< 1 Wafalme 8 >

1 Kisha Sulemani akawakusanya wazee wa Israeli, wakuu wote wa makabila, na viongozi wa familia za wana wa Israeli, mbele yake kuleYerusalemu, ili waliingize ndani lile sanduku la agano la BWANA kutoka mji wa Daudi, ambao ni Sayuni.
Then Solomon assembles the elderly of Israel, and all the heads of the tribes, princes of the fathers of the sons of Israel, to King Solomon, to Jerusalem, to bring up the Ark of the Covenant of YHWH from the City of David—it [is] Zion;
2 Wanaume wote wa Israeli walikusanyika mbele ya mfalme Sulemani kwenye sherehe, katika mwezi wa Ethanim, ambao ndio mwezi wa saba.
and all the men of Israel are assembled to King Solomon, in the month of Ethanim, in the festival (the seventh month).
3 Wazee wote wa Israeli walikuja, na makuhani wakalibeba lile sanduku.
And all [the] elderly of Israel come in, and the priests lift up the Ark,
4 Wakalileta lile sanduku la BWANA, lIle hema la kukutania na mapambo yote matakatifu ambayo yalikuwa kwenye hema. Makuhani na Walawi wakavileta vitu hivi.
and bring up the Ark of YHWH, and the Tent of Meeting, and all the holy vessels that [are] in the tent, indeed, the priests and the Levites bring them up.
5 Mfame Sulemani na mkutano wote wa Israeli wakaja pamoja mbele ya sanduku, wakatoa sadaka za kondoo na makisai ambazo hazikuweza kuhasabika.
And King Solomon and all the congregation of Israel who are assembled to him [are] with him before the Ark, sacrificing sheep and oxen, that are not counted nor numbered for multitude.
6 Makuhani wakalingiza ndani lile sanduku la agano la BWANA na wakaliweka mahali pake, ndani ya chumba cha ndani, patakatifu sana, chini ya yale mabawa ya makerubi.
And the priests bring in the Ark of the Covenant of YHWH to its place, to the oracle of the house, to the Holy of Holies, to the place of the wings of the cherubim;
7 Kwa kuwa makerubi walitandaza mabawa yao hadi mahali pa sanduku la agano, na walifunika sanduku na miti yake kwani ilitumika kulibeba.
for the cherubim are spreading forth two wings to the place of the Ark, and the cherubim cover over the Ark, and over its poles from above;
8 Ile miti ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba miishio yake ilionekana tokea kwenye eneo takatifu mbele ya chumba cha ndani, lakini haikuweza kuonekana kutokea nje. Miti hiyo iko mpaka leo.
and they lengthen the poles, and the heads of the poles are seen from the holy [place] on the front of the oracle, and are not seen outside, and they are there to this day.
9 Ndani ya sanduku hapakuwemo na kitu chochote isipokuwa vile vidonge vya mawe ambavyo Musa aliviweka alipokuwa mlima Horebu, wakati BWANA alipofanya agano na watu wa Israeli walipotoka kwenye nchi ya Misri.
There is nothing in the Ark, only the two tablets of stone which Moses put there in Horeb when YHWH covenanted with the sons of Israel in their going out of the land of Egypt.
10 Ilitokea kwamba wakati makuhani walipotoka mahali patakatifu, lile wingu lilifunika hekalu la BWANA.
And it comes to pass, in the going out of the priests from the holy [place], that the cloud has filled the house of YHWH,
11 Makuhani hawakuweza kusimama kwa ajili ya kutumika kwa sababu utukufu wa BWANA ulifunika hekalu.
and the priests have not been able to stand to minister because of the cloud, for the glory of YHWH has filled the house of YHWH.
12 Kisha Sulemani akasema, “BWANA amsema kuwa anaweza kuishi hata kwenye giza nene,
Then Solomon said, “YHWH has said [He is] to dwell in thick darkness;
13 Lakinni nimekujengea makao ya kujivunia, mahali pako pa kuishi milele.”
I have surely built a house of habitation for You; a fixed place for Your abiding for all ages.”
14 Kisha mfalme akageuka na kuwabariki mkusanyiko wa watu wa Israeli, wakati huo mkusanyiko wa Waisraeli walikuwa wamesimama.
And the king turns his face around, and blesses the whole assembly of Israel; and all the assembly of Israel is standing.
15 Akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, asifiwe, ambaye alisema na baba yangu Daudi, na ametimiza kwa mikono yake, akisema,
And he says, “Blessed [is] YHWH, God of Israel, who spoke by His mouth with my father David, and by His hand has fulfilled [it], saying,
16 'Tangu siku ile niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji wowote toka kwa makabila yote ya Israeli ambako ningeijenga nyumba, kwa ajili ya jina langu kuwemo humo. Hata hivyo, nilimchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.
From the day that I brought out My people, even Israel, from Egypt, I have not fixed on a city out of all the tribes of Israel, to build a house for My Name being there; and I fix on David to be over My people Israel.
17 Sasa ilikuwa kwenye moyo wa Daudi baba yangu kujenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wa Israeli.
And it is with the heart of my father David to build a house for the Name of YHWH, God of Israel,
18 Lakini BWANA alimwambia baba yangu Daudi, 'Ilikuwa ndani ya moyo wako kunijengea nyumba kwa jina langu, ulifanya vyema kwa hilo kuwa ndani ya moyo wako.
and YHWH says to my father David, Because that it has been with your heart to build a house for My Name, you have done well that it has been with your heart;
19 Ingawa hutanijengea nyumba; badala yake mwanao, mmoja wa wanao atakayezaliwa toka viunoni mwako, atanijengea nyumba kwa jina langu,'
only, you do not build the house, but your son who is coming out from your loins, he builds the house for My Name.
20 BWANA amelibeba lile neno slilokuwa amesema, kwa kuwa nimeinuka mahali pa baba yangu Daudi, na nimeketi kwenye kiti cha enzi cha Israeli, kama BWANA alivyoahidi. Nimeijenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wa Israeli.
And YHWH establishes His word which He spoke, and I am risen up instead of my father David, and I sit on the throne of Israel, as YHWH spoke, and build the house for the Name of YHWH, God of Israel,
21 Nimetengeneza mahali kwa ajili ya sanduku ndani yake, ambamo ndani yake kuna agano la BWANA, ambalo alifanya na baba zetu alipowatoa toka nchi ya Misri,”
and I set a place for the Ark there, where the covenant of YHWH [is], which He made with our fathers in His bringing them out from the land of Egypt.”
22 Sulemani alisimama mbele ya madhabahu ya BWANA, mbela ya mkusanyiko wote wa Waisraeli, naye akanyosha mikono yake kuelekea mbinguni.
And Solomon stands before the altar of YHWH, in front of all the assembly of Israel, and spreads his hands toward the heavens,
23 Akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni au chini duniani, ambaye hutunza agano lake kwa uaminifu kwa watumishi wako ambao hutembea mbele yako kwa mioyo yao yote;
and says, “YHWH, God of Israel, there is not a God like You, in the heavens above and on the earth below, keeping the covenant and the kindness for Your servants, those walking before You with all their heart,
24 wewe ambaye umetunza ahadi yako na mtumishi wako Daudi baba yangu ile uliyomwahidi. Naam, ulisema kwa kinywa chako na sasa umeitimiza kwa mkono wako, kama ilivyo leo.
which You have kept for Your servant, my father David, that which You spoke to him; indeed, You speak with Your mouth, and with Your hand have fulfilled [it], as [at] this day.
25 Sasa basi, BWANA, Mungu wa Israeli, timiza kile ulichomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu, pale uliposema, 'Hautashindwa kunipa mtu mbele ya macho yangu ambaye ataketi katika kiti cha enzi cha Israeli, kama tu uzao wako watakuwa waangalifu kutembea mbele yangu, kama vile wewe ulivyotembea mbele yangu.'
And now, YHWH, God of Israel, keep for Your servant, my father David, that which You spoke to him, saying, A man of yours is never cut off from before My face, sitting on the throne of Israel—only, if your sons watch their way, to walk before Me as you have walked before Me.
26 Sasa basi, Mungu wa Israeli, Ninaomba kwamba ile ahadi uliyofanya kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, itimie.
And now, O God of Israel, please let Your word be established which You have spoken to Your servant, my father David.
27 Je, ni kweli kwamba Mungu ataishi duniani? Tazama, Ulimwengu wote na mbingu hazikutoshi - sembuse nyumba hii niliyoijenga!
But is it true [that] God dwells on the earth? Behold, the heavens and the heavens of the heavens cannot contain You, how much less this house which I have built!
28 Kwa hiyo Mungu naomba uyajali maombi haya ya mtumishi wako na maombi yake, BWANA, Mungu wangu; sikiliza kilio na maombi ambayo mtumishi wako anakuomba leo.
Then You have turned to the prayer of Your servant, and to his supplication, O YHWH my God, to listen to the cry and to the prayer which Your servant is praying before You today,
29 Naomba ulitazame hekalu hili mchana na usiku, mahali ambapo ulisema, 'Jina langu na uwepo wangu utakuwa' - ili niweze kuwa nasikiliza maombi ambayo mtumishi wako ataomba mahali hapa.
for Your eyes being open toward this house night and day, toward the place of which You have said, My Name is there; to listen to the prayer which Your servant prays toward this place.
30 Kwa hiyo sikia maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli tunapokuwa tunaomba mahali hapa. Ndiyo, sikia kutokea mahali ambapo unaishi, kutoka katika mbingu za mbingu; na unaposikia tafadhali samehe.
Then You have listened to the supplication of Your servant, and of Your people Israel, which they pray toward this place; indeed, You listen in the place of Your dwelling, in the heavens—and You have listened, and have forgiven,
31 Kama mtu atamtendea uovu jirani yake na anapewa sharti la kiapo, na kama atakuja na kuapa mbele ya madhabahu yako katika nyumba hii,
that which a man sins against his neighbor, and he has lifted up an oath on him to cause him to swear, and the oath has come in before Your altar in this house,
32 basi usikie kutoka mbinguni ukatende na kuwahukumu watumishi wako, ukamhukumu mwovu, ili kuwaletea tabia zake kichwani mwake, na kumtunza mwenye haki kuwa hana hatia, na kumpa thawabu yake ya haki.
then You hear in the heavens, and have done, and have judged Your servants, to declare wicked the wicked, to put his way on his [own] head, and to declare righteous the righteous, to give him according to his righteousness.
33 Watu wako Israeli watakapopigwa na adui kwa sabau ya kutenda dhambi dhidi yako, na kama watakurudia, na kulikiri jina lako, na kukusihi, na kuomba msamaha kwako katika hekalu hili-
In Your people Israel being struck before an enemy, because they sin against You, and they have turned back to You, and have confessed Your Name, and prayed, and made supplication to You in this house,
34 tafadhali nakuomba usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi za watu wako Israeli; uwarudishe katika nchi ambayo uliwapa mababu zao.
then you hear in the heavens, and have forgiven the sin of Your people Israel, and brought them back to the ground that You gave to their fathers.
35 Kama mbingu zitafungwa na mvua hazinyeshi kwa sababu watu wamekutenda dhambi wewe - na kama wataomba mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kugeuka toka dhambi zao na kama umewapiga -
In the heavens being restrained, and there is no rain, because they sin against You, and they have prayed toward this place, and confessed Your Name, and turn back from their sin, for You afflict them,
36 basi sikia tokea mbinguni na usamehe dhambi za watumishi wako na za watu wako Israeli, utakapowafundisha njia njema inayowapasa; basi uinyeshee mvua nchi yako, ambayo uliwapa watu wako kuwa urithi.
then You hear in the heavens, and have forgiven the sin of Your servants, and of Your people Israel, for You direct them [to] the good way in which they go, and have given rain on Your land which You have given to Your people for inheritance.
37 Na kama kuna njaa katika nchi, au kama kuna magonjwa, au ukungu, nzige au funza; au kama adui atavamia malango ya mji katika nchi yao, kama kuna tauni au magonjwa yeyote -
Famine—when it is in the land; pestilence—when it is [in the land]; blasting, mildew, locust; caterpillar—when it is [in the land]; when its enemy has distressed it in the land [in] its gates, any plague, any sickness—
38 na kama kuna mtu au wata wa Israeli wataomba - kila mmoja akaijua hiyo tauni katika moyo wake wakati akinyosha mikono yake katika hekalu hili.
any prayer, any supplication that [is] of any man of all Your people Israel, each who knows the plague of his own heart, and has spread his hands toward this house,
39 Basi usikie kutoka mbinguni, mahali unapoishi, utende na kusamehe, na umpe kila mtu thawabu anayostahili kwa kile anachofanya; wewe unajua moyo wake, kwa sababu ni wewe pekee yako ujuaye mioyo ya watu.
then You hear in the heavens, the settled place of Your dwelling, and have forgiven, and have done, and have given to each according to all his ways, whose heart You know (for You have known—You alone—the heart of all the sons of man),
40 Fanya hivi ili kwamba wawe na hofu kwako katika siku zote za maisha yao wanayoishi katika nchi uliyowapa mababu zetu.
so that they fear You all the days that they are living on the face of the ground that You have given to our fathers.
41 Na nyongeza yake, kuhusiana na mgeni ambaye si mtu wako wa Israeli: atakapokuja kutokea nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako -
And also, to the stranger who is not of Your people Israel, and has come from a far-off land for Your Name’s sake—
42 kwa sababu watasikia jina lako lilivyo kuu, mkono wako wenye nguvu, na mkono wako ulioinuliwa - atakapokuja na kuomba mahali hapa pa hekalu,
for they hear of Your great Name, and of Your strong hand, and of Your outstretched arm—and he has come in and prayed toward this house,
43 tafadhali usikie kutokea katika mbingu, mahali unapoishi, na umfanyie huyo mgeni akuombacho. Fanya hivi ili makundi ya wtu wote duniani wakujue jina lako na kukuhofia, kama wanavyofanya watu Israeli. Fanya hivyo ili wajue kwamba nyumba hii niliyoijenga inaitwa kwa jina lako.
You hear in the heavens, the settled place of Your dwelling, and have done according to all that the stranger calls to You for, in order that all the peoples of the earth may know Your Name, to fear You like Your people Israel, and to know that Your Name has been called on this house which I have built.
44 Na kama watu wko wataenda vitani dhidi ya adui, kwa njia yeyote unayoweza kuwatuma, na kama watakuomba wewe, BWANA, kuelekea mji huu uliuchagua, na kuekea nyumba ambayo nimeijenga kwa jina lako.
When Your people go out to battle against its enemy, in the way that You send them, and they have prayed to YHWH [in] the way of the city which you have fixed on, and of the house which I have built for Your Name,
45 Basi sikia tokea mbinguni maombi yao, dua zao, na uwasaidie wanachohitaji.
then You have heard their prayer and their supplication in the heavens, and have maintained their cause.
46 Na kama watafanya dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna hata mtu mmoja asiyefanya dhambi, na kama una hasira dhidi yao na kuwapeleka kwa maadui, ili kwamba maadui wawachukue mateka katika nchi yao, mbali au karibu.
When they sin against You (for there is not a man who does not sin), and You have been angry with them, and have given them up before an enemy, and they have taken captive their captivity to the land of the enemy far off or near;
47 Na kama watatambua kuwa wako katika nchi ya utumwa, na kama watatubu na kuomba neema kwako kutokea katika nchi ya watekaji. Na kama watasema, 'tumetenda kwa ukaidi na tumefanya dhambi. Tumetenda kwa uovu.'
and they have turned [it] back to their heart in the land to where they have been taken captive, and have turned back, and made supplication to You in the land of their captors, saying, We have sinned and done perversely—we have done wickedly;
48 Na kama watarudi kwako kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote katika chi ya maadui ambao wanawakamata, na kama watakuomba wewe kuelekea nchi yao, ambayo uliwapa mababu zao, na kuelekea katika mji uliouchagua, nakuelekea kaika nyumba ambayo nimeijenga kwa jina lako.
indeed, they have turned back to You with all their heart and with all their soul, in the land of their enemies who have taken them captive, and have prayed to You [in] the way of their land, which You gave to their fathers, the city which You have chosen, and the house which I have built for Your Name:
49 Basi usikie maombi yao, na dua zao tokea mbinguni, mahali unapoishi, na ukaitetee haki yao.
then You have heard in the heavens, the settled place of Your dwelling, their prayer and their supplication, and have maintained their cause,
50 Wasamehe watu wako waliotenda dhambi dhidi yako, na dhambi zao zote ambazo kwazo wamekukosea wewe dhidi ya amri zako. Uwahurumie mbele ya maadui zao ambao waliwachukua mateka, ili kwamba maadui zao pia wawahurumie watu wako.
and have forgiven Your people who have sinned against You, even all their transgressions which they have transgressed against You, and have given them mercies before their captors, and they have had mercy [on] them—
51 Hawa ni watu wako uliowachagau, ambao uliwaokoa toka nchi ya Misri kama kwamba walikuwa katikati ya tanuru amabamo vyuma huyeyushwa.
for they [are] Your people and Your inheritance, whom You brought out of Egypt, out of the midst of the furnace of iron—
52 Naomba kwamba macho yako yatazame dua za mtumishi wako na kwa dua za watu wako Issraeli, ili uwasike kila wanapokulilia.
for Your eyes being open to the supplication of Your servant, and to the supplication of Your people Israel, to listen to them in all they call to You for;
53 Kwa kuwa uliwatenga toka kwa watu wengine wa duniani ili wawe wako nakupokea ahadi zako, kama vile ulivyomwambia Musa mtumishi wako, wakati ulipowatoa babazetu toka Misri, BWANA.”
for You have separated them to Yourself for an inheritance, out of all the peoples of the earth, as You spoke by the hand of Your servant Moses, in Your bringing out our fathers from Egypt, O Lord YHWH.”
54 Kwa hiyo ilitokea wakati Sulemaeni alipomaliza kuomba maombi haya na dua zake kwa BWANA, aliamka toka madhabahu ya BWANA, pale alipokuwa amepiga magoti na mikono yake ikiwa imenyoshwa kuelekea mbinguni.
And it comes to pass, at Solomon’s finishing to pray to YHWH all this prayer and supplication, he has risen from before the altar of YHWH, from bending on his knees and [having] his hands spread out to the heavens,
55 Alisimama na kuubariki mkutano wote wa Israeli kwa sauti kuu, alisema,
and he stands and blesses all the assembly of Israel [with] a loud voice, saying,
56 “Asifiwe BWANA, aliywapatia pumziko watu hawa Israeli, akitunza ahadi zake zote. Hakuna hata moja ambayo haijatekelezwa katika ahadi njema za BWANA ambazo aliahidi akiwa na Musa mtumishi wake.
“Blessed [is] YHWH who has given rest to His people Israel, according to all that He has spoken; not [even] one word has fallen of all His good word, which He spoke by the hand of His servant Moses.
57 BWANA, mungu wetu awe pamoja nasi, kama alivyokuwa pamoja na mababu zetu. Asituache wala kututelekeza,
Our God YHWH is with us as He has been with our fathers; He does not forsake us nor leave us;
58 kwamba aunganishe mioyo yetu na yeye, ili tuishi katika njia zake na kuzishika amri zake na taratibu zake na maagizo yake, ambayo aliwaagiza baba zetu.
to incline our heart to Himself, to walk in all His ways, and to keep His commands, and His statutes, and His judgments, which He commanded our fathers;
59 Na maeneo haya ambayo nimesema, ambayo nimesihi mbele ya BWANA, yawe karibu n a BWANA, Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba awasadie katika haki za mtumishi wake na haki za watu wake Israeli, kama watakavyoomba kila siku;
and these, my words, with which I have made supplication before YHWH, are near to our God YHWH by day and by night, to maintain the cause of His servant, and the cause of His people Israel, the matter of a day in its day,
60 kwamba watu wote duniani wajue kwamba BWANA, ndiye Mungu, na hakuna Mungu mwingine!
that all the peoples of the earth may know that He, YHWH, [is] God; there is none else;
61 Kwa hiyo ifanyeni mioyo yenu iwe ya haki mbele ya BWANA. Mungu wetu, ili tutembee katika maagizo na kuzishika amri zake, kama ilivyo leo.
and your heart has been perfect with our God YHWH, to walk in His statutes, and to keep His commands, as [at] this day.”
62 Kwa hiyo mfalme na watu wote pamoja naye wakatoa sadaka kwa BWANA.
And the king and all Israel with him are sacrificing a sacrifice before YHWH;
63 Sulemani akatoa sadaka ya amani, ambayo aliifanya kwa BWANA: Nayo ilikuwa makisai elfu ishirini na mbili, na kondoo 120, 000. Kwa hiyo mfalme na watu wa Israeli wakaiweka wakfu nyumba ya BWANA.
and Solomon sacrifices the sacrifice of peace-offerings, which he has sacrificed to YHWH: twenty-two thousand oxen and one hundred and twenty thousand sheep; and the king and all the sons of Israel dedicate the house of YHWH.
64 Siku hiyo mfalme aliweka wakfu behewa ya katikati mbele ya hekalu la BWANA, kwa kuwa pale ndipo alipotoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za unga, na sadaka za mafuta ya amani, kwa sababu ile madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele ya BWANA ilikuwa ndogo sana kwa sadaka za kuteketezwa, sadaka za unga, na mafuta ya sadaka za amani.
On that day the king has sanctified the middle of the court that [is] before the house of YHWH, for he has made the burnt-offering, and the present, and the fat of the peace-offerings there; for the altar of bronze that [is] before YHWH [is] too small to contain the burnt-offering, and the present, and the fat of the peace-offerings.
65 Kwa hiyo Sulemani akafanya sherehe wakati huo, Nayo Israeli yote pamoja naye, mkutano mkubwa, kutoka Lebo Hamathi hadi kijito cha Misri, wakaja mbele ya BWANA, Mungu wetu kwa muda wa siku saba na pia kwa siku saba zingine, ambayo jumla yake ni siku kumi na nne.
And Solomon makes, at that time, the festival—and all Israel with him, a great assembly from the entering in of Hamath to the Brook of Egypt—before our God YHWH, [for] seven days and seven [more] days—fourteen days.
66 Na ilipofika siku ya nane aliwatawanya watu, nao wakambariki mfalme kisha wakaenda nyumbani kwao kwa furaha na mioyo ya shangwe kwa wema wote ambao BWANA alimwonyesha Daudi, mtumishi wake, na kwa watu wake, Israeli.
On the eighth day he has sent the people away, and they bless the king, and go to their tents, rejoicing and glad of heart for all the good that YHWH has done to His servant David, and to His people Israel.

< 1 Wafalme 8 >