< 1 Wafalme 7 >
1 Ilimchukua Sulemani miaka kumi na tatu kujenga ikulu yake.
Forsothe Salomon bildide his owne hows in thrittene yeer, and brouyte it til to perfeccioun.
2 Aliijenga ikulu iliyoitwa mwitu wa Lebanoni. Urefu wake ulikuwa mita 46, na upanawake ulikuwa mita 23, na kimo chake kilikuwa mita 14. Nayo ilikuwa na safu nne ya nguzo za mierezi na mithili ya mwerezi juu ya nguzo.
He bildide an hows of the forest of Liban, of an hundrid cubitis of lengthe, and of fifti cubitis of breede, and of thretti cubitis of hiythe; and he bildide foure aleis bitwixe the pilers of cedre; for he hadde hewe doun trees of cedres in to pilers.
3 Paa la ikulu lilikuwa la mwerezi ambalo lilikaa juu ya mihimili. Mihili hiyo ilikuwa imeshikiliwa na nguzo. Kulikuwa na mihimili arobaini na tano, ambayo ilikuwa katika safu kumi na tano.
And he clothide al the chaumbir with wallis of cedris; which chaumbir was susteyned with fyue and fourti pileris. Sotheli oon ordre hadde fiftene pileris, set ayens hem silf togidere,
4 Nayo mihimili ilikuwa safu tatu, na kila dirisha lilikabili dirisha lingine katika madaraja matatu.
and biholdynge hem silf euene ayens, bi euene space bitwixe the pilers;
5 Milango yote na miimo ilitengenezwa kwa mraba, na madirisha yalikuwa yakikabiliana katika madaraja matatu
and on the pilers weren foure square trees, euene in alle thingis.
6 Akatengeneza baraza lenye uerfu wa mita 23 na upana wa mita 14. Mbele yake kulikuwa na ukumbi ulioezekwa.
And he made a porche of pilers of fifti cubitis of lengthe, and of thritti cubitis of breede; and `he made an other porche in the face of the gretter porche; and he made pileris, and pomels on the pileris.
7 Sulemani akajenga baraza yenye kiti cha enzi ambacho alitolea hukumu ya haki. Nayo ilikuwa imeezekwa kwa mwerezi kutoka sakafu moja hadi nyingine.
Also he maad a porche of the kyngis seete, in which the seete of doom was; and he hilide with trees of cedre, fro the pawment `til to the hiynesse.
8 Nyumba ya Sulemani ambayo alikusudia kuishi, katika behewa nyingine ndani ya sehemu ya chini ya ikulu, ilitengenezwa kwa kazi hiyo hiyo. Pia alimjengea binti wa Farao nyumba kama hii, ambaye alikuwa mke wake
And a litil hows, in which he sat to deme, was in the myddil porche, bi lijk werk. Also Salomon made an hows to the douyter of Farao, whom he hadde weddid, bi sich werk, bi what maner werk he made and this porche.
9 Majengo haya yalipmbwa kwa vitu vya thamaini, mawe ya thamani, yaliyochongwa na kukatwa kwa msimeno kufuata vipimo sahihi na kulainishwa pande zote. Mawe ya namna hii ndiyo yale yaliyotumika kuanzia kwenye msingi hadi juu, pia na nje hadi kwenye baraza.
He made alle thingis of preciouse stoonys, that weren sawid at sum reule and mesure, bothe with ynne and with outforth, fro the foundement `til to the hiynesse of wallis, and with ynne and `til to the gretter street, ethir court.
10 Msingi ulijengwa kwa mawe makubwa sana na ya thamani yenye urefu wa mita 3. 7 na mengine mita 4. 8.
Sotheli the foundementis weren of preciouse stoonys, grete stoonys of ten, ethir of eiyte cubitis;
11 Kwa juu ilipambwa kwa, mawe ya thamani yaliyochongwa sawa sawa kwa msimeno na kwa mihimili ya mierezi.
and preciouse stoonys hewun of euene mesure weren aboue; in lijk maner and of cedre.
12 Na behewa kubwa iliyokuwa ikizunguka ikulu ilikuwa na safu tatu za mawe yaliyokatwa na safu moja ya mihimili ya mierezi kama ilivyo kwenye baraza la ndani la hekalu la BWANA na ule ukumbi wa hekalu.
And the gretter court, `ethir voide space, was round, of thre ordris of hewun stonus, and of oon ordre of hewun cedre; also and in the ynnere large strete of the hows of the Lord, and in the porche of the hows of the Lord.
13 Mfalme Sulemani alituma watu kumleta Huramu kutoka Tiro.
Also kyng Salomon sente, and brouyte fro Tire Hiram, the sone of a womman widewe,
14 Huramu alikuwa mwana wa mjane wa kabila ya Naftali; baba yake alikuwa mtu wa Tiro, mfua shaba. Huramu alikuwa mwingi wa hekima na ufahamu na stadi za kufanya kazi kubwa za shaba. Aliletwa kwa mfalme ili kufanya kazi zilizohusiana na shaba kwa mfalme.
of the lynage of Neptalym, of the fadir a man of Tyre, Hiram, a crafty man of brasse, and ful of wisdom, and vndirstondynge, and doctryn, to make al werk of bras. And whanne he hadde come to kyng Salomon, he made al hys werk.
15 Huramu alizilemba zile nguzo mbili za shaba, kila moja ilikuwa na kimo cha mita 8. 3 na mzingo wa mita 5. 5.
And he made twey pilers of bras, o piler of eiytene cubitis of hiythe; and a lyne of twelue cubitis cumpasside euer either piler.
16 Akatengeneza taji mbili za shaba za kuwekwa juu ya zile nguzo. Kimo cha kila taji ilikuwa mita 2. 3.
Also he made twei pomels, yotun of bras, that weren set on the heedis of the pilers; o pomel of fyue cubitis of hiythe, and the tothir pomel of fyue cubitis of heiythe; and bi the maner of a net,
17 Kulikuwa na nyavu za kuwa kama kazi ya kusuka, na masongo ya mikufu, kwa ajili ya kuvipamba vile vichwa vya nguzo, nayo yailikuwa saba kwa kila kichwa.
and of chaynes knyt to gidere to hem, bi wonderful werk. Euer either pomel of the pilers was yotun; seuen werkis lijk nettis of orders weren in o pomel, and seuen werkis lijk nettis weren in the tother pomel.
18 Kwa hiyo Huramu akafanya safu mbili za komamanga kuzunguka vile vichwa vya nguzo ili kuvipamba vile vichwa.
And he made perfitli the pilers, and twei ordris `bi cumpas of alle werkis lijk nettis, that tho schulden hile the pomels, that weren on the hiynesse of pumgarnadis; in the same maner he dide also to the secounde pomel.
19 Zile taji kwenye vile vichwa vya nguzo za ukumbi zilikuwa zimepambwa kwa maua, yenye vimo vya mita 1. 8.
Sotheli the pomels, that weren on the heedis of the pilers in the porche, weren maad as bi the werk of lilye, of foure cubitis;
20 Hizo taji kwenye hizo nguzo mbili kwenye vichwa vyake, karibu yake kulikuwa na makomamanga mia mbili yote yakiwa kwenye safu.
and eft othere pomels in the hiynesse of pilers aboue, bi the mesure of the piler, ayens the werkis lijk nettis; forsothe twey hundrid ordris of pumgarnadis weren in the cumpas of the secounde pomel.
21 Alisimamisha nguzo kwenye ukumbi wa hekalu. Ile nguzo ya kuume akaipa jina la Yakini, na ile ya kushoto akaipa jina la Boazi.
And he settide the twey pilers in the porche of the temple; and whanne he hadde set the riythalf pilere, he clepide it bi name Jachym; in lijk maner he reiside the secounde pilere, and he clepide the name therof Booz.
22 Na juu ya zile nguzo kulikuwa na mapambo kama maua. Hivyo ndivyo zile nguzo zilivyotengenezwa.
And he settide on the heedis of the pilers a werk bi the maner of a lilie; and the werk of the pilers was maad perfit.
23 Tena akafanya bahari ya kusubu ya, yenye mita 2. 3 kutoka ukingo hadi ukingo, kimo chake kilikuwa mita 4. 6, mziingo wake ulikuwa mita 13. 7.
Also he made a yotun see, that is, a waisching vessel for preestis, round in cumpas, of ten cubitis fro brynke til to the brinke; the heiynesse therof was of fyue cubitis; and a corde of thretti cubitis yede aboute it bi cumpas.
24 Na chini ya ile bahari kulikuwa na vibuyu vilivyoizunguka, vilikuwa vibuyu kumi na nane katika kila mita, vilivyowekwa katika kila hicho kipande wakati bahari inapokuwa kalibu.
And grauyng vndir the brynke cumpasside it, and cumpasside the see bi ten cubitis; tweyne ordris of grauyngis conteynynge summe stories weren yotun, and stoden on twelue oxis;
25 Bahari ikakaa juu ya makisai kumi na mbili, tatu, zilitazama kaskazini, tatu zikitazama magharibi, tatu zikitazama kusini na tatu zikitazama kaskazini. Ile bahari iliwekwa juu yao, na pande zao zote za nyuma zilikuwa ndani.
of whiche oxis thre bihelden to the north, and thre to the west, and thre to the south, and three to the eest; and the see was aboue on tho oxis, of whiche alle the hyndere thingis weren hid `with ynne.
26 Bahari ilikuwa nene kama upana wa mkono, na ukingo wake ulikuwakama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi huingia bathi elfu mbili za maji.
Sotheli the thicknesse of the see was of thre ounces, and the brynke therof was as the brynke of a cuppe, and as the leef of a lilie crokid ayen; the see took twei thousynde bathus, thre thousynde metretis.
27 Huramu akatengeneza makalio kumi ya shaba. Kila kalio lilkuwa na urefu wa mita 1. 8, upana wa mita 1. 8, na kimo cha mita 1. 3.
And he made ten brasun foundementes, ech foundement of foure cubites of lengthe, and of foure cubitis of brede, and of thre cubitis of hiynes.
28 Hivi ndivyo kazi za makalio zilivyofanywa. Yalikuwa na papi ambazo zilikaa kati kati ya vipandio,
And thilke werk of foundementis was rasid bitwixe; and grauyngis weren bitwixe the ioynturis.
29 na juu ya papi na vipandio kulikuwa na simba, makisai, na makerubi. Chini na juu simba kulikuwa na masongo ya kazi ya kufuliwa.
And bitwixe the litil corouns and serclis weren liouns, oxis, and cherubyns; and in the ioynturis in lijk maner aboue; and vndir the lyouns and oxis weren as reynes of bridels of bras hangynge doun.
30 Kila kalio lilikuwa na magurudumu ya shaba na vipini, na pande zake nne na miguu yake minne ilikuwa na mataruma chini ya birika. Chini ya birika yalikuweko mataruma ya kusubu yenye masongo katika kila upande.
And bi ech foundement weren foure wheelis, and brasun extrees; and bi foure partis weren as litle schuldryngis vndir the waischyng vessel, `the schuldryngis yotun, and biholdynge ayens hemsilf togidere.
31 Na kinywa chake kilikuwa cha kuviringana, chenye upana wa sentimita araobaini na sita, na ile taji ilikuwa na sentimita ishirini na tatu. Na kinywa chake kilikuwa na nakshi, na papi zake zilikuwa za mraba, na wala siyo za mvringo.
And the mouth of the waischyng vessel with ynne was in the hiynesse of the heed, and that, that apperide with outforth, was of o cubit, and it was al round, and hadde togidere o cubit and an half; sotheli dyuerse grauyngis weren in the corneris of pilers, and the mydil piler bitwixe was square, not round.
32 Yale magurudumu mawili yalikuwa chini ya papi, na mikono ya magurudumu yalikuwa ndani ya makalio. Kimo cha yale magurudumu kilikuwa sentimeta sitini na tisa.
And the foure wheelis, that weren bi foure corneris of the foundement, cleuyden togidere to hem silf vndir the foundement; o wheele hadde o cubit and an half of hiythe.
33 Yale magurudumu yalikuwa kama ya gari. Mikono yake, na maduara, matindi yake, na vipande vya ndani vyote vilikuwa vya kusubu.
Sotheli the wheelis weren siche, whiche maner wheelis ben wont to be maad in a chare; and the extrees, and the `naue stockis, and the spokis, and dowlis of tho wheelis, alle thingis weren yotun.
34 Kulikuwa na mataruma manne katika pande zake nne za makalio, yaliyokuwa yameshikamanishwa na kalio lenyewe.
For also the foure litle schuldryngis, bi alle the corners of o foundement, weren ioyned to gidere, and yotun of that foundement.
35 Juu ya makalio kulikuwa na duara yenye kina cha sentimita ishirini na tatu, na juu ya makalio mashikio yake na papi zake zikiwa zimeshikamanishwa.
Sotheli in the hiynesse of the foundement was sum roundenesse, of o cubite and an half, so maad craftili, that the waischyng vessel myyte be set aboue, hauynge his purtreiyngis, and dyuerse grauyngis of it silf.
36 Juu ya mabamba na papi zake Huramu akachora makerubi, simba, na mitende ambayo ilifunika nafasi ya juu, nayo ilikuwa imezungukwa na masongo.
Also he grauyde in tho wallis, that weren of bras, and in the corneris, cherubyns, and liouns, and palmes, as bi the licnesse of a man stondynge, that tho semeden not grauun, but put to bi cumpas.
37 Alitengeneza makalio kumi kwa jinsi hii. Yote yalikuwa yametengenezwa kwa kufanana, na yalikuwa ya vipimo sawa, na sura inayofanana.
Bi this maner he made ten foundementis, bi o yetyng and mesure, and lijk grauyng.
38 Huramu akatengeneza birika kumi za shaba. Birika moja liliweza kubeba bathi arobaini za maji. Kila birika lilikuwa mita 1. 8 toka birika moja hadi jingine na kulikuwa na birika moja katika kila kalio kati ya yale kumi.
Also he made ten waischyng vessels of bras; o waischyng vessel took fourti bathus, and it was of foure cubitis; and he puttide ech waischyng vessel bi it silf bi ech foundement bi it silf, that is, ten.
39 Alitengeneza makalio tano upande wa kusini unaoelekea upande wa hekalu. Akatengeneza bahari katika upande wa mashariki, ukielekea upande wa kusini wa hekalu.
And he made ten foundementis, fyue at the riyt half of the temple, and fyue at the left half; sotheli he settide the see at the riyt half of the temple, ayens the eest, at the south.
40 Huramu akatengeneza birika na koleo na besini la kunyunyizia. Kisha akamaliza kazi yote aliyofanya kwa mfalme Sulemani katika hekalu la BWANA:
Also Hiram made cawdrouns, and pannes, and wyn vessels; and he made perfitli al the werk of kyng Salomon in the temple of the Lord.
41 Zile nguzo mbili, na lile besini lakawa kama taji ambalo lilikuwa juu ya zile nguzo, na nyavu mbili za mapambo za kufunika zile besini mbili za kuwa kama taji zilizokuwa juu ya nguzo.
He made twey pilers, and twei cordis of pomels on the pomels of pilers, and twei werkis lijk nettis, that tho schulden hile twey cordis, that weren on the heedis of pileris.
42 Kisha akatengeneza makomamanga mia nne kwa ajili ya zile nyavu mbili za mapambo: safu mbili za makomamamanga kwa kila kazi ya nyavu kwa ajili ya kufunikia zile besini mbili kama taji iliyo juu ya nguzo,
And `he made pumgarnadis foure hundrid in twey werkis lijk nettis; `he made tweyne ordris of pumgarnadis in ech werk lijk a net, to hile the cordis of the pomels, that weren on the heedis of pilers.
43 yale makalio kumi, na birika kumi kwenye makalio.
And he made ten foundementis, and ten waischyng vessels on the foundementis;
44 Akatengeneza bahari na makisai kumi chini yake;
and o se, `that is, a waischyng vessel for preestis, and twelue oxis vndur the see;
45 na masufuria, koleo, birika na vyombo vingine vyote. Huramu akivitengeneza kwa shaba iliyosuguliwa, kwa ajili ya mfalme Sulemani, na kawa ajili ya hekalu la BWANA.
and `he made cawdruns, and pannys, and wyn vessels. Alle vessels, whiche Hiram made to kyng Salomon in the hows of the Lord, weren of latoun.
46 Mfalme alivisubu katika uwanda wa Yorodani, katika udongo mfinyanzi kati ya Sukoti na Zarethani.
And the kyng yetide tho vessels in the feeldi cuntrey of Jordan, in cleyi lond, bitwixe Sochot and Sarcham.
47 Sulemani hakuvipima vyombo vyote kwa sababu vilikuwa vingi mno kuvipima, na kwa sababu uzito wa shaba ulikuwa hauwezi kupimwa.
And Salomon settide alle the vessels; forsothe for greet multitude no weiyte was of bras, `that is, it passide al comyn weiyte.
48 Sulemani akatengeneza mapambo yote yaliyokuwa kwenye hekalu la BWANA kwa kutumia dhahabu: Ile madhabahu ya dhahabu na ile meza ambayo iliwekwa mikate ya wonyesho.
And Salomon made alle vessels in the hows of the Lord; sotheli he made the golden auter, `that is, the auter of encense, that was with ynne the temple, and the goldun boord, on whych the loouys of settynge forth weren set;
49 Vile vinara vya dhahabu, ambavyo vitano vilikuwa upande wa kulia na vitano mkono wa kushoto, mbele ya chumba cha ndani, vilikuwa vya dhahabu safi, na maua, na taa na koleo zilikuwa za dhahabu.
and he made goldun candilstikis, fyue at the riyt half, and fyue at the left half, ayens Goddis answerynge place, `of purest gold; and he made as the flouris of a lilie, and goldun lanterns aboue, and goldun tongis; and pottis,
50 Vile vikombe, na makasi, mabakuri, na vijiko, na vyetezo vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi. na bawaba za dhahabu za milango ya ndani, ambazoo ndio mahali patakatifu sana, na milango ya ukumbi mkubwa, vyote vilitengenezwa kwa dhahabu.
and hokis, and violis, and morteris, and censeris of pureste gold; and the herris, ether heengis, of the doris of the ynnere hows of the hooli of hooli thingis, and of the doris of the hows of the temple weren of gold.
51 Kwa njia hii, kazi yote ambayo mfalme Sulemani alifanya kwa ajili ya hekalu ilimalizika. Kwa Sulemani akaviingiza ndani yake vitu vile vilivyokuwa vimewekwa wakfu na Daudi, baba yake, na fedha na dhahabu, na mapambo, na vile vya ndani ya hazina ya BWANA.
And Salomon performyde al the werk, which he made in the hows of the Lord; and he brouyte ynne the thingis, whiche Dauid, his fadir, hadde halewid; siluer, and gold, and vessels; and he kepte in the tresours of the hows of the Lord.