< 1 Wafalme 7 >

1 Ilimchukua Sulemani miaka kumi na tatu kujenga ikulu yake.
Salomón estuvo trece años construyendo una casa para sí mismo hasta que estuvo completa.
2 Aliijenga ikulu iliyoitwa mwitu wa Lebanoni. Urefu wake ulikuwa mita 46, na upanawake ulikuwa mita 23, na kimo chake kilikuwa mita 14. Nayo ilikuwa na safu nne ya nguzo za mierezi na mithili ya mwerezi juu ya nguzo.
E hizo la casa del bosque del Líbano, que tenía cien codos de largo, cincuenta codos de ancho y treinta codos de alto, apoyada en cuatro líneas de pilares de madera de cedro con soportes de madera de cedro sobre los pilares.
3 Paa la ikulu lilikuwa la mwerezi ambalo lilikaa juu ya mihimili. Mihili hiyo ilikuwa imeshikiliwa na nguzo. Kulikuwa na mihimili arobaini na tano, ambayo ilikuwa katika safu kumi na tano.
Y se cubrió con cedro sobre los cuarenta y cinco soportes que estaban en los pilares, quince en una línea.
4 Nayo mihimili ilikuwa safu tatu, na kila dirisha lilikabili dirisha lingine katika madaraja matatu.
Había tres líneas de marcos de ventanas, ventana que daba a la ventana en cada línea.
5 Milango yote na miimo ilitengenezwa kwa mraba, na madirisha yalikuwa yakikabiliana katika madaraja matatu
Y todas las puertas y ventanas tenían marcos cuadrados, con las ventanas enfrentadas en tres líneas.
6 Akatengeneza baraza lenye uerfu wa mita 23 na upana wa mita 14. Mbele yake kulikuwa na ukumbi ulioezekwa.
E hizo un pórtico de columnas, de cincuenta codos de largo y treinta codos de ancho, y otro pórtico con columnas y techo delante de él.
7 Sulemani akajenga baraza yenye kiti cha enzi ambacho alitolea hukumu ya haki. Nayo ilikuwa imeezekwa kwa mwerezi kutoka sakafu moja hadi nyingine.
Luego hizo un pórtico para su trono donde había de juzgar; este era el pórtico del juicio; Estaba cubierto con madera de cedro desde el suelo hasta el techo.
8 Nyumba ya Sulemani ambayo alikusudia kuishi, katika behewa nyingine ndani ya sehemu ya chini ya ikulu, ilitengenezwa kwa kazi hiyo hiyo. Pia alimjengea binti wa Farao nyumba kama hii, ambaye alikuwa mke wake
Y la casa para su morada, tenía otro atrio abierto en el pórtico en la parte de atrás, se hizo de la misma manera. Y luego hizo una casa como esta para la hija de Faraón, a quien Salomón había tomado como su esposa.
9 Majengo haya yalipmbwa kwa vitu vya thamaini, mawe ya thamani, yaliyochongwa na kukatwa kwa msimeno kufuata vipimo sahihi na kulainishwa pande zote. Mawe ya namna hii ndiyo yale yaliyotumika kuanzia kwenye msingi hadi juu, pia na nje hadi kwenye baraza.
Todos estos edificios se hicieron, por dentro y por fuera, desde la base hasta las vigas, con piedras cortadas y desde el exterior hasta el gran atrio, de piedras costosas, cortadas a la medida.
10 Msingi ulijengwa kwa mawe makubwa sana na ya thamani yenye urefu wa mita 3. 7 na mengine mita 4. 8.
Y la base era de piedras grandes, muy costosas, unos diez codos y unos ocho codos cuadrados.
11 Kwa juu ilipambwa kwa, mawe ya thamani yaliyochongwa sawa sawa kwa msimeno na kwa mihimili ya mierezi.
Sobre su cabeza había piedras de alto precio cortadas a medida y madera de cedro.
12 Na behewa kubwa iliyokuwa ikizunguka ikulu ilikuwa na safu tatu za mawe yaliyokatwa na safu moja ya mihimili ya mierezi kama ilivyo kwenye baraza la ndani la hekalu la BWANA na ule ukumbi wa hekalu.
La gran plaza exterior de todo era amurallada con tres líneas de piedras cuadradas y una línea de tablas de madera de cedro, alrededor de la plaza abierta dentro de la casa del Señor y la habitación cubierta de la casa del rey.
13 Mfalme Sulemani alituma watu kumleta Huramu kutoka Tiro.
Entonces el rey Salomón hizo venir a Hiram de Tiro.
14 Huramu alikuwa mwana wa mjane wa kabila ya Naftali; baba yake alikuwa mtu wa Tiro, mfua shaba. Huramu alikuwa mwingi wa hekima na ufahamu na stadi za kufanya kazi kubwa za shaba. Aliletwa kwa mfalme ili kufanya kazi zilizohusiana na shaba kwa mfalme.
Era hijo de una viuda de la tribu de Neftalí, y su padre era un hombre de Tiro, obrero de bronce. Estaba lleno de sabiduría y conocimiento y un trabajador experto en bronce. Vino al rey Salomón e hizo toda su obra por él.
15 Huramu alizilemba zile nguzo mbili za shaba, kila moja ilikuwa na kimo cha mita 8. 3 na mzingo wa mita 5. 5.
El fue quien hizo las dos columnas de bronce; el primer pilar tenía dieciocho codos de altura, y una línea de doce codos la rodeaba; Y el segundo fue el mismo.
16 Akatengeneza taji mbili za shaba za kuwekwa juu ya zile nguzo. Kimo cha kila taji ilikuwa mita 2. 3.
E hizo las dos coronas para que fueran colocadas en la parte superior de los pilares, en forma de trenza y cadena de bronce fundido en el fuego; las coronas tenían cinco codos de alto.
17 Kulikuwa na nyavu za kuwa kama kazi ya kusuka, na masongo ya mikufu, kwa ajili ya kuvipamba vile vichwa vya nguzo, nayo yailikuwa saba kwa kila kichwa.
Hizo dos rejas para las coronas en la parte superior de los pilares, una reja para cada capitel; siete para cada capitel.
18 Kwa hiyo Huramu akafanya safu mbili za komamanga kuzunguka vile vichwa vya nguzo ili kuvipamba vile vichwa.
E hizo ornamentos de granadas; y dos líneas de granadas alrededor de la reja, que cubren las coronas de los pilares, las dos coronas de la misma manera.
19 Zile taji kwenye vile vichwa vya nguzo za ukumbi zilikuwa zimepambwa kwa maua, yenye vimo vya mita 1. 8.
Las coronas en la parte superior de los pilares estaban adornadas con un diseño de lirios, y tenían cuatro codos de ancho.
20 Hizo taji kwenye hizo nguzo mbili kwenye vichwa vyake, karibu yake kulikuwa na makomamanga mia mbili yote yakiwa kwenye safu.
Y había coronas en los dos pilares cerca de la parte redonda por reja, y había doscientas granadas en líneas alrededor de cada corona.
21 Alisimamisha nguzo kwenye ukumbi wa hekalu. Ile nguzo ya kuume akaipa jina la Yakini, na ile ya kushoto akaipa jina la Boazi.
Puso los pilares en la entrada del Templo, nombrando el de la derecha Jaquin, y el de la izquierda Boaz.
22 Na juu ya zile nguzo kulikuwa na mapambo kama maua. Hivyo ndivyo zile nguzo zilivyotengenezwa.
Las copas de los pilares tenían un diseño de lirios; y el trabajo de los pilares fue completo.
23 Tena akafanya bahari ya kusubu ya, yenye mita 2. 3 kutoka ukingo hadi ukingo, kimo chake kilikuwa mita 4. 6, mziingo wake ulikuwa mita 13. 7.
E hizo un gran recipiente redondo metálico de agua de diez codos de borde a borde, cinco codos de alto y treinta codos.
24 Na chini ya ile bahari kulikuwa na vibuyu vilivyoizunguka, vilikuwa vibuyu kumi na nane katika kila mita, vilivyowekwa katika kila hicho kipande wakati bahari inapokuwa kalibu.
Y debajo del borde, rodeando todo alrededor de diez codos, había dos líneas de capullos de flores, hechas con metal fundido.
25 Bahari ikakaa juu ya makisai kumi na mbili, tatu, zilitazama kaskazini, tatu zikitazama magharibi, tatu zikitazama kusini na tatu zikitazama kaskazini. Ile bahari iliwekwa juu yao, na pande zao zote za nyuma zilikuwa ndani.
Se apoyaba en doce bueyes, con sus partes traseras giradas hacia el centro, tres de ellos mirando hacia el norte, tres hacia el oeste, tres hacia el sur y tres hacia el este.
26 Bahari ilikuwa nene kama upana wa mkono, na ukingo wake ulikuwakama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi huingia bathi elfu mbili za maji.
Era tan gruesa como la mano abierta de un hombre, y estaba curvada como el borde de una taza, como la flor de un lirio; tenía capacidad para 2000 batos, (medida hebreo).
27 Huramu akatengeneza makalio kumi ya shaba. Kila kalio lilkuwa na urefu wa mita 1. 8, upana wa mita 1. 8, na kimo cha mita 1. 3.
E hizo diez bases de bronce con ruedas; cada uno de cuatro codos de largo, cuatro codos de ancho y tres codos de alto.
28 Hivi ndivyo kazi za makalio zilivyofanywa. Yalikuwa na papi ambazo zilikaa kati kati ya vipandio,
Y las bases fueron hechas de esta manera; Sus lados eran cuadrados, fijados en un marco;
29 na juu ya papi na vipandio kulikuwa na simba, makisai, na makerubi. Chini na juu simba kulikuwa na masongo ya kazi ya kufuliwa.
Y en los lados cuadrados entre los marcos estaban los leones, los bueyes y los seres alados; y lo mismo en el marco; y sobre y debajo de los leones y los bueyes y los seres alados, había añadiduras de bajo relieve.
30 Kila kalio lilikuwa na magurudumu ya shaba na vipini, na pande zake nne na miguu yake minne ilikuwa na mataruma chini ya birika. Chini ya birika yalikuweko mataruma ya kusubu yenye masongo katika kila upande.
Cada base tenía cuatro ruedas de bronce, girando sobre varillas de bronce, y sus cuatro ángulos tenían placas de ángulo debajo de ellas; Las placas angulares debajo de la base eran de bronce, y había adornos de guirnaldas al lado de cada uno.
31 Na kinywa chake kilikuwa cha kuviringana, chenye upana wa sentimita araobaini na sita, na ile taji ilikuwa na sentimita ishirini na tatu. Na kinywa chake kilikuwa na nakshi, na papi zake zilikuwa za mraba, na wala siyo za mvringo.
Su boca dentro de la placa angular tenía un codo de diámetro; era redonda como un pilar, de un codo y medio de ancho; tenía diseños recortados en ella; Los lados eran cuadrados.
32 Yale magurudumu mawili yalikuwa chini ya papi, na mikono ya magurudumu yalikuwa ndani ya makalio. Kimo cha yale magurudumu kilikuwa sentimeta sitini na tisa.
Las cuatro ruedas estaban debajo de los marcos, y las barras sobre las cuales estaban fijas estaban en la base; Las ruedas tenían un codo y medio de altura.
33 Yale magurudumu yalikuwa kama ya gari. Mikono yake, na maduara, matindi yake, na vipande vya ndani vyote vilikuwa vya kusubu.
Las ruedas estaban hechas como ruedas de carro, las barras sobre las cuales estaban fijas, las partes que formaban sus bordes, sus barras y los puntos centrales de las mismas, todas estaban hechas de bronce.
34 Kulikuwa na mataruma manne katika pande zake nne za makalio, yaliyokuwa yameshikamanishwa na kalio lenyewe.
Y había cuatro placas angulares en los cuatro ángulos de cada base, formando parte de la estructura de la base.
35 Juu ya makalio kulikuwa na duara yenye kina cha sentimita ishirini na tatu, na juu ya makalio mashikio yake na papi zake zikiwa zimeshikamanishwa.
Y en la parte superior de la base había un recipiente redondo, de medio codo de altura;
36 Juu ya mabamba na papi zake Huramu akachora makerubi, simba, na mitende ambayo ilifunika nafasi ya juu, nayo ilikuwa imezungukwa na masongo.
En los espacios de los lados planos y en los marcos de ellos, hizo diseños de seres alados, leones y palmeras, con bordes de guirnalda alrededor.
37 Alitengeneza makalio kumi kwa jinsi hii. Yote yalikuwa yametengenezwa kwa kufanana, na yalikuwa ya vipimo sawa, na sura inayofanana.
Todas las diez bases se hicieron de esta manera, después del mismo diseño, del mismo tamaño y forma.
38 Huramu akatengeneza birika kumi za shaba. Birika moja liliweza kubeba bathi arobaini za maji. Kila birika lilikuwa mita 1. 8 toka birika moja hadi jingine na kulikuwa na birika moja katika kila kalio kati ya yale kumi.
E hizo diez lavaderos de bronce, todos tomando cuarenta baños y midiendo cuatro codos; Se colocó un recipiente en cada una de las diez bases.
39 Alitengeneza makalio tano upande wa kusini unaoelekea upande wa hekalu. Akatengeneza bahari katika upande wa mashariki, ukielekea upande wa kusini wa hekalu.
Y puso las bases junto a la casa, cinco en el lado derecho y cinco en el izquierdo; y puso el gran recipiente de agua en el lado derecho de la casa, hacia el este, mirando hacia el sur.
40 Huramu akatengeneza birika na koleo na besini la kunyunyizia. Kisha akamaliza kazi yote aliyofanya kwa mfalme Sulemani katika hekalu la BWANA:
E Hiram hizo las ollas, las espadas y los tazones. Entonces Hiram llegó al final de todo el trabajo que hizo para el rey Salomón en la casa del Señor:
41 Zile nguzo mbili, na lile besini lakawa kama taji ambalo lilikuwa juu ya zile nguzo, na nyavu mbili za mapambo za kufunika zile besini mbili za kuwa kama taji zilizokuwa juu ya nguzo.
Los dos pilares y las dos copas de las coronas que estaban en la parte superior de los dos pilares; y la reja que cubre las dos copas de las coronas en la parte superior de los pilares,
42 Kisha akatengeneza makomamanga mia nne kwa ajili ya zile nyavu mbili za mapambo: safu mbili za makomamamanga kwa kila kazi ya nyavu kwa ajili ya kufunikia zile besini mbili kama taji iliyo juu ya nguzo,
Y las cuatrocientas granadas para la reja, dos líneas de granadas para cada reja, cubriendo las dos copas de las coronas sobre los pilares;
43 yale makalio kumi, na birika kumi kwenye makalio.
Y las diez bases, con los diez recipientes de lavado sobre ellos;
44 Akatengeneza bahari na makisai kumi chini yake;
Y la gran vasija de agua, con los doce bueyes debajo de ella;
45 na masufuria, koleo, birika na vyombo vingine vyote. Huramu akivitengeneza kwa shaba iliyosuguliwa, kwa ajili ya mfalme Sulemani, na kawa ajili ya hekalu la BWANA.
Y las ollas y las palas y los tazones; Todas las vasijas que Hiram hizo para el rey Salomón, para la casa del Señor, eran de bronce pulido.
46 Mfalme alivisubu katika uwanda wa Yorodani, katika udongo mfinyanzi kati ya Sukoti na Zarethani.
Los hizo de bronce fundido en las tierras bajas de Jordania, en moldes de barro, en el camino al otro lado del río, en Adama, entre Sucot y Saretan.
47 Sulemani hakuvipima vyombo vyote kwa sababu vilikuwa vingi mno kuvipima, na kwa sababu uzito wa shaba ulikuwa hauwezi kupimwa.
No se midió el peso de todos estos vasos, porque había tantos; No fue posible conseguir el peso del bronce.
48 Sulemani akatengeneza mapambo yote yaliyokuwa kwenye hekalu la BWANA kwa kutumia dhahabu: Ile madhabahu ya dhahabu na ile meza ambayo iliwekwa mikate ya wonyesho.
Y Salomón mandó hacer todos los vasos que habían en la casa del Señor: el altar de oro y la mesa de oro sobre la cual se colocó el pan santo;
49 Vile vinara vya dhahabu, ambavyo vitano vilikuwa upande wa kulia na vitano mkono wa kushoto, mbele ya chumba cha ndani, vilikuwa vya dhahabu safi, na maua, na taa na koleo zilikuwa za dhahabu.
Y los candelabros para las luces, cinco en el lado derecho y cinco en el izquierdo enfrente del lugar santísimo, de oro puro; y las flores y las luces y todos los instrumentos de oro;
50 Vile vikombe, na makasi, mabakuri, na vijiko, na vyetezo vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi. na bawaba za dhahabu za milango ya ndani, ambazoo ndio mahali patakatifu sana, na milango ya ukumbi mkubwa, vyote vilitengenezwa kwa dhahabu.
Y las copas y las tijeras y los platos y las cucharas y los incensarios, todas de oro; y las clavijas sobre las que giraban las puertas, las puertas de la casa interior, el lugar más sagrado, y las puertas del Templo, todas de oro.
51 Kwa njia hii, kazi yote ambayo mfalme Sulemani alifanya kwa ajili ya hekalu ilimalizika. Kwa Sulemani akaviingiza ndani yake vitu vile vilivyokuwa vimewekwa wakfu na Daudi, baba yake, na fedha na dhahabu, na mapambo, na vile vya ndani ya hazina ya BWANA.
Así, toda la obra que el rey Salomón había hecho en la casa del Señor estaba completa. Entonces Salomón tomó las cosas santas que David su padre había dado, la plata y el oro y todas las vasijas, y las puso en los almacenes de la casa del Señor.

< 1 Wafalme 7 >