia? Hiramu akaiita nchi ya Kabuli mpaka leo.
and he says, “What [are] these cities that you have given to me, my brother?” And one calls them the land of Cabul to this day.
14 Hiramu alikuwa amemtumia mfalme tani nne za dhahabu.
And Hiram sends one hundred and twenty talents of gold to the king.
15 Vifuatavyo ndivyo vigezo ambavyo mfalme Sulemani aliweka: ili kulijenga hekalu la BWANA na ikulu yake, kuijenga Milo na ukuta wa Yerusalemu, na Hazori, Megido, na Gezari.
And this [is] the matter of the tribute that King Solomon has lifted up, to build the house of YHWH, and his own house, and Millo, and the wall of Jerusalem, and Hazor, and Megiddo, and Gezer
16 Farao mfalme wa Misri alikuwa ameenda kuitwaa Gezeri, akaichoma moto, na kuwaua Wakanaani katika mji. Kisha Farao akampatia binti yake ule mji, mke wa Sulemani kuwa zawadi ya arusi.
(Pharaoh king of Egypt has gone up and captures Gezer, and burns it with fire, and he has slain the Canaanite who is dwelling in the city, and gives it [as] presents to his daughter, wife of Solomon).
17 Kwa hiyo Sulemani akaijenga Gezeri na Bethi Horoni ya Loweri,
And Solomon builds Gezer, and the lower Beth-Horon,
18 Baalathi na Tamari jangwani katika nchi ya Yuda,
and Ba‘alath, and Tadmor in the wilderness, in the land,
19 na miji yote ya hazina yote iliyokuwa yake, na miji ya magari yake, na miji ya wapanda farasi wake, na hata kama alipenda kuijenga kwa ajili ya fahari yake kule Yerusalemu, Lebanoni, na katika nchi yote kwenye utawala wake.
and all the cities of stores that King Solomon has, and the cities of the chariots, and the cities of the horsemen, and the desire of Solomon that he desired to build in Jerusalem, and in Lebanon, and in all the land of his dominion.
20 Na kwa watu wote waliokuwa wamesalia wa Waamori, Wahiti, Waperezi, Wahivi, na Yebu, ambao hawakuwa Waisraeli,
The whole of the people that is left of the Amorite, the Hittite, the Perizzite, the Hivite, and the Jebusite, who [are] not of the sons of Israel—
21 na uzao wao waliokuwa wamesalia baada yao katika nchi, ambao Waisraeli hawakuweza kuwaangamiza kabisa - Sulemani akawafanya kuwa vibarua, ambao wako hata leo.
their sons who are left behind them in the land, whom the sons of Israel have not been able to devote—he has even lifted up a tribute of service [on] them to this day.
22 Hata hivyo, Sulemani hakuwafanya kuwa shokoa watu wa Israeli. Badala yake, walifanyika kuwa wanajeshi wake na watumishi wake, maakida wake, na wakuu wake, na majemedari wake na wapanda farasi wake.
And Solomon has not appointed a servant out of the sons of Israel, for they [are] the men of war, and his servants, and his heads, and his captains, and the heads of his chariots, and his horsemen.
23 Hawa ndio waliokuwa maakida wakuu waliokuwa wakiwasimamia kazi za Sulemani, watu 550, walikuwa wasimamizi wa watu waliokuwa wakifanya kazi.
These [are] the five hundred and fifty heads of the officers who [are] over the work of Solomon, those ruling among the people who are laboring in the work.
24 Binti wa Farao alihama kutoka mji wa Daudi kwenda kwenye ile nyumba ambayo Sulemani alimjengea. Baadaye, Sulemani akaijenga Milo.
Only, the daughter of Pharaoh went up out of the City of David to her house that [Solomon] built for her; then he built Millo.
25 Mara tatu kwa kila mwaka Sulemani alitoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani katika madhabahu ambayo alimjengea BWANA, akifukiza uvumba pamoja nazo juu ya madhabahu ilyokuwa mbele ya BWANA. Kwa hiyo akalimalizia hekalu na sasa alikuwa akilitumia.
And Solomon caused burnt-offerings and peace-offerings to ascend three times in a year on the altar that he built for YHWH, and he burned it as incense with that which [is] before YHWH, and finished the house.
26 Tena Sulemani alitengeneza merikebu kule Ezioni Geberi, ambayo iko karibu na Elathi katika ufukwe wa bahari ya shamu, katika nchi ya Edomu.
And King Solomon has made a navy in Ezion-Geber, that is beside Eloth, on the edge of the Sea of Suph, in the land of Edom.
27 Hiramu alituma watumishi kwenye merikebu ya Sulemani, wanamaji wanaoijua bahari, pamoja na watumishi wake Sulemani.
And Hiram sends his servants in the navy, shipmen knowing the sea, with servants of Solomon,
28 Walikwenda kwa Ofri pamoja na watumishi wa Sulemani. Kutoka huko walileta takribani tani 14. 5 za dhahabu kwa Sulemani.
and they come to Ophir, and take four hundred and twenty talents of gold from there, and bring [it] to King Solomon.

< 1 Wafalme 9 >