< 1 Wafalme 6 >

1 Kwa hiyo Sulemani akaanza kulijenga hekalu. Hii ilikuwa mwaka wa 480 baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Sulemani huko Israeli, katika mwezi wa Ziv, ambao ndio mwezi wa pili.
So Solomon began to build the temple of Yahweh. This happened in the 480th year after the people of Israel came out of the land of Egypt, in the fourth year of Solomon's reign over Israel, in the month of Ziv, which is the second month.
2 Hekalu ambalo mfalme Sulemani alimjengea BWANA lilikuwa na urefu wa mita 27, na upana wa mita 9, na kimo cha mita 13. 5.
The temple that King Solomon built for Yahweh was sixty cubits long, twenty cubits wide, and thirty cubits high.
3 Na ukumbi uliokuwa mbele ya hekalu ulikuwa na urefu wa mita 9 na upana wa mita 4. 5 sawa na upana wa sehemu kuu ya hekalu.
The portico in front of the temple's main hall was twenty cubits in length, equal to the width of the temple, and ten cubits deep in front of the temple.
4 Lile hekalu alilitengenezea madirisha ambayo fremu zake kwa nje yalifanya yaonekane membamba kuliko ile sehemu ya ndani.
For the house he made windows with frames that made them more narrow at the outside than on the inside.
5 Na ukuta wa nyumba aliuzungushia vyumba kuzunguka pande zake, kushikamana na vyumba vya nje na vya ndani ya hekalu. Akajenga vyumba katika pande zote.
Against the walls of the main chamber he built rooms around it, around both the outer room and the inner room. He built rooms all around the sides.
6 Kile chumba cha chini kilikuwa na upana wa mita 2. 3, kile cha kati kilikuwa na upana wa mita 2. 8. na kile cha tatu kilikuwa na upana wa mita 3. 2. upande wa nje akaupunguza ukuta wa nyumba pande zote, ili boriti zisishikamane ukutani mwa nyumba.
The lowest story was five cubits wide, the middle was six cubits wide, and the third was seven cubits wide. For on the outside he made offsets in the wall of the house all around so that the beams would not be inserted in the walls of the house.
7 Hekalu lilijengwa kwa mawe yaliyokuwa yamechongwa chimboni. Hakuna nyundo, wala shoka au chombo chochote cha chuma kilisikika wakati hekalu lilipokuwa likjengwa.
The house was built of stones prepared at the quarry. No hammer, ax, or any iron tool was heard in the house while it was being built.
8 Upande wa kusini wa hekalu kulikuwa na lango la chini, ambalo mtu hupanda kwa madaraja mpaka juu kwenye chumba cha kati, na kutoka chumba cha kati hadi chumba cha tatu.
On the south side of the temple there was an entrance at the ground level, then one went up by stairs to the middle level, and from the middle to the third level.
9 Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza, akalifunika hekalu kwa boriti na mbao za mwerezi.
So Solomon built the temple and finished it; he covered the house with beams and planks of cedar.
10 Akajenga vyumba vya pembeni mwa hekalu, kila upande mita 2. 3 kwenda juu. Navyo vikaunganishwa na hekalu kwa mbao za mierezi.
He built the side rooms against the inner chambers of the temple, each side five cubits high; they were joined to the house with timbers of cedar.
11 Neno la BWANA likamjia Sulemani, likisema,
The word of Yahweh came to Solomon, saying,
12 “Kuhusu hili hekalu ambalo unajenga, kama utatatembea katika maagizo yangu na kuhukumu kwa haki, na kutunza amri zangu na kuishi kwa hizo, ndipo ntakapozithibitisha ahadi zangu na wewe ambazo niliziahidi kwa baba yako Daudi.
“Concerning this temple which you are building, if you walk in my statutes and do justice, keep all my commandments and walk in them, then I will confirm my promise with you that I had made to David your father.
13 Nitaishi kati ya watu wa Israeli nami sitawatupa.”
I will live among the people of Israel and will not forsake them.”
14 Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza.
So Solomon built the house and finished it.
15 Kisha akajenga kuta za ndani za hekalu kwa mbao za mwerezi. Kuanzia sakafu ya hekalu hadi boriti za juu, kwa ndani akazifunika kwa miti, na akaifunika sakafu kwa mbao za miberoshi.
Then he built the interior walls of the house with boards of cedar. From the floor of the house to the ceiling, he covered them on the inside with wood, and he covered the floor of the house with cypress boards.
16 Alijenga mita 9 ndani ya hekalu kwa mbao za miberoshi kutoka sakafuni hadi juu. Hiki ni chumba cha ndani, cha patakatifu sana.
He built twenty cubits onto the rear of the house with boards of cedar from the floor to the ceiling. He built this room to be the inner room, the most holy place.
17 Ule ukumbu mkuu, ulikuwa mahali pakatifu amabao ulikuwa mbele ya patakatifu sana, ulikuwa wa mita 18. hapo kulikwa na mbao za mwerezi ndani ya hekalu, zilizokuwa zimechongwa kwa sura ya vibuyu na maua yaliyochanua.
The main hall, that is, the holy place that was in front of the most holy place, was forty cubits long.
18 Zote zilikuwa za mierezi kwa ndani. Hapakuonekana chochote ndani kilichokuwa kimetengenezwa kwa mawe.
There was cedar inside the house, carved in the shape of gourds and open flowers. All was cedar inside. No stonework was visible on the inside.
19 Sulemani alitengeneza kile chumba cha ndani kwa lengo la kuweka sanduku la agano la BWANA.
Solomon prepared the inner room inside the house in order to place the ark of the covenant of Yahweh there.
20 Kile chumba cha ndani kilikuwa na upana wa mita 9, na kimo cha mita 9. Sulemani alizifunika kuta kwa dhabahu na madhabahu aliifunika kwa mbao za mierezi.
The inner room was twenty cubits in length, twenty cubits in width, and twenty cubits in height. Solomon overlaid the walls with pure gold and covered the altar with cedar wood.
21 Sulemani alifunika ndani ya hekalu kwa dhahabu safi na akaweka mikufu ya dhahabu iliyopita mbele ya chumba cha ndani, na kulifunika eneo la mbele kwa dhabahu.
Solomon overlaid the inside of the temple with pure gold, and he placed chains of gold across the front of the inner room, and overlaid the front with gold.
22 Akalisakafia kwa dhahabu eneo lote la ndani mpaka akamaliza hekalu lote. Pia akalisakafia kwa dhahabu madhahabu yote ya chumba cha ndani.
He overlaid the entire interior with gold until all the temple was finished. He also overlaid with gold the whole altar that belonged to the inner room.
23 Sulemani akatengeneza makerubi mawili kwa mbao za mizeituni, kila moja lilikuwa na kimo cha mita 4. 5 kwa ajili ya chumba cha ndani.
Solomon made two cherubim of olivewood, each ten cubits high, for the inner room.
24 Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa mita 2. 3. Kwa hiyo kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa lingine kulikuwa na umbali wa mita 4. 5. Yule
One wing of the first cherub was five cubits long and its other wing was also five cubits long. So from the tip of one wing to the tip of the other there was a distance of ten cubits.
25 kerubi mwingine naye alikuwa na bawa lenye kipimo cha mita 4. 5 Makerubi hawa walikuwa wanafanana kwa umbo na kwa vipimo.
The other cherub also had a wingspan ten cubits. Both the cherubim were of the same dimensions and shape.
26 Kimo cha kerubi mmoja kilikuwa mita 4. 5 na yule wa pili alikuwa hivyo hivyo.
The height of one cherub was ten cubits and the other cherub was the same.
27 Sulemani aliwaweka hao kerubi kwenye chumba cha patakatifu sana. Bawa moja la kerubi lilikuwa limeenea kiasi kwamba bawa moja liligusa ukuta huu na bawa la yule wa pili nalo liligusa ukuta wa upande mwingine. Hayo mabawa yalikuwa yanakutana katikati ya chumba cha patakatifu sana.
Solomon placed the cherubim in the innermost room. The wings of the cherubim were stretched out so that the wing of one touched one wall and the wing of the other cherub touched the other wall. Their wings touched one another in the middle of the most holy place.
28 Sulemani aliwafunika hao kerubi kwa dhahabu.
Solomon overlaid the cherubim with gold.
29 Akazinakshi kuta zote kwa sura za makerubi, miti ya mitende, na maua yaliyochanua, kwa vyumba vya nje na vya ndani.
He carved all the walls of the house around about with figures of cherubim, palm trees, and open flowers, in the outer and inner rooms.
30 Sulemani akalisakafia hekalu kwa dhahabu, kwa vyumba vyote vya ndani na vya nje.
Solomon overlaid the floor of the house with gold, in both the outer and inner rooms.
31 Sulemani akatengeneza milango ya mbao za mizeituni kwenye lango la kuingia ndani. Aliweka vizingiti na miimo kwenye pande tano.
Solomon made doors of olivewood for the entrance to the inner room. The lintel and doorposts had five indented sections.
32 Kwa hiyo akatengeneza na milango miwili ya mizeituni, na akainakshi kwa makerubi, na mitende, na maua yaliyochanua. Akasakafia kwa dhahabu na akatandaza dhahabu kwenye makerubi na kwenye mitende.
So he made two doors of olivewood, and he made on them carvings of cherubim, palm trees, and open flowers. He overlaid them with gold and he spread the gold on the cherubim and palm trees.
33 Kwa njia hii, akalitengenezea hekalu miimo miwili ya mbao za mizeituni yenye pande nne
In this way, Solomon also made for the temple entrance doorposts of olive wood having four indented sections
34 na milango miwili ya mbao za mierezi. Zile mbao mbili za mlango mmoja zilikuwa zikijikunja na mbao mbili za mlango wa pili nazo zilikuwa zikijikunja pia.
and two doors of cypress wood. The two leaves of the one door were folding and the two leaves of the other door were folding.
35 Akazinakshi kwa makerubi, mitende, na maua yaliyochanua, na pia akazisakafia kwa dhahabu juu ya zile nakshi.
He carved on them cherubim, palm trees, and open flowers, and he evenly overlaid gold on the carved work.
36 Akalijengs Korido la ndani kwa safu tatu za mawe ya kuchongwa na safu moja ya mhimili wa mierezi.
He built the inner courtyard with three rows of cut stone and a row of cedar beams.
37 Msingi wa hekalu ulijengwa katika mwaka wa nne, wa mwezi wa Ziv.
The foundation of the house of Yahweh was laid in the fourth year, in the month of Ziv.
38 Mwaka wa kumi na moja mwezi wa Buli, ambao ndio mwezi wa nane, sehemu zote za hekalu zilimalizika na sharti zake zote. Sulemani alilijenga hekalu kwa miaka saba.
In the eleventh year, in the month of Bul, which is the eighth month, the house was finished in all its parts and conforming to all its specifications. Solomon took seven years to build the temple.

< 1 Wafalme 6 >